About


Karibu ujiunge na chuo cha kisasa cha Easy Tech.Computer kwa mafanikio yako,Walimu waliobobea katika fani hiyo wanapatikana chuoni hapo

elimak

elimak

Pages - Menu

Monday, August 15, 2011

Diwani wa Kata ya Mshangano Faustin Mhagama akitoa tamko la wananchi wa kata hiyo kuhusu kumtaka Mkurugenzi wa Halmashauri ya Manispaa ya Songea kuiruhusu Kampuni ya ARDHI PLAN ipime maeneo ya wananchi mshangano




WANANCHI WATANGAZA MGOGORO MKUBWA WA ARDHI SONGEA
Na Stephano Mango,Songea

WANANCHI zaidi ya 1200 wa Kata ya Mshangano Halmashauri ya Manispaa ya Songea mkoani Ruvuma wameitaka Halmashauri ya Manispaa ya Songea  kurasimisha mali zao kwa kuiruhusu Kampuni ya Ardhi Plan  iwapimie viwanja na makazi walioanza kuyaendeleza kiholela.

Wakizungumza kwenye mkutano wa hadhara wa wananchi wa kata hiyo ambao chini ya uenyekiti wa Diwani wa Kata hiyo Faustine Mhagama walisema kuwa kata yao imekumbwa na mgogoro mkubwa wa ardhi baina ya wananchi wa eneo hilo na Halmashauri ya Manispaa ya Songea

Mkutano huo ambao pia ulihudhuriwa na madiwani mbalimbali na viongozi wa serikali uliofanyika jana kwenye viwanja vya ofisi ya kata  waliohudhuria wengi wao wakiwa wanawake walisema kuwa kwa muda mrefu wamekuwa wakipata usumbufu mkubwa kurasimisha mali zao na kupata hati miliki za maeneo yao ili waweze kufanya kazi za kujipatia kipato na kukuza uchumi wao kutokana na urasimu wanaofanyiwa na Idara ya mipango miji ya Manispaa hiyo

Walisema kuwa maeneo yao wanataka kuyaendeleza kwa kuyafanyia shughuli mbalimbali za kiuchumi lakini hawajapimiwa na wala hayana hati hivyo wananchi kwa kushirikisha serikali zao za mitaa na kata hiyo kwa mamlaka iliyokuwa nazo ziliamua kuitafuta kampuni na kuweka michoro stahiki ya eneo hilo na kuiwasilisha kwenye Halmashauri hiyo ili waweze kupimiwa ardhi yao.

Anastasia Ndumbaro mkazi wa kata hiyo alisema kwa uchungu mkubwa huku akidondosha machozi kuwa wanasikitika kwa kitendo cha Manispaa ya songea kukwamisha zoezi hilo.
“tunasikitika kwa kitendo cha kuizuia kampuni kutupimia viwanja vyetu kwani tumekuwa tukihitaji sana kurasimishiwa maeneo yetu ili tuyaendeleze,”alisema Ndumbaro.

Ndumbaro alisema kuwa familia yake ina mashamba ya ekari 10 katika eneo hilo na Baba yake alifariki toka mwaka 1992 ambako amekuwa akifuatilia idara ya mipango miji ili iweze kumpimia viwanja hivyo na kugawana na ndugu zake mirathi lakini amekuwa akiyumbishwa hadi leo hii.

Naye Mwenyekiti  wa mkutano huo Diwani  Faustine Mhagama akifunga mkutano huo alisema kuwa amesikiliza kwa umakini kilio cha wapiga kura wake na matamko mbalimbali waliyoyatoa na kwamba anawaunga mkono.

Mhagama alisema atayawakilisha maazimio ya mkutano huo kwa maandishi  kumtaka Mgurugenzi wa Halmashauri ya Manispaa ya Songea Zakaria Nachoa kukaa na kuutazama mpango huo mzuri wa wananchi wa kata hiyo na kuiruhusu kampuni hiyo iwapimie wananchi maeneo yao.

Alifafanua zaidi kuwa ardhi hiyo ni mali ya wananchi wa kata hiyo na wao wameitaka kampuni iwapimie maeneo yao ili waweze kufanya shughuli zao za kukuza uchumi na kwamba kampuni kwa kushirikiana na viongozi wa mitaa yote ya kata hiyo walifanya mikutano na wananchi walipeleka taarifa kwenye mamlaka husika bila kupata majibu kwa wakati ambapo sheria inatamka muda wa majibu ukichelewa ina maanisha mpango umekubaliwa

Alieleza zaidi kuwa Kampuni hiyo imekubali kuwapimia wananchi maeneo yao ili kurasmisha mali zao na kuendeleza makazi holela waliyonayo, kuweka alama maeneo hayo, kuwatafutia wananchi hati za kumiliki maeneo yao,kuchonga barabara za eneo hilo kwa gharama nafuu kwa lengo la kuharakisha maendeleo kama masterplan inavyoelekeza.
 “Tunamtaka Mkurugenzi ndani ya siku saba airuhusu kampuni kuendelea na kazi iliyoelekezwa na wananchi endapo atakaidi agizo hilo wananchi wataamua vinginevyo ikiwa ni pamoja na kufanya maandamano ya amani ili kushinikiza Mgurugenzi na Afisa Mipango miji waondolewe kwenye nafasi zao na kumpeleka mahakamani,” lilisema azimio hilo.

