About


Karibu ujiunge na chuo cha kisasa cha Easy Tech.Computer kwa mafanikio yako,Walimu waliobobea katika fani hiyo wanapatikana chuoni hapo

elimak

elimak

Pages - Menu

Tuesday, July 30, 2013

DC NALICHO AWATIMUA WAVAMIZI MSITU WA SHAMBA LA BIBI

Na Steven Augustino, Tunduru
MWENYEKITI wa kamati ya Ulinzi ya Wilaya ya Tunduru, Mkuu wa Wilaya hiyo Mkoani Ruvuma Chande Nalicho ametoa wiki moja kwa Wakulima na Wafugaji wa jamii ya Kisukuma kuondoka katika eneo la hifadhi ya msitu wa Shamba la Bibi vinginevyo hatua kali za Kisheria zitachukuliwa dhidi yao.
Dc, Nalicho alitoa maagizo hayo baada ya kamati ya Ulinzi na Usalama ya Wilaya hiyo kufanya ziara ya kushtukiza katika msitu huo na kujionea hali halisi ya uhalibifu wa vyanzo vya maji, mabwawa na misitu iliyopo katika hifadhi hiyo inayo unganisha Vijiji vya Nangunguru, Majala na Mkalekawana katika Tarafa ya Nampungu kata ya Nandenbo Wilayani humo.
Alisema anatoa siku Saba kwa watu wote waliovamia msitu huo wa hifadhi kuondoka kwani haiwezekani watu waendelee kuishi wanavyo penda na kuharibu mazingira katika vyanzo vya maji na hifadhi ya misitu kana kwamba serikali haipo
Mkuu huyo aliwataka Watendaji Kata ,Vijiji kwa kushirikiana na Maafisa Tarafa Wilayani humo kutekeleza majukumu yao ikiwemo kuwaelekeza wafugaji kufuata taratibu za kuonana na viongozi wa Vijiji husika, kufanya mikutano inayo wahusisha wananchi katika maamuzi ya kuwapokea wafugaji hao ili kuyaondoa maeneo yao katika migogoro ya aina hiyo.
“Kwavile mifugo ni muhimu kwetu na endapo itatumika vizuri na kwa kuzingatia kanuni, miongozo na maelekezo yanayotolewa na Serikali italeta manufaa kwa Wananchi wetu” alisema Dc, Nalicho na kuongeza kuwa mtindo wa kuishi kwa uhasama kati ya wafugaji na wakulima hauwezi kuwa na tija.
Awali akiongea katika ziara hiyo Afisa misitu wa Wilaya la Tunduru  Rashid Mtotela alimweleza Dc, Nalicho kuwa Wakulima na wafugaji hao walivamia msitu huo mwaka 2006 /2007 na kuendelea kujiimarisha kila mwaka baada ya kubaini kutokuwepo kwa vikwazo vyovyote kutoka Serikalini.
Alisema hifadhi hiyo ambayo awali ilikuwa imeunganishwa na Hifadhi ya Taifa (Selous) tangu mwaka 1974 na baadae kuunda hifadhi shirikishi mwaka 2007 kupitia mradi wa Jont participatory Forest Menegement (JPFM) liyounganisha Vijiji vya Nangunguru, Mkalekawana na Majala kila Kijiji kimekuwa kikikwepa majukumu yake ya kulinda hifadhi hiyo hali ambayo imechangia kuendelea kuhalibika kwa mazingira hayo.
Wakiongea kwaniaba ya Wananchi wa Vijiji hivyo Mwenyekiti wa Kijiji cha Nangunguru Bw.Said Rashid Mkwekwele, Mtendaji wa Kijiji hicho Zainabu Twaha na Afisa Tarafa wa Nampungu Joshua John wakawashushia lawama baadhi ya wakuu wa Idara katika halmashauri ya Wilaya hiyo kuwa umekuwa na kigugumizi katika ufuatiliaji na uchukuzi wa maamuzi juu ya migogoro hiyo.

