About


Karibu ujiunge na chuo cha kisasa cha Easy Tech.Computer kwa mafanikio yako,Walimu waliobobea katika fani hiyo wanapatikana chuoni hapo

elimak

elimak

Pages - Menu

Tuesday, November 22, 2011

USHIRIKI WAKO KATIKA SIKU 16 ZA KUPINGA UKATILI WA KIJINSIA KANDA YA KUSINI NI NGUZO MUHIMU KUIMARISHA TANZANIA HURU

 Mmiliki wa mtandao wa www.stephanomango.blogspot.com, Ndugu Stephano T.Mango anaungana na wanaharakati wengine nchini na nje ya nchi akiwemo Dada yangu Yasinta Ngonyani na Mzee Mbelle kwenye maandalizi ya kuadhimisha siku hizo 16 na kwa wale wote ambao kwa sababu zilizo nje ya uwezo wao wameshindwa kushiriki siku hizo,Nawapa Pole na tuzidi kuombeana kwani naamini walipenda kushiriki lakini wasihofu naomba waniruhusu niwawakilishe

Mwanabloga Mwenzangu,Mwandishi Mwenzangu wa Habari,Mwalimu Mwenzangu,Mwaharakati Mwenzangu bila kusahau Baba yangu Juma Nyumayo akionyesha bango linaloonyesha ukatili wa kijinsia kwa waandishi wa habari
Na Stephano Mango,Songea
MKOA wa Ruvuma umepewa heshima ya kuadhimisha siku 16 za kupinga Ukatili wa Kijinsia Kanda ya Kusini inayojumuisha Mikoa ya Iringa,Mbeya,Ruvuma,Lindi na Mtwara kuanzia Tarehe 25/11/2011 hadi 10/12/2011
Katika siku hizo 16 za maadhimisho wadau wanategemea kufanya maandamano,kutoa elimu ya jinsia kwa makundi mbalimbali na kutoa msaada wa sheria katika kata nne zilizopo Halmashauri ya Manispaa ya Songea chni ya kauli mbiu” Miaka 50 ya Uhuru pinga ukatili wa kijinsia kuimarisha Tanzania huru”
Vikundi mbalimbali vya sanaa vitatumbuiza vikiwa na ujumbe lengwa hivyo wadau wote wanatakiwa kuhudhuria kwani ushuhuda mbalimbali wa ukatili wa kijinsia utatolewa na wahusika waliofanyiwa vitendo hivyo

WAWILI WABAKWA KATIKA MATUKIO MAWILI TOFAUTI NA KUACHIWA MAUMIVU MAKALI SEHEMU ZAO ZA SIRI

Kamanda wa Polisi Mkoa wa Ruvuma Michael Kamuhanda
Na Mwandishi Wetu, Songea
JESHI la Polisi Mkoani Ruvuma linamshikilia Jaibu Alli ambaye umri wake haukuweza kufahamika mara moja kwa tuhuma za kumbaka msichana wa umri wa miaka kumi na sita ambaye jina lake limehifadhiwa anayesoma katika Shule ya Sekondari ya kutwa ya Kalembo iliyopo Halmashauri ya Manispaa ya Songea na kumsababishia maumivu makali sehemu za siri.

Akizungumza na mtandao wa www.stephanomango.blogspot.com  jana ofisini kwake Kamanda wa Polisi wa Mkoa wa Ruvuma Michael Kamuhanda amesema kuwa tukio hilo limetokea juzi jioni majira saa kumi  jioni huko katika eneo la Matogoro Songea Mjini nyumbani kwa Wazazi wake.

Kamuhanda amefafanua kuwa inadaiwa siku hiyo ya tukio msichana huyo akiwa jirani na nyumbani kwake alikutana na Jaibu ambaye alikuwa ni Mwanafunzi mwenzake katika Shule ya Kalembo na amehitimu Elimu ya Sekondari mwezi mmoja uliopita na walisalimiana na baadaye mvulana huyo alianza kumwambia maneno ambayo msichana huyo hakukubaliana nayo .

Ameeleza zaidi kuwa baada ya Jaibu kuona kuwa msichana huyo hakubaliani na maelezo aliyoyatoa ya kumtaka afanye mapenzi naye ndipo inadaiwa kuwa aliamua kumbaka kwa kutumia nguvu na kumsabishia sehemu za siri kuharibika na baadaye alikimbizwa katika hospitali ya Serikali ya Mkoa kwa matibabu ambako amelazwa akiendelea kupata matibabu.

Amesema mara tu baada ya kutokea tukio hilo mzazi wa msichana alitoa taarifa katika kituo kikuu cha polisi cah Songea na askari walipokwenda kwenye eneo la tukio walifanya upelelezi wa awali kisha walifanikisha kumkamata Jaibu.

Hata hivyo Kamanda Kamuhanda amesema kuwa Polisi bado inaendelea kufanya upelelezi zaidi kuhusiana na tukio hilo na kwamba ukikamilika mtuhumiwa atapelekwa mahakamani kujibu shtaka linalomkabili.

WAKATI HUOHUO Jeshi la Polisi Mkoani Ruvuma linamsaka mtu mmoja aliyefahamika kwa jina moja la Simon Mkazi wa Soko la wakulima Mbinga Mjini kwa tuhuma za kumbaka Mwanafunzi wa darasa la saba katika Shule ya Msingi Kiwanjani Mbinga Mjini ambaye jina lake limehifadhiwa.

Kamuhanda amesema tukio hilo lilitokea novemba 20 mwaka huu majira ya saa nane mchana huko katika eneo la mtaa wa soko la wakulima lililopo Mbinga Mjini ambako inadaiwa kuwa msichana wa umri wa miaka 12 akiwa nyumbani kwa wazazi wake alivamiwa na kubakwa na mtu mmoja ajulikanae kwa jina moja la Simon.

Amesema kuwa mtuhumiwa alitoroka mara tuu baada ya kumfanyia kitendo cha kinyama msichana huyo na kwamba kwasasa hivi Jeshi la polisi Mkoani Ruvuma  linamtafuta mtuhumiwa huyo ambaye anadaiwa kuwa amekimbia na kutokomea kusikojulikana.
MWISHO