About


Karibu ujiunge na chuo cha kisasa cha Easy Tech.Computer kwa mafanikio yako,Walimu waliobobea katika fani hiyo wanapatikana chuoni hapo

elimak

elimak

Pages - Menu

Friday, May 18, 2012

MKUU WA MKOA WA RUKWA AWAAPISHA WAKUU WA WILAYA WAPYA MKOANI HUMO JANA NA KUWAPA MAAGIZO 16 YA KUANZA NAYO KAZI

Mkuu Mpya wa Wilaya ya Sumbawanga Mathew S. Sedoyeka akila kiapo cha utii mbele ya Mkuu wa Mkoa wa Rukwa Injinia Stella Manyanya leo katika ukumbi wa Ikulu ndogo katika Manispaa ya Sumbawanga baada ya uteuzi wa hivi karibuni wa Mhe. Rais Dkt. Jakaya Mrisho Kikwete kushika madaraka hayo kutoka kwa aliyekuwa Mkuu wa Wilaya hiyo Kanali John Antonyo Mzurikwao.
Mhe. Sedoyeka akisaini kiapo hicho mbele ya Mkuu wa Mkoa wa Rukwa Stella Manyanya.
Mkuu wa Wilaya mpya ya Kalambo Luteni Edward O. Lenga akila kiapo cha kuiongoza Wilaya hiyo mpya mbele ya Mkuu wa Mkoa wa Rukwa Injinia Stella Manyanya baada ya kuteuliwa hivi karibuni na Mhe. Rais Dkt. Jakaya Mrisho Kikwete kuwa Mkuu wa Wilaya wa Kwanza wa Wilaya hiyo mpya iliyomegwa kutoka katika Wilaya ya Sumbawanga.
Mkuu wa Mkoa wa Rukwa Injinia Stella Manyanya akimkabidhi kitendea kazi Mkuu wa Wilaya mpya ya Kalambo Luteni Edward Lenga ambayo ni Katiba ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania atayoitumia kama muongozo wa shughuli zake za kila siku awapo madarakani.
Mkuu mpya wa Wilaya ya Nkasi Iddi Kimanta akila kiapo mbele ya Mkuu wa Mkoa wa Rukwa Injinia Stella Manyanya leo katika ukumbi wa Ikulu ndogo Mkoani Rukwa. Mkuu huyo wa Wilaya maechukua nafasi ya aliyekuwa Mkuu wa Wilaya hiyo Joyce Mgana baada ya uteuzi wa hivi karibuni wa Mhe. Rais Dkt. Jakaya Mrisho Kikwete.
Mkuu wa Mkoa wa Rukwa Injinia Stella Manyanya akisaini hati ya kiapo cha Mhe. Iddi Kimanta baada ya kuwaapisha wakuu wote watatu wa Wilaya za Sumbawanga, Kalambo na Nkasi.

PICHA, HOTUBA NA MATUKIO ZAIDI