About


Karibu ujiunge na chuo cha kisasa cha Easy Tech.Computer kwa mafanikio yako,Walimu waliobobea katika fani hiyo wanapatikana chuoni hapo

elimak

elimak

Pages - Menu

Friday, January 27, 2012

TIMU YA MLALE JKT YASAJIRI KINDA KUTOKA KAHAMA UNITED

Na Stephano Mango, Songea
 
TIMU ya soka ya Mlale JKT ya Songea imesajili kinda  kutoka Kahama United ya Shinyanga katika nafasi ya kiungo katika usajili wa dirisha dogo kabla ya kuanza kwa ligi ya Daraja la kwanza mzunguko wa pili, ligi hiyo ambayo inatarajiwa kuanza Februari, 4 mwaka huu.
 
Akizungumza mjini hapa jana kocha msaidizi wa Maafande hao, Edger Msabaila alimtaja kinda hilo kuwa Dotto Mrisho ambaye alikuwa akichezea nafasi ya kiungo katika timu yake ya Kahama United na kuwa tishio kwa timu nyingine za mkoa huo.
 
Alisema wamechukua uhamuzi huo wa kusajili nafasi hiyo moja ya kiungo baada ya kukaa chini na kamati ya ufundi wa timu hiyo na kuweza kubaini kulikuwepo na pengo katika mechi zake za mzunguko wa kwanza wa ligi hiyo kutokana na mchezaji anayechezea nafasi hiyo, Patrick Batweri kusumbuliwa  na maumivu ya mara kwa mara ya kifundo cha mguu.
 
Alieleza usajili huo wa kinda hilo umepelekea timu yao kukamilika kila idara zake na kuwataka wapenzi wa soka wa mkoa wa Ruvuma wawe na matumaini ya kuvuka ungwe hiyo na kucheza tisa bora na hatimaye kucheza ligi kuu ya Bara msimu ujao
 
Alisema moyo wa matumaini hayo yamekuja kufuatia uwezo mkubwa aliouonyesha kinda huyo wa kuweza kumiliki nafasi hiyo ya kiungo ambao anauonyesha katika mazoezi na kuwa kivutio kwa watazamaji wanaofurika kushuhudia mazoezi yao yanaendelea kwenye uwanja wa Majimaji mjini hapa.
 
Mlale JKT katika mchezo wake wa kwanza duru la mzunguko wa pili wamepangwa kukutana na ndugu zao Majimaji kabla ya kucheza na Small Boys ya Rukwa na mchezo wake wa tatu itasafiri na kwenda  kukutana na Maafande a Polisi Iringa, kabla ya kurudi nyumbani na kuzisubili timu za Mbeya City na Prisons ya Mbeya.
 
MWISHO.

MDAHALO JIMBO LA SONGEA MJINI WAMALIZIKA MCHANA HUU KATIKA UKUMBI WA CHUO CHA UALIMU CHA MATOGORO SONGEA

 Washiriki wa Mdahalo huo wakiendelea kusikiliza hoja mbalimbali
 Dereva wa Sonngo Shilingi kushoto akiwa na Mjumbe wa Roa Venas Komba
 Katibu wa Mbunge wa Jimbo la Songea Mjini akijibu hoja mbalimbali zilizoelekezwa kwenye ofisi ya Mbunge
 Mratibu wa MVIWATA mkoa wa Ruvuma Bigambo Ladslaus akieleza jambo wakati wa mdahalo
 Mtoa Mada Oddo Hekela akiwasilisha mada kwenye mdahalo huo
 Katibu wa Sonngo Mathew Ngarimanayo akifafanua jambo wakati wa Mdahalo huo
Mtoa Mada Bashiru Mgwasa akiwasilisha mada ya umuhimu wa viongozi na wajibu wa wananchi