Mwisho.

Mkuu wa Mkoa wa Ruvuma Dkt Christine Ishengoma akimpongeza Mmiliki wa Blog hii Ndugu Stephano Theofrida Mango mara baada ya kupewa Tuzo ya Mwanahabari bora wa Utalii na Maliasili Tanzania katika sherehe za kitaifa za Tamasha la Kumbukizi la Kihistoria la MASHUJAA wa vita vya MAJIMAJI Februari 27,2011na Waziri wa Maliasili na Utalii Ezekiel Maige katika viwanja vya Mashujaa Mjini Songea

Kutoka kushoto ni Diwani wa kata ya Seedfarm Chistiani Matembo,Mkuu wa Wilaya ya Songea Thomas Oley Sabaya,Katibu wa CCM mkoa wa Ruvuma Emmenual Mteming'ombe,Chifu wa Wangoni Emmanuel Zullu, Aliyekuwa Katibu Mkuu Wizara ya Maliasili na Utalii Dkt Ladislaus Komba

Naibu Meya wa Halmashauri ya Manispaa ya Songea akiwa kwenye moja ya vikao vya Baraza la Madiwani wa Halmashauri hiyo akifuatilia vikao kwa umakini mkubwa kabla ajakutana na kindumbwedumbwe cha kukatisha uwepo wake kwenye kiti hicho kwenye kikao kilichofuata

DIWANI WA KATA YA RUVUMA,HALMASHAURI YA MANISPAA YA SONGEA VICTOR NGONGI AKITOA UFAFANUZI WA KANUNI KATIKA KIKAO CHA BARAZA LA MADIWANI KILICHOFANYIKA HIVI KARIBUNI KATIKA UKUMBI WA CHAMA CHA WALIMU MAJENGO








NAIBU MEYA SONGEA CHUPUCHUPU AFUKUZWE KUONGOZA KIKAO
Na Stephano Mango,Songea
MADIWANI wa Halmashauri ya Manispaa ya Songea walitofautiana kwa muda wa zaidi ya saa moja kwa kutaka kumuondoa Naibu Meya wa Manispaa hiyo Mariam Dizumba  kwa madai kuwa muda wake wa uongozi umekwisha

Wakichangia hoja mbalimbali Madiwani hao katika kikao cha Baraza la Madiwani kilichofanyika jana kwenye ukumbi wa Saccos ya Walimu wa Manispaa ya Songea ambacho kilikuwa kinaongozwa naye walimtaka Naibu huyo aondoke kwenye kiti chake ili uchaguzi wa Naibu Meya ufanyike

Diwani wa kata ya Ruhuwiko Gerald Ndimbo alisema katika kikao hicho kuwa kabla ya kuendelea na kikao ni vema madiwani tukapata ufafanuzi juu ya kikao kama ni kikao cha kawaida au ni kikao cha mwaka ambapo katibu wa kikao hicho ambaye ni Mkurugenzi wa Manispaa hiyo Nachoa Zakaria alijibu kuwa ni kikao cha kawaida

Ndipo Diwani wa Kata ya Ruvuma Victor Ngongi alipoingilia kati kwa kutoa ufafanuzi juu ya kanuni za kudumu za mikutano na shughuli za Halmashauri namba 6 ambayo ilifanyiwa marekebisho mwaka 2005

Ngongi alieleza zaidi kuwa kanuni tajwa inasema kuwa kama ni mkutano wa kawaida basi agenda ya ratiba ya vikao mbalimbali vya Halmashauri iondolewe kwani agenda hiyo inaambatana na mambo makuu manne

Alisema kuwa mambo hayo ni pamoja na uchaguzi wa Naibu Meya,kuteua wajumbe wa kamati mbalimbali za kudumu, kujadili taarifa ya utendaji na uwajibikaji kwa mwaka uliopita na ratiba ya vikao

“Kutokana na mabadiliko hayo ya mwaka 2005,vikao vyote vya mwaka vinaishia mwezi juni ambapo mwezi julai tunaanza mwaka mpya wa fedha na uchaguzi wa unaibu meya na kamati zake zinatakiwa ziwe sambamba na mwaka wa fedha”alieleza Ngongi

Ngongi alimtaka Mkurugenzi wa Manispaa hiyo aliombe radhi baraza kwa kukiuka kanuni na kuwasumbua madiwani bila sababu za msingi kuelezwa kabla

Akifunga kikao hicho Naibu Meya Mariam Dizumba alioneka kuwa na hasira na kutamka kuwa kama madiwani wana roho ya kwanini waendelee kusubiri muda wa uchaguzi utakapofika
MWISHO