About


Karibu ujiunge na chuo cha kisasa cha Easy Tech.Computer kwa mafanikio yako,Walimu waliobobea katika fani hiyo wanapatikana chuoni hapo

elimak

elimak

Pages - Menu

Monday, March 3, 2014

MWANJA ; MAFANIKIO YA MBIO ZA BENDERA YAMELETA HAMASA MPYA CCM



Ni miaka minne sasa toka nilipoandika makala haya, leo kutokana na umuhimu wake naomba ndugu wasomaji wa Blog hii muweze kujikumbusha nilichokiandika na kama itawapendeza niko tayari kufanya uchambuzi mpya na wa kina kuhusu makala haya, endelea kutafakari kupitia maandisha haya 

picha nitaziweka hivi punde

MWANJA ; MAFANIKIO YA MBIO ZA BENDERA YAMELETA HAMASA MPYA CCM

Na: Stephano Mango, Songea
MIONGONI mwa kazi za chama cha siasa kilichopo Madarakani ni kuwa daraja la kuwaunganisha watu na serikali waliyoichagua katika kufanikisha ahadi zilizo ahidiwa wakati wa kampeni.

Mbali na jukumu  hilo, wajibu wa chama ni kusaidia watu kuielewa serikali yao inafanya nini kwa wakati gani na kwa lengo lipi.

Ni wajibu wa chama kutumia mbinu mbalimbali za kidemokrasia kuwahamasisha watu ili washirikiane na serikali yao ili kuwaondolea matatizo sugu ya umaskini, maradhi na ujinga ambao umewaelemea.

Chama pia kina wajibu wa kuhakikisha kuwa serikali inaendelea kuyajua maoni, shida na matakwa ya watu katika kufanikisha vita dhidi ya maadui ujinga, umaskini na maradhi.
Hata hivyo, chama kinawajibu wa kuwakemea wanachama wanaokwenda kinyume na matakwa ya kanuni na taratibu za chama.

Ingawa pia kina wajibu wa kuwaelimisha watu na wanachama wote kwa ujumla ili waweze kuona shughuli zinazofanywa na serikali yao katika kuwaletea maendeleo kusudiwa.

Hivyo basi, chama cha mapinduzi (CCM) kuelekea uchaguzi wa Serikali za mitaa mwaka huu, na mwaka 2010 katika uchaguzi wa Madiwani, Wabunge na Rais

Kimejiandaa kushinda kwa kishindo katika chaguzi hizo kwa sababu katika uwanja mpana wa siasa mwisho wa uchaguzi mmoja ni mwanzo wa uchaguzi mwingine

Na lengo kubwa la Chama chochote cha siasa katika Nchi yoyote duniani ni kushinda katika uchaguzi Mkuu na kuunda Serikali yaani kukamata dola

Kwa mantiki hiyo, Uongozi wa Chama Cha Mapinduzi Mkoa wa Ruvuma kwa kushirikiana na kamati ya Siasa ya Halmashauri Kuu ya CCM Mkoa wa Ruvuma iliamua kupeleka ujumbe kwa Wanachama na Wananchi kwa kutumia mbio za Bendera ya Chama Cha Mapinduzi

Mbio hizo za Bendera zilizinduwa rasmi Mei 28 mwaka huu wa 2009 Wilayani Tunduru katika Kijiji cha Matemanga Mkoani Ruvuma na Mwenyekiti wa CCM Mkoa wa  Ruvuma  Coleneus Msuha.

Akizungumzia malengo ya mbio hizo za Bendera Katibu wa Chama Cha Mapinduzi Mkoa wa Ruvuma Bw. Emmanuel Mteming’ombe anasema kuwa mbio za Bendera ni ngeni na kwa mara ya kwanza zimekimbizwa Mkoa wa Ruvuma na kuleta mafanikio.

Anasema malengo ya mbio hizo za Bendera ni kukifanya Chama kionekane kwa watu na kwa Wanachama, kisha kisikike na watu waonyeshe dalili ya kusikia uwepo wa Chama hicho.

