About


Karibu ujiunge na chuo cha kisasa cha Easy Tech.Computer kwa mafanikio yako,Walimu waliobobea katika fani hiyo wanapatikana chuoni hapo

elimak

elimak

Pages - Menu

Sunday, September 25, 2011

SAKATA LA UMEYA SONGEA LAWAKUTANISHA WAANDISHI WA HABARI MKOA WA RUVUMA NA WAZIRI DKT NCHIMBI

 Waziri wa Habari,Utamaduni na Michezo Dkt Emmanuel Nchimbi katikati akizungumza na waandishi wa habari kuhusu sakata la kukimbia na sanduku la kura wakati wa uchaguzi wa umeya uliofanyika hivi karibuni kwenye ukumbi wa Saccos wa Halmashauri ya Manispaa ya Songea,kushoto ni Charles Mhagama anayedaiwa kuwa Mstahiki Meya wa Halmashauri ya Manispaa ya Songea,kulia ni Kaimu Mkurugenzi wa Halmashauri ya Manispaa ya Songea Naftan Saiyoloi
 Waandishi wa habari wakiendelea kusikiliza hoja mbalimbali katika kikao cha waandishi wa habari na Waziri Dkt Nchimbi
 Waziri Dkt Nchimbi aliyekaa katikati akiwa kwenye picha ya pamoja na waandishi wa habari nje ya ukumbi wa Halmashauri ya Manispaa ya Songea
Waliokaa kutoka kushoto Charles Mhagama(Anayedaiwa kuwa Mstahiki Meya),Waziri wa Habari,Utamaduni na Michezo Dkt Nchimbi,Endre w Kuchonjoma(Mwenyekiti wa Ruvuma Press Club),Waliosimama kutoka kulia Nathan Mtega(Katibu Msaidizi wa Chama cha Waandishi wa Habari mkoani Ruvuma),Endrew Chatwanga(Katibu wa Mbunge wa Jimbo la Songea Mjini),Gerson Msigwa(TBC),Emmanuel Msigwa(Channel Ten) Ngaiyona Nkondora(Star Tv na Redio Free) Juma Nyumayo(Uhuru Fm) Alpius Mchucha(HabariLeo)Stephano Mango(Dira ya Mtanzania) Amon Mtega(Mtanzania) Joseph Mwambije(Majira) Anuciata Ngatunga(Ps wa Dkt Nchimbi)Cresencia Kapinga(Majira) Meja Mgumba(Msaidizi wa Waziri) Joyce Joliga(Mwananchi) Naftan Saiyoloi(Kaimu Mkurugenzi wa Halmashauri ya Manispaa ya Songea
Na Mwandishi wetu
 WAZIRI wa Habari Utamaduni na Michezo Dkt Emmanuel Nchimbi amekutana na waandishi wa habari na kuzungumzia sakata la kudaiwa kukimbia na sanduku la kura kabla ya kudhibitiwa na Madiwani wa Chadema juzi katika uchaguzi wa nafasi wazi ya Mstahiki Meya wa Halmashauri ya Manispaa ya Songea

Akisoma tamko lake katika ukumbi wa Halmashauri ya Manispaa ya Songea alisema kuwa amesikitishwa na vyombo vya habari,magazeti ya Tanzania Daima,Majira na Mwananchi vilivyolipoti habari hiyo iliyojaa upotoshaji mkubwa

Dkt Nchimbi amevitaka vyombo hivyo kukanusha na kumuomba radhi katika matoleo yao ya Septemba 26 katika ukulasa wa mbele kwani vimemshushia hadhi yake katika jamii na kumjengea misingi ya ukosefu wa uaminifu

Alisema kuwa mnamo tarehe 23 Septemba 2011 magazeti ya Tanzania Daima,Mwananchi na Majira yaliripoti taarifa inayofanana kwamba Waziri wa Habari,Vijana,Utamaduni na Michezo amekimbia na sanduku la kura kufuatia vurugu zilizotokea katika uchaguzi wa Meya wa Manispaa ya Songea

“Napenda kuutaarifu umma kwamba habari hizo siyo za kweli na ni uzushi mtupu,ukweli ni kwamba mimi katika kikao hicho sikukimbia na sanduku la kura wala hakuna diwani yeyote aliyetoka au kukimbia nje ya ukumbi na sanduku la kura kama ilivoripotiwa na magazeti hayo”alisema Dkt Nchimbi

