About


Karibu ujiunge na chuo cha kisasa cha Easy Tech.Computer kwa mafanikio yako,Walimu waliobobea katika fani hiyo wanapatikana chuoni hapo

elimak

elimak

Pages - Menu

Monday, June 4, 2012

ISPEKTA CHACHA AHIMIZA USAWA WA KIJINSI KWA MAENDELEO ENDELEVU

Na Stephano Mango, Songea
WANANCHI wametakiwa kuheshimu usawa wa kijinsia katika mchakato mzima wa kuleta mabadiliko ya kijamii ,kiuchumi, kisiasa na kiutamaduni ili kuleta maendeleo endelevu katika jamii zetu kwa kuzingatia uangalifu wa kisheria
Wito huo umetolewa leo na makamu Mwenyekiti wa Mtandao wa Polisi Wanawake Mkoani Ruvuma Ispekta Fadhira Chacha wakati akitoa mada kwenye mdahalo wa wazi ya Usawa wa Kijinsia kwa Maendeleo uliofanyika Kata ya Magagura Jimbo la Peramiho, Wilaya ya Songea ulioitishwa na Mtandao wa Asasi za Kiraia Wilaya ya Songea(Sonngo) kwa ufadhiri wa The Foundation For Civil Society
Ispekta Chacha alisema kuwa wanawake na wanaume ni mawakala wakuu wa maendeleo na sio wapokeaji wa maendeleo na mabadiliko ambayo yanaiwezesha jamii kuweza kupata mahitaji yake na kuboresha maisha kwa kuzingatia mgawanyo sawa wa rasilimali
Alisema kuwa ili kuleta maendeleo uchambuzi wa mahitaji ya wake kwa waume waweza kufanyika kwa uwepo majadiliano,kuthubutu,kutoa mrejesho,kulinganisha na kuchanganua ni vitu vipi vinavyotakiwa ili kuleta maendeleo sawa
Kwa upande wake Katibu wa Sonngo Mathew Ngarimanayo alieleza kwenye mdahalo huo kuwa vitendo vya ukatili vinavyoendelea kuathiri maisha ya watu wengi katika jamii zetu jambo ambalo husababisha madhara kimwili na kiakili
Ngarimanayo alisema kuwa ukatili wa kijinsia hudumaza maendeleo kwani waathirika hushindwa kufanya majukumu yao,kupoteza fedha,muda katika kutibu majeraha,ongezeko la walemavu na kutoweka kwa upendo
Awali akieleza maudhui ya mdahalo huo Mwenyekiti wa Sonngo Siwajibu Gama alisema kuwa lengo kubwa ni kuelimishana,kuhabarishana na kujengana uwezo wa kujiletea maendeleo kwa kuzingatia usawa wa kijinsia, hivyo elimu hiyo inapaswa iwe mbegu ya kuleta mbegu ambayo itazaa matunda stahiki katika jamii
MWISHO

NAPE NNAUYE AFANYA MAKAMUZI MAKUBWA KATIKA UWANJA WA MAJIMAJI JANA



Msafara wa pikipiki ukiongoza msafara wa  Nape kwenda Uwanja wa Maji Maji ambako alizungumza mambo mbalimbali yenye kuleta mustakabali mzuri wa CCM na Serikali.
Nape akishiriki kucheza ngoma baada ya kuwasili Uwanja wa MajiMaji .
Nape akisalimiana na wakazi wa mji wa Songea waliojitokeza katika viwanja vya majimaji kuja kumsikiliza katika mkutano wa hadhara pindi alipokuwa akiiingia kiwanjani.

Nape akipita kwenye kanga zilizotandikwa na kina mama waliovutiwa na hotuba yake



Nape akiagana na wananchi wa Songea waliojitokeza kwa wingi katika uwanja wa majimaji kuja kumsikiliza.
Nape akisisitiza jambo alipokuwa akihutubia mamia ya wakazi wa songea walipojitokeza kuja kumsikiliza katika uwanja wa majimaji.