About


Karibu ujiunge na chuo cha kisasa cha Easy Tech.Computer kwa mafanikio yako,Walimu waliobobea katika fani hiyo wanapatikana chuoni hapo

elimak

elimak

Pages - Menu

Wednesday, November 2, 2011

KIONGOZI WA CHAMA AKIFUATILIA HABARI MBALIMBALI KWENYE KIJIWE CHA KUUZIA MAGAZETI SONGEA

Katibu wa Chama Cha Mapinduzi (CCM) Wilaya ya Songea Mjini Alfonce Siwale akiperuzi magazeti mbalimbali hivi karibuni mjini hapa wakati huu muhimu wa kuvuana magamba ndani ya chama hicho

ABIRIA 19 WANUSURIKA KUFA BAADA YA GARI LAO KUACHA NJIA NA KUPINDUKA

Na Gideon Mwakanosya ,Songea.

WATU 19 wamenusurika kufa baada ya basi dogo maarufu kwa jina la daladala walilokuwa wamepanda kuacha njia na kupinduka katika mteremko uliopo katika barabara ya Bombambili katika Manispaa ya Songea na kusababisha watu watatu kati yao kujeruhiwa vibaya.

Akizungumza na waandishi wa habari jana ofisini kwake Kaimu Kamanda wa Polisi mkoa wa Ruvuma  Naftan Mantamba alisema kuwa tukio hilo limetokea jana majira ya saa 11 jioni huko katika eneo la mteremko wa Bombambili .

Alisema kuwa gari hilo lenye namba za usajiri T301 AQD aina ya Nissan Haice ambayo ilikuwa inaendeshwa na Frenk Honde iliacha njia na kupinduka na baada ya tukio hilo dereva alikimbia.

Mantamba alisema kuwa baada ya gari hilo kupinduka abiria  19 wamejeruhiwa lakini kati yao abiria 3 wamejeruhiwa vibaya sana na hali zao ni mbaya kwa sasa wamelazwa katika Hospitali ya Mkoa  kwa matibabu na wengine walitibiwa na kuruhusiwa kurudi majumbani mwao.

Amewataja majeruhi ambao hali zao ni mbaya kuwa ni Sakila Ramji(22) Abdul Mohamed (34) na Emma Komba(30) wote wakazi wa Songea mjini.

Chanzo cha ajari inadaiwa kuwa gari iliaribika likiwa kwenye mwendo mkali na kusababisha dereva kushindwa kumudu usukani kisha likaacha njia na kupinduka.

Kwa upoande wake Mganga Mkuu Mfawidhi wa Hospitali ya Serikali ya Mkoa Songea Dkt. Benedkto Ngaiza amethibitisha kupokea majeruhi wa ajari hiyo ambapo alieleza kuwa walioletwa walikuwa 19 lakini ambao hali zao ni mbaya wapo watatu na wamelazwa kwenye wodi ya majeruhi.

MWISHO

WATU 26 WAMENUSURIKA KUFA BAADA YA GARI YAO KUGONGA LORI BOVU

Na Gideon Mwakanosya,Songea
WATU 26 wamenusurika kufa baada ya basi dogo waliokuwa wakisafilia kutoka Songea Mjini kwenda Chipole kuligonga loli lililokuwa limeegeshwa kandokando ya barabara kwenye kona karibu na Daraja la mto Mlale ambalo lilikuwa bovu linasubiri kutengenezwa.
Kaimu kamanda Polisi Mkoa wa Ruvuma Naftari Mantamba amesema kuwa tukio hilo limetokea oktoba 31 mwaka huu majira ya saa 10:45 jioni huko kwenye eneo la daraja mto mlale uliopo katika kijiji cha Msanga Wilaya ya Songea vijijini
Mantamba amefafanua zaidi kuwa basi hilo dogo linalofahamika kwa jina la Tumaini ambalo linamilikiwa na kanisa Katoliki Jimbo kuu la Songea , Parokia ya Chipole lilikuwa linatoka Songea Mjini kwenda Chipole huku likiwa limebeba abilia 26 akiwemo Dereva wa gari hilo pamoja na tingo wake.
Ameeleza kuwa basi hilo dogo ambalo lilikuwa linaendeshwa na Christofa Mapunda (42), iliigonga lori lenye namba za usajili T 770 AYL aina ya skania ambalo lilikuwa limeegeshwa kandokando ya barabara bila kuweka alama ya aina yeyote ya kuashilia kuwa mbele kuna gari bovu.
Amebainisha zaidi kuwa basi hilo dogo lenye namba za usajili T 182 ANV aina ya Isuzu baada ya kuligonga loli imesababisha watu wa 5 wakiwemo dereva na tingo wake kujeruhiwa vibaya na kwamba kwasasa majeruhi wamekimbizwa katika hospitali ya Peramiho kwa matibabu zaidi na abilia wengine wamepata majeraha madogo madogo na kwamba wamepata huduma ya kwanza katika zahanati ya Misheni katoliki parokia Chipole na kuruhusiwa kurudi majumbani kwao.
Amewataja majeruhi walio pelekwa Peramiho ambao hali za mbaya kuwa ni dereva wa gali hilo Christofa mapunda (42) mkazi wa Songea Mjini, utingo wa basi hilo Englibeti Mbepera (26) mkazi wa Mbinga Mjini Sista HapiƱes Kihwili na Sista Leliana Muhanje miaka (25) wote wanatoka Shirika la chipole pamoja na mwalimu Velinaundi Kawonga (48) wa Shule ya Msingi chipole
Amesema kuwa gali hilo ambalo lilikuwa na abilia 26 ambapo kati yao walio jeruhiwa vibaya ni wale waliokuwa wamekaa kwenye viti vya mbele na chanzo cha ajali hiyo ni kuwa lori likuwa limegeshwa kandokando ya  barabara karibu na daraja bila kuweka alama ya aina yeyote ambayo ingemwonyesha dereva wa basi dogo kuwa mbele kuna gari bovu limeengeshwa kandokando ya babara na kusababisha kuligonga.