About


Karibu ujiunge na chuo cha kisasa cha Easy Tech.Computer kwa mafanikio yako,Walimu waliobobea katika fani hiyo wanapatikana chuoni hapo

elimak

elimak

Pages - Menu

Thursday, October 6, 2011

AJINYONGA KWA KUMKATAA MKE MWENZA WILAYANI MBINGA


 Na Gideon Mwakanosya, Songea
MWANAMKE  mmoja Apolonjali Hyera (45) Mkazi wa Kitongoji cha Mapendano kilichopo katika Kijiji cha Mzuzu Wilayani Mbinga amekufa kwa kujinyonga kwa kutumia kamba ya katani baada ya mume wake kuoa mwanamke mwingine.
Habari zilizopatikana jana mjini hapa ambazo zimethibitishwa na Kaimu Kamanda wa Polisi Mkoa wa Ruvuma Naftani Mantamba zimesema kuwa tukio hilo limetokea Octoba 5 mwaka huu majira ya saa 6 mchana huko katika Kitongoji cha Mapendano kilichopo katika Kijiji cha Mzuzu Wilayani Mbinga.
Mantamba amesema kuwa siku hiyo ya tukio inadaiwa Apolonjali alikutwa akiwa amejinyonga kwa kutumia kamba ya katani  kwa kujining’iniza juu ya mti kwenye msitu mkubwa wa Kijiji hicho.
Ameeleza zaidi kuwa Apolonjali anadaiwa kuwa aliamua kujinyonga baada ya kumtuhumu mume wake kuamua kuoa mwanamke mwingine wakati yeye ametoka nyumbani kwa wazazi wao na yupo kwaajili yake hivyo alikuwa akijiuliza ni kwanini ameamua kuchukua uamuzi huo.
Amefafanua zaidi kuwa kutokana na kuwepo kwa mvutano huo kati yake na mume wake Kelvin Sesilisi (45) ndiyo aliamua kuchukua uamuzi wa kujiua na kuacha maagizo kuwa ameamua aondoke amuache mwanamke aliyempata
Mantamba amesema kuwa chanzo cha tukio hilo ni wivu wa mapenzi ambao umemsababishia Apolonjali kufikia uamuzi wa kujiua kwa kujinyonga kwa kujining’iniza kwenye mti uliopo katikati ya msitu

ANYWA SUMU,AFARIKI BAADA YA KUONYWA KUACHA UASHERATI MBAMBABAY

Na Mwandishi Wetu,Songea
JANETH Mwanjali ni msichana mwenye umri wa miaka 15 mkazi wa mji mdogo wa Mbamba bay uliopo Wilayani Nyasa Mkoa wa Ruvuma amefariki dunia baada ya kunywa dawa ya kuulia panya iliyokuwa imehifadhiwa nyumbani kwa wazazi wake.
Akizungumza na mtandao huu wa http://www.stephanomango.blogspot.com/  Kaimu Kamanda wa Polisi Mkoa wa Ruvuma Naftani Mantamba amesema kuwa tukio hilo limetokea juzi majira ya saa 4 asubuhi nyumbani kwa wazazi wa Janeth.
Mantamba amesema kuwa siku hiyo kabla ya tukio kutokea  inadaiwa kuwa Janeth aliitwa na mama yake mzazi Anna Kalima ambaye alikuwa akimuonya aache tabia ya kulala kwa wanaume na baadaye ulitokea ugomvi kati yake na mama yake ambaye alikuwa akimtuhumu kuwa anamuonea wivu kisha alikwenda ndani ya nyumba na kutafuta dawa ya kuulia panya ambayo aliinywa.
Amesema kuwa baada ya kuinywa dawa hiyo muda mfupi alianza kubadilika na hali yake ikawa mbaya hivyo mama yake mzazi aliamua kumchukua na kumpeleka hadi Kituo cha afya cha Mbamba bay ambako muda mfupi baadaye alifariki dunia akiendelea kupatiwa matibabu.
Mantamba amesema kuwa Chanzo cha tukio hilo ni kwamba Janeth alikuwa amegombana na mama yake mzazi aliyekuwa akimkanya kuwa aache tabia ya kulala nje kwa wanaume jambo ambalo lilimtia hasirĂ¡ na kuchukua uamuzi wa kutafuta dawa ya kuulia panya na kunywa kwa lengo la kujiua.
Hata hivyo Kaimu Kamanda wa Polisi Mkoa wa Ruvuma Mantamba ameeleza kuwa kwasasa Polisi wanaendelea kufanya upelelezi wa kina kuhusiana na tukio hilo licha ya kuwa Upelelezi wa awali umebaini kuwa Janeth alipandwa na hasira wakati anaonywa na mama yake mzazi.