About


Karibu ujiunge na chuo cha kisasa cha Easy Tech.Computer kwa mafanikio yako,Walimu waliobobea katika fani hiyo wanapatikana chuoni hapo

elimak

elimak

Pages - Menu

Wednesday, June 6, 2012

WAPIGAKURA WAHAMASISHWA KUMKATAA MBUNGE WA CCM MWAKA 2015

Na Steven Augustino, Tunduru.

CHAMA cha  Demokrasaia na Maendeleo (CHADEMA) kimewaomba wananchi wa Jimbo la Tunduru Kaskazini kumkataa kwa kuto mchagua Mbunge wa Jimbo hilo  Eng. Ramo Makani katika uchaguzi ujao.

Katika hotoba iliyotolewa na viongozi wandamizi wa  CHADEMA Wilayani Tunduru walidai kuwa kutochaguliwa kwa Mbunge huyo kunatokana na msimamo wake wa kukataa kujengwa kwa Barabara ya  lami katika Mji huo akishinikiza fedha hizo zikajenge barabara za vumbi vijijini.

Viongozi hao Mwiodadi Saidi (Mwenyekiti) , Nyenje Abbas (Katibu), Hadja Said  Mratibu wa Umoja wa akinamama  Wilayani humo na Ajonga Rajab Mwenyekiti wa Vijana wa Chama hicho Wilaya waliyasema hayo wakati wakiongea na wananchi katika Mkutano uliofanyika katika viwanja vya Baraza la Idd mjini hapa.

Wakifafanua hotuba zao viongozi hao walisema kuwa kitendo cha Mbunge huyo kukataa  kujengwa kwa kilometa tatu zilizo pangiwa Shilingi Milioni 300 kunalenga kuendelea kuudumaza mji wao hali ambayo walidai kuwa haitakiwi kukubalika .

Walisema Wilaya hiyo ambayo ilitangazwa kuwa Boma mwaka 1940 hadi sasa imeonekana kutopiga hatua za kimaendeleo kutokana na wananchi wake kuchagua viongozi wasio kuwa na huruma na Wilaya na wananchi wake kutoka CCM na kwamba sasa wanapaswa kubadilika kuchagua viongozi bora bila kujali chama .

Aidha viongozi hao pia walikemea tabia ya Mbunge huyo kuwatukana hadharani madiwanai wa halmashauri hiyo kuwa Umbumbu wao ndio unao wafanya washindwe kusimamia miradi na kuwafanya Watendaji wasio waaminifu kujinufaisha.

Walisema kitendo hicho kinaonesha kuwa Mbunge huyo ama hafahamu taratibu na sheria katika kuwatumikia wananchi na kuongeza kuwa tuhuma hizo alipaswa kuzisemea ndani na si kuropoka katika mikutano ya hadhara na kujidai kuwa yeye si miongoni mwa walioshindwa kusimamia miradi hiyo.

Mwisho