About


Karibu ujiunge na chuo cha kisasa cha Easy Tech.Computer kwa mafanikio yako,Walimu waliobobea katika fani hiyo wanapatikana chuoni hapo

elimak

elimak

Pages - Menu

Tuesday, September 13, 2011

WANAHARAKATI WAZIKEMEA SERIKALI ZA AFRIKA KWA UKANDAMIZAJI

 Mkurugenzi Mtendaji wa Mtandao wa Jinsia Tanzania (TGNP)  Ussu Mallya akielezea tamasha la jinsia 2011 linaloendelea kufanyika jijini Dar Es Salaam
 Waandishi wa habari wakiwa kwenye moja ya vikao kwa ajili ya maandalizi ya kulipoti habari mbalimbali
 Wanaharakati mbalimbali wakiwa wanafuatilia mada zinazowasilishwa na wadau mbalimbali wa haki za binadamu
 Wanahabari mbalimbali kutoka katika vyombo tofauti tofauti wakiendelea kuchapa kazi wakati wa tamasha la jinsia 2011 linaloendelea kufanyika katika viwanja vya TGNP Jijini Dar Es Salaam
 Kikundi cha ngoma ya asili kikitumbuiza wakati wa tamasha
 Mwenyekiti wa chama cha waandishi wa habari wanawake nchini Ananilea Nkya akizungumza na waandishi wa habari katika ukumbi wa mtandao wa jinsia tanzania TGNP ikiwa ni maandalizi ya kuhabarisha umma
WANAHARAKATI WAZIKEMEA SERIKALI ZA AFRIKA KWA UKANDAMIZAJI
 Na Stephano Mango,Dar Es Salaam
WANAHARAKATI nchini wamezitaka Serikali  za nchi barani Afrika, kuhakikisha rasilimali zinawanufaisha wananchi hususani wanawake na watoto wanaoishi pembezoni ili kuweza kupunguza matabaka ya wenye nacho na wasio kuwa nacho ili kuweza kujenga jamii iliyostaarabika

Mwanaharakati wa masuala ya ardhi nchini Ghana, Profesa Dzodzi Tsilsata, alisema jana alipokuwa akifungua Tamasha la Jinsia, linalofanyika katika viwanja vya TGNP, Jijini Dar es Salaam.

Kwa mujibu wa Tsilsata, miaka michache iliyopita kumekuwepo na ongezeko kubwa kati ya wenye nacho na wasinacho hali inayosababisha kuwepo na matukio mengi ya uvunjifu wa amani, kwa kuandamana, kugoma ama vurugu mbalimbali.

Alisema, Serikali badala ya kupunguza hali hiyo imekuwa ikizembea kuchukua hatua stahiki na badala yake inawaongezea makali ya maisha wananchi wake kwa kuwaachia viongozi wake wakifanya vitendo viovu vya ubadhilifu wa rasilimali za taifa.

Alisema kuwa, Afrika inakabiliwa na changamoto mbalimbali ikiwemo ya kukubali sera mbovu kutoka katika mataifa ya magharibi na taasisi za fedha za kimataifa ambazo zimekuwa zikiwakandamiza wananchi wengi.

Naye Mwenyekiti wa tamasha hilo, Mary Rusimbi alisema kuwa Serikali za Afrika zimekuwa zikishindwa kutengeneza sera stahiki kwa wananchi wake na kupelekea hisia za kuwa na ukoloni mamboleo

Rusimbi alieleza kuwa Tanzania imetimiza miaka 50 baada ya uhuru lakini bado haijaweza kujitegemea kiuchumi,kisiasa,kidini,kijamii,kijeshi na kiutamaduni kwani imekuwa ikitawaliwa na utegemezi mkubwa kwa nchi za magharibi kupitia makampuni makubwa ya kimataifa ya uwekezaji
.
Alisema kuwa Serikali hutekeleza kwa niaba ya nchi za magharibi sera za utandawazi kupitia sera za ulegezaji wa uchumi na uuzaji wa bidhaa nje ili kuweka mazingira wezeshi kwa makampuni ya kibepari badala ya wazalishaji wadogowadogo

Alieleza kuwa matokeo yake mapato ya serikali yanazidi kutegemea makampuni machache yanayouza nje bidhaa kama vile madini,mbogamboga , maua,utalii na viwanda ambapo wanawake ndio wamekuwa waathirika wakubwa wa mifumo ya unyonyaji

