About


Karibu ujiunge na chuo cha kisasa cha Easy Tech.Computer kwa mafanikio yako,Walimu waliobobea katika fani hiyo wanapatikana chuoni hapo

elimak

elimak

Pages - Menu

Thursday, October 27, 2011

WANANCHI WAENDELEA KUMPOKEA KWA SHANGWE MBUNGE STELLA MANYANYA NA MKUU WA MKOA WA RUKWA KATIKA ZIARA YAKE YA KIKAZI MKOANI RUVUMA

Mbunge Mhandisi Sella Manyanya wa kwanza kulia akipiga ngoma ya Beta baada ya kufurahia mapokezi mazuri katika ziara yake,wa kwanza kushoto ni Katibu wa Mkuu wa Mkoa wa Rukwa Frank Maten akishuhudia mapokezi hayo

Mhandisi Stella Manyanya ambaye ni Mkuu wa Mkoa wa Rukwa na Mbunge wa Viti Maalumu Mkoa wa Ruvuma akimpatia Katibu wa UWT Wilaya ya Songea Mjini shillingi laki mbili kwa ajili ya mahitaji madogo madogo ya ofisi ya UWT Wilaya ya Songea Mjini,baada ya kupokea ripoti ya utekelezaji kwa kipindi cha mwaka 2011, katikati ni Katibu wa UWT Mkoa wa Ruvuma Mariam Yusuph

Viongozi wa Chama na Serikali wakifanya maombi kwenye kabuli la Nduna Songea Mbano

Mjukuu wa Nduna Songea Mbano,Aidan Mbano akizungumza na Wazee Mashujaa 66 waliozikwa kwenye kabuli la pamoja ikiwa ni dua maalum kwa Mbunge na Mkuu wa Mkoa wa Rukwa na Mwenyekiti wa Kamati ya Ushauri wa Makumbusho ya Taifa ya Majimaji Songea Mhandisi Stella Manyanya alipotembelea Makumbusho hayo ili kupata baraka za Wazee hao ikiwa ni desturi yake kabla ya kuanza ziara zake mkoani Ruvuma

Viongozi mbalimbali wa chama na Serikali wakimkaribisha Mbunge na Mkuu wa Mkoa wa Rukwa Mhandisi Stella Manyanya kwenye viwanja vya mkutano vya Makumbusho ya Taifa ya Majimaji Songea

Mama wa Kimasai akimpatia zawadi za kabila hilo Mbunge Mhandisi
Stella Manyanya baada ya kuwahutubia wananchi wa Songea Mjini katika viwanja vya Makumbusho ya Taifa ya Majimaji
Viongozi wa chama wa Wilaya ya Namtumbo wakimpokea Mbunge Mhandisi Stella Manyanya

MAKANISA NDUGU KUFANYA TAMASHA LA UIMBAJI MIAKA 50 YA UHURU WA TANZANIA


                    Mhashamu Askofu Mkuu Norbert Mtega
Na Gideon Mwakanosya,Songea
WAUMINI wa Makanisa ndugu katika Halmashauri ya Manispaa ya Songea Mkoani  Ruvuma wanatarajia kufanya tamasha kubwa la uimbaji  la Jubilei  ya miaka 50 ya uhuru wa Taifa la Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Oktoba 29 Mwaka huu ambapo mgeni rasmi kwenye tamasha hilo ni Waziri wa Habari utamaduni na michezo Dr. Emmanuel  Nchimbi.
Akizungumza na mtandao wa www.stephanomango.blogspot.com  jana ofisini kwake Katibu wa umoja wa Makanisa ndugu katika Halmashauri ya Manispaa ya Songea Mackie Mguhi amesema kuwa tamasha hilo ambalo linatarajiwa kuhuzuliwa na mamia ya waumini wa Makanisa ndugu wakiwemo Askofu Mkuu wa Kanisa katoliki jimbo kuu la Songea Norbert Mtega, Askofu wa dayosisi wa Ruvuma kanisa la Angelikana  Dr. Martenius Kapinga, Mkuu wa kanisa la kiinjili la kiliteli Tanzania (KKKT) Mchungaji Nashoni kikalawa Pamoja na mkuu wa mkoa wa Ruvuma Saidi Mwambungu 
Mguhi ameyataja Makanisa yanayeunda umoja huo ambao umeandaa tamasha kubwa ni kanisa katoliki Parokia za Songea,Mjimwema na Bombambili kanisa la kinjili la kiluteli Tanzania (KKKT) Usharika na Songea mjini na Msamala kanisa la Anglikana Songea Mjini pamoja na kanisa la Moraviani Tanzania ushirika wa Songea.
Ameeleza zaidi kuwa Tamasha hilo litafanyika siku ya jumamosi oktoba 29 mwaka huu katika uwanja wa michezo wa mpira wa miguu wa Majimaji ambalo litatanguliwa na maandamano makubwa  ya waumini wa Makanisa ndugu yatakayoanzia katika kanisa la Luthelani Songea Mjini hadi uwanja wa Majimaji.
Amesema kuwa lengo la tamasha hilo ni kuonyesha furaha kubwa kwa waumini wa Makanisa ndugu katika manispaa ya Songea kwa jubilee ya nchi ya Tanzania Kwa vitendo pili kuendelea kumshukuru mungu na kumuomba kwa upendo ,Amani na uvumilivu aliyo ijalia nchi ya Tanzania pamoja na viongozi  na wananchi kwa ujumla .
Amebainisha zaidi kuwa  katika tamasha hilo pia litaudhuliwa na wanafunzi wa chuo cha elimu ya Taifa Songea , Shule ya wasichana na Wavulana Songea na kwaya zaidi ya ishirini zimesibitisha kushiriki kwenye tamasha hili na viongozi wa makanisa hayo wanatarajiwa kuongoza ibada ya maalumu ya kuiombea amani kwa mwenyezi mungu kwani  Tanzania toka ipate uhuru hawajawai kupata misuko suko ya aina yoyote tofauti  na nchi zingine zikiwemo baadhi ya nchi zilizo pakana na Tanzania ambazo wananchi wake wakipata shida kutokana na vita.