About


Karibu ujiunge na chuo cha kisasa cha Easy Tech.Computer kwa mafanikio yako,Walimu waliobobea katika fani hiyo wanapatikana chuoni hapo

elimak

elimak

Pages - Menu

Sunday, February 26, 2012

CHAMA KIKUU CHA USHIRIKA WA WAKULIMA WILAYA YA TUNDURU KIMEELEMEWA NA MZIGO WA MADENI

Na,Steven Augustino Tunduru

WAKATI Makampuni ya Wanunuzi wa Korosho Nchini wakiendele kutunishiana misuli na Serikali Chama Kikuu cha Ushirika wa Wakulima wa Wilaya ya Tunduru (TAMCU) kimekiri kuelemewa na mzigo wa Madeni ya Wakulima yaliyotokana na Chama hicho kununua Korosho za Wakulima wa
zao hilo.

Hayo yameeelezwa na Meneja wa Chama hicho Imani Kalembo wakati akitoa taarifa kwa Mkuu wa Wilaya ya Tunduru Juma Madaha wakati wa kikao cha pamoja na Wadau wa Kilimo na viongozi wa Vyama vya Siasa .

Katika taarifa yake, Meneja huyo alifafanua kuwa hadi sasa chama hicho kupitia vyama vikuu vya Ushirika vya wakulima wa zao hilo kinadaiwa Jumla ya Shilingi Bilioni 2,441,870,350 .

Taarifa hiyo iliendelea kueleza kuwa fedha hizo zimetokana na chama hicho kununua jumla ya Kilo 6,976,821 ambazo Chama hicho kupitia vyama vya msingi vimeweza kuzilipia kwa asilimia 70% pekee .

Alisema sambamba na Deni hilo pia Tamcu bado inakabiriwa na deni la Shilingi Milioni.608,260,000 zilizo tokana na Mkopo wa  kilo 506,855 za Korosho za zilizo kopeshwa na wakulima kwa vyama vya Msingi .

Kalembo aliendelea kueleza kuwa wakati hayo yakiendelea Chama hicho pia  kinakabiliwa na changamoto ya Chama kushindwa kununua jumla
ya kilo 86,324 zenye thamani ya Shilingi Milioni 17,264,800 ambazo bado zipo mikononi mwa wakulima wa zao hilo hali inayo endelea
kuwakatisha tamaa ya kuendelea na kilimo hicho.

Akizungumzia hali uzalishaji wa zao hilo katika Msinu wa mavuno wa
mwaka 2011/2012,Kalembo alisema kuwa Takwimu za manunuzi na Korosho
zilizopo mikononi mwa wakulima zinazonesha kuwa Jumla ya Kilo 7,570,000
zilizalimwa katika kipindi hicho.

Akizungumzia madhara yaliyo sababishwa na mgomo wa  Makampuni ya Wanunuzi zao hili Mkuu wa Wilaya hiyo Juma Madaha aliwataka wakulima kupitia wadau hao kuwa na uvumilivu wakati Serikali ikitafuta
suluhisho la kudumu la soko la mazao hayo.

Mwisho

MADEREVA YEBOYEBO WAMTEMEA NYONGO RC MWAMBUNGU RUVUMA

                              MKUU WA MKOA WA RUVUMA SAID MWAMBUNGU
Na Kassian Nyandindi, Songea

MADEREVA wanaoendesha pikipiki maarufu kwa jina la 'yeboyebo' katika Manispaa ya Songea mkoani Ruvuma, wamemlalamikia mkuu wa mkoa huo Said Mwambungu wakisema kuwa chanzo cha machafuko na mauaji ya raia wawili waliopigwa risasi na askari polisi, yametokana na jeshi hilo kupuuza taarifa za uhalifu zilizokuwa zikitolewa na wakazi wa manispaa hiyo.

Malalamiko hayo yalitolewa na madereva hao kutokana na vifo vingi vinavyojitokeza katika manispaa hiyo wengi wanaouawa ni wao, walipokuwa wakizungumza katika kikao kilichoitishwa na mkuu wa mkoa huo kwa lengo la kujenga ushirikiano baina ya serikali na madereva hao ili machafuko yaliyotokea hivi karibuni yasiweze kuendelea.

Akichangia hoja katika kikao hicho mmoja kati ya madereva hao  Bonventura Njogopa, alisema kuwa mara nyingi askari polisi wapelelezi wamekuwa wakikaa vijiweni katika maeneo ya mjini na kuwafuatilia madereva hao kwa madai kwamba wanajihusisha na vitendo vya ujambazi wakati sio kweli badala yake walimweleza Bw. Mwambungu kuwa askari hao ni vyema muda mwingi wawe wanazunguka pembezoni mwa mji ambako mara nyingi wamekuwa wakijificha majambazi.

"Mheshimiwa mkuu wa mkoa askari wako wapelelezi wanatuambia sisi ndio chanzo cha kuwepo kwa majambazi, hii si kweli sisi ni raia wema tunachohitaji waache kukaa muda mwingi vijiweni hapa mjini badala yake wawe wanazunguka na sehemu zingine katika mji wetu wa songea ambako ndiko wahalifu wengi wanajificha", alisema Njogopa.

Naye Ali Omary alisema kwa muda mrefu polisi wamekuwa wakiwataka wao kama madereva wa pikipiki ambao huzunguka katika maeneo mbalimbali, kujenga ushirikiano na jeshi hilo kwa kutoa taarifa kwa njia ya simu au vinginevyo pale wanapobaini kuna dalili za uhalifu mahali fulani, lakini pamoja na wao kujitahidi kufanya mawasiliano na askari hao wamekuwa wakipuuzwa.

"Tunaiomba serikali yako hususani hawa polisi wakamate majambazi, lakini pia waache habari za kutuumiza sisi madereva wa pikipiki kwa kutupiga ovyo", alisema.

Pia walimweleza mkuu huyo wa mkoa kwamba askari wa usalama barabarani na polisi wa kawaida wote kwa pamoja wamekuwa wakijihusisha na ukamataji wa pikipiki jambo ambalo linawafanya washindwe kutambua nani hasa anapaswa kukagua vyombo hivyo vya moto.

Walielekeza malalamiko yao kwa mkuu wa usalama barabarani (RTO) mkoani Ruvuma  Sebastian Mtaki wakisema kuwa wanapotoa taarifa kwake, juu ya vitendo hivyo vinavyofanywa na askari wake hupuuzwa na hakuna hatua zinazochukuliwa.

"Utakuta pikipiki inakamatwa na kupelekwa kituoni, unapotakiwa kwenda kulipa faini ya makosa yako tunaambia tumfuate askari fulani kwenye baa fulani, je mkuu huu ndio utendaji halali wa kazi au ni ofisi zao binafsi", walihoji.

Kwa upande wake akijibu hoja hizo mkuu wa mkoa wa Ruvuma Mwambungu alisema kimsingi atafuatilia malalamiko yao na kuyafanyia kazi haraka na kwamba aliwataka kuheshimu sheria na taratibu zilizowekwa ili kuepuka uwezekano wa uvunjifu wa amani kama ilivyojitokeza siku mbili zilizopita.

Hata hivyo aliongeza kuwa ofisi yake imekwisha unda tume ya watu nane ambayo itachunguza machafuko na mauaji ya raia yaliyojitokeza mjini Songea na kutoa majibu kwake kwa kippindi cha siku saba zijazo.

MWISHO.