DC NALICHO AWATIMUA WAVAMIZI MSITU WA SHAMBA LA BIBI

Na Steven Augustino, Tunduru
MWENYEKITI wa kamati ya Ulinzi ya Wilaya ya Tunduru, Mkuu wa Wilaya hiyo Mkoani Ruvuma Chande Nalicho ametoa wiki moja kwa Wakulima na Wafugaji wa jamii ya Kisukuma kuondoka katika eneo la hifadhi ya msitu wa Shamba la Bibi vinginevyo hatua kali za Kisheria zitachukuliwa dhidi yao.
Dc, Nalicho alitoa maagizo hayo baada ya kamati ya Ulinzi na Usalama ya Wilaya hiyo kufanya ziara ya kushtukiza katika msitu huo na kujionea hali halisi ya uhalibifu wa vyanzo vya maji, mabwawa na misitu iliyopo katika hifadhi hiyo inayo unganisha Vijiji vya Nangunguru, Majala na Mkalekawana katika Tarafa ya Nampungu kata ya Nandenbo Wilayani humo.
Alisema anatoa siku Saba kwa watu wote waliovamia msitu huo wa hifadhi kuondoka kwani haiwezekani watu waendelee kuishi wanavyo penda na kuharibu mazingira katika vyanzo vya maji na hifadhi ya misitu kana kwamba serikali haipo
Mkuu huyo aliwataka Watendaji Kata ,Vijiji kwa kushirikiana na Maafisa Tarafa Wilayani humo kutekeleza majukumu yao ikiwemo kuwaelekeza wafugaji kufuata taratibu za kuonana na viongozi wa Vijiji husika, kufanya mikutano inayo wahusisha wananchi katika maamuzi ya kuwapokea wafugaji hao ili kuyaondoa maeneo yao katika migogoro ya aina hiyo.
“Kwavile mifugo ni muhimu kwetu na endapo itatumika vizuri na kwa kuzingatia kanuni, miongozo na maelekezo yanayotolewa na Serikali italeta manufaa kwa Wananchi wetu” alisema Dc, Nalicho na kuongeza kuwa mtindo wa kuishi kwa uhasama kati ya wafugaji na wakulima hauwezi kuwa na tija.
Awali akiongea katika ziara hiyo Afisa misitu wa Wilaya la Tunduru  Rashid Mtotela alimweleza Dc, Nalicho kuwa Wakulima na wafugaji hao walivamia msitu huo mwaka 2006 /2007 na kuendelea kujiimarisha kila mwaka baada ya kubaini kutokuwepo kwa vikwazo vyovyote kutoka Serikalini.
Alisema hifadhi hiyo ambayo awali ilikuwa imeunganishwa na Hifadhi ya Taifa (Selous) tangu mwaka 1974 na baadae kuunda hifadhi shirikishi mwaka 2007 kupitia mradi wa Jont participatory Forest Menegement (JPFM) liyounganisha Vijiji vya Nangunguru, Mkalekawana na Majala kila Kijiji kimekuwa kikikwepa majukumu yake ya kulinda hifadhi hiyo hali ambayo imechangia kuendelea kuhalibika kwa mazingira hayo.
Wakiongea kwaniaba ya Wananchi wa Vijiji hivyo Mwenyekiti wa Kijiji cha Nangunguru Bw.Said Rashid Mkwekwele, Mtendaji wa Kijiji hicho Zainabu Twaha na Afisa Tarafa wa Nampungu Joshua John wakawashushia lawama baadhi ya wakuu wa Idara katika halmashauri ya Wilaya hiyo kuwa umekuwa na kigugumizi katika ufuatiliaji na uchukuzi wa maamuzi juu ya migogoro hiyo.

DC NALICHO AWATIMUA WAVAMIZI MSITU WA SHAMBA LA BIBI

Na Steven Augustino, Tunduru
MWENYEKITI wa kamati ya Ulinzi ya Wilaya ya Tunduru, Mkuu wa Wilaya hiyo Mkoani Ruvuma Chande Nalicho ametoa wiki moja kwa Wakulima na Wafugaji wa jamii ya Kisukuma kuondoka katika eneo la hifadhi ya msitu wa Shamba la Bibi vinginevyo hatua kali za Kisheria zitachukuliwa dhidi yao.
Dc, Nalicho alitoa maagizo hayo baada ya kamati ya Ulinzi na Usalama ya Wilaya hiyo kufanya ziara ya kushtukiza katika msitu huo na kujionea hali halisi ya uhalibifu wa vyanzo vya maji, mabwawa na misitu iliyopo katika hifadhi hiyo inayo unganisha Vijiji vya Nangunguru, Majala na Mkalekawana katika Tarafa ya Nampungu kata ya Nandenbo Wilayani humo.
Alisema anatoa siku Saba kwa watu wote waliovamia msitu huo wa hifadhi kuondoka kwani haiwezekani watu waendelee kuishi wanavyo penda na kuharibu mazingira katika vyanzo vya maji na hifadhi ya misitu kana kwamba serikali haipo
Mkuu huyo aliwataka Watendaji Kata ,Vijiji kwa kushirikiana na Maafisa Tarafa Wilayani humo kutekeleza majukumu yao ikiwemo kuwaelekeza wafugaji kufuata taratibu za kuonana na viongozi wa Vijiji husika, kufanya mikutano inayo wahusisha wananchi katika maamuzi ya kuwapokea wafugaji hao ili kuyaondoa maeneo yao katika migogoro ya aina hiyo.
“Kwavile mifugo ni muhimu kwetu na endapo itatumika vizuri na kwa kuzingatia kanuni, miongozo na maelekezo yanayotolewa na Serikali italeta manufaa kwa Wananchi wetu” alisema Dc, Nalicho na kuongeza kuwa mtindo wa kuishi kwa uhasama kati ya wafugaji na wakulima hauwezi kuwa na tija.
Awali akiongea katika ziara hiyo Afisa misitu wa Wilaya la Tunduru  Rashid Mtotela alimweleza Dc, Nalicho kuwa Wakulima na wafugaji hao walivamia msitu huo mwaka 2006 /2007 na kuendelea kujiimarisha kila mwaka baada ya kubaini kutokuwepo kwa vikwazo vyovyote kutoka Serikalini.
Alisema hifadhi hiyo ambayo awali ilikuwa imeunganishwa na Hifadhi ya Taifa (Selous) tangu mwaka 1974 na baadae kuunda hifadhi shirikishi mwaka 2007 kupitia mradi wa Jont participatory Forest Menegement (JPFM) liyounganisha Vijiji vya Nangunguru, Mkalekawana na Majala kila Kijiji kimekuwa kikikwepa majukumu yake ya kulinda hifadhi hiyo hali ambayo imechangia kuendelea kuhalibika kwa mazingira hayo.
Wakiongea kwaniaba ya Wananchi wa Vijiji hivyo Mwenyekiti wa Kijiji cha Nangunguru Bw.Said Rashid Mkwekwele, Mtendaji wa Kijiji hicho Zainabu Twaha na Afisa Tarafa wa Nampungu Joshua John wakawashushia lawama baadhi ya wakuu wa Idara katika halmashauri ya Wilaya hiyo kuwa umekuwa na kigugumizi katika ufuatiliaji na uchukuzi wa maamuzi juu ya migogoro hiyo.

