About


Karibu ujiunge na chuo cha kisasa cha Easy Tech.Computer kwa mafanikio yako,Walimu waliobobea katika fani hiyo wanapatikana chuoni hapo

elimak

elimak

Pages - Menu

Wednesday, February 4, 2015

KICHANGA CHATUPWA CHOONI, MWINGINE ATUMBUKIA KISIMANI



NA, STEPHANO MANGO,SONGEA

JESHI la polisi mkoni Ruvuma linawasaka wanawake watatu akiwemo mmoja ambaye jina lake limehifadhiwa mwenye umri kati miaka 20 na 24 mkazi wa eneo la mahenge C manispaa ya Songea  ambaye anadaiwa kutoa  mimba kisha kukitupa kichanga kwenye shimo la choo huku kikiwa kimeviringishwa mfuko wa Rambo.


Akizungumza na Tanzania Daima jana mchana ofisini kwake kamanda wa polisi mkoani Ruvuma Mihayo Msikhela alisema kuwa tukio hilo limetokea juzi majira ya saa 6:20 mchana huko katika eneo la Mahenge C.


Alifafanua zaidi kuwa inadaiwa siku hiyo ya tukio aliopolewa mtoto mchanga anayekadiliwa kuwa na miezi kati 7 na 8 wa jinsia ya kike akiwa amefungwa ndani ya mfuko wa Rambo kwenye shimo la choo ambacho kipo kwenye nyumba inayomilikiwa na Philibert Komba (60) mkazi wa Mbagala jijini Dar es salaam.

Alisema kuwa taarifa za awali zinaonyesha kuwa mwanamke huyo anayedaiwa kutoa mimba na kutupa kichanga chooni alishirikiana na wanawake wenzake wawili ambao ndio waliomsaidia  kutimiza hadma yake hiyo ya kutupa kichanga na kwamba kwa sasa hivi polisi inawasaka na kwamba wakipatikana watafikishwa mahakamani kujibu mashtaka yanayo wakabili.

WAKATI huo huo Salah Silenge(10) ambaye  ni mwanafunzi wa darasa la tatu katika shule ya msingi kilimani wilaya ya Songea vijijini amefariki dunia baada kutumbukia kwenye kisima cha maji wakati alipokuwa akicheza na wenzake.

Alieleza zaidi kuwa inadaiwa siku hiyo ya tukio mwili wa marehemu ulikutwa ndani ya kisima cha maji na askari polisi walipofika kwenye eneo la tukio wakiwa wameongozana na mganga walikutwa salah ameshakufa kwa kunywa maji mengi.

MWISHO