About


Karibu ujiunge na chuo cha kisasa cha Easy Tech.Computer kwa mafanikio yako,Walimu waliobobea katika fani hiyo wanapatikana chuoni hapo

elimak

elimak

Pages - Menu

Thursday, September 22, 2011

AZALIWA AKIWA NA UVIMBE KICHWANI NA KUPELEKWA KATIKA HOSPITAL YA MKOA WA SONGEA KWA AJILI YA MATIBABU ZAIDI

 Asante Umbulu mwenye umri wa miezi 3 akiwa amelazwa katika Hospital ya Mkoa ya Songea kwa ajili ya kupata matibabu ya uvimbe wa kichwa,mtoto huyo anatakiwa kupelekwa katika Hospital ya Taifa ya Muhimbili kwa ajili ya matibabu kwani katika Hospital ya Mkoa ya Songea haiwezi kumfanyia Operesheni kutokana na kukosekana kwa vifaa na wataalamu wenye vigezo stahiki

Mtoto huyo anahitaji msaada wa kufika Jijini Dar es Salaam na kupatiwa matibabu,yeyote anayetaka kumsaidia mtoto huyo aende katika Hospital ya Mkoa wa Songea na aonane na DKT NGAIZA kwa maelezo zaidi au piga simu 0755-33 50 51utaunganishwa na Dkt Ngaiza


Waandishi wa habari wakizungumza na mama wa mtoto Asante Umbulu katika Hospital ya mkoa wa Songea,Martina Nombo,kutoka kushoto ni mwandishi wa gazeti la Mwananchi,Joyce Joliga,katika ni Cresencia Kapinga mwandishi wa gazeti la Majira

Mtandao huu wa http://www.stephanomango.blogspot.com/ unatoa pole kwa familia ya Martina Nombo kwa kumuuguza mwanao Asante Umbulu

Maskini mtoto IVVO PONERA anavyoteseka baada ya kuungua moto shambani baada ya kibanda alimukuwepo kuungua moto


 
 Mtoto IVVO PONERA mwenye umri wa mwaka mmoja akiwa amelazwa katika Hospital ya mkoa wa Songea baada ya kufikishwa Hospital hapo akitokea kijijini kwao Mchomolo Wilayani Namtumbo,

Mama wa mtoto huyo Paulina Lwambo akizungumza na mtandao huu wa http://www.stephanomango.blogspot.com/ katika hospital hiyo alisema kuwa IVVO alikuwa analelewa kwenye kibanda shambani na kaka yake aitwaye Jackson Ponera wakati yeye anaendelea na shughuli za kuvuna mahindi

Alisema kuwa katika kibanda hicho alikuwa amepika chakula ili waweze kujipatia mlo baada ya kumaliza kuvuna,ghafla akasikia mwanaye Jackson anamwita huku akisema kibanda kinaungua moto

"Niliacha kuvuna na kukimbilia kwenye kibanda na kukuta kibanda kinaungua na mtoto IVVO yupo ndani,nilichanganyikiwa lakini nilifanikiwa kumuokoa akiwa ameharibika mwili wake kwa kuungua"alisema Lwambo

Alieleza zaidi kuwa nilimchukua kwa umakini mkubwa na kumleta hapa Hospital kwa ajili ya matibabu na anaendelea vizuri na matibabu

MTOTO AZALIWA NA UVIMBE KICHWANI,WENGI WANASEMA HUENDA ANA VICHWA VIWILI

Na Stephano Mango ,Songea

Martina Nombo (27) mkazi wa kijiji cha Lulambo Wilayani Mbinga Mkoani Ruvuma amejifungua Mtoto wa kike ambaye anadaiwa kuwa na vichwa viwili ameomba msaada kwa watu wenye uwezo wamsaidie wakiwemo wataalam wa upasuaji wa Kichwa wamsaidie kuhokoa maisha ya Mwanaye.

Akizungumza na mtandao huu wa www.stephanomango.blogspot.com  katika wodi namba tano  ambapo amelazwa na Mwanaye huyo hospitali ya Mkoa wa Ruvuma jana mara baada ya  kupata rufaa kutoka hospitali ya  Mbuyula iliyopo Wilaya ya Mbinga

 Mama wa Mtoto huyo amesema, alijifungua salama  kwa njia ya kawaida mapema  9 juni mwaka huu katika hospitali ya Mbuyula ambapo mara baada ya kukabidhiwa mwanaye na wauguzi aligundua kuwepo kwa tatizo hilo na aliwaarifu nao walimweleza kuwa aendelee kuwa na subira.

Amesema, tangu alipojifungua katika hospitali ya Mbuyula kichwa cha mtoto waki kilizidi kukua na kutengeneza kitu kama uvimbe ambapo mtoto  aliendelea kutibiwa hospitalini hapo hadi madaktari walipompatia rufaa ya kumwamishia  katika hospitali ya mkoa jana  kwa ajili ya matibabu zaidi.

Kwa upande Daktari Bingwa wa upasuaji wa hospitali hiyo Hassan Lumbe amesema, picha ya  X-ray imeonyesha kuwa ndani ya kichwa kuna shimo ambalo linasababisha ubongo utoke na kuingia kwenye  uvimbe ,pia mifupa ya kichwa aijajiunga vizuri.

Amesema,upasuaji wa mtoto huyo katika hospitali hiyo hauwezi kufanyika  kutokana na kutokuwa na vifaa  na utaalamu walionao hawakidhi viwango vya kutoa tiba kwa mtoto huyo hivyo wanamrufaa kwenda muhimbili .

Amesema,kesi kama hizo ni chache kuripotiwa katika Hospital hiyo na kwamba wao walimpokea  baada ya kupewa rufaa toka katika hospitali aliyozaliwa ya  Mbinga  nao wanatarajia kumpatia rufaa kwenda hospitali ya taifa ya  Mhubili kwani wamefanya vipimo na vimeonyesha kuwa opelesheni hiyo haiwezi kufanywa hapo na wanachofanya ni kuandaa rufaa pamoja na fedha kidogo ya kumsaidia kumsafirisha Mama huyo na Mwanaye.

Mwisho.



WATATU WAFIKISHWA MAHAKAMANI KWA KUITAPELI BENKI YA NMB

Na Gideon Mwakanosya, Songea
WATU watatu wamefikishwa Mahakamani  kwa kosa la kula njama na kutenda kosa la jinai  la kufanya udanganyifu  na kujipatia mkopo wa fedha toka  katika Benki ya NMB tawi la Songea Mkoani Ruvuma .

Wakisomewa shitaka hilo jana na  Hakimu mkazi Mfawidhi Mwandamizi Baptisti Mhelela amesema,washitakiwa  wote kwa pamoja walitenda  kosa hilo  kati ya oktoba 22 mwaka 2008 na desemba  5 mwaka 2010 .

Amesema,katika kosa la pili mshitakiwa namba moja Cosmas Haule (35) anashitakiwa peke yake kwa kujipatia mkopo wa fedha   shilingi milioni arobaini kwa udanganyifu  kati ya kipindi hicho hicho cha oktoba 22 mwaka 2008 na 5 desemba 2010 na aliposomewa kosa alikana.

Amesema,mshitakiwa Cosmas yupo nje kwa dhamana  na  ametoa hati ya nyumba na dhamana ya mali isiyo hamishika yenye thamani ya shilingi milioni kumi pamoja na dhamana ya milioni 15  kesi hiyo inatarajiwa kutajwa septemba 30 mwaka huu,upelelezi bado haujakamilika.

Katika kosa la tatu,Mshitakiwa namba tatu Asha Banda (35) anashitakiwa kwa kosa la kujifanya  mmiliki wa nyumba namba 22 kitalu L L Mateka B wakati ilikuwa siyo jambo la kweli na kubadili jina kuwa anaitwa Consolata Alphonce Soko .

Inadaiwa kuwa mshitakiwa alitenda kosa hilo kati ya tarehe hizo hizo  oktoba 22 ,2008 na 5 desemba 2010 katika benki ya NMB tawi la Songea.

Mshitakiwa amekana shitaka na yupo nje kwa dhamana ya shilingi milioni tano ,na mshitakiwa namba 2 Onesmo Soko  naye yupo nje kwa dhamana  ya milioni tano.
Mwisho.

