About


Karibu ujiunge na chuo cha kisasa cha Easy Tech.Computer kwa mafanikio yako,Walimu waliobobea katika fani hiyo wanapatikana chuoni hapo

elimak

elimak

Pages - Menu

Thursday, June 6, 2013

MFEREJI WATAFUNA MAMILIONI YA FEDHA NA BADO HAUJAKAMILIKA


Na Mwandishi Wetu, Namtumbo
MFEREJI  wa maji uliojengwa kwa  fedha za Serikali kwa  ajili  ya  kilimo  cha  umwagiliaji katika  Kijiji cha Namahoka Kata  ya  Ligera Wilayani Namtumbo Mkoani Ruvuma wadaiwa umesombwa  na  maji ya  mvua iliyonyesha  hivi karibuni.
Mwenyekiti wa kikundi  cha Songambele kinachojengewa mradi  huo, Gaudens  Komba amesema kuwa mfereji huo umesombwa  na  maji kutokana na tuta lililowekwa na Mkandarasi kukinga mfereji  huo lilikuwa dogo na baadhi  ya  sehemu  ya  mfereji  huo zilititia.
Komba alisema kuwa hiyo ni  mara  ya pili sasa  kwa  mfereji huo  kutokea  dosari kwani mwaka 2007 mwezi mei  Serikali  ilitumia shilingi milioni 67 kujenga mfereji  huo chini  ya  kampuni ya Legele civil works iliyokuwa  ikimilikiwa na Dastan  Mtembele ambapo kabla ya kukamilika kwake mfereji  huo ulititia na  kushindwa kupitisha maji kwenda  mashambani.
Aliongeza kuwa pamoja na  hayo Serikali ilitenga tena fedha kiasi cha milioni 297 kwa  ajili  ya kufanya marekebisho ya  mfereji huo kwa kuipatia  tenda kampuni ya Modspan chini ya usimamizi  wa Ernest  Mbawa kufanya kazi ya  kuurekebisha mfereji  huo ambapo mpaka  sasa kampuni  hiyo imelipwa milioni 83 na baadhi ya sehemu iliyofanyiwa marekebisho imesombwa na  maji na zingine kutitia.
Fundi mkuu msaidizi anayejenga mfereji huo Shafii  Magoto alisema  kuwa sehemu iliyosombwa  na  maji imetokana na mkandarasi kuweka tuta dogo la  kukinga mfereji huo na kuruhusu maji ya mvua kusomba tuta hilo kiurahisi na kuufanya mfereji huo kuvunjika.
 Hata hivyo Magoto alisema  kuwa ujenzi wa mfereji huo umesimama kwa muda wa miezi sita sasa kutokana na wao kutolipwa fedha yao kutoka kwa mwajiri wao Ernest Mbawa na wanaishi katika mazingira magumu na wanashindwa kurudi kwao kutokana na kukosa  fedha za  kurudia na  hivi sasa wanajikita katika kufanya  kazi binafsi  ili kujipatia fedha  ya kula .
 Mkandarasi Mbawa kwa  upande wake anawalalamikia viongozi wa kikundi cha Songambele  kwa kumcheleweshea kumwizinishia kuchukua fedha kwa wakati ili aendelee kujenga mfereji  huo na badala  yake viongozi hao hupenda  kuendeleza malumbano na kuingiza  migogoro isiyokuwa ya lazima na kutumia muda mwingi kushughulikia migogoro inayoibuka kila  kukicha ndani ya kamati.
Mbawa aliwataka viongozi wa kamati kumwizinishia fedha ili arekebishe sehemu iliyosombwa na maji ya mvua na kuwalipa mafundi wake na waendelee na kazi.
Baadhi ya wanakikundi wakiwemo Mohamedi Mangambila  na Mohamedi Akida waliuambia mtandao huu kuwa wamechoshwa na utendaji kazi wa Mkandarasi huyo walidai kuwa wataandika barua kwa Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri  ya Wilaya ya Namtumbo kuomba kusimamisha mkataba wake kwa hoja ya kushindwa kujenga mradi huo kwa wakati kuendelea kujenga mradi huo nje ya mkataba na pia mkandarasi  kutokuwa na mahusiano mazuri na kamati.
Mhandisi wa halmashauri  ya wilaya ya Namtumbo Izakiel Nyirenda amethibitisha kuwepo na mgogoro katika mradi huo na kusema kuwa sababu kubwa inayofanya mradi huo kuyumba ni viongozi wa kikundi kuiona fedha katika mradi huo ni  kubwa na kwa namna fulani wanataka nao wapate mgao hali inayopelekea kuwepo na migogoro katika mradi  huo kila kukicha na mkandarasi kulazimika kutofanya kazi kwa muda mrefu na kutotaka  kumwizinishia fedha iliaendelee kujenga mradi  huo.
Nyirenda alidai kuwa sehemu ilisombwa  na maji inarekebishika kwa haraka na kuruhusu maji kupita kama kawaida licha ya wanakikundi hao kutomtaka Mkandarasi huyo kwani  wanakikundi wenyewe ndio waliopendekeza jina la Kampuni ya MODSPAN Inayosimamiwa na Ernesti Mbawa kujenga mradi huona kuziacha kampuni zingine nne zilizoomba kujenga  mradi  huo alisema  nyirenda.

Kampuni ya MODSPAN ilisaini mkataba wa miezi sita toka tarehe30 mwezi  novemba mwaka 2011 wa kurekebisha mfereji huo ambapo mpaka mei 2012 mkataba wake uliisha na wanakikundi inaonesha wazi hawakuridhika na utendaji kazi wa mkandarasi huyo na walifia uwamuzi wa kumwandika barua mkurugenziwa halmashauri  ya wilaya hiyo ya kutaka kumsimamisha mkandarasi huyo na ndipo mgogoro ulipoanzia na mradi huo  ukasimama  mpaka hivi sasa. Mradi wa ujenzi wa mfereji huo umesimamisha kilimo cha umwagiliaji katika eneo hilo na kuwaacha wananchi kuziba mito kienyeji na kuendesha kilimo cha umwagiliaji kwa kujichimbia mifereji  yao   wenyewe  na   kuendesha  shughuliza  kilimo cha umwagiliaji.
Hata hivyo mwenyekiti wa halmashauri ya wilaya ya Namtumbo Steven  Nana alipohojiwa na Mtandao huu kuhusiana na mgogoro  wa mradi huo wa kilimo cha umwagiliaji alikili kuwa matatizo yapo lakini hawezi kuelezea lolote mpaka awepo ofisini kwake ambako angedai kuwa angeweza kupata ufafanuzi mzuri kutoka kwa maafisa wake wa kilimo  na si vinginevyo.
MWISHO