DC NALICHO AWATIMUA WAVAMIZI MSITU WA SHAMBA LA BIBI

Na Steven Augustino, Tunduru
MWENYEKITI wa kamati ya Ulinzi ya Wilaya ya Tunduru, Mkuu wa Wilaya hiyo Mkoani Ruvuma Chande Nalicho ametoa wiki moja kwa Wakulima na Wafugaji wa jamii ya Kisukuma kuondoka katika eneo la hifadhi ya msitu wa Shamba la Bibi vinginevyo hatua kali za Kisheria zitachukuliwa dhidi yao.
Dc, Nalicho alitoa maagizo hayo baada ya kamati ya Ulinzi na Usalama ya Wilaya hiyo kufanya ziara ya kushtukiza katika msitu huo na kujionea hali halisi ya uhalibifu wa vyanzo vya maji, mabwawa na misitu iliyopo katika hifadhi hiyo inayo unganisha Vijiji vya Nangunguru, Majala na Mkalekawana katika Tarafa ya Nampungu kata ya Nandenbo Wilayani humo.
Alisema anatoa siku Saba kwa watu wote waliovamia msitu huo wa hifadhi kuondoka kwani haiwezekani watu waendelee kuishi wanavyo penda na kuharibu mazingira katika vyanzo vya maji na hifadhi ya misitu kana kwamba serikali haipo
Mkuu huyo aliwataka Watendaji Kata ,Vijiji kwa kushirikiana na Maafisa Tarafa Wilayani humo kutekeleza majukumu yao ikiwemo kuwaelekeza wafugaji kufuata taratibu za kuonana na viongozi wa Vijiji husika, kufanya mikutano inayo wahusisha wananchi katika maamuzi ya kuwapokea wafugaji hao ili kuyaondoa maeneo yao katika migogoro ya aina hiyo.
“Kwavile mifugo ni muhimu kwetu na endapo itatumika vizuri na kwa kuzingatia kanuni, miongozo na maelekezo yanayotolewa na Serikali italeta manufaa kwa Wananchi wetu” alisema Dc, Nalicho na kuongeza kuwa mtindo wa kuishi kwa uhasama kati ya wafugaji na wakulima hauwezi kuwa na tija.
Awali akiongea katika ziara hiyo Afisa misitu wa Wilaya la Tunduru  Rashid Mtotela alimweleza Dc, Nalicho kuwa Wakulima na wafugaji hao walivamia msitu huo mwaka 2006 /2007 na kuendelea kujiimarisha kila mwaka baada ya kubaini kutokuwepo kwa vikwazo vyovyote kutoka Serikalini.
Alisema hifadhi hiyo ambayo awali ilikuwa imeunganishwa na Hifadhi ya Taifa (Selous) tangu mwaka 1974 na baadae kuunda hifadhi shirikishi mwaka 2007 kupitia mradi wa Jont participatory Forest Menegement (JPFM) liyounganisha Vijiji vya Nangunguru, Mkalekawana na Majala kila Kijiji kimekuwa kikikwepa majukumu yake ya kulinda hifadhi hiyo hali ambayo imechangia kuendelea kuhalibika kwa mazingira hayo.
Wakiongea kwaniaba ya Wananchi wa Vijiji hivyo Mwenyekiti wa Kijiji cha Nangunguru Bw.Said Rashid Mkwekwele, Mtendaji wa Kijiji hicho Zainabu Twaha na Afisa Tarafa wa Nampungu Joshua John wakawashushia lawama baadhi ya wakuu wa Idara katika halmashauri ya Wilaya hiyo kuwa umekuwa na kigugumizi katika ufuatiliaji na uchukuzi wa maamuzi juu ya migogoro hiyo.

