About


Karibu ujiunge na chuo cha kisasa cha Easy Tech.Computer kwa mafanikio yako,Walimu waliobobea katika fani hiyo wanapatikana chuoni hapo

elimak

elimak

Pages - Menu

Tuesday, May 29, 2012

WAZEE WILAYANI TUNDURU WALILIA MATIBABU BURE

Na Steven Augustino, Tunduru

WAKATI Serikali ikitamba kutoa matibabu bure kwa Wazee na  Watoto chini ya miaka mitano,Wazee Wilayani Tunduru Mkoani Ruvuma wamelalamikia kutozwa fedha pindi wanapoenda kupata huduma za
matibabu,

Hayo yalibainishwa na Shekhe Mkuu wa Baraza la Waislamu Tanzania ( Bakwata) Wilayani humo Alhaji Waziri Alli Chilakweche wakati akiongea na Viongozi wa madhehebu hayo na viongozi wa kimila  katika ibada maalumu ya Hitma ya kuwakumbuka marehemu na wanafamilia wa Mwenyekiti Mstaafu wa Jumuiya ya Wazazi wa CCM Ndawambeb Mugwa iliyofanyika katika Kijiji cha Muhuwesi.

Akifafanua katika hotuba hiyo alhaji Chilakweche alisema kuwa kinacho washangaza wazee hao ni kutotekelezwa kwa ahadi za Serikali katika utoaji wa huduma za matibabu hayo bure mbali na kuwepo kwa taarifa za wazi juuu ya haki kwa wazee hao kupata huduma hiyo bure,

Alisema kama kweli Serikali ilitoa maagizo na maelekezo hayo kwa moyo wote kwanini wanashindwa kusimamia utekelezaji wake? Alihoji Shekhe Chilakweche na kuongeza kuwa kinacho tatanisha ni vitendo vya waliopewa mamlaka kutotambua hata vitambulisho vya misamaha kwa wazee vilivyo tolewa katika ngazi na maeneo tofauti wakidai kuwa wakitaka huduma waende huko.

Alhaji Chilakweche aliendelea kufafanua kuwa endapo Serikali inawapenda wazee na kuthamini mchango wao inapaswa kuzingatia maelekezo hayo ili kuwaokoa wasife kwa kukosa dawa kutokana na kukosa fedha .

Aidha katika hotuba hiyo pia Alhaji Chilakweche akatumia nafasi hiyo kuwaagiza Mashekhe wa Misikiti yote Wilayani humo na viongozi wa kimila kutumia nafasi zao kuwaomba wananchi kujitokeza kwa wingi na kuhakikisha wanahesabiwa katika zoezi la sensa iliyopangwa kufanyika Agosti 26 mwaka huu na kuhakikisha kuwa wanatoa maoni yao katika zoezi la kutafuta maoni ya kuandika katiba mpya.

Mwisho

Sunday, May 27, 2012

MWENGE WA UHURU KUANZA MBIO ZAKE RUVUMA


Kaimu Katibu Tawala Mkoa Ruvuma Severine Tossi Akizungumza na Waaandishi wa Habari jana
Na Stephano Chitete,Songea.

MWENGE wa uhuru unatarajiwa kuzindua ,kuweka mawe ya msingi,kukaguwa na kufunguwa miradi mbalimbali ya maendeleo ipatayo 51 yenye thamani ya jumla ya  sh.1,930,357,902 mkoani Ruvuma iliyojengwa kwa nguvu za wananchi na Serikali.

Akizungumza kwa niaba ya Mkuu wa Mkoa wa Ruvuma Said Mwambu kaimu katibu tawala wa Mkoa wa huo Severine Tossi alisema mbio za mwenge mkoani humo zinatarajiwa kuanza mei 28 mwaka huu hadi juni 3 mwaka huu ambapo utakabidhiwa katika kijiji cha Lumesