About


Karibu ujiunge na chuo cha kisasa cha Easy Tech.Computer kwa mafanikio yako,Walimu waliobobea katika fani hiyo wanapatikana chuoni hapo

elimak

elimak

Pages - Menu

Friday, November 25, 2011

MCHINA ACHEZEA KIPIGO KUTOKA KWA MTANZANIA NA KUNYANG'ANYWA SIMU TATU ZENYE THAMANI YA LAKI SITA MBINGA

Kamanda wa Polisi Mkoa wa Ruvuma Michael Kamuhanda
Na Gideon Mwakanosya,Songea

JESHI la Polisi Mkoani Ruvuma linamsaka Dereva wa Kampuni ya Sinohydro inayotengeneza barabara kwa kiwango cha lami kutoka Songea kwenda Mbinga Said Ibrahim kwa tuhuma za kumnyang’anya Simu tatu za mkononi zenye thamani ya shilingi laki 6 na kumjeruhi kwa kumpiga na nondo kichwani Majianxin mwenye umri wa miaka (40) ambaye ni raia wa China mfanyakazi wa Kampuni hiyo ya ujenzi.

Kamanda wa Polisi wa Moka wa Ruvuma Michael Kamuhanda ameuambia mtandao huu wa http://www.stephanomango.blogspot.com/ kuwa tukio lilitokea jana majira ya saa nane mchana kwenye eneo la Mkako Wilayani Mbinga.

Amesema kuwa inadaiwa siku hiyo ya tukio  Majianxin mwenye asili ya kichina akiwa kwenye shughuli zake za ujenzi wa barabara majira ya saa nane mchana alinyang’anywa simu tatu za mkononi na dereva wa Kampuni ya Sinohydro aliyejulikana kwa jina la Said Ibrahimu.

Amefafanua kuwa inadaiwa kabla ya Ibrahimu kumnyang’anya simu hizo alichukua nondo na kumpiga Majianxin na badae alikimbia na kutokomea kusikojulikana na kwasasa hivi Majianxin amepata majeraha makubwa kichwani na anaendelea kupata matibabu kwenye hospitali ya Wilaya Mbinga.

Ameeleza zaidi kuwa Majianxin alinyang’anywa simu tatu ambapo kati ya hizo mbili ni za aina ya Samsung na nyingine ni aina ya nokia zote zikiwa na thamani ya shilingi laki 6.

Hata hivyo Kamuhanda alisema kuwa kufuatia tukio hilo kutokea kwasasa hivi Jeshi la Polisi Mkoani humo linaendelea kumsaka mtuhumiwa ambaye anadaiwa kuwa ametorokea katika Mikoa ya Lindi na Mtwara.

MWISHO



MBARONI KWA TUHUMA ZA KUMUUA MTOTO KWA KUMPIGA NA MTI KICHWANI

Na Mwandishi Wetu,Songea

POLISI Mkoani Ruvuma imemtia mbaroni Joseph Ndunguru Mkazi wa Kijiji cha Mkumbi kilichopo Wilayani Mbinga Mkoa wa Ruvuma kwa tuhuma za kumuua mtoto mwenye umri wa miaka miwili na nusu kwa kumpiga na mti kichwani wakati anasindikizwa na mama yake kwenda chooni kujisaidia.

Akizungumza na mtandao wa www.stephanomango.blogspot.com Jana ofisini kwake Kamanda wa Polisi Mkoa wa Ruvuma Michael Kamuhanda amemtaja mtoto aliyeuwawa kuwa ni Agnes Ndimbo Mkazi wa Kijiji cha Mkumbi Wilayani Mbinga.

Amefafanua kuwa inadaiwa siku hiyo ya tukio novemba 22 mwaka huu majira ya saa moja usiku huko katika Kijiji cha Mkumbi Prisca Nditi (38) akiwa nyumbani kwake mtoto wake Agnes alimuomba amsindikize kwenda kujisaidia .

Amesema kuwa baada ya mtoto huyo kumuomba mama yake ampeleke chooni ndipo Prisca aliondoka na mwanaye wakaelekea nje ya nyumba kwenye eneo la choo ambapo wakati wanarudi mara tuu baada ya mtoto huyo kujisaidia inadaiwa kuwa Ndunguru alivizia na kumpiga mtoto na mti kichwani na kumsababishia kifo papo hapo.

Hata hivyo amesema kuwa habari zaidi kutoka Kijijini Mkumbi zinaeleza kuwa Ndunguru maarufu kwa jina la Kapalanza kwa muda mrefu amekuwa akisumbuliwa na ugonjwa wa akili ambao unahofiwa kuwa ndio ulisababisha atende kosa hilo na Jeshi la Polisi linaendelea kufanya upelelezi wa kina juu ya tukio hilo na utakapokamilika mshtakiwa atafikishwa mahakamani kujibu shtaka linalomkabili.

MWISHO