About


Karibu ujiunge na chuo cha kisasa cha Easy Tech.Computer kwa mafanikio yako,Walimu waliobobea katika fani hiyo wanapatikana chuoni hapo

elimak

elimak

Pages - Menu

Tuesday, September 20, 2011

HII, NIMIONGONI MWA SHUGHULI ZINAZOFANYWA NA TCCIA MKOA WA RUVUMA KATIKA KUTANGAZA BIIDHAA ZA WAJASILIAMALI WANAOLELEWA NA TAASISI HIYO MUHIMU KWA WAJASILIAMALI

 Afisa Mtendaji wa TCCIA Mkoa wa Ruvuma Philemon Moyo akiangalia bidhaa aina ya mvinyo ikiwa katika aina mbalimbali zilizowekwa kwenye fremu maalum katika ofisi za TCCIA mkoa wa Ruvuma zilizopo kwenye jengo la NSSF mjini hapa

AJIKUTA MIKONONI MWA DOLA KWA KUSABABISHA KIFO CHA ADERINA KWA MADAI YA WIVU WA KIMAPENZI


                             Na Gideon Mwakanosya,Songea
JESHI la Polisi Mkoani Ruvuma linamshikilia Mfanyabiashara mkazi wa  wa Mbinga mjini Timotheo Komba (21) kwa tuhuma za kumuua muhudumu ya baa ya Mbuji iliyopo mjini humo ambaye awali alikuwa mpenzi wake

Akizungumza na Mwaandishi wa mtandao huu wa www.stephanomango.blogspot.com  jana ofisini kwake Kamanda wa Polisi wa Mkoa wa Ruvuma Michael Kamuhanda alimtaja mwanamke aliyeuawa kuwa ni Aderina Nchimbi(21) ambaye ni mkazi wa mtaa wa eneo la Shule ya Msingi Kiwanjani Mbinga Mjini

Kamuhanda alisema kuwa tukio hilo lilitokea Septemba 20 mwaka huu,majira ya saa moja asubuhi huko katika mtaa wa eneo la Shule ya Msingi Kiwanjani
Alisema kuwa inadaiwa siku ya tukio Afisa Upelelezi wa makosa ya jinai wa Wilaya ya Mbinga Mrakibu Msaidizi wa Polisi Edward Kavalambi akiwa na Askari wenzake wa kitengo cha Upelelezi ambao walikuwa doria waligundua kuuawa kwa Aderina ambaye alikutwa kando kando ya barabara jilani kabisa na nyumbani kwake

Alifafanua zaidi kuwa Maaskari kanzu hao baada ya kugundua tukio hilo la mauaji muda mfupi walifanikiwa kumkamata Komba ambaye anadaiwa kuwa katika kipindi cha nyuma alikuwa mpenzi wake tangu walipokuwa wakiishi katika Kijiji cha Mpepai

Alisema kuwa chanzo cha tukio hilo la mauaji kinasadikiwa kuwa ni wivu wa kimapenzi ambapo inadaiwa kuwa marehemu Aderina kabla ya mauti hayajamkuta alikuwa akilazimishwa kufanya mapenzi na Mfanyabiashara huyo Komba ambaye alikuwa akijitahidi kumshawishi warudiane tena na mahusiano yao kama awali lakini mwanamke huyo alikuwa anakataa

Kamuhanda alisema kuwa mara upelelezi utakapokamilika mtuhumiwa Komba anatarajiwa kufikishwa mahakamani ili kujibu tuhuma zinazomkabili,

MWENDESHA PIKIPIKI ASABABISHA KIFO CHA MTEMBEA KWA MIGUU

 
                    Na Gideon Mwakanosya,Songea
POLISI wilayani Mbinga Mkoani Ruvuma wanamshikilia Mwendesha Pikipiki Felix Ndimbo (18) mkazi wa Kijiji cha Langilo kwa tuhuma za kumgonga mtembea kwa miguu Joseph Ndimbo (76) mkazi wa Kijiji cha Mkoha wilayani humo na kumsababishia kifo papo hapo

Habari zilizopatikana jana mjini hapa ambazo zimethibitishwa na Kamanda wa Polisi wa Mkoa wa Ruvuma zimeeleza kuwa lilitokea juzi majira ya 1:30 usiku kwenye barabara inayotoka Mbinga kwenda kijiji cha Langilo

Kamuhanda alibainisha zaidi kuwa siku hiyo ya tukio kwenye barabara hiyo Felix akiwa anaendesha Pikipiki ambayo haina namba za usajili aina ya SanLg ilimgonga mtembea kwa miguu mzee Joseph Ndimbo ambaye alikuwa anatoka Kijiji cha Langilo kwenda katika Kijiji cha Mkoha na kumsababishia kifo papo hapo

Alieleza zaidi kuwa chanzo cha tukio hilo mwendesha Pikipiki Felix akiwa anatokea Kijiji cha Mkoha kuelekea Kijiji cha Langilo akiwa kwenye mwendo mkali alimgonga mtembea kwa miguu Joseph ambaye alikuwa anatembea kandokando ya barabara upande wa kulia

Kamuhanda alisema kuwa mtuhumiwa Felix amekamatwa na anaendelea kuhojiwa na Polisi ambapo upelelezi wa tukio hilo ukikamilika atafikishwa mahakamani kujibu mashtaka yanayomkabili
MWISHO