Ni lazima Chama kitumie mbinu mpya katika kujipenyeza kwa Wananchi katika Siasa za ushindani ili kuweza kuwahamasisha waingie Chamani anasema Kiongozi wa Mbio za Bendera Nestory Mwanja

Mwanja anaendelea kufafanua kuwa tumeamua kukimbiza Bendera ili kuwahamasisha Wanachama wawe hai kwa kulipia ada zao za Uanachama na kuhudhuria vikao vya Chama kuanzia ngazi ya mashina, matawi, Wilaya na Mkoa. 

Mbio hizo za Bendera zimefanya kazi kubwa ya kuwaeleza Wanachama wote ujumbe kutoka Halmashauri Kuu ya CCM Taifa NEC kuhusu mabadiliko ya upigaji kura za maoni kuhusu kumpigia kura Diwani, Mbunge na Rais anasema Kiongozi huyo.

Anasema pia mbio hizo zimetumika kupeleka ujumbe kwa Wananchi kuhusu umuhimu wa kujiandikisha katika daftari la wapiga kura katika 

Misingi ya Demokrasia.Kueleza Sera imara za CCM kwa Wananchi ili waweza kuzitafakari na kushawishika kuingia Chamani
Kwani kila Chama kinapaswa kujipambanua kwa Wananchi ili waweze kuchukua maamuzi sahihi ya Chama gani Wajiunge nacho anasema Kiongozi huyo wa CCM  Mwanja

Kinachoonekana sasa, baadhi ya Watu wanakimbilia kujiunga katika Chama chochote cha Siasa, wanakimbilia katika hivyo sio kwa sababu ya kuvutiwa na itikadi zake zinazo ambatana na imani, bali wanakwenda kwa sababu wamevutiwa na sera papo kwa papo ambazo huwa zinamwagwa jukwaani bila kuwepo kwa mikakati stahiki ya kuzitekeleza sera hizo anasema Mwanja

Mbio za Bendera zimetumika pia kuwahamasisha Wanachama kuanzisha miradi mipya na kuiendeleza miradi ya zamani ya Chama ili kijikwamue Kiuchumi. Kwa sababu Siasa ni Uchumi bila Uchumi imara hatuwezi kufanya Siasa katika Chama hivyo Chama imara ni chenye Uchumi imara anasema Mwanja

Anaendelea kufafanua kuwa, mbio hizo za Bendera zimetumika kuelezea bayana mafanikio ambayo Serikali ya CCM imeyapata kwa kipindi cha miaka mitatu iliyopita. 

Kwani kuyaanika hadharani mafanikio hayo kutawafanya Wananchi waelewe jinsi ilani ya Chama Cha Mapinduzi ilivyotekelezwa chini ya Mwenyekiti wa Chama hicho Taifa ambaye ndiye Rais wa Jamhuri ya Muungano, Dkt Jakaya Mrisho Kikwete.

Kwani tunatambua kufanya hivyo kutaziba mianya kwa Viongozi wa vyama vya upinzani ambao kila kukicha wanajifanya vipofu na viziwi kwa kudai eti hakuna jambo lolote la maendeleo ya Watanzania linalofanywa na Serikali ya CCM huku wakijua wanayoyasema sio ya kweli anasema Mwanja

 Anaendlea kufafanua kuwa, CCM bado ni Chama makini kilicho na malengo makubwa ya kuwainua Wananchi wake hivyo wanapaswa kuwa na subira na kuridhika kwa yale mazuri yanayofanywa na Serikali pamoja na Chama tawala.

Kwani mambo mengi tumetekeleza kama ilani inavyoelekeza na katika maeneo mengine hasa katika Nyanja za miundo mbinu ya barabara, maji, afya na elimu, kuna mipango mbalimbali ya utekelezaji inaendelea  anasema kiongozi huyo.

Mwanja anasema kuwa mbio hizo zimetumika pia kumpongeza Rais Kikwete kwa kazi nzuri alayoifanya ya kutekeleza vyema ilani ya Chama Cha Mapinduzi. Kwani ni dhahiri juhudi zake za kuanzisha saccos na kutoa mitaji kwa wajasiriamali, kukuza Demokrasia katika misingi ya amani.utulivu na mshikamano.