CHADEMA WAKATAA KUSIMAMISHA MGOMBEA UMEYA SONGEA





                                     Katibu wa Chadema Jimbo la Songea Masumbuko Paulo
CHAMA cha Demokrasia na Maendeleo(Chadema) wilaya ya Songea  kimemuandikia barua Mkurugenzi wa Halmashauri ya Manispaa ya Songea kuhusu dhamira ya chama hicho kutosimamisha mgombea wa nafasi wazi ya Mstahiki Meya wa Manispaa hiyo kutokana na mizengwe na ghiliba zinazofanywa na Mkurugenzi huyo

Akizungumza na waandishi wa habari jana katika ofisi za Chama hicho zilizopo kata ya Mfaranyaki Katibu wa Chadema Jimbo la Songea Masumbuko Paulo alisema kuwa Chama chake kimeamua kutosimamisha mgombea wa kuziba nafasi hiyo kutokana na mizengwe mingi inayoendelea katika harakati za uchaguzi huo

Paulo alisema kuwa Viongozi wa Chadema wamekutana na kutoa msimamo wao kuhusu muenendo huo na kuamua kumjulisha Mkurugenzi wa Manispaa kuwa Chadema hakitasimamisha mgombea katika uchaguzi wa Septemba 23 mwaka huuu

Alisema kuwa Chadema kimemtaka Mkurugenzi wa Halmashauri ya Manispaa ya Songea kutopindisha kanuni na sheria kwa maslahi ya Chama Cha Mapinduzi alivyofanya katika uchaguzi uliopita wa kumpata Meya

“Chama kinakukumbusha kufuata kanuni ili kuondoa migongano isiyo ya lazima tena tunamtaadharisha kutoegemea kwa upande mmoja kama unavyofanya sasa”alisema Paulo

Mtandao huu umefanikiwa kuipata barua hiyo ya tarehe 21 Septemba 2011 iliyoenda kwa Mkurugenzi wa Halmashauri ya Manispaa ya Songea yenye kumbukumbu namba CH/SMJ/RV/18 yenye kichwa cha habari “Taarifa ya kutosimamisha mgombea wa nafasi wazi ya Mstahiki Meya Manispaa”

Sehemu ya barua hiyo inasomeka “….uchaguzi uliopita wa aina hii haukuwa huru na haki kwani mazingira ya kupiga kura hayakuwa ya siri wala hukuandaa eneo la siri la mtu kupiga kura badala yake ulifanya wajumbe wapiga kura wapige kura ya wajumbe iwe inaonekana kwa wazi tu”

Katika mkutano huo na waandishi Paulo alisema kuwa Chadema ina madiwani 7 ambapo Chama cha Mapinduzi (Ccm) ina madiwani 20 na wabunge wawili kwa maana ya mbunge wa Jimbo la Songea Mjini Dkt Emmanuel Nchimbi,na Mbunge wa Viti Maalum Mkoa wa Ruvuma Devota Likokola na kufanya kuwa Ccm iwe na Madiwani 22

Katika uchaguzi huo Ccm imemsimamisha Diwani wa Kata ya Matogoro Charles Mhagama kutokana na Chadema kutomsimamisha mgombea wa kuziba nafasi wazi ya Meya wa Manispaa kunamfanya Charles Mhagama kuwa mgombea pekee wa nafasi

Uchunguzi uliofanywa na mtandao huu umebaini kuwa watu wengi hawajaridhiki na kitendo cha Ccm  kumpitisha Charles Mhagama kuwa mgombea Umeya kutokana na nafasi hiyo kuwa nyeti katika kusukuma mbele gurudumu la maendeleo
Imebainika kuwa baadhi ya madiwani wa Ccm wanamkakati kabambe wa kumpigia kura za hapana mgombea wao ili uchaguzi uhitishwe upya kutokana na Charles Mhagama kutokuwa na mahusiano mazuri na madiwani wezake na kuonekana sio chaguo stahiki

Akizungumza na mtandao huu wa http://www.stephanomango.blogspot.com/ Mkurugenzi wa Halmashauri ya Manispaa ya Songea Nachoa Zakaria alikiri kupokea barua ya Chadema na kueleza kuwa kanuni zinaruhusu kufanya uchaguzi ambapo kutakuwa na kura ya ndiyo au hapana

