About


Karibu ujiunge na chuo cha kisasa cha Easy Tech.Computer kwa mafanikio yako,Walimu waliobobea katika fani hiyo wanapatikana chuoni hapo

elimak

elimak

Pages - Menu

Sunday, February 12, 2012

WANANCHI WAVAMIA OFISI YA SERIKALI NA OFISI YA CHAMA KWA SABABU MGANGA WA JADI AMEKOSA KIBALI CHA KUSHUGHULIKA NA WACHAWI



                      

MKUU WA WILAYA YA MBINGA KANALI EDMUND MJENGWA

Na Stephano Mango, Songea

KUNDI la wananchi wenye hasira kali katika Mji mdogo wa Mbambabay  wilaya mpya  ya Nyasa Mkoani Ruvuma wamevamia baadhi ya ofisi za serikali na CCM pamoja na baadhi ya nyumba za makazi ya watu na kuharibu samani za ofisi  na za watu kisha kuchoma nyaraka za Serikali na CCM zilizokuwa zimeifadhiwa kwenye majengo hayo yaliyo kuwa yamevamiwa

Baadhi ya watu walioshuhudia tukio hilo walieleza kuwa lilitokea baada ya uongozi wa Serikali  kata ya Mbambabay kukataa kutoa kibali cha kumruhusu Mganga wa Jadi aliyetoka Jijini Tanga kwa lengo la kufanya kazi ya kuwafichua  baadhi ya watu wanaojishughulisha  na imani za ushirikina  kwenye  mji mdogo wa Mbambabay .

Watu hao ambao hawakutaka majina yao  yatajwe gazetini walieleza kuwa  Mganga  huyo anaitwa  Fakii Yahaya  maarufu kwa jina la Jongo ambaye alikuwa amefika wilayani humo kuja kufanya kazi hiyo kwenye kijiji cha Ndengele ambako tayari alikuwa amesha fanya kazi ya kuwabaini  watu wanaofanya shughuli za ushirikina na  wananchi wa kijiji hiko walitangaza kuwakataa, hadharani wale wote waliobainika kuwa ni wachawi .

Walisema kuwa kufuatia hali hiyo baadhi ya wananchi wa mji mdogo wa Mbamba-bay walimwomba Mganga huyo ili aende akawasaidie kuwafichua  watu wanaojihusisha na mambo ya ushirikina katika mji huo,jambo ambalo lilipingwa na uongozi wa Serikali ya kata ambayo inadaiwa kuwa ilikataa kutoa kibali cha  kumhidhinisha Mganga huyo kufanya kazi  Mbamba bay  .

Walieleza kuwa  baada ya Serikali kutokubali kumruhusu Mganga huyo  kutofanya kazi ndipo wananchi wenye hasira kali walikusanyika na kuanza kuvamia baadhi ya majengo ya Serikali na ofisi ya CCM ya kata hiyo kisha waliaribu samani za ofisi na kuchoma moto nyaraka zote na baadaye walitawanyika.

Kwa upande wake  Mkuu wa wilaya ya Mbinga Kanali   Mstaafu Edmundi Mjengwa alipoulizwa na mtandao wa http://www.stephanomango.blogspot.com/  kwa njia ya simu kuhusiana na tukio hilo alithibitisha kutokea kwa tukio hilo na kuwepo uharibifu wa mali lakini alikataa kuelezea zaidi kwa madai  alikuwa safarini vijijini  kwa shughuli za kikazi .

Naye Kamanda wa polisi wa Mkoa wa Ruvuma Michael Kamuhanda  amethibitisha kuwepo kwa tukio hilo ambalo alidai limetokea February 9 mwaka huu majira ya saa 4 asubuhi huko Mbamba -bay  ambako kundi kubwa la watu wenye hasira kali lilivamia majengo mbalimbali  ya Serikali zikiwemo ofisi  ya Afisa  Mfawidhi  wa bandari  ya Mbambabay ambako waling’oa madirisha matatu ya jengo hilo ,ofisi ya Afisa tarafa ya Ruhekei ambako walibomoa mlango na kisha kuchoma  moto nyaraka zilizokuwa zimehifadhiwa ndani ya ofisi hiyo  na baadaye walikwenda ofisi ya CCM nako walivunja mlango na kuzichoma moto nyaraka zilizomo .

Alifafanua  kuwa baadhi ya samani zilizo haribiwa na kundi la wananchi wenye hasira kali ni pamoja na pikipiki aliyokuwa akiitumia Afisa Tarafa ,umemejua (sola) , Radio pamoja na mashine ya kupigia chapa  ambazo ni mali ya bandari na ofisi ya Tarafa .


Kamanda Kamuhanda alisema kuwa chanzo cha vurugu hizo ni baada ya Mganga wa Jadi Yahaya (Jongo) kunyimwa kibali cha kuwafichua na kuwatambua  watu wanaodaiwa kuwa ni wachawi kataka mji huo,hata hivyo mpaka sasa hakuna mtu yeyote anayeshikiriwa kuhusiana na tukio hilo na polisi inaendelea kufanya upelelezi wa kina .
MWISHO