About


Karibu ujiunge na chuo cha kisasa cha Easy Tech.Computer kwa mafanikio yako,Walimu waliobobea katika fani hiyo wanapatikana chuoni hapo

elimak

elimak

Pages - Menu

Sunday, May 27, 2012

MWENGE WA UHURU KUANZA MBIO ZAKE RUVUMA


Kaimu Katibu Tawala Mkoa Ruvuma Severine Tossi Akizungumza na Waaandishi wa Habari jana
Na Stephano Chitete,Songea.

MWENGE wa uhuru unatarajiwa kuzindua ,kuweka mawe ya msingi,kukaguwa na kufunguwa miradi mbalimbali ya maendeleo ipatayo 51 yenye thamani ya jumla ya  sh.1,930,357,902 mkoani Ruvuma iliyojengwa kwa nguvu za wananchi na Serikali.

Akizungumza kwa niaba ya Mkuu wa Mkoa wa Ruvuma Said Mwambu kaimu katibu tawala wa Mkoa wa huo Severine Tossi alisema mbio za mwenge mkoani humo zinatarajiwa kuanza mei 28 mwaka huu hadi juni 3 mwaka huu ambapo utakabidhiwa katika kijiji cha Lumesule kilichopo mkoani Mtwara.

Alisema kuwa miradi itakayozinduliwa iliyojengwa kwa nguvu za wananchi inagharimu sh.206,022,645,halmashauri za Wilaya na Manispaa sh.204,486,125, Serikali kuu sh.773,599,581,wadau wa Maendeleo sh.458,809,551 na ya watu binafsi sh.287,440,000.

Aidha amewataka wananchi wa Mkoa huo kujitokeza kwa wingi kuupokea na kuushangilia mwenge huo wa uhuru ili waweze kupata ujumbe wa mwenge wa mwaka huu usemao "Sensa ni msingi wa mipango ya maendeleo yetu" wenye kauli mbiu shiriki kuhesabiwa Agosti 26 mwaka huu.

Akizungumzia kuhusu maandalizi ya sensa alisema yamekamilika na kufafanuwa kuwa mkoa huu unatarafa 24,kata 140,vijiji 509 na mitaa 79 na kwamba maeneo ya kuhesabiwa watu yaliyotengwa yapo 3,024 na maeneo ya usimamizi yapo 816.

Alifafanuwa kuwa kwa sasa Mkoa unajumla ya wakazi 1,412,084 kwa mujibu wa Sensa ya mwaka 2002 sawa na asilimia ya 2.5 ya ongezeko la watu.

Kaimu katibu Tawala huyo alisema Mwenge huo utakimbizwa katika wilaya mpya ya Nyasa, Mbinga,Songea,Namtumbo,na Tunduru ambapo Juni 3 mwaka huu utakabidhiwa kwa uongozi wa Mkoa wa Mtwara.

MWISHO.