Alifafanua zaidi kuwa kutokana na hali hiyo wanawake wengi waliopo pembezoni wamekuwa wakinyang’anywa rasilimali zao na kupewa watu wenye nguvu ya kiuchumi kutokana na mwingiliano wa mifumo kandamizi ya kibeberu na kibepari na mfumo dume unaowaacha wanawake wengi wakiwa mikono mitupu
mwisho

KAZI IMEANZA SASA BAADA YA KUTUA NANGA KATIKA VIWANJA VYA MTANDAO WA JINSIA TANZANIA ILI KUWEZA KUWALETEA HABARI MBALIMBALI ZINAZOENDELEA KUJILI KATIKA TAMASHA LA JINSIA 2011 LINALOENDELEA KUFANYIKA KATIKA VIWANJA VYA TGNP-MABIBO JIJINI DAR ES SALAAM

 Mmiliki wa mtandao huu wa http://www.stephanomango.blogspot.com,ndugu/ Stephano Mango akiwa amefika katika ofisi za TGNP kwa lengo la kuwahabarisha wasomaji wa mtandao huu kinachoendelea kwenye tamasha la jinsia 2011 ambapo wanaharakati zaidi ya 2500 wanatarajia kushiriki
 Moja ya picha za kiuhanaharakati ikiwa imepamba moja ya kuta kwenye jengo la mtandao wa jinsia Tanzania,picha hiyo inawakilisha akina mama wajawazito wanavyopata tabu ya huduma bora wanapokuwa wajawazito,wakati wa kujifungua na baada ya kujifungua

 Ukifika TGNP-Mabibo jijini Dar Es Salaam wakati huu wa tamasha utaona bango kubwa linalokupa maelekezo ya awali ya uwepo wa Tamasha hilo
Bango hili ndilo lililonipa ishara ya kuiona Ofisi ya TGNP ili niweze kukutana na wanaharakati wenzangu kwa lengo la kujiandaa kushiriki Tamasha la Jinsia la 2011 na kuweza kupata yanayoendelea kujili katika viwanja hivyo kwa ajili ya wasomaji

MENEJA WA SHIRIKA LA POSTA RUVUMA ADAIWA KUWANYANYASA WAFANYA KAZI WAKE

                                               Na Gideon Mwakanosya,Songea.

WAFANYAKAZI wa shirika la Posta Tanzania mkoani Ruvuma wameulalamikia uongozi wa shirika hilo mkoani humo kwa vitendo vya unyanyasaji kwa wafanyakazi likiwemo cha wafanyakazi wawili kusimamishwa na kufukuzwa kazi kwa madai kuwa wameiba fedha kiasi cha sh.10,620 mali ya shirika hilo.

Wafanyakazi hao ambao walitoa malalamiko yao kwa masharti ya kutotajwa majina kwa kuhofia ajira zao walisema kuwa unyanyasaji uliopo katika shirika hilo unaofanywa na Meneja wa Shirika hilo mkoani Ruvuma Rochus Assenga unawafanya wawe wanafanya kazi kwa hofu kubwa.

Walisema kuwa kitendo cha kuwasimamisha wafanyakazi wenzao na mmoja kumwachisha kazi kinaonesha wazi ukiukwaji wa haki za wafanyakazi kwani wafanyakazi hao mpaka sasa hakuna kosa lolote la msingi linaloweza kuwafanya wasimamishwe au kuachishwa kazi.

Mfanyakazi aliyesimamishwa kazi ametajwa kwa jina la Johnson Miyola na aliyeachishwa kazi Peter Sendama ambaye mpaka sasa barua ya kuachishwa kazi ajakabidhiwa ingawa amepewa taarifa hiyo ya kuachishwa kazi na meneja kwa mdomo na kutakiwa asiingie kwenye ofisi za shirika hilo wakati uongozi unamuandalia barua pamoja na mafao ya kuachishwa kazi.

Uchunguzi uliofanywa na waandishi wa habari umebaini kuwa licha ya kuwasimamisha kazi  na kumwachisha  mmoja tayari wafanyakazi hao walishapelekwa polisi na kufunguliwa kesi ya wizi namba SO\ IR\3962\2011 katika kituo kikuu cha Songea tangu Agosti 19 mwaka huu.

Mfanyakazi mmoja aliyeachishwa kazi Sendama alipoulizwa na waandishi wa habari amekiri kuchishwa kazi kwa mdomo na kwamba barua ya kuachishwa kazi pamoja na mafao atapewa siku ya Ijumaa kwa mujibu wa maelezo aliyoyatoa meneja wa shirika hilo Assenga

Alisema ameshangazwa kuona atua kali zikichukuliwa dhidi yake ambapo awali tangu aanze kazi kwenye shirika hilo hajawi kupewa barua ya onyo au kalipio kali kabla mfanyakazi hajaachishwa kazi.