Zakaria alisema kuwa ikiwa wajumbe therusi mbili wakipiga kura za hapana uchaguzi huo utaitishwa upya kwa mujibu wa kanuzi za uchaguzi wa nafasi hiyo ya umeya na kuongeza kuwa uongozi anatoa Mungu na kwamba Halmashauri hiyo inahitaji apatikane Meya na ipo siku atapatikana

Alisema kuwa katika uchaguzi huo atasimamia kikamilifu kanuni na sheria za uchaguzi kwa maslahi ya Halmashauri na wananchi na kudai kuwa madai ya Chadema katika barua yao sio ya msingi kwa kuwa wanalalamikia kitu kilichopita badala ya kuzungumzia uchaguzi uliopo

Uchaguzi huo unafanyika kuziba pengo lililoachwa wazi na marehemu Ally Said Manya aliyefariki Julai 29 mwaka huu katika hospitari ya Misheni ya Peramiho baada ya kuugua muda mrefu maradhi ya moyo na kisukari

AWALI Chadema walimcharukia mgombea wa nafasi ya Umeya wa Halmashauri ya Manispaa ya Songea kupitia Chama cha Mapinduzi(Ccm) Charles Mhagama kwa madai kuwa sio kiongozi makini na muadilifu anayeweza kulisukuma mbele gurudumu la maendeleo kwa maslahi ya wananchi

Akihutubia mamia ya wakazi wa Manispaa ya Songea  hivi karibuni katika viwanja vya soko la Manzese,kata ya Misufini Mwenyekiti wa chama hicho Mkoa wa Ruvuma Joseph Fuime alisema kuwa nafasi ya Umeya ni nafasi nyeti sana katika Halmashauri ya Manispaa ya Songea hivyo ina hitaji mtu makini na muadilifu wa kuweza kushirikiana na wadau mbalimbali kuweza kulisukuma gurudumu la maendeleo

Fuime alisema kuwa kutokana na umuhimu huo mgombea aliyepitishwa na Chama cha Mapinduzi (Ccm)Charles Mhagama ili kuweza kuziba nafasi ya Umeya iliyoachwa wazi na Marehemu Ally Manya aliyefariki mwezi julai 29 mwaka huu,kuwa hana uwezo wa kushika nafasi hiyo kutokana na kujaa tamaa ya kujitajirisha kiharamu kupitia fedha za wananchi

Alieleza kuwa Mhagama ni kiongozi mbabe na mwenye kupenda rushwa hali inayodhorotesha maendeleo ya wananchi kwani alishawahi kufanya vitendo viovu ikiwa ni pamoja na kuwepo kwa ushawishi wa rushwa katika ununuzi wa gari ya kuzima moto,uuzwaji wa Katapila la Halmashauri akiwa ni Diwani wa kata ya Matogoro na kiongozi wa Kamati mbalimbali za baraza la madiwani

“Mhagama hawezi kuwa kiongozi bora na atakayeweza kutupeleka kwenye ustawi stahiki wa maisha kwani vitendo vyake vingi ni viovu kwani kuna kipindi alikuwa na mahusiano na mwanafunzi mmoja miaka ya nyuma ambapo alikutwa naye kwenye nyumba ya wageni na wazazi wa mwanafunzi huyo na kupelekewa kupigwa viboko hadharani”alieleza Fuime

Alifafanua kuwa vitendo hivyo vinadhihirisha ni jinsi gain alivyokuwa mchafu na kiongozi mbovu asiyestahili kupewa majukumu makubwa ya Umeya hasa katika kipindi hiki kilichogubikwa na ufisadi,rushwa na urasimu mkubwa Serikalini

Alisema kuwa siku zote Chama cha Mapinduzi kimekuwa kikiwaacha viongozi wazuri na kuwateua viongozi wabovu ili waweze kukinufaisha chama kwa maslahi yao binafsi hivyo hatuwezi kuongozwa na kiongozi wa aina hiyo na ndio maana tunapaza sauti ili umma ujue na kuwaambia Madiwani wao waliowachagua kutokumpigia kura mgombea huyo wa Ccm kwenye uchaguzi wa Serikali unaotegemewa kufanyika Septemba 23 mwaka huu na kuongeza pia Halmashauri ya Manispaa ya Songea ni mali ya wananchi wote na sio mali ya kikundi cha watu wachache wenye malengo yao binafsi
MWISHO