Hata kuendeleza miradi ya Afya, barabara, maji, elimu na maboresho mbalimbali ya mishahara katika Sekta za Umma na mengineyo ni miongoni mwa utekelezaji mzuri wa ilani ya Chama Cha Mapinduzi anasema Mwanja

Anaendelea kufafanua  Mwanja , mbio hizo za Bendera zimepita kwenye mashina na Matawi yote ya Chama Cha Mapinduzi Mkoani Ruvuma na kufanikiwa kuingiza jumla ya wanachama wapya 3951.

Na imezindua jumla ya miradi 35 ya Chama kwa Mkoa mzima, yaani imeweka mawe ya Msingi katika Ofisi za Matawi na pia zimefanikiwa kufungua Ofisi tano za Matawi.

Miradi hiyo imeghalimu jumla ya shilingi Milioni 380 ikiwa ni jitihada za Wanachama kutoka kwenye mashina na Matawi kwa ushirikiano Mkubwa na Uongozi wa CCM Mkoa.

Hata hivyo anasema mbio hizo zimepita kuangalia pia miradi ya Maendeleo inayotekelezwa na Serikali ya awamu ya nne.
Pia zimepita kuangalia miradi ya Wananchi na Wanachama wa CCM ya ufugaji wa Kuku, mbuzi,ng’ombe pamoja na ujenzi wa nyumba bora za watu binafsi ambapo miradi hiyo yote inagharimu Milioni  750.

 Katibu wa CCM Mkoa Ruvuma Emmanuel Mteming’ombe, amewashukuru wakimbiza Bendera kutoka katika Jumuiya ya umoja wa Vijana wa CCM Mkoa UVCCM.   

Ambao amewataja majina ya Mwanahamisi Ngaje kutoka Wilaya ya Namtumbo, Doris Ngareka kutoka Mbinga, Hamis Nkali kutoka Tunduru, Mkandu Ngonji kutoka Songea Vijijni, Nestory Mwanja ambaye ndio Kiongozi Mkuu, Hilda Mgao na Mwajuma Rashid kutoka Songea Mjini,   

Mteming’ombe anamalizia kwa kusema mbio hizo zenye mafanikio makubwa zilifikia kilele chake Juni  19 katika Kata ya Mletele iliyopo Manispaa ya Songea ambapo mgeni Rasmi alikuwa Mwenyekiti wa CCM Mkoa Coleneus Msuha.

Hata hivyo, Nestory Mwanja ambaye ndiye kiongozi wa mbio hizo za bendera amewataka Vijana wajiunge katika Chama kwani mhimili wa Taifa lolote ni Vijana.

Mwandishi wa Makala hii
Anaptikana kwa simu no.   0755 335051
Barua pepe:  Stephano12mango@yahoo.com



Sunday, March 2, 2014

FUIME ATANGAZA NIA YA UBUNGE 2015 JIMBO LA SONGEA MJINI KUPITIA CHADEMA


MWENYEKITI WA CHADEMA RUVUMA AMTIMULIA VUMBI DKT NCHIMBI



 MTANGAZA NIA YA UBUNGE JIMBO LA SONGEA MJINI JOSEPH FUIME AKIHUTUBIA MOJA YA MIKUTANO YAKE
MAMIA YA WAKAZI WAKIMSIKILIZA MTANGA NIA YA KUGOMBEA UBUNGE KATIKA KATA YA LIZABONI

Na Stephano Mango, Songea


MWENYEKITI wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA) mkoa wa Ruvuma Joseph  Lusius Fuime ametangaza nia ya  kugombea Ubunge kwa tiketi ya Chama hicho katika Jimbo la uchaguzi la Songea mjini ifikapo mwaka 2015 katika kinyang’anyiro cha uchaguzi mkuu