“ Sina kosa jingine ambalo meneja alishanionya mara tatu kwa kujaza fomu tatu ambazo mfanyakazi kabla hajaachishwa hujazwa na kabla ya hapo meneja hajawahi kunipa onyo wala fedha hizo anazodai nimeiba si kweli bali kulikuwa na tatizo la kiufundi lililojitokeza kwenye mtandao na kusababisha kumwandikia mteja risiti kwa mkono.”alisema Bw. Sendama.

Hata hivyo baadhi ya wafanyakazi wa shirika hilo tawi la Songea wameeleza kuwa tangu meneja huyo Assenga afike Mkoa wa Ruvuma baada ya meneja aliyekuwepo kustaafu amekuwa na tabia ya kuwanyanyasa na kudai kuwa yeye amuogopi mtu wa aina yeyote kwani ametokea makao makuu ya shirika hilo na kwamba Posta masta mkuu ni swaiba wake hivyo hawezi kumfanya kitu chochote na ni lazima amsikilize anachosema.

Naye Meneja wa shirika hilo mkoani Ruvuma  Assenga alipofuatwa na waandishi wa habari ofisini kwake kutaka atoe ufafanuzi juu ya malalamiko dhidi yake alidai kuwa yeye sio msemaji wa shirika na kuwataka waandishi wamtafute posta masta mkuu wa shirika hilo ndio msemaji na baadae alipoona waandishi wa habari wanaendelea kumuliza maswali aliondoka ofisini kwake na kuwaacha waandishi wa habari wakiduwaa kwenye jengo la shirika hilo.

Kwa upande wake mwenyekiti wa chama cha wafanyakazi wa shirika la posta Tanzania tawi la Songea Gisla Mhagama alipotafutwa na  waandishi wa habari ili ataoe ufafanuzi juu ya malalamiko ya wafanyakazi dhidi ya uongozi hakuweza kupatikana kwa njia ya simu kwa kuwa yuko safarini nje ya Mkoa.

Hata hivyo waandishi wa habari waliwatafuta viongozi wa chama hicho (COTWU) kanda ya Mbeya kwa njia ya simu ambapo walifanikiwa kumpata katibu wa chama hicho  Getrud Mlai na mwenyekiti wake Peter Songela walishangazwa kusikia kuwa wafanyakazi wa tawi la Songea wamekuwa na malalamiko mazito dhidi ya uongozi na walidai kuwa wao bado hawajapata malalamiko rasmi lakini wanafanya taratibu za kwenda Songea kwenda kusikiliza kilio cha wafanyakazi wiki ijayo.

Akizungumza kwa njia ya simu Posta masta mkuu wa shirika la Posta Tanzania Deos Mndeme alieleza kuwa ni kweli ofisi yake inataarifa kuwa kunawafanyakazi wawili wa shirika hilo ambao walipelekwa polisi wakituhumiwa kuwa ni wezi wameiba fedha sh.10,620 lakini hana taarifa ya aina yeyote kama wafanyakazi hao wamesimamishwa na kuachishwa kazi kwani maswala ya utawala yanamgawanyo na mambo ya utawala wa mikoani yanaishia mikoani yeye anashughulikia mambo makubwa.

Aidha mndemi alikanusha kauli ya meneja wa shirika hilo mkoani Ruvuma Assenga ya kusema kuwa yeye yuko jirani naye na ni swaiba yake jambo ambalo alidai kuwa linaleta mazingira ya kumchafua kwani yeye ni mtawala wa shirika na wafanyakzi wote bila kuwa na ubaguzi labda uhusianao huo katika yangu na yeye anaujuwa yeye na si vinginevyo.

Kamanda wa Polisi Mkoa wa Ruvuma  Michael Kamuhanda alipoulizwa na waandishi wa habarĂ­ kuhusiana na wafanyakazi wawili wa shirika la posta kukamatwa na kuwekwa mahabusu kwa tuhuma za wizi wa sh. 10,620 za shirika hilo amekiri kushikiriwa kwa wafanyakzi hao lakini ameeleza kuwa jambo hilo liko kwenye upelelezi na bado halijathibitishwa kama wafanyakazi hao kama waliiba au la.

MWISHO.