DC NALICHO AWATIMUA WAVAMIZI MSITU WA SHAMBA LA BIBI

Na Steven Augustino, Tunduru
MWENYEKITI wa kamati ya Ulinzi ya Wilaya ya Tunduru, Mkuu wa Wilaya hiyo Mkoani Ruvuma Chande Nalicho ametoa wiki moja kwa Wakulima na Wafugaji wa jamii ya Kisukuma kuondoka katika eneo la hifadhi ya msitu wa Shamba la Bibi vinginevyo hatua kali za Kisheria zitachukuliwa dhidi yao.
Dc, Nalicho alitoa maagizo hayo baada ya kamati ya Ulinzi na Usalama ya Wilaya hiyo kufanya ziara ya kushtukiza katika msitu huo na kujionea hali halisi ya uhalibifu wa vyanzo vya maji, mabwawa na misitu iliyopo katika hifadhi hiyo inayo unganisha Vijiji vya Nangunguru, Majala na Mkalekawana katika Tarafa ya Nampungu kata ya Nandenbo Wilayani humo.
Alisema anatoa siku Saba kwa watu wote waliovamia msitu huo wa hifadhi kuondoka kwani haiwezekani watu waendelee kuishi wanavyo penda na kuharibu mazingira katika vyanzo vya maji na hifadhi ya misitu kana kwamba serikali haipo
Mkuu huyo aliwataka Watendaji Kata ,Vijiji kwa kushirikiana na Maafisa Tarafa Wilayani humo kutekeleza majukumu yao ikiwemo kuwaelekeza wafugaji kufuata taratibu za kuonana na viongozi wa Vijiji husika, kufanya mikutano inayo wahusisha wananchi katika maamuzi ya kuwapokea wafugaji hao ili kuyaondoa maeneo yao katika migogoro ya aina hiyo.
“Kwavile mifugo ni muhimu kwetu na endapo itatumika vizuri na kwa kuzingatia kanuni, miongozo na maelekezo yanayotolewa na Serikali italeta manufaa kwa Wananchi wetu” alisema Dc, Nalicho na kuongeza kuwa mtindo wa kuishi kwa uhasama kati ya wafugaji na wakulima hauwezi kuwa na tija.
Awali akiongea katika ziara hiyo Afisa misitu wa Wilaya la Tunduru  Rashid Mtotela alimweleza Dc, Nalicho kuwa Wakulima na wafugaji hao walivamia msitu huo mwaka 2006 /2007 na kuendelea kujiimarisha kila mwaka baada ya kubaini kutokuwepo kwa vikwazo vyovyote kutoka Serikalini.
Alisema hifadhi hiyo ambayo awali ilikuwa imeunganishwa na Hifadhi ya Taifa (Selous) tangu mwaka 1974 na baadae kuunda hifadhi shirikishi mwaka 2007 kupitia mradi wa Jont participatory Forest Menegement (JPFM) liyounganisha Vijiji vya Nangunguru, Mkalekawana na Majala kila Kijiji kimekuwa kikikwepa majukumu yake ya kulinda hifadhi hiyo hali ambayo imechangia kuendelea kuhalibika kwa mazingira hayo.
Wakiongea kwaniaba ya Wananchi wa Vijiji hivyo Mwenyekiti wa Kijiji cha Nangunguru Bw.Said Rashid Mkwekwele, Mtendaji wa Kijiji hicho Zainabu Twaha na Afisa Tarafa wa Nampungu Joshua John wakawashushia lawama baadhi ya wakuu wa Idara katika halmashauri ya Wilaya hiyo kuwa umekuwa na kigugumizi katika ufuatiliaji na uchukuzi wa maamuzi juu ya migogoro hiyo.

Friday, July 26, 2013

WAFANYABIASHARA SOKO KUU SONGEA WAPINGA MPANGO WA MANISPAA

Kulia ni Mwenyekiti wa Umoja wa Wafanyabiashara wa Masoko Manispaa ya Songea(UWABIMASO) Karim Matumla akiwa na Makamu Mwenyekiti wa Uwabimaso Leonard Chiunga wakifuatilia hoja mbalimbali kutoka kwa wanachama wa Uwabimaso
Wanachama wa Uwabimaso wakifuatilia kwa makini kikao hicho chenye lengo la kupinga ongezeko la kodi la Vibanda vya Soko Kuu na Kupinga tangazo la Zabuni lililotangazwa hivi karibuni


   
Na Stephano Mango, Songea
          
WAFANYABIASHARA katika Soko Kuu la Halmashauri ya Manispaa ya Songea Mkoani Ruvuma wamepinga ongezeko la pango kwa asilimia 100 na tangazo la Zabuni  la ukodishaji wa Vibanda hivyo lililotolewa na Halmashauri hiyo hivi karibuni
Akitoa maazimio ya kikao cha Umoja wa Wafanyabiashara Masoko ya Manispaa ya Songea(UWABIMASO) kilichofanyika jana mjini hapa  kwenye ukumbi wa Saccos ya Walimu Songea Vijijini Mwenyekiti wa Uwabimaso Karim Matumla alisema kuwa wafanyabiashara wamepinga kwa nguvu zote mpango wa kifisadi ulioletwa na viongozi wabovu wa  Halmashauri hiyo wa kuongeza kiwango cha kodi kwa asilimia 100 na tangazo la Zabuni
Matumla alisema kuwa mipango ya Halmashauri kuhusu Masoko yake haina ushirikishwaji wa pamoja kutoka pande zote mbili kwa maana Wafanyabiashara(Uwabimaso)  na Halmashauri hiyo hali inayosababisha migogoro mara kwa mara
Alisema kuwa kwa muda mfupi tumepokea barua mbili zenye malengo tofauti ndani ya kipindi cha mwezi mmoja jambo ambalo linaleta mashaka sana katika dhamira za viongozi wa Halmashauri hiyo yenye mipango dhalimu
Alisema kuwa kitendo cha Mkurugenzi kutoheshimu wala kutimiza makubaliano yetu yaliyomtaka kuondoa kero zinazowapata wafanyabiashara katika Masoko ya Halmashauri ni kitendo cha dharau kwa wafanyabiashara ambao wanachangia pato la Halmashauri
“ Tulimtaka Mkurugenzi katika vikao vyetu kuondoa mashimo na kuboresha mifereji na miundombinu mingine ndani ya Masoko, wauza matunda watafutiwe eneo maalumu la biashara yao kwani kwa sasa wanazuia mizigo kuingia ndani na wateja wanapata kero ya kuhudumiwa, unyanyasaji unaofanywa na Afisa Masoko uachwe na pia tulimuomba atukutanishe na Viongozi wa Halmashauri ili tutoe maoni yetu, lakini yeye amekaidi”alisema Matumla
Alisema kuwa mei 22 mwaka huu Halmashauri ilileta barua Uwabimaso ikitoa taarifa ya ongezeko la kodi ya pango kwa asilimia 80 kulingana na ukubwa wa chumba cha biashara kuanzia julai 1 mwaka huu, kabla hatujaanza kuitekeleza, julai 9 mwaka huu wanaleta barua na wanatangaza Zabuni ya ukodishaji wa vibanda hivyo, baada ya Uwabimaso kupinga ongezeko la pango la asilimia 80
Alieleza kuwa kumekuwepo na mgongano wa kimaagizo kutoka katika Ofisi ya Mkurugenzi wa Halmashauri hiyo kitendo ambacho kinaibua maswali mengi, hivyo Uwabimaso imeamua kwenda kwa Mwanasheria ili aweke zuio la mpango wa upandishaji wa Kodi na Utangazaji wa Zabuni yenye lengo la kuwaondoa wafanyabiashara wote wa maduka katika soko hilo
Akizungumza na gazeti hili kwa njia ya simu Mkurugenzi wa Halmashauri hiyo Zakaria Nachoa alisema kuwa Halmashauri imekusudia kuongeza mapato yake kupitia miradi yake, hivyo mfanyabiashara ambaye hataki kuendana na utaratibu aache kibanda ili mfanyabiashara mwingine achukue
MWISHO

