About


Karibu ujiunge na chuo cha kisasa cha Easy Tech.Computer kwa mafanikio yako,Walimu waliobobea katika fani hiyo wanapatikana chuoni hapo

elimak

elimak

Pages - Menu

Thursday, November 17, 2011

WANANCHI WATAADHARISHWA UZAGAAJI WA NOTI BANDIA MKOANI RUVUMA

Na Gideon Mwakanosya, Songea

JESHI la polisi Mkoani Ruvuma limewataadharisha wananchi wakiwemo wakulima na wafanyabiashara kuwa makini wanapofanya shughuli zao za kila siku hasa wanapouza mazao au wanaponunua bidhaa za biashara zao kwani katika Mkoa huo noti bandia za shilingi Elfu 5000 na shilingi Elfu 10,000 zimezagaa ambapo kufuatia hali hiyo Polisi imefanikiwa kuwanasa watu wawili wakiwa na noti bandia za shilingi alfu 10 kila mmoja zenye thamani ya shilingi laki 5.

Tahadhali hiyo imetolewa jana na Kamanda wa Polisi wa Mkoa wa Ruvuma Michael Kamuhanda wakati alipokuwa akiongea na Waandishi wa habari ofisini kwake.

Kamuhanda amewataja wanoshikiliwa na polisi kuwa ni Joseph Kilagi ( 25) na Francis Nkunji (19) wote wakazi wa jijini Dar es salaam ambao walitiwa mbaroni tangu Novemba 13 mwaka huu majira ya saa mbili usiku kwenye kituo kikuu cha mabasi cha Mjini Songea wakiwa wanateremka kwenye basi wakitokea Dar es salaam.

Amesema kuwa askari ambao walikuwa doria kwenye eneo la Kituo cha mabasi waliwakamata watuhumiwa hao wakiwa na noti bandia 50 ambazo kila noti  moja ni shilingi elfu 10 zote zikiwa na thamani ya shilingi laki 5.

Amefafanua zaidi kuwa noti hizo bandia zilizokamatwa zina namba AC.0011601 kila moja na kwamba watuhumiwa walipohojiwa na askari hao waliokuwa doria walidai kuwa wametokea Dar es salaam na wamekuja Songea kufanya biashara ya kununua mahindi.

Kamanda Kamuhanda ameeleza kuwa kwasasa hivi polisi inaendelea kufanya upelelezi kuhusiana na tukio hilo na kwamba watuhumiwa hao watafikishwa Mahakami kujibu shtaka linalowakabili mara tu upelelezi utakapokamilika.

Amewataadhalisha wafanyabiashara wa Wilaya zote za Mkoa wa Ruvuma kuwa wanapofanyabiashara zao kuwa waangalifu pale wanapokutana na noti za shilingi Elfu 5000 na Elfu 10,000ambazo zinadaiwa ndiyo noti bandia zimezagaa kwenye magulio,minada na maeneo mengine ya biashara za jumla na rejareja na kwamba wananchi watakaowagundua watu wenye tabia mbaya ya kusambaza noti bandia watoe taarifa katika kituo chochote cha polisi kilicho karibu.

WASHIRIKI WA MAJADILIANO YA PAMOJA KUHUSU UTAFITI MDOGO WA VYOMBO VYA HABARI RUVUMA WAMALIZA WARSHA YA SIKU MBILI NA KUAZIMIA NJIA BORA YA KUKUSANYA NA KUSAMBAZA TAARIFA KWENYE VIKUNDI NA MITANDAO YA JAMII

 Washiriki wa warsha hiyo wakiwa kwenye picha ya pamoja mara baada ya kumaliza mafunzo husika
 Washiriki wakiendelea na mijadala mbalimbali kwenye ukumbi wa warsha
 Bi Jenni akiwasirisha mada iliyojadiliwa kwenye kikundi chake wakati wa warsha
Washiriki wakisikiliza mada iliyokuwa inawasilishwa na Mwezeshaji kutoka TGNP Badi Darusi

TGNP NA DHANA YA UMUHIMU WA KUANZISHA VITUO VYA TAARIFA KWENYE VIKUNDI NA MITANDAO YA KIJAMII

VITUO VYA TAARIFA NA MAALIFA KATIKA JAMII
Na Stephano Mango,Songea
Ni sehemu maalumu ya kukutana kwa lengo la kujifunza na kuhabarishana masuala mbalimbali yanayohusu jamii zetu kwa faida ya vizazi vilivyopo na vijavyo
KWANINI VITUO HIVYO
-Kuleta chachu ya harakati za ukombozi wa mwanamke wa kimapinduzi katika jamii
-Kusaidia ujenzi wa nguvu za pamoja kwa kutumia kukusanya na kusambaza taarifa
-Kuendesha mijadala ya wazi na kuweka kumbukumbu kuhusu mijadala hiyo
-Kufanya uchambuzi na ufuatiliaji wa masuala au kero zinazoikabili jamii husika na kuchukua hatua za pamoja
LENGO KUU
-Kuwawezesha wanaharakati wa ukombozi wa mwanamke wa kimapinduzi,vikundi,mitandao ya jamii kufikia fursa za kupashana,kubadilishana maarifa na taarifa
-Kuongeza hamasa katika masuala yanayohusu haki za binadamu kwa mlengo wa ukombozi wa mwanamke wa kimapinduzi
MALENGO MAHSUSI YA VITUO
-Kuwa na eneo la vituo vya wanawake,vikundi na kuhamasishana ili kuchukua hatua za pamoja kuleta mabadiliko
-Kukita vuguvugu la ukombozi wa mwanamke wa kimapinduzi katika ngazi ya jamii kwa kuwawezesha wanawake na vikundi vya wanaharakati na mitandao kuweka kumbukumbu na kupashana habari
-Kuboresha na kuimarisha mahusiano na kupashana habari kati ya wanaharakati na vikundi ili kupunguza pengo kati ya wanaofaidi taarifa muhimu na wale ambao hawapati taarifa hizo kwa wakati muafaka