About


Karibu ujiunge na chuo cha kisasa cha Easy Tech.Computer kwa mafanikio yako,Walimu waliobobea katika fani hiyo wanapatikana chuoni hapo

elimak

elimak

Pages - Menu

Saturday, November 12, 2011

MAGARI YA ABIRIA YAKWAMA KITUO CHA MABASI KUTOKANA NA MVUA

Mkurugenzi wa Halmashauri ya Manispaa ya Songea Nachoa Zakaria
Na Mwandishi Wetu, Songea
WAKAZI  wa Manispaa ya Songea Mkoani Ruvuma wakiwemo wamiliki wa mabasi yanayo safirisha abiria wameulalamikia uongozi wa Halmashauri ya Manspaa hiyo kutokana  na kushindwa kuzifanyia ukarabati barabara pamoja na kituo kikuu cha mabasi ambacho kimekithili kuwa na ubovu ambao umesababisha kuwepo na mashimo mengi katikati ya kituo hicho na kupelekea magari kukwama wakati mvua zinaendelea kunyesha

Mtandao huu wa stephanomango.blogspot.com ulitembelea kituo hicho cha mabasi kwa lengo la kujionea hali halisi ya ubovu wa miundo mbinu kwenye eneo hilo ambalo lilikuwa limejaa tope wakati mvua zinaendelea kunyesha huku mabasi yaliyosheheni abiria yakiwa yametitia kwenye tope hilo.

Uharibifu huo ambao umechangia kwa kiasi kikubwa kujaa kwa tope  na kusababisha wananchi na magari kupita kwa tabu na mengine kukwama kabisa kutokana na utelezi uliotokana na uongozi wa  Halmashauri hiyo kuridhia  kumwaga kifusi cha udongo wa mfinyaji katikati ya kituo hicho kwa madai kuwa wanafukia mashimo yaliyokithili kwenye  eneo hilo jambo ambalo limeonekana kuwa ni kero kubwa kwa wakazi wa Songea wakiwemo abiria na wamiliki wa mabasi .  

 Hali hiyo ndiyo iliyopelekea watumiaji wa kituo hicho kutoa malalamiko yao kwa Halmashauri ya Manispaa ya Songea wakidai kilio chao cha kutengenezewa stendi hiyo kimekuwa ni cha muda mrefu na kitu cha kushangaza hakuna hatua zozote zinazo chukuliwa kwa ajiri  ya kukinusuru kituo hicho ambacho kipo katikati ya Manispaa hiyo

Mmoja  wa wakazi wa Manispaa ya Songea Lucas Haule alisema  inashangaza kuona kituo hicho ambacho kimekuwa kikilalamikiwa kwa muda mrefu kutokana na miundo mbinu yake kuwa mibovu huku Halmashauri ikitoza ushuru  mkubwa kwa magari yanayo ingia kwenye kituo hicho yakiwemo mabasi ya kusafirishia abiria .

Nae mmoja wa watumiaji wa kituo hicho cha mabasi Paulo Ndunguru  alisema kuwa  anashangazwa kuona kituo hicho kilicho kithiri mashimo kinatengenezwa kiholela bila kufuata utaalamu  na kudai kwamba endapo kama ungetumika utaalamu yakinifu tatizo hilo la kukwama kwa magari katikati ya kituo lisingeweza kujitokeza .

Hata hivyo jitihada zilizofanywa  na mtandao huu za kumpata mkurugenzi wa Halmashauri ya Manispaa hiyo Nachoa Zakaria ziligonga mwamba baada ya kutopatikana ofsini kwake ambapo Katibu muhutasi wake alieleza kuwa Mkurugenzi alikuwa kwenye vikao vya maandalizi ya mapokezi ya mwenge na maadhimisho ya miaka 50 ya uhuru na kwamba simu yake ya kiganjani alipopigiwa mara tatu iliita bila kupokelewa.
MWISHO

WANANCHI WATWANGANA KUGOMBEA ARDHI WILAYANI TUNDURU

                             Mkuu wa Wilaya ya Tunduru Juma Madaha

Na Augustino Chindiye,Tunduru    

MAPIGANO makali ya kugombea Ardhi ya kulima  yamezuka kati ya wakazi wa vijiji vya  Semeni Chikomo Wilayani Tunduru Mkoani Ruvuma na kumjeruhi kwa kukata kata kwa Mapanga mtu mmoja aliyefahamika kwa jina  la Mohamed Abdalah.

Kufuatia tukio hilo majeruhi huyo amelazwa katika Hospitali ya Missioni ya Mbesa baaya ya kujeruhi vibaya sehemu mbali mbali za mwili wake hali iliyo pelekea zaidi ya watu 50 wakazi wa kijiji cha Chikomo Wilayani humo wanatafutwa na Polisi ili waweze kujibu tuhuma hizo zilizotokaka na wananchi wa vijiji hivyo kuanzisha mapigano hayo.

Wakizungumzia tukio hilo kwa nyakati tofauti mbali na kukiri kutokea kwa ugomvi huo madiwani wa Kata za Mtina Mahamudu Katomondo na Kata ya Mbesa , Mohamedi Mtiko kila mmoja wao alitoa lawama kuwa wananchi wa kijiji jirani ndio chanzo cha mgogoro huo.

Upande wa Diwani wa kata ya mtina Katomondo yeye alidai kuwa wananchi wa kijiji cha Chikomo ndio waliofanya makosa ya kuvamia mipaka ya kijiji chake akidai kuwa mpaka unaotenganisha kijiji cha Semeni na Chikomo iliwekwa eneo la ng’ambo ya Mto Lukumbule.

Wakati diwani huyo akitoa madai hayo Diwani wa Kata ya Mbesa Mtiko yeye alidai kuwa na watu watatu waliohusika wakati wa upimaji wa mipaka hiyo mwaka 1978 na wanayo ramani hiyo inayo onesha mipaka ya vijiji hivyo  na kwamba ugomvi uliopo kati ya vijiji hivyo umetokana na wananchi wa kijiji cha Semeni kukaidi kulipa ushuru unaotakiwa kutozwa pindi wakulima wanapovuka mipaka na kwenda kulima kijiji jirani.

Akiongea kwa niaba ya Mkuu wa Wilaya hiyo,Katibu tawala wa Wilaya ya Tunduru  Martini Mulwafu mbali na kukiri kuwepo kwa mgogoro huo alisema kuwa ofisi yake imepanga kufanya mazungumzo kati ya viongozi kutoka katika Tarafa, kata na vijiji vinavyohusika na mgogoro huo ili kutafuta ufumbuzi wa kudumu.

ASHIKILIWA NA POLISI KWA TUHUMA ZA KUMUUA BABA YAKE WILAYANI TUNDURU

Kamanda wa Polisi Mkoa wa Ruvuma Michael Kamuhanda

Na Augustino Chindiye ,Tunduru

KIJANA wa miaka 21 aliyetambulika kwa jina la Hasan Adam Chimsala anashikiliwa na Polisi kwa tuhuma za kumuua Baba yake mzazi Mwalimu mstaafu Mwl. Adamu Isaa Chimsala (60).

Kwa mujibu wa taarifa kutoka ndani ya familia hiyo pamoja na kijana huyo kudaiwa kushindikana kutokana na tabia yake ya unywaji wa pombe na uvutaji bangi wa kupindukiwa  inadaiwa kijana huyo alichukua uamuzi huo kwa kumtuhumu baba yake huyo kuwa amekuwa hampatii matunzo kwa muda mrefu.

Kamanda wa Polisi wa Mkoa wa Ruvuma Michael kamuhanda alisema kuwa tukio hilo lilitokea katika kijiji cha Chemchem Wilayani Tunduru.

Kamanda Kamuhanda aliendelea kufafanua kuwa tukio hilo lilitokea usiku wa kuamkia Novemba 11 mwaka huu wakati mzee huyo akiwa amejipumzisha kwa ajili ya kusubiri chakula cha jioni.

Alisema wakati marehemu akiwa katika maandalizi hayo ghafla kijana kuyo alimvamia na kuanza kumshambulia kwa kumtoboa na kitu chenye ncha kali kichwani na sehemu mbali mbali za mwili wake.

Taarifa zilizotolewa na Mganga aliyeufanyia mwili wa marehemu Chimsala uchunguzi Dkt.Jeshi Daraja zinasema kuwa kifo hicho kilisababishwa na kutokwa na damu nyingi zilizosababishwa na majeraha hayo.

Alisema marehemu Chimsala alijeruhiwa vibaya kichwani ambako alipasuka fuvu la kichwa chake na kusababisha damu kutoka kwa wingi kupitia masikioni,puani na mdomoni.

Mwisho