Saturday, July 6, 2013

AMINA CHIFUPA HUYU HAPA, AWASUMBUA VIJANA



             AMINA CHIFUPA AKIWA KATIKA POZI ENZI ZA UHAI WAKE

Na; Stephano Mango, Songea

JUNI 26 mwaka 2007 Tanzania hususani jamii ya vijana ilikumbwa na msiba mzito wa kuondokewa na Mwanaharakati wa Vijana,mpendwa wetu Amina Chifupa Mpakanjia.

Hadi anafariki dunia baada ya kuugua kwa muda mfupi katika hospitari ya Jeshi la wananchi wa Tanzania (JWTZ) ya Lugalo alikokuwa amelazwa akiugua homa kali na kisukali alikuwa ni Mbunge wa Viti Maalumu kupitia tiketi ya Umoja wa Vijana wa Chama cha Mapinduzi(UV-CCM)

Amina Chifupa amefariki akiwa na umri wa miaka 26 ya kuzaliwa kwake, tarehe aliyofariki ni siku ya upingaji wa madawa ya kulevya Dunia ambayo yeye ndie alikuwa miongoni mwa Vijana ambao wanapinga matumizi ya madawa hayo

Kimsingi msiba ule ulikuwa ni pigo kubwa sana kwa wanajamii wote na hasa vijana tulio katika mapambano ya kukabiliana na changamoto mbalimbali zinazotukabili katika maisha yetu.

Mazishi ya mwanadada huyo chipukizi na jasiri katika kuwakomboa Vijana na makundi mengine yaliyopembezoni yalifanyika katika kijiji cha Lupembe,wilayani Njombe katika mkoa wa Iringa zamani.

Katika maombolezo ya Mbunge huyo ilithibitika pasipo na shaka hata chembe kwamba alikuwa anakubalika na watu wengi na ni mtu wa watu ,na kwa kweli ujasiri aliouonyesha katika kipindi kifupi alichofanya kazi akiwa Mbunge,kilithibitisha kuwa jamii ilimkubali.

Pamoja na umri wake mdogo (26) akiwa Mbunge wa Viti Maalum na aliyekaa Bungeni kwa kipindi cha miezi kumi na nane (18),habari za msiba wake na namna watu walivyouomboleza ni mambo yaliyoonyesha dhahiri njia bora inayowafaa wabunge na viongozi wetu kutimiza wajibu wao

Kujitokeza kwa watu wenye hadhi ya juu kabisa kitaifa na kimataifa katika mazishi yake na wingi wa wananchi wa kada mbalimbali nyumbani kwa baba yake Mikocheni na huko Njombe ambako yalifanyika mazishi yake, ni ushahidi unatuonesha kuwa dada huyu alikuwa mpiganaji wa kweli katika mambo mazito ambapo kifo chake kilipaswa kuguswa na wengi hususani vijana.

Ingawa imekuwa ni desturi kwetu kuwaenzi watu waliokufa hata wakati mwingine kwa wale ambao hawastahili sifa tunazowapa, lakini kwa Amina hali hiyo ni tofauti kabisa, kwani kila sifa ambayo amekuwa akipewa imekuwa ni sehemu ya mambo ya msingi aliyoyafanya na wananchi wakasikia au kushuhudia kwa macho yao

Hakika kifo cha Amina Chifupa kiliibua mambo mengi sana , wapo waliohusisha kifo chake na siasa kwa kuwa alitamani kuwa kiongozi wa juu katika umoja wa vijana wa chama cha mapinduzi (UV-CCM).

Wapo waliofananisha kifo chake na cha Horace Kolimba ambaye alikuwa Katibu Mkuu wa CCM ambapo aliwaambia wenzake waziwazi kuwa “CCM haina dira wala mwelekeo” lakini hawakumwelewa, na wakamwita Dodoma ajieleze kwenye kikao maalumu, alipowapatia maelezo, ghafla tukasikia Kolimba amefariki dunia.

Wengine walithubutu kukifananisha kifo cha Amina Chifupa na cha Ipyana Malecele ambaye alikuwa ni mtoto wa kiongozi na Mbunge mkongwe hapa nchini John Malecele.

