About


Karibu ujiunge na chuo cha kisasa cha Easy Tech.Computer kwa mafanikio yako,Walimu waliobobea katika fani hiyo wanapatikana chuoni hapo

elimak

elimak

Pages - Menu

Thursday, November 3, 2011

KOICA KUISAIDIA WILAYA YA TUNDURU MKOANI RUVUMA WALIMU WA SAYANSI

                    Mkuu wa Wilaya ya Tunduru Juma Solomon Madaha
Na, Augustino Chndiye Tunduru

JUMUIYA ya watu wa Korea (KOICA) imeahidi kutoa msaada wenye jumla ya Walimu sita (6) ili wasaidie kufundisha Masomo ya sayansi katika Shule Tano kati ya Shule 20 za Sekondari zilizopo Wilayani Tunduru Mkoani Ruvuma.

Hayo yamesemwa na Meneja wa Jumuiya hiyo Hwng Jin Hee katika hafla fupi ya kukabidhi Mwalimu Mmoja kati ya walimu hao iliyofanyika katika ofisi za Afisa Elimu wa Shule za Sekondari wa Wilayani humo kwa maelekezo kuwa Mwalimu huyo  Lee Hyoo Kyung ataanza mara moja kufundisha katika Shule ya Tunduru Sekondari.

Jin Hee alisema kuwa KOICA imepokea kilio cha ukosefu wa walimu wa masomo ya Sayansi kwa vitendo ambapo kwa kuanzia wamemleta mwl. Hyoo Kyung na baada ya muda mfupi ujao watawaleta walimu wengine wanne ambao wamepangwa kufundisha katika shule za Sekondari Mataka, Masonya,FrenkWeston, Nandembo na Mbesa zilizopo wilayani humo.

Alisema nia ya nchi yake ni kusaidia Tanzani Walimu wengi zaidi wa Masomo ya Sayansi ambao wameonekana kuwa na upungufu mkubwa hapa nchini na kwamba hadi sasa KOREA imekwisha leta jumla ya Walimu 100 kupitia Shirika hilo na wanaendelea kutoa huduma hiyo katika maeneo mbalimbali ya Tanzani.
 
 Akizungumzia msaada huo  Afisa elimu Shule za Sekondari wa Wilaya ya Tunduru Alli Mtamila alisema kuwa msaada huo umefika kwa wakati na kwamba idara yake inaamini kuwa Walimu hao watawasaidia wanafunzi wa Shule hizo kuwainua kitaaluma.

Mwl. Mtamila aliendelea kueleza kuwa wakati hayo yakiendelea takwimu zinaonesha kuwa idara yake inakabiliwa na upungufu wa walimu 158 kati ya walimu 289 wanaohitajika kufundisha katika Shule hizo huku takwimu hizo zikionesha kuwa walimu waliopo ni 164 tu.

TANI 7000 ZA KOROSHO KUNUNULIWA MSIMU WA 2011/2012 WILAYANI TUNDURU

Na Augustino Chindiye ,Tunduru
JUMLA  ya Tani 7000 za Korosho kutoka kwa  Wakulima wa Wilayani Tunduru zimepangwa kununuliwa na Chama kikuu cha Ushirika cha wakulima wa Wilaya hiyo (TAMCU) katika msimu wa Mwaka 2011/2012.

Hayo yamesemwa na Meneja Mkuu wa chama hicho Imani Kalembo na kuongeza kuwa ununuzi huo utaanza kufanyika Novemba 10 mwaka huu baada ya kukamirika kwa taratibu za mkopo wa Shilingi Bilioni 5.986 kutoka Benki ya CRDB.

Kalembo aliendelea kufafanua kuwa katika msimu huu ambao chama hicho kinaendelea kununua kupitia mfumo wa Stakabadhi Gharani mkulima atalipawa mkononi Shilingi 850/= kwa kila kilo atakayoiuza na baada ya Korosho hizo kuuzwa na chama hicho mkulima atapatiwa fedha zake zilizo bakia ambazo ni  Tsh.350/= na kufanya jumla ya Tsh.1200/=  ambayo ndiyo bei ya soko kwa kila kilo moja ya zao hilo katika msimu huu.

Kalembo aliendelea kueleza kuwa kufuatia hali hiyo kwa kuanzia Chama hicho kimekwisha leta Shehena ya magunia 72,300 zenye thamani ya zaidi ya Shilingi Milioni 300  zenye  uwezo wa kununulia wastani wa Tani 6000. 

Alisema katika kuhakikisha kuwa mpango huo unafanikiwa na kuhakikisha kuwa korosho zote zinauzwa ndani ya Wilaya hiyo na kuiwezesha halmashauri yao kukusanya Ushuru wake TAMCU imeandaa mitego na mikakati mbalimbali ya kuwanasa walanguzi ambao hununua Korosho hizo kwa kutumia vipimo visivyo kuwa halali maalufu kwa jina la Kangomba.

Meneja huyo alibainisha baadhi ya mikakati hiyo kuwa ni pamoja na kuunda vikosi kazi vinavyo shirikiana na viongozi na waandishi wa Vyama vya Msingi (AMCOs LTD) pamoja na kupeleka fedha na kuanza kununulia Korosho zilizopo katika vyama vya msingi vya Namitili na Mtetesi mpakani mwa Wilaya za Tunduru Mkoani Ruvuma na Wilaya ya Nanyumbu Mkoani Mtwara zikiwa ni mbinu za kuwadhibiti walanguzi hao na kwamba atakaye kwepa katika maeneo hayo na kukamatwa wakati wa mauzo ya Korosho hizo atanyang`anywa korosho zote bila malipo.

Nae Mwenyekiti wa Chama hicho Wilaya ya Tunduru Mahamudu Katomondo akizungumzia ucheleweshwaji wa zoezi la kuanza kununua Korosho hizo kutoka kwa wakulima ikiwa ni zaidi ya mwezi mmoja toka Bodi ya Korosho Tanzania itangaze kufunguliwa kwa msimu kuanzia Oktoba 1 mwaka huu alisema kuwa hali hiyo ilitokana na kuchelewa kuiva kwa Korosho za wakulima wa Wilaya hiyo.
Mwisho