About


Karibu ujiunge na chuo cha kisasa cha Easy Tech.Computer kwa mafanikio yako,Walimu waliobobea katika fani hiyo wanapatikana chuoni hapo

elimak

elimak

Pages - Menu

Tuesday, July 30, 2013

DC NALICHO AWATIMUA WAVAMIZI MSITU WA SHAMBA LA BIBI

Na Steven Augustino, Tunduru
MWENYEKITI wa kamati ya Ulinzi ya Wilaya ya Tunduru, Mkuu wa Wilaya hiyo Mkoani Ruvuma Chande Nalicho ametoa wiki moja kwa Wakulima na Wafugaji wa jamii ya Kisukuma kuondoka katika eneo la hifadhi ya msitu wa Shamba la Bibi vinginevyo hatua kali za Kisheria zitachukuliwa dhidi yao.
Dc, Nalicho alitoa maagizo hayo baada ya kamati ya Ulinzi na Usalama ya Wilaya hiyo kufanya ziara ya kushtukiza katika msitu huo na kujionea hali halisi ya uhalibifu wa vyanzo vya maji, mabwawa na misitu iliyopo katika hifadhi hiyo inayo unganisha Vijiji vya Nangunguru, Majala na Mkalekawana katika Tarafa ya Nampungu kata ya Nandenbo Wilayani humo.
Alisema anatoa siku Saba kwa watu wote waliovamia msitu huo wa hifadhi kuondoka kwani haiwezekani watu waendelee kuishi wanavyo penda na kuharibu mazingira katika vyanzo vya maji na hifadhi ya misitu kana kwamba serikali haipo
Mkuu huyo aliwataka Watendaji Kata ,Vijiji kwa kushirikiana na Maafisa Tarafa Wilayani humo kutekeleza majukumu yao ikiwemo kuwaelekeza wafugaji kufuata taratibu za kuonana na viongozi wa Vijiji husika, kufanya mikutano inayo wahusisha wananchi katika maamuzi ya kuwapokea wafugaji hao ili kuyaondoa maeneo yao katika migogoro ya aina hiyo.
“Kwavile mifugo ni muhimu kwetu na endapo itatumika vizuri na kwa kuzingatia kanuni, miongozo na maelekezo yanayotolewa na Serikali italeta manufaa kwa Wananchi wetu” alisema Dc, Nalicho na kuongeza kuwa mtindo wa kuishi kwa uhasama kati ya wafugaji na wakulima hauwezi kuwa na tija.
Awali akiongea katika ziara hiyo Afisa misitu wa Wilaya la Tunduru  Rashid Mtotela alimweleza Dc, Nalicho kuwa Wakulima na wafugaji hao walivamia msitu huo mwaka 2006 /2007 na kuendelea kujiimarisha kila mwaka baada ya kubaini kutokuwepo kwa vikwazo vyovyote kutoka Serikalini.
Alisema hifadhi hiyo ambayo awali ilikuwa imeunganishwa na Hifadhi ya Taifa (Selous) tangu mwaka 1974 na baadae kuunda hifadhi shirikishi mwaka 2007 kupitia mradi wa Jont participatory Forest Menegement (JPFM) liyounganisha Vijiji vya Nangunguru, Mkalekawana na Majala kila Kijiji kimekuwa kikikwepa majukumu yake ya kulinda hifadhi hiyo hali ambayo imechangia kuendelea kuhalibika kwa mazingira hayo.
Wakiongea kwaniaba ya Wananchi wa Vijiji hivyo Mwenyekiti wa Kijiji cha Nangunguru Bw.Said Rashid Mkwekwele, Mtendaji wa Kijiji hicho Zainabu Twaha na Afisa Tarafa wa Nampungu Joshua John wakawashushia lawama baadhi ya wakuu wa Idara katika halmashauri ya Wilaya hiyo kuwa umekuwa na kigugumizi katika ufuatiliaji na uchukuzi wa maamuzi juu ya migogoro hiyo.