Ingawa mzee Malecele na mwenzake Hamis Chifupa walikana waziwazi kuwatuhumu Binadamu wenzetu kwamba ndio waliofanya vitendo vya kigaidi na kijasusi na kusababisha vifo kwa vijana hao

Ni katika mazingira tofauti walitoa kauli zao na kuwaasa watanzania waamini kuwa vifo hivyo vilitokana na mipango ya Mungu na kuwaomba watanzania wasihusishe vifo vya watoto wao na harakati za kisiasa.

Hata hivyo wapo waliohusisha kifo hicho na harakati zake za kupinga na kutaka kuwataja hadharani wauzaji na vigogo wa madawa ya kulevya hapa nchini, ndiyo maana wakasema kwa kuwa alihaidi kuwataja vigogo hao siku ya kupiga vita dawa za kulevya Duniani ambapo kimsingi inaadhimishwa Duniani kote Juni 26 ndiyo maana wakawahi kumwondoa mapema kabla hajasema kitu siku husika.

Lakini kuna baadhi ya watu wamefananisha kifo chake na cha Princess Diana wa Uingereza. Kwa sababu Diana alikufa katika umri mdogo wa miaka 36 na alipendwa na watu wengi na wenye nyadhifa mbalimbali

Diana na Amina maisha yao yalikatishwa ghafla na kuwaacha watu wakiwahitaji katika kuchangia maendeleo katika jamii zao na kutufanya tudondoshe machozi katika kuwaomboleza.

Hata hivyo watanzania wasingeweza kufanya makosa pale wanafananisha kifo cha Amina na cha Ipyana, kijana mdogo ambaye kama alivyokuwa Amina alikuwa ameanza harakati za kuwania uongozi wa juu ndani ya UVCCM, wote wawili walikutwa na janga na baadaye walipotea katika mazingira yenye utata na kigugumizi wakiwa wanahitajika katika harakati husika.

Lakini kimsingi katika kumkumbuka Amina chifupa tunapaswa kutambua kuwa kila nafsi katika ulimwengu huu itaonja mauti, ingawa kila mja kabla hajaumbwa, mwenyezi mungu alimjua na kumtaka atimize wajibu wake kama kiumbe hai.
Natambua na kuamini kila mtu ana sababu zake za kuumbwa na kuwekwa katika ulimwengu na ana wajibu stahiki ambao amelazimika kuja kuutimiza hapa Duniani.

Hii haimaanishi kila mmoja wetu kutimiza wajibu wake kikamilifu, ingawa wajibu huo tumepewa na muumba wetu kuja kuutimiza kwa kutumia utashi wetu ulio kamilifu.

Kwa muda mfupi alioishi Amina Chifupa alipokuwa Bungeni amedhihirisha jinsi alivyotimiza wajibu wake, ameweza kuwa chachu kwa kuibua mambo mazito ambayo yalitoa cheche kali na kuzua mijadala mikali ndani na nje ya Bunge la tisa.

Akiwa kijana mtanzania na kwa kuzingatia majukumu yake aliweza kutimiza wajibu wake ipasavyo kama Mbunge na Mwakilishi wa Vijana, ni ukweli uliowazi kuwa tunapaswa kuziendeleza juhudi alizoziacha .

Naamini alipokuwa Bungeni hoja alizoibua na jinsi zilivyokuwa na hamasa na kuweza kufufua matumaini ya wengi na kukuza hadhi ya vijana wenye nia ya dhati katika kupigania nchi yao , ndiyo kilichonifanya niendelee kumkumbuka na kumuenzi daima leo akiwa ametimiza miaka 6 toka atutoke

Hicho ndicho haswa kilichofanya kifo chake kumshtua kila mtu bila kujali rika awe aliyekuwa anamfahamu vizuri marehemu aula. Kwa sababu ni miongoni mwa waheshimiwa waliokuwa na nia thabiti ya kurejesha hadhi ya Bunge na kufanya litimize wajibu wake.

Kwani alitambua kuwa cheo ni dhamana na kwamba uheshimiwa aliopewa ulikuwa unamaanisha utumishi kwa wananchi na kuzingatia kundi alilopaswa kulitumikia kikamilifu ambalo ndilo lililompa dhamana (Vijana).

Kwa nguvu zake zote aliamua kutoa mchango wake ili kuwezesha vita dhidi ya madawa ya kulevya ishinde, kwa kuwa madawa ya kulevya yanaangamiza vijana wengi wa nchi hii ambao yeye alikuwa na wajibu wa moja kwa moja wa kuwatetea.

Sina hakika kama kuna mtanzania mwenye akili timamu anaweza kubisha kwamba Amina Chifupa alikuwa nuru ya matumaini kwa vijana na harakati zetu za kujiletea maendeleo.

Ni ukweli kuwa Taifa lolote Duniani haliwezi kuwa imara kiuchumi ,kisiasa, kiutamaduni na kijamii katika mapambano dhidi ya umaskini, ujinga na maradhi bila kundi kubwa la vijana kulitengenezea mazingara ya kujikomboa.

Katika ulimwengu asilimia kubwa ni vijana na ndio viongozi wa leo na kesho na nguvu yao inategemewa sana katika jamii zetu.

Ndio maana mwanaharakati wa Vijana marehemu Amina Chifupa alijikita zaidi katika kutukomboa katika changamoto mbalimbali zinazotukabili ili atuoneshe njia stahiki na katika ustawi imara.

Hakuna ubishi kuwa Vijana ndio tumaini pekee la Taifa letu, kwaniTaifa lisilokuwa na vijana wazalendo na walio tayari kutetea taifa lao kwa gharama yoyote. basi nashawishika kuamini taifa hilo limepoteza mwelekeo (dira) na lipo hatarini.

Katika harakati za kuwakomboa Vijana na kupinga maovu naamini Amina Chifupa amekufa kifo cha kishujaa na ametutangulia mbele ya haki baada ya kutimiza baadhi ya wajibu wake
Mashujaa wapo wengi ambao wameshafariki ila kimsingi kila shujaa ameondoka akiwa na sifa zilizomfanya atambulike na aheshimike katika jamii iliyokuwa inamzunguka.

Mara nyingi shujaa hufikia hatua hiyo kutokana na ujasiri wake, uwezo wa kufikiri, kubuni,busara na pengine kujitoa kafara katika kuokoa watu wengine ambao kimsingi wamepotea

Ushujaa haupatikani kirahisi, mara nyingi mtu ambaye anaveshwa cheo cha ushujaa ni lazima akumbwe na vizingiti vingi (Maadui)ili afikie lengo husika la ukombozi na zawadi

Mwanaharakati Amina Chifupa alipata mapito magumu sana kimaisha katika safari yake hapa duniani na uwanaharakati wake kiujumla..Ingawa kifo chake kimeacha gumzo kubwa katika fikra za vijana.

Mwanaharakati huyu alikuwa tayari kufa akiongozwa na nanga ya kijasiri ya kusema ukweli na uwekaji wa mambo mengi bayana kwa kuipenda nchi yake na hasa jamii ya Vijana kwa kuyavalia njuga mambo mazito ambayo kimsingi yanaharibu maisha ya vijana.

Alitumia muda mfupi ndani ya Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kuonyesha uwezo na ujasiri mkubwa, kuwa Vijana wa leo wakipewa majukumu mazito wanaweza kufanya vizuri na wanastahili kupata dhamana hiyo.

Ni dhahiri kuwa Amina ni shujaa kwa kuwa kifo chake ni kielelezo kwa Vijana kuwa wakati wote tupo tayari kufa kwa ajili ya kutetea nchi yetu na kupambana na ufisadi ambao unalenga kuipeleka nchi mahali pabaya na kuharibu malengo ya vijana na Taifa kiujumla

Ni wazi kuwa katika harakati za Amina Chifupa za kusema na kudhamiria kufichua maovu alikuwa akizungukwa na maadui wa ndani na nje na pengine wengi ni wale wa nchi za nje ambao nia yao kuitumia nchi hii kama dampo la kuzalisha vijana matahira kutokana na Dawa za kulevya.

Maadui hao nia yao ni kuhakikisha kizazi chote cha Vijana kama Amina Chifupa kinaathirika na dawa za kulevya ili nchi hii iweze kutawaliwa kirahisi baada ya kuziharibu bongo zote za Vijana makini na wasomi ambao wanashawishika kutumia dawa za kulevya.

Jambo muhimu kwa sasa ni wajibu wa kuiga na kuendeleza mapambano dhidi ya dhuruma na masuala yote aliyopigania Mwanasiasa huyu, viongozi wetu wanao wajibu wa kutumia fikra za Amina kwa kuwa bado zinaishi kusahihisha makosa wanayofanya ambayo wamekuwa wakiambiwa mara kadhaa na makundi mbalimbali ya jamii lakini kwa makusudi wanayapuuza.

Uwakilishi wa Amina Chifupa haukuishia kuchangia mijadala Bungeni tu, bali tulimsikia na kumwona akifanya shughuli nyingine mbalimbali za kijamii,kwani aliwatembelea vijana na watoto wenye matatizo mbalimbali na kuwafariji na kuwapa misaada mbalimbali

Hivyo Vijana ndio tunatakiwa kuwa mstari wa mbele kwa kumuenzi Amina Chifupa na kuhakikisha kuwa Nchi hii haiendi mrama, ni vyema tukadhihirisha kumuenzi Amina Chifupa kwa vitendo vyetu, kwa kuwa tumeachiwa changamoto nyingi tunapaswa kuzitatua na kuweka mambo sawa katika harakati zetu za kujikomboa

Pamoja na kumkumbuka Amina ni vyema Vijana na wanajamii tukajiuliza tumejifunza nini kutoka kwake? Nani mtetezi wa Vijana aliyebaki Bungeni? Ni Zitto Kabwe, Dk Emmanuel Nchimbi , Deo Filikunjombe, Livingston Lusinde, Joshua Nassari, John Mnyika, Ester Bulaya au Waziri Mwenye dhamana ya Vijana?

Ni kweli kuwa Amina Chifupa hatunae tena katika ulimwengu huu, amefariki dunia, amelala na hatutamwona tena katika maisha haya ,lakini kauli na fikra zake zipo na zitaishi milele na itakuwa pumzi katika kizazi hiki na kijacho.

Amina tunakukumbuka na kukuenzi kwa yale yote uliyotuachia na tutashirikiana vyema na Mzee Hamis Chifupa kutoa mchango wetu katika taasisi yako ya Amina Chifupa Foundation ambayo ipo chini ya Mkurungezi Mzee Hamis Chifupa na ni jambo jema kuwa taasisi yako tayari imesajiriwa na Serikali na enaendelea kutimiza wajibu wake wa kusajiriwa

Kama mwenyezi mungu alivyotoa ndivyo alivyotwaa, Vijana sote tulikupenda na tutaendeleza juhudi zako ulizoziacha , sisi kama waja hatuna budi kumshukuru kwa kila jambo Mwenyezi mungu atupe faraja na busara katika kukabiliana na changamoto zinazotukabili watanzania wote.

