About


Karibu ujiunge na chuo cha kisasa cha Easy Tech.Computer kwa mafanikio yako,Walimu waliobobea katika fani hiyo wanapatikana chuoni hapo

elimak

elimak

Pages - Menu

Wednesday, September 11, 2013

WANAJESHI WAJERUHI RAIA, KAMANDA AKANUSHA




Na Julieth Mkireri, Kisarawe

MKAZI wa Tondoroni, Wilaya ya Kisarawe, mkoani Pwani, Omary Mohamed (47), amejeruhiwa kwa kupigwa risasi na watu wanaodaiwa kuwa ni wanajeshi katika mapishano yanayodaiwa kuhusiana na kugombea mpaka.

Tukio hilo lilitokea juzi, majira ya saa 3 asubuhi baada ya wanajeshi hao kutembelea katika eneo lao na kukuta familia moja ikiwa imejenga nyumba katika eneo ambalo linadaiwa kuwa ni mali ya jeshi.

Inaelezwa wanajeshi hao walijaribu kuzungumza na familia hiyo kwa kuwasihi kuondoka, lakini hali hiyo iliibua mzozo mkali kutokana na wanafamilia kukaidi amri hiyo.

Hata hivyo, baada ya kuona hakuna maelewano, ghafla Mohamed alipigwa risasi moja na watu hao wanaodaiwa kuwa wanajeshi.

Baada ya tukio la kupigwa risasi kwa mwananchi huyo, wanajeshi hao walitokomea kusikojulikana na ndipo wananchi waliamua kufunga barabara hadi polisi walipofika na kwenda kutuliza ghasia.

Kamanda wa Polisi mkoani Pwani, Ulrich Matei, amethibitisha kuwepo kwa tukio hilo na kusema majeruhi huyo amepigwa na kitu chenye ncha kali na kuwa bado haijajulikana kama waliomjeruhi ni askari ama la na kama amepigwa na risasi.

Alisema kuwa kwa sasa anafanya mawasiliano na kiongozi wa jeshi ili kubaini ukweli kama ni askari wa jeshi na wametumwa kwenda kwa wananchi hao au walikwenda wenyewe.

Kamanda Matei alisistiza kuwa si rahisi kumtambua askari kwa kuwa tu amevalia sare za polisi lakini pia ni lazima namba za wahusika zijulikane, kambi gani na uthibitisho kutoka kwa kiongozi wa jeshi kwani baadhi ya watu huvalia mavazi hayo kwa manufaa binafsi.

Mganga Mkuu wa Hospitali ya Rufaa ya Tumbi, Peter Datani, amekiri kumpokea majeruhi huyo akiwa na jeraha kwenye mguu wake wa kulia, na hali yake inaendelea vizuri.