DC NALICHO AWATIMUA WAVAMIZI MSITU WA SHAMBA LA BIBI

Na Steven Augustino, Tunduru
MWENYEKITI wa kamati ya Ulinzi ya Wilaya ya Tunduru, Mkuu wa Wilaya hiyo Mkoani Ruvuma Chande Nalicho ametoa wiki moja kwa Wakulima na Wafugaji wa jamii ya Kisukuma kuondoka katika eneo la hifadhi ya msitu wa Shamba la Bibi vinginevyo hatua kali za Kisheria zitachukuliwa dhidi yao.
Dc, Nalicho alitoa maagizo hayo baada ya kamati ya Ulinzi na Usalama ya Wilaya hiyo kufanya ziara ya kushtukiza katika msitu huo na kujionea hali halisi ya uhalibifu wa vyanzo vya maji, mabwawa na misitu iliyopo katika hifadhi hiyo inayo unganisha Vijiji vya Nangunguru, Majala na Mkalekawana katika Tarafa ya Nampungu kata ya Nandenbo Wilayani humo.
Alisema anatoa siku Saba kwa watu wote waliovamia msitu huo wa hifadhi kuondoka kwani haiwezekani watu waendelee kuishi wanavyo penda na kuharibu mazingira katika vyanzo vya maji na hifadhi ya misitu kana kwamba serikali haipo
Mkuu huyo aliwataka Watendaji Kata ,Vijiji kwa kushirikiana na Maafisa Tarafa Wilayani humo kutekeleza majukumu yao ikiwemo kuwaelekeza wafugaji kufuata taratibu za kuonana na viongozi wa Vijiji husika, kufanya mikutano inayo wahusisha wananchi katika maamuzi ya kuwapokea wafugaji hao ili kuyaondoa maeneo yao katika migogoro ya aina hiyo.
“Kwavile mifugo ni muhimu kwetu na endapo itatumika vizuri na kwa kuzingatia kanuni, miongozo na maelekezo yanayotolewa na Serikali italeta manufaa kwa Wananchi wetu” alisema Dc, Nalicho na kuongeza kuwa mtindo wa kuishi kwa uhasama kati ya wafugaji na wakulima hauwezi kuwa na tija.
Awali akiongea katika ziara hiyo Afisa misitu wa Wilaya la Tunduru  Rashid Mtotela alimweleza Dc, Nalicho kuwa Wakulima na wafugaji hao walivamia msitu huo mwaka 2006 /2007 na kuendelea kujiimarisha kila mwaka baada ya kubaini kutokuwepo kwa vikwazo vyovyote kutoka Serikalini.
Alisema hifadhi hiyo ambayo awali ilikuwa imeunganishwa na Hifadhi ya Taifa (Selous) tangu mwaka 1974 na baadae kuunda hifadhi shirikishi mwaka 2007 kupitia mradi wa Jont participatory Forest Menegement (JPFM) liyounganisha Vijiji vya Nangunguru, Mkalekawana na Majala kila Kijiji kimekuwa kikikwepa majukumu yake ya kulinda hifadhi hiyo hali ambayo imechangia kuendelea kuhalibika kwa mazingira hayo.
Wakiongea kwaniaba ya Wananchi wa Vijiji hivyo Mwenyekiti wa Kijiji cha Nangunguru Bw.Said Rashid Mkwekwele, Mtendaji wa Kijiji hicho Zainabu Twaha na Afisa Tarafa wa Nampungu Joshua John wakawashushia lawama baadhi ya wakuu wa Idara katika halmashauri ya Wilaya hiyo kuwa umekuwa na kigugumizi katika ufuatiliaji na uchukuzi wa maamuzi juu ya migogoro hiyo.

