About


Karibu ujiunge na chuo cha kisasa cha Easy Tech.Computer kwa mafanikio yako,Walimu waliobobea katika fani hiyo wanapatikana chuoni hapo

elimak

elimak

Pages - Menu

Wednesday, October 19, 2011

JAMAA AINGIA CHOONI NA KUSHANGAA KUMUONA MTENDAJI AKININ'GINIA KWENYE PAA LA CHOO BAADA YA KUJINYONGA

Na Gideon Mwakanosya, Songea

AFISA Mtendaji wa Kijiji cha Ngahokola kilichopo katika Kata ya Magagula Wilaya ya Songea Vijijini Mkoa wa Ruvuma Cremence Mbogoro (48) amekutwa amekufa kwa kujinyonga kwa kutumia shuka ambalo alikuwa amelifunga shingoni na kujining’iniza kwenye mti wa boriti wa paa la choo cha nyumba yake.

Akizungumza na Mwandishi wa mtandao wa http://www.stephanomango.blogspot.com/ Gideon Mwakanosya Ofisini kwake kaimu Kamanda wa Polisi Mkoa wa Ruvuma Naftari Mantamba amesema kuwa tukio hilo limetokea octoba 18 majira ya saa nne asubuhi huko kwenye eneo la Choo cha nyumba yake.

Amesema kuwa inadaiwa siku hiyo ya tukio Mbogoro alikutwa akiwa ananing’inia juu kwenye paa la choo na mtu mmoja ambaye alikwenda kutaka kujisaidia akiwa amejinyonga kwa kutumia shuka ambalo alijifunga shingoni.

Amefafanua zaidi kuwa mtu huyo aliyekuwa ameomba kwenda kujisaidia baada ya kugundua tukio hilo alitoa taarifa kwa majirani ambao walifika kwenye eneo la tukio na kumkuta Afisa Mtendaji wa Kijiji hicho Mbogoro akiwa ananing’inia chooni baada ya kujinyonga.

Ameelezwa zaidi kuwa baada ya tukio hilo kufahamika kwa majirani uongozi wa Serikali ya Kijiji cha Ngahokola ulitoa taarifa polisi juu ya tukio hilo ambapo askari polisi pamoja na daktari walifika kwenye eneo la tukio na kuukuta mwili wa Afisa Mtendaji wa Kijiji hicho Mbogoro ukiwa unaning’inia baada ya kujinyonga kwa kutumia shuka ambalo alikuwa amejifunga shingoni na kujining’iniza kwenye boriti ya mti wa  choo ambao ulikuwa umewekwa kwenye paa.

Mantamba ameeleza zaidi kuwa chanzo cha tukio hilo bado kinachunguzwa licha ya kuwa uchunguzi wa awali wa polisi umebaini kuwa Afisa Mtendaji wa Kijiji cha Ngahokola Mbogoro kabla hajafikia uamuzi wa kujiua kwa kujinyonga alikuwa akimlalamikia mwajiri wake kuwa kwanini anashindwa kumuhamisha kwenye Kijiji hicho kwakuwa hapo awali alikuwa ameomba kuhamia Kijiji cha Igawisenga ambako ndiyo nyumbani kwake alikozaliwa.

Hata hivyo uchunguzi huo pia umebaini kuwa Mbogoro akiwa kama Afisa Mtendaji wa Kijiji hicho anadaiwa kuwa alikuwa amewachangisha wananchi fedha kwa ajili ya ujenzi wa daraja fedha ambazo idadi yake haifahamiki na zinasadikiwa kuwa zimeliwa jambo ambalo lilimfanya alazimike kumuomba mwajiri wake kuhama kwenye Kijiji hicho bila kuwa na mafanikio na polisi bado inaendelea kufanya upelelezi zaidi kuhusiana na tukio hilo.
MWISHO  