Alieleza kuwa ukisoma upotoshwaji huu katika magazeti yaliyoandika habari hizo utagundua kwamba habari hizo zimeandikwa na mtu mmoja na kuwagawia waandishi wenzake wa magazeti mengine bila kuthibitisha wakazipeleka kwenye magazeti yao

“Taarifa hizo zilizopotoshwa kwa makusudi zimenidhalilisha,kunichafulia jina langu na kunifanya kuwa mtu nisiyeaminika kitaifa na kimataifa”alisema Dkt Nchimbi

Alieleza zaidi kuwa tabia iliyoanza kuzoeleka hivi sasa ya mwandishi mmoja kuandika kisha kuwasambazia wenzake unawazalilisha waandishi wenyewe na vyombo wanavyoviandikia

Alisema kuwa kwa taarifa hii nayataka magazeti ya Tanzania Daima,Mwananchi na Majira kukanusha na kusahihisha taarifa hizo kwenye magazeti yao ya kesho tarehe 26 September 2011
 Kwenye ukurasa wa mbele na kuniomba radhi
MWISHO

KUNDI LA TEMBO LASABABISHA MAUAJI YA BINADAMU TUNDURU

Na Augustino Chindiye ,Tunduru

MKAZI wa kitongoji cha Ndola kilichopo katika kijiji cha marumba Wilayani Tunduru Daud Rashid (50) amefariki dunia baada ya kuvamiwa na kushambuliwa na kundi la tembo.

Mashuhuda wa tukio hilo wamesema kuwa tukio hilo lilitokea wakati marehemu akiende shambani ambako inadaiwa kuwa alikuwa akienda kufanya maandalizi ya shamba la kulima msimu ujao.

Akizungumzia tukio hilo Kaimu Afisa Wanyama pori wa Wilaya ya Tunduru Mkoani Ruvuma  Abdalah Mbanganike mbali na kukiri kuwepo kwa tukio hilo alisema kuwa marehemu alifariki dunia kutokana na kuchomwa na meno ya Tembo hao.

Alisema kufuatia hali hiyo idara yake imetoa askari watatu waliongozwa na Ally Salumu kwa ajili ya kuwasaka tembo hao na wameruhusiwa ku ua ili wasilete madhara mengine.

Akizungumzia tukio hilo Kamanda wa Polisi wa Mkoa wa Ruvuma  Michael kamuhanda katika maelezo yake alitumia nafasi hiyo kuwaasa wananchi kujenga tabia ya kutembea katika makundi ili waweze kusaidiana.

Mganga aliye ufanyia uchunguzi mwili wa marehemu Rashid Dkt. Moses Mwahasunga amesema kuwa kifo chake kimesababishwa na kutokwa na damu nyingi pamoja na kutobolewa tumbo na kuhalibu mfumo wa utendaji kazi wa viungo vilivyopo ndani ya mwili wa binadamu

Mwisho



CCM TUNDURU PECHEPECHE KWA UDHAIFU WA VIONGOZI WAKE WA WILAYA

Na Augustino Chindiye ,Tunduru

VIONGOZI,Wanachama na Wakereketwa wa Chama Cha Mapinduzi CCM Tarafa ya Nakapanya wametoa siku tatu kwa viongozi wa Chama hicho ngazi ya Wilaya kwenda kujieleza kwa nini wasichukuliwe hatua zikiwemo za kufukuzwa kwa kupigiwa kura za kuto kuwa na imani nao.

Tamko hilo limetolewa na wanachama hao katika kikao kilicho wahusisha viongozi wa Chama na jumuiya zake kilicho fanyika katika ukumbi wa ofisi ya Serikali ya Kata ya Namiungo kikiwa na nia ya kujadili mikakati ya kukinusuru chama hicho ili kisifanye vibaya katika chaguzi zijazo.
Sambamba na tamko hilo pia wanachama hao wametishia kutopiga kura katika uchaguzi ujao ama ikiwezekana watamuomba Mwenyekiti wa CCM Taifa, Rais wa Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. Jakaya Kikwete awaruhusu wajiunge na kupiga kura katika Jimbo la Nanyumbu lililopo Mkoani Mtwara.