MDAHALO JIMBO LA SONGEA MJINI WAENDELEA CHUO CHA UALIMU SONGEA

 Kushoto ni Mwandishi wa Radio Maria Songea,Julius Konala,Mwandishi wa Gazeti la Majira Crecensia Kapinga
 Mtaalamu wa ICT wa Asasi ya Sonngo Boniface Bundala akifuatilia Mdahalo wa wananchi wa Jimbo la Songea unaofanyika kwenye ukumbi wa Chuo cha Ualimu Songea
 Washiriki wakiendelea kufuatilia Mdahalo huo
Wa kwanza kutoka kushoto Dereva wa Sonngo Bucard Mkuwa (Maarufu kwa jina la SHILINGI) wa pili ni Mtoa huduma wa watoto HBC wa Asasi ya Roa na Mwanaharakati na Mtaalamu wa Zana za Kilimo Wilaya ya Songea Venas Komba,wa tatu ni Mkurugenzi wa Asasi Rumed David Kakoyo
Wa kwanza kutoka kulia ni Katibu Muhtasi (Msaidizi wa Ofisi) wa Sonngo Sophia Limbuya akizungumza jambo na Mtaalum wa ICT wa Asasi ya Sonngo Boniface Bundala

WANANCHI JIMBO LA SONGEA MJINI WAANZA MDAHALO WA WAZI WENYE LENGO LA KUPATA TASWIRA YA UWAJIBIKAJI WA VIONGOZI KWA WANANCHI WAO

Mwenyekiti wa Mtandao wa SONNGO Siwajibu Gama akifungua Mdahalo,wa kwanza kutoka kulia Katibu wa Mbunge wa Jimbo la Songea Mjini Andrew Chatwanga,wa pili Mkurugenzi wa Halmashauri ya Manispaa ya Songea Nachoa Zakaria,wa kwanza kutoka kushoto Katibu wa Sonngo Mathew Ngarimanayo,wa pili ni Meya wa Manispaa ya Songea Charles Mhagama

Kutoka kushoto Afisa Kazi Ruvuma Oddo Hekela,Diwani wa Kata ya Matarawe James Makane,Diwani wa Viti maalum Genfrida Haule

Wakuu wa Idara wa Halmashauri ya Manispaa ya Songea wakifuatilia Mdahalo

ABAKWA NA WATU WATANO NA KUMSABABISHIA KIFO

Na Gideon Mwakanosya,Songea
JESHI la Polisi mkoani  Ruvuma linawasaka watu watano wasiofahamika wakazi wa eneo la Lilambo Manispaa ya Songea kwa tuhuma za kuvamia  na kuingia ndani ya nyumba  kisha kumbaka Mwanamke  mwenye umri wa miaka 20  kwa kupokezana wakati akiwa amelala  na kumsababishia Kifo.
Akizungumza na waandishi wa habari jana ofisini kwake kamanda wa Polisi mkoani Ruvuma Michael Kamuhanda  alisema kuwa tukio hilo lilitokea juzi  majira ya saa nne usiku  kata ya Lilambo nje kidogo ya mji wa Songea.
Amesema,Inadaiwa siku ya tukio  majira ya saa nne usiku watuhumiwa hao walifanya kitendo hicho cha kinyama  na kumsababishia maumivu makali  sehemu nyeti  marehemu  ambaye hata hivyo jina lake limehifadhiwa .
Ameeleza zaidi  kuwa  watuhumiwa hao  inadaiwa baada ya kumfanyia kitendo cha unyama mwanamke huyo walimchukua  toka nyumbani kwake na kwenda kumtupa nje ya nyumba kwenye shamba la migomba  ambapo watu waliokuwa wakipita kwenye eneo hilo walishituka kuona mwili wa marehemu ukiwa umelazwa  katika shamba hilo.
Amefafanua zaidi kuwa mara baada ya wananchi wa kata hiyo kuona mwili huo walitoa taarifa kwa viongozi wa  serikali ya kata  ambao ndio waliotoa taarifa kwenye kituo kikuu cha polisi cha Songea , na kuwa askari polisi wakiwa wameongozana na daktari walifika katika eneo la tukio na kuuchukua kwa ajili ya uchunguzi zaidi ambapo waligundua kuwa sehemu zake za siri zinamchubuko.
Kamanda Kamuhand amesema kuwa wakati Polisi wanaendelea kuwasaka watuhumiwa  bado  inaendelea kufanya uchunguzi zaidi kuhusiana na tukio hilo.
Mwisho.