Mheshimiwa Amina Chifupa uiombee nchi yako ili mafisadi wasiendele kuwaua kila kukicha eti kwa sababu za harakati ambazo wewe uliziasisi na watanzania wengine wasio na hatia ambao wanakosa Raslimali stahiki kwa sababu mafisadi wamezimaliza maliasili hizo kwa kuibia. Tunatambua kuwa wewe mbele sisi nyuma. Mungu Baba aipumzishe Roho yako katika mahali pa faraja na amani , Ameni.

Mwandishi wa Makala hii

Anapatikana kwenye, www.stephanomango.blogspot.com

Simu namba,0755 -0715 -0784 ,33 50 51

Friday, July 5, 2013

LOWASSA ADAIWA KUCHEZA KALATA VIZURI KASHFA YA RISHMOND


Aliyekuwa kuwa Waziro Mkuu, Edward Lowassa akiteta jambo na aliyekuwa Spika wa Bunge la Tisa Samwel Sitta



WAZIRI Mkuu aliyejihudhuru Edward Lowassa mwaka 2006 kwa tuhuma za ufisadi kupitia kampuni ya kufua umeme Richmoind, sasa imebainika kuwa alitolewa mbuzi wa kafara baada ya mitambo hiyo kuzinduliwa na Rais wa Marekani Barck Obama ikiwa na jina la Symbion.


Kwanza waliosuka mpango wa kumchafua Lowassa walisema Richmond ni Kampuni ya mfukoni, na ni ya Lowassa, haina uwezo wa kuzalisha Umeme wala kufunga balbu.

Wakasema Dowans ni pacha na Richmond, Wapambe wachache wakasema Serikali isinunue Mitambo hiyo maana haifai, sasa ni Simbyon Power.

Mitambo hiyo hiyo ndiyo imezinduliwa juzi na Obama, je?amezindua mitambo mibovu isio na uwezo wa kuzalisha Umeme wala kufunga balbu? je Obama naye ni fisadi? au kwasababu akina fulani wakisema ndimi zao zinaaminika zaidi ya wengine?

Wachambuzi wa masuala ya siasa wanasema kuwa Lowassa alikuwa anaona mbali sana na alikuwa sahihi, ila alihujumiwa kisiasa tu na wasioitakia Nchi yetu mema bali kwa maslahi yao maana mitambo hiyo wakati inazinduliwa mpaka Rais Jakaya Kikwete na vionmgozi wengine wa nchi walionekana wakipiga makofi!

Thursday, July 4, 2013

MAMBO 10 YA MUHTASARI WA ZIARA YA RAIS OBAMA BARANI AFRIKA


Ametusemea Waafrika wote. Hasa katika swala la kujenga viwanda hapa hapa Afrika ambavyo vitatoa ajira kwa vijana wetu. Africa tusikubali kudanganywa kwa kuuza malighafi kwenda nje na kuhamishia ajira nchi za nje.

Amekemea sana swala la uongozi mbaya, rushwa, upendeleo katika swala la ajira kuwa vinakwamisha maendeleo Afrika.

Yeye na Rais wa Afrika Kusini, wamezungumzia swala la ICC na Afrika. Walisema kama Afrika inafikira kuwa ICC inaionea, ni bora Afrika izungumze na ICC. Lakini Rais Obama alitoa angalizo kwa viongozi wa Afrika kwa makini na madai yao ndani ya ICC.

Hapa Afrika kusini, alizungumzia swala la uchafuzi wa anga na hatua ambazo Marekani inachukuwa kupungaza hatari hiyo. Pia alielezea hatua ambazo China, India na Japan wanachukuwa. Alishauri kila mtu, watu na nchi wote tuhusike na swala hii la uchafuzi wa anga na maeneo tunayo ishi.

Alizungumzia, idadi ya wanafunzi darasani. Alisikitika kusikia kuwa darasa moja Afrika lina wanafuzi 90, ambapo Marekani dalasa moja lina wanafunzi 25 hadi 35 ambao bado waonaona ni wengi. Alishauri kuwepo utalaamu wa kisasa wa kufundishia darasa vikundi vikundi.

Aliwapa changamoto vijana wote wa Afrika ya kusoma sana hasa masomo ya hesabu na ufundi, kuwa tayari kwa ajira za viwandani. Aliahidi kuwapa msaada wa elimu kwa swala hili.

Aliwaambia vijana kuwa tayari kuwania nafasi za juu serikalini na kuwajibisha serekali zao kwa njia za amani.

Alikanusha uvumi uliopo kuwa anataka kuweka kituo cha Jeshi Africa. Pia safari ya Afrika hakusababishwa na uhusiano wa China-Afrika.
Amesema Afrika itajengwa na Waafrika kwa faida ya Afrika wote, ila wao wako tayari kuchangia mawazo, utalaamu na soko.

Aliwajibu Wakenya kuwa ahadi ya kuwatembelea bado ipo pale pale, maana bado ana miaka 3 na miezi 6 ofisini.

Ahsante.

Samuel G Mossama

Pretoria

+27 782 372 288