Fuime  ambaye Diwani wa Kata ya Mjini katika Halmashauri ya Manispaa ya Songea akitangaza nia hiyo  jana ya kutaka kugombea jimbo ambalo kwa sasalinaongozwa na aliyekuwa Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi Dkt Emmanuel Nchimbi  kwenye mkutano wa hazara uliofanyika kwenye viwanja vya Soko kuu la Songea Mjini alisema kuwa ametafakari kwa muda mrefu pia ameombwa na makundi mbalimbali ya jamii ya Songea kuchukua fomu ya kugombea kiti hicho


Alisema kuwa baada ya kutafakari ameamua kwa dhati kusikiliza kilio cha makundi hayo na kugombea ubunge kwa tiketi ya CHADEMA  ili kwa pamoja kuweza kuondoa kero mbalimbali ambazo zinawasumbua wakazi hao


“Naomba niwaondoe hofu wanachama wenzangu ndani ya Chadema kuwa kutangaza kwangu nia  ya kutaka kugombea Ubunge hakuna maana kuwa wanachama wengine wanaotaka kugombea washindwe kutangaza nia ya kuwania nafasi hiyo”


Alisema kuwa wanachama ndio wenyewe  mamlaka ya kumchagua mgombea mwenye kujua matatizo ya wakazi wa Manispaa ya Songea na mbinu ya kushirikiana na wananchi hao kuweza kuyatatua kwa maslahi mapana ya ustawi wa jamii hiyo, pia atakayeweza kupambana na mgombea wa Ubunge kwa tiketi ya ccm.


Alieleza zaidi kuwa baada ya kufikia uamuzi huo kabla ya kutangaza nia aliamua kukaa na wazee wote wa Songea Mjini ambao wote kwa pamoja wameonyesha ushirikiano mkubwa na wamemwakikishia kuwa mwaka 2015 wakati wa uchaguzi watamuunga mkono kama walivyomuomba


Fuime ambaye pia ni Mwenyekiti wa Serikali ya Mtaa wa Ccm katika Halmashauri ya Manispaa ya Songea alijigamba na kuwaeleza wakazi wa Songea kuwa yeye ndiye anayefaa kupambana na Mbunge wa Songea Mjini kwa tiketi ya Ccm  Dkt Emmanuel Nchimbi.


Alifafanua zaidi kuwa Chadema imejipanga kwa dhati kutotoa nafasi tena ya uongozi kwenye Jimbo la uchaguzi la Songea Mjini kuchukuliwa na Ccm ambalo lina kata 21 na kati ya hizo 8 zinaongozwa na Madiwani wa Chama cha Chadema na kwamba mwaka 2015 kata zilizobaki zitanyang’anywa na Chadema.


Aliongeza kusema kuwa dawa ya kupambana na manyang’au waliomo ndani ya Ccm ni kujipanga na kuwabana kwa kutowapa nafasi ya aina yeyote kuanzia sasa na mpaka ifikapo 2015 kwani hivi sasa miradi mbalimbali katika Halmashauri ya Manispa ya Songea imekuwa ikijengwa chini ya viwango ambapo alitoa mfano kuwa miundombinu ya barabara, ujenzi wa vyumba vya madarasa na ofisi zimekuwa zikijengwa chini ya viwango huku manyang’au wa Ccm wakineemeka.


Alisema kuwa Wananchi wa Songea ambao wamekuwa wakikabiliwa na shida mbalimbali kutokana na ombwe la uongozi unaotokana na mfumo mbovu wa Ccm wana kila sababu ya kuunga mkono wazo lake la kuwania kiti cha Ubunge ili kuweza kufanikisha ustawi bora wa maisha ya wakazi wote kwa ushirikiano


Awali katika vipindi viwili vya uchaguzi mkuu vilivyopita Chama cha Demokrasia na Maendeleo kilikuwa kinamnadi Wakiri wa kujitegemea Edson Osward Mbogoro kugombea nafasi hiyo ambapo alikuwa akibwagwa na Mgombea wa Ccm  Dkt Emmanuel Nchimbi  ambaye ndiye Mbunge wa Jimbo la Songea Mjini hadi sasa.


MWISHO