MWAMBUNGU AWATAKA WANANCHI KUHESHIMU HAKI ZA BINADAMU

                                       Mkuu wa Mkoa wa Ruvuma Said Mwambungu
Na Stephano Mango,Mbinga
WANANCHI Wilayani Mbinga mkoani Ruvuma wametakiwa kuheshimi haki za binadamu kwa kuzingatia kanuni,taratibu na sheria ili kila mtu aweze kuishi kwa amani na upendo katika jamii yake na nchi kwa ujumla
Wito huo umetolewa jana kwenye Viwanja vya Magereza Kitai na Mkuu wa Mkoa wa Ruvuma Said Mwambungu mara baada ya kupokea taarifa ya maendeleo ya Halmashauri ya Wilaya ya Mbinga iliyosomwa na Mkurugenzi wa Halmashauri hiyo Shaib Mnunduma
Mwambungu ambaye yupo kwenye ziara ya kikazi ya siku moja Wilayani Mbinga alisema kuwa kila siku ninaposoma taarifa ya maendeleo ya mkoa nakutana na taarifa ya vifo vya kujinyonga,kupigana,kuchinjana kutokanana  na mahusiano ya kimapenzi na matatizo mengine ya kijamii na kwamba takwimu za vifo vingi vinatoka Wilaya ya Mbinga
“Nasikitishwa sana na taarifa hizo kwani mtu unayempenda huwezi kumuua kwa sababu za kukunyima penzi au kumkuta mpenzi wako na mwanaume mwingine au na mwanamke mwingine hivyo kama kweli unampenda utamlinda na vishawishi vinavyoweza kupunguza upendo wake kwako na sio kumuua”alisema Mwambungu
Alisema kuwa haki ya kuishi ni haki kubwa kuliko zote na kwamba hakuna mtu mwenye mamlaka ya kuondoa uhai wa mwenzake kwa sababu yoyote ile kwani mwenye uwezo na mamlaka hayo ni mwenyezi mungu pekee yake ni vema kazi yake tukamuachia
Alisema kuwa jambo hilo halipaswi kuvumiliwa hata kidogo hivyo ni vema viongozi wa dini na wakijamii pamoja na Serikali kushirikiana kikamilifu kudhibiti jambo hilo kwani kabla vifo havijatokea kunakuwepo na dalili za kutokuwa na amani miongoni mwa wapenzi hao tujaribu kusuluhisha migogoro kwa taratibu za mila na desturi na kwamba ikishindikana basi sheria itumike kudhibiti vifo hivyo
Awali akisoma taarifa ya maendeleo ya Wilaya ya Mbinga Mkurugenzi wa Halmashauri ya Wilaya hiyo Shaib Mnunduma alisema kuwa katika mwaka wa fedha wa 2011/2012 Halmashauri imekadilia kutumia Tsh 39,600,654,467.00 kwa ajili ya kutekeleza miradi ya maendeleo na shughuli za utawala
Mnunduma alisema kuwa vipaumbele katika kutekeleza bajeti hiyo ni kuimarisha ukusanyaji wa mapato na kufikia lengo lililopangwa,kuimarisha utoaji wa huduma za afya kwa kufanya ukarabati wa Zahanati,Vituo vya Afya,Kupanua Hospitali ya Wilaya na kuhamasisha ujenzi wa Zahanati kwenye kila Kijiji
Aliitaja miradi mingine ni kuendeleza kilimo cha umwagiliaji na kuongeza uzalishaji wa mazao ya chakula na biashara,kuimarisha sekta ya mikopo kwa kuendeleza vyama vya kuweka na kukopa9Saccos),kufanikisha adhima ya kuwezesha wanafunzi wote waliofaulu elimu ya msingi kujiunga na elimu ya sekondari
Mnunduma aliongeza zaidi kuwa miradi mingine ni ya kuboresha huduma za jamii na kusaidia miradi iliyoibuliwa kwa mbinu shirikishi jamii hasa ile ya elimu,afya,kilimo,maji na barabara na kuimarisha shughuli za hifadhi ya mazingira na hasa upandaji miti,kuzuia uchomaji moto misitu na kuhamasisha kilimo cha ngoro na makinga maji
MWISHO

MKUU WA MKOA WA RUVUMA ATEMBELEA WILAYA YA MBINGA NA YA NYASA

Na Mwandishi Wetu,Songea
MKUU wa Ruvuma Said Mwambungu amefanya ziara ya siku mbili Octoba 17 na Octoba 18 mwaka huu katika Wilaya ya Mbinga na Wilaya mpya ya Nyasa na kutembelea miradi mbalimbali na kujitambulisha kwa wananchi wa maeneo hayo
Ziara hiyo ya Mwambungu siku ya kwanza alianza kwa kukagua mradi wa ujenzi wa barabara kwa kiwango cha lami kuanzia pacha ya Peramiho hadi Mbinga,kukagua ujenzi wa Zahanati ya Gereza la Kitai ambapo pia alizungumza na wananchi,kuzungumza na Watumishi wa Halmashauri ya Wilaya ya Mbinga na Wafanyakazi wa Ofisi ya Mkuu wa Wilaya
Katika ziara hiyo Mkuu wa Mkoa Mwambungu alitembelea Kijiji cha Mtupale kata ya Chiwanda na kuzungumza na wananchi ambako ilielezwa kuwa katika kijiji hicho ukiachia Wabunge na wakuu wa Wilaya waliowahi kuongoza Wilaya hiyo, kiongozi wa kwanza wa kitaifa kufika hapo ni Mkuu wa Majeshi na Ulinzi Jenerali David Mwamunyange ambapo alitembelea kijiji hicho mwaka huu na Mkuu wa Mkoa wa Ruvuma Said Mwambungu
Siku ya pili Mkuu wa Mkoa wa Ruvuma Said Mwambungu alikagua bandari ndogo ya Mbamba bay,kukagua ujenzi wa bandari ndogo ya Ndumbi ambapo pia alizungumza na wananchi,kukagua kivuko cha mto Ruhuhu(Feri ya Lituhi)na kutembelea na kukagua eneo la machimbo ya makaa ya mawe Ruanda