About


Karibu ujiunge na chuo cha kisasa cha Easy Tech.Computer kwa mafanikio yako,Walimu waliobobea katika fani hiyo wanapatikana chuoni hapo

elimak

elimak

Pages - Menu

Saturday, January 21, 2012

SONNGO WAWAKUTANISHA WANANCHI WA MTYANGIMBOLE KWENYE MDAHALO WA WAZI KUHUSU KUIMARISHA MAHUSIANO KATI YA WABUNGE NA WANANCHI WAO

 Kutoka kulia ni Afisa Maendeleo ya Jamii,Halmashauri ya Wilaya ya Songea Bashiru Mgwassa,Diwani wa Kata ya Mtyangimbole Meckezedeck Mwella, Mwenyekiti wa Sonngo Siwajibu Gama,Kaimu Mkurugenzi wa Halmashauri ya Wilaya Mwl,Mwingira,Makamu Mwenyekiti wa Sonngo Ifigenia Mbawala,wa kwanza kutoka kushoni ni Katibu wa Sonngo Mathew Ngarimanayo
 Washiriki wa mdahalo huo wakisikiliza kwa makini mada zilizokuwa zinatolewa na wataalamu wa masuala ya uwajibikaji wa wa viongozi kwa wananchi wake

 Waandishi wa Habari wakiendelea kunasa matukio mbalimbali kwenye mdahalo huo,kutoka kushoto ni Mpiga picha Mpenda Mvula,Fundi Mitambo Boniface Bundala,Mwandishi wa Star Tv na Radio Free Africa Adam Nindi
 Mjumbe wa Kamati ya Utekelezaji ya Sonngo Jongo Haule
 Mwendesha ratiba katika Mdahalo huo MC Juma Nyumayo akitoa muongozo kwa washiriki
 Dj Ras akirekebisha mitambo ili washiriki wa mdahalo waendelee na libeneke husika
 Viongozi wa Asasi ya Sonno wakiwa kwenye dawati la usajiri wa washiriki wa mdahalo huo

Mzee Said Ramadhan akichangia hoja katika mdahalo huo

APANDISHWA KIZIMBANI KWA KOSA LA KUMBAKA MWANAFUNZI WA KIDATO CHA TATU

Na Gideon Mwakanosya,Songea

MTU mmoja mkazi wa mtaa wa Ruvuma katika Manispaa ya Songea mkoani Ruvuma amefikishwa katika Mahakama ya Hakimu mkazi mkoani humo kwa
tuhuma ya kumpa ujauzito mwanafunzi wa kidato cha tatu.

Ilidaiwa Mahakamani hapo na Mwendesha Mashtaka Wakili wa Serikali Shaban Mwegole mbele ya Hakimu Mkazi wa Mahakama hiyo Jenifer Changani
kuwa mnamo kati ya Januari na Mei mwaka jana, mshtakiwa Sababu Iddi(18) ambaye ni mkazi wa mtaa huo alitenda kosa hilo.

Mwendesha mashtaka huyo aliendelea kudai kuwa mwanafunzi huyo anasoma shule ya sekondari Ruvuma ambapo mshtakiwa ameonekana kutenda kosa hilo huku akijua kwamba ni kosa kisheria kufanya mapenzi na mwanafunzi jambo ambalo lilisababisha kukatisha masomo.

Kadhalika wakati kesi hiyo ikiendelea mahakamani hapo Hakimu mkazi wa Mahakama ya mkoa wa Ruvuma Shangani alisema mshtakiwa ana kesi ya kujibu kutokana na shtaka linalomkabili na kwamba anapaswa kuleta utetezi wake mahakamani.

Hata hivyo kesi hiyo imeahirishwa hadi Februari 14 mwaka huu itakapoletwa mahakamani kwa ajili ya kuanza kusikiliza utetezi wa mshtakiwa na kwamba mshtakiwa amerudishwa mahabusu kutokana na kukosa
mdhamini.

MWISHO.

VILABU MANISPAA YA SONGEA KUANZA KUCHUKUA FOMU USHIRIKI LIGI YA SANGA ONE

 Mwenyekiti wa SUFA Golden Sanga, Maarufu kwa jina la Sanga One
Diwani Mstaafu na Mdau wa Michezo Golden Sanga(Sanga One) akisisitiza jambo wakati akizungumza na waandishi wa habari kuhusu ligi ambayo inatarajia kuanza hivi karibuni mjini hapa

Na Stephano Mango,Songea

CHAMA cha mpira wa miguu katika Manispaa ya Songea(SUFA) kimezitaka vilabu kujitokeza kuchukua fomu kwa ajili ya kushiriki  mashindano ya Sanga One Cup ambayo yamepangwa kufanyika kwenye uwanja wa shule ya msingi Sokoine katika Manispaa hiyo.
 
Akizungumza mjini hapa jana, Katibu msaidizi wa SUFA, Godfrey Mvula alisema kuwa mashindano hayo yatahusisha vilabu vyote ndani ya Manispaa hiyo ambavyo vina usajili wa kudumu kutoka kwa msajili wa vyama vya michezo nchini na vile visivyokuwa na usajili huo.
 
Mvula alisema mashindano hayo yatadhaminiwa na mmoja wa wadau wa soka na pia Mwenyekiti wa SUFA katika Manispaa hiyo, Golden Sanga  maarufu kwa jina la Sanga One  yenye lengo la kusaka vipaji vipya na kuviibua ili kuwafanya wachezaji hao kuwa tegemeo na hazina kwa Manispaa mkoa na Taifa kwa ujumla.
 
Alisema mashindano hayo yatakuwa chachu na mbinu ambayo itasaidia SUFA  kuwapata wachezaji wenye vipaji na wanaojituma wawapo uwanjani badala ya kuwatafuta kwa kuwateua kupitia  kwenye mashindano ya ligi ya wilaya au mkoa na kuishia kutafuta maslahi yao binafsi badala ya mpira uliomweka hapo.
 
 Alieleza kuwa bingwa wa mashindano hayo ataondoka na kitita cha fedha taslimu Sh. 200,000/=,  wa pili atazawadiwa fedha Sh. 100,000/= na  mshindi wa tatu ataambulia fedha Sh.70,000/=, mchezaji bora atazawadiwa fedha taaslim Sh.20,000/= na timu itakayoonyesha nidhamu ya ndani na nje ya uwanja watapata fedha Sh.20,000/=.
 
Alisema gharama ya uchukuaji wa fomu imepangwa kulipia  Sh.10,000/= ambayo itapenda kushiriki mashindano hayo na zitarejeshwa fomu hizo Januari 26 mwaka huu saa 10:30 jioni kwenye ofisi za SUFA alidai mchezaji atakaye bainika amesajiliwa na timu zaidi ya moja jina lake litaondolewa kushiriki mashindano hayo.
 
MWISHO