Wakiongea kwa jaziba wana CCM hao kutoka katika Kata za Nakapanya ambao waliongozwa na Mjumbe wa Mkutano wa  Halmashauri kuu ya Chama Cha Mapinduzi Wilaya ya Tunduru  Likambale Omari, Shaib Akijo kutoka Kata ya Mindu, Yasini Kaweje kutoka Kata ya Ngapa na Mjumbe wa halmashuri Kuu ya CCM Wilaya Maimuna Bora kutoka Kata ya Muhuwesi walisema wameamua kuchukua maamuzi hayo baada ya kubaini kuwepo kwa ubabaishaji uliokithiri ndani ya Chama hicho huku kukiwa na taarifa za kubebana na kuwachagulia wananchi viongozi wanaotoa fedha kwao.

Aidha wanachama hao wakatolea mfano ubabaishaji wa taarifa za kuteuliwa kwa Diwani wa Viti Maalumu Wanawake wa Tarafa hiyo Salima Limbalambala ambaye mbali na kushiriki katika uchaguzi wa Mwenyekiti wa Halmashauri hiyo  Faridu Khamisi baadae zilitolewa taarifa zenye utata za kutenguliwa kwa wadhifa huo na kuiweka Tarafa yao katika mkanganyiko ambao hadi leo Uongozi wa Chama hicho ngazi ya Wilaya haujatolea kauli yoyote ikiwa ni tofauti na walivyofanya baada ya kutenguliwa kwa udiwani wa Selemani Chisopa aliyetuhumiwa kufanyia kampeni vyama vya upinzani katika uchaguzi mdogo wa Kuziba nafasi ya aliyekuwa Mbunge wa Jimbo la Tunduru Marehemu Juma Akukweti.

Nao Diwani mstaafu  Hasan Futali, Dastan Amlima na Husen Ndayani ambao pamoja na mambo mengine walihoji vigezo na sababu za uhalali wa kutenguliwa kwa udiwani wa Salima Limbalambala ambaye jina lake lipo katika barua zilizo andikwa na kusainiwa na Mkurugenzi wa Uchaguzi Taifa Rajab Kiravu na badala yake viongozi wa CCM Wilaya wakapendekeza na kumchagua Diwani wa Viti Maalumu wanaweke kutoka Tarafa ya Mjini Siwema Kalipungu ambaye hakupiga kura za Kumchagua mwenyekiti wa halmashuri huyo huku matokeo ya kuchaguliwa kwake yakiendelea kuheshimiwa.

Kwa ujumla maelezo ya viongozi hao Kero kubwa inayotembea vichwani na katika midomo yao ni Usimamizi mbovu wa Viongozi wa Chama hicho ngazi ya Wilaya ambao wamedai kuwa umeshindwa kusimamia haki kwa wanachama wake, hawafanyi mikutano ya uhamasishaji na wanasema uongozi huo kuwa umepoteza Dira na wakaendelea kutahadharisha  kwamba endapo CCM Taifa itawaachilia waendelee kuiongoza Wilaya hiyo kuna hatari ya chama hicho kufanya vibaya zaidi katika chaguzi zijao ukiwewmo uchaguzi Mkuu wa Mwaka 2015.

Hata hivyo baada ya kutoa dukuduku zao hizo zenye maneno makali kwa uongozi wao ukafuata wasaa wa kutoa tamko la kuita kikao cha dhalula kilicho pangwa kufanyika Septembar 28 mwaka huu na kwamba watakao tolewa kafala katika kikaango hicho ni  uongozi wa CCM Wilaya unao ongozwa na Mwenyekiti wa CCM Wilaya  Mustafa Bora, Katibu wa CCM Wilaya Ramadhan Amer. Katibu Mwenezi CCM Wilaya Hasan Kindamba.

Wakizungumzia mgogoro huo baadhi ya madadisi wa masuala ya siasa walisema kuwa kupotea kwa mwelekeo na utashi wa viongozi wa chama Tawala CCM kunatokana na mfumo mbovu wa ufuatiliaji na upembuzi wa viongozi wanao takiwa kuwekwa madarakani tofauti na mfumo wa wasisi wa taifa hili Baba wa taifa hayati Mwl. Julius Nyerere  ambao wakati wao walikuwa makini nia viongozi wao na walikuwa wakihakikisha kuwa kiongozi anayefaa ni yule aliyepikwa na kuifa kisiasa.