DC NALICHO AWATIMUA WAVAMIZI MSITU WA SHAMBA LA BIBI

Na Steven Augustino, Tunduru
MWENYEKITI wa kamati ya Ulinzi ya Wilaya ya Tunduru, Mkuu wa Wilaya hiyo Mkoani Ruvuma Chande Nalicho ametoa wiki moja kwa Wakulima na Wafugaji wa jamii ya Kisukuma kuondoka katika eneo la hifadhi ya msitu wa Shamba la Bibi vinginevyo hatua kali za Kisheria zitachukuliwa dhidi yao.
Dc, Nalicho alitoa maagizo hayo baada ya kamati ya Ulinzi na Usalama ya Wilaya hiyo kufanya ziara ya kushtukiza katika msitu huo na kujionea hali halisi ya uhalibifu wa vyanzo vya maji, mabwawa na misitu iliyopo katika hifadhi hiyo inayo unganisha Vijiji vya Nangunguru, Majala na Mkalekawana katika Tarafa ya Nampungu kata ya Nandenbo Wilayani humo.
Alisema anatoa siku Saba kwa watu wote waliovamia msitu huo wa hifadhi kuondoka kwani haiwezekani watu waendelee kuishi wanavyo penda na kuharibu mazingira katika vyanzo vya maji na hifadhi ya misitu kana kwamba serikali haipo
Mkuu huyo aliwataka Watendaji Kata ,Vijiji kwa kushirikiana na Maafisa Tarafa Wilayani humo kutekeleza majukumu yao ikiwemo kuwaelekeza wafugaji kufuata taratibu za kuonana na viongozi wa Vijiji husika, kufanya mikutano inayo wahusisha wananchi katika maamuzi ya kuwapokea wafugaji hao ili kuyaondoa maeneo yao katika migogoro ya aina hiyo.
“Kwavile mifugo ni muhimu kwetu na endapo itatumika vizuri na kwa kuzingatia kanuni, miongozo na maelekezo yanayotolewa na Serikali italeta manufaa kwa Wananchi wetu” alisema Dc, Nalicho na kuongeza kuwa mtindo wa kuishi kwa uhasama kati ya wafugaji na wakulima hauwezi kuwa na tija.
Awali akiongea katika ziara hiyo Afisa misitu wa Wilaya la Tunduru  Rashid Mtotela alimweleza Dc, Nalicho kuwa Wakulima na wafugaji hao walivamia msitu huo mwaka 2006 /2007 na kuendelea kujiimarisha kila mwaka baada ya kubaini kutokuwepo kwa vikwazo vyovyote kutoka Serikalini.
Alisema hifadhi hiyo ambayo awali ilikuwa imeunganishwa na Hifadhi ya Taifa (Selous) tangu mwaka 1974 na baadae kuunda hifadhi shirikishi mwaka 2007 kupitia mradi wa Jont participatory Forest Menegement (JPFM) liyounganisha Vijiji vya Nangunguru, Mkalekawana na Majala kila Kijiji kimekuwa kikikwepa majukumu yake ya kulinda hifadhi hiyo hali ambayo imechangia kuendelea kuhalibika kwa mazingira hayo.
Wakiongea kwaniaba ya Wananchi wa Vijiji hivyo Mwenyekiti wa Kijiji cha Nangunguru Bw.Said Rashid Mkwekwele, Mtendaji wa Kijiji hicho Zainabu Twaha na Afisa Tarafa wa Nampungu Joshua John wakawashushia lawama baadhi ya wakuu wa Idara katika halmashauri ya Wilaya hiyo kuwa umekuwa na kigugumizi katika ufuatiliaji na uchukuzi wa maamuzi juu ya migogoro hiyo.

DC NALICHO AWATIMUA WAVAMIZI MSITU WA SHAMBA LA BIBI

Na Steven Augustino, Tunduru
MWENYEKITI wa kamati ya Ulinzi ya Wilaya ya Tunduru, Mkuu wa Wilaya hiyo Mkoani Ruvuma Chande Nalicho ametoa wiki moja kwa Wakulima na Wafugaji wa jamii ya Kisukuma kuondoka katika eneo la hifadhi ya msitu wa Shamba la Bibi vinginevyo hatua kali za Kisheria zitachukuliwa dhidi yao.
Dc, Nalicho alitoa maagizo hayo baada ya kamati ya Ulinzi na Usalama ya Wilaya hiyo kufanya ziara ya kushtukiza katika msitu huo na kujionea hali halisi ya uhalibifu wa vyanzo vya maji, mabwawa na misitu iliyopo katika hifadhi hiyo inayo unganisha Vijiji vya Nangunguru, Majala na Mkalekawana katika Tarafa ya Nampungu kata ya Nandenbo Wilayani humo.
Alisema anatoa siku Saba kwa watu wote waliovamia msitu huo wa hifadhi kuondoka kwani haiwezekani watu waendelee kuishi wanavyo penda na kuharibu mazingira katika vyanzo vya maji na hifadhi ya misitu kana kwamba serikali haipo
Mkuu huyo aliwataka Watendaji Kata ,Vijiji kwa kushirikiana na Maafisa Tarafa Wilayani humo kutekeleza majukumu yao ikiwemo kuwaelekeza wafugaji kufuata taratibu za kuonana na viongozi wa Vijiji husika, kufanya mikutano inayo wahusisha wananchi katika maamuzi ya kuwapokea wafugaji hao ili kuyaondoa maeneo yao katika migogoro ya aina hiyo.
“Kwavile mifugo ni muhimu kwetu na endapo itatumika vizuri na kwa kuzingatia kanuni, miongozo na maelekezo yanayotolewa na Serikali italeta manufaa kwa Wananchi wetu” alisema Dc, Nalicho na kuongeza kuwa mtindo wa kuishi kwa uhasama kati ya wafugaji na wakulima hauwezi kuwa na tija.
Awali akiongea katika ziara hiyo Afisa misitu wa Wilaya la Tunduru  Rashid Mtotela alimweleza Dc, Nalicho kuwa Wakulima na wafugaji hao walivamia msitu huo mwaka 2006 /2007 na kuendelea kujiimarisha kila mwaka baada ya kubaini kutokuwepo kwa vikwazo vyovyote kutoka Serikalini.
Alisema hifadhi hiyo ambayo awali ilikuwa imeunganishwa na Hifadhi ya Taifa (Selous) tangu mwaka 1974 na baadae kuunda hifadhi shirikishi mwaka 2007 kupitia mradi wa Jont participatory Forest Menegement (JPFM) liyounganisha Vijiji vya Nangunguru, Mkalekawana na Majala kila Kijiji kimekuwa kikikwepa majukumu yake ya kulinda hifadhi hiyo hali ambayo imechangia kuendelea kuhalibika kwa mazingira hayo.
Wakiongea kwaniaba ya Wananchi wa Vijiji hivyo Mwenyekiti wa Kijiji cha Nangunguru Bw.Said Rashid Mkwekwele, Mtendaji wa Kijiji hicho Zainabu Twaha na Afisa Tarafa wa Nampungu Joshua John wakawashushia lawama baadhi ya wakuu wa Idara katika halmashauri ya Wilaya hiyo kuwa umekuwa na kigugumizi katika ufuatiliaji na uchukuzi wa maamuzi juu ya migogoro hiyo.

DC NALICHO AWATIMUA WAVAMIZI MSITU WA SHAMBA LA BIBI

Na Steven Augustino, Tunduru
MWENYEKITI wa kamati ya Ulinzi ya Wilaya ya Tunduru, Mkuu wa Wilaya hiyo Mkoani Ruvuma Chande Nalicho ametoa wiki moja kwa Wakulima na Wafugaji wa jamii ya Kisukuma kuondoka katika eneo la hifadhi ya msitu wa Shamba la Bibi vinginevyo hatua kali za Kisheria zitachukuliwa dhidi yao.
Dc, Nalicho alitoa maagizo hayo baada ya kamati ya Ulinzi na Usalama ya Wilaya hiyo kufanya ziara ya kushtukiza katika msitu huo na kujionea hali halisi ya uhalibifu wa vyanzo vya maji, mabwawa na misitu iliyopo katika hifadhi hiyo inayo unganisha Vijiji vya Nangunguru, Majala na Mkalekawana katika Tarafa ya Nampungu kata ya Nandenbo Wilayani humo.
Alisema anatoa siku Saba kwa watu wote waliovamia msitu huo wa hifadhi kuondoka kwani haiwezekani watu waendelee kuishi wanavyo penda na kuharibu mazingira katika vyanzo vya maji na hifadhi ya misitu kana kwamba serikali haipo
Mkuu huyo aliwataka Watendaji Kata ,Vijiji kwa kushirikiana na Maafisa Tarafa Wilayani humo kutekeleza majukumu yao ikiwemo kuwaelekeza wafugaji kufuata taratibu za kuonana na viongozi wa Vijiji husika, kufanya mikutano inayo wahusisha wananchi katika maamuzi ya kuwapokea wafugaji hao ili kuyaondoa maeneo yao katika migogoro ya aina hiyo.
“Kwavile mifugo ni muhimu kwetu na endapo itatumika vizuri na kwa kuzingatia kanuni, miongozo na maelekezo yanayotolewa na Serikali italeta manufaa kwa Wananchi wetu” alisema Dc, Nalicho na kuongeza kuwa mtindo wa kuishi kwa uhasama kati ya wafugaji na wakulima hauwezi kuwa na tija.
Awali akiongea katika ziara hiyo Afisa misitu wa Wilaya la Tunduru  Rashid Mtotela alimweleza Dc, Nalicho kuwa Wakulima na wafugaji hao walivamia msitu huo mwaka 2006 /2007 na kuendelea kujiimarisha kila mwaka baada ya kubaini kutokuwepo kwa vikwazo vyovyote kutoka Serikalini.
Alisema hifadhi hiyo ambayo awali ilikuwa imeunganishwa na Hifadhi ya Taifa (Selous) tangu mwaka 1974 na baadae kuunda hifadhi shirikishi mwaka 2007 kupitia mradi wa Jont participatory Forest Menegement (JPFM) liyounganisha Vijiji vya Nangunguru, Mkalekawana na Majala kila Kijiji kimekuwa kikikwepa majukumu yake ya kulinda hifadhi hiyo hali ambayo imechangia kuendelea kuhalibika kwa mazingira hayo.
Wakiongea kwaniaba ya Wananchi wa Vijiji hivyo Mwenyekiti wa Kijiji cha Nangunguru Bw.Said Rashid Mkwekwele, Mtendaji wa Kijiji hicho Zainabu Twaha na Afisa Tarafa wa Nampungu Joshua John wakawashushia lawama baadhi ya wakuu wa Idara katika halmashauri ya Wilaya hiyo kuwa umekuwa na kigugumizi katika ufuatiliaji na uchukuzi wa maamuzi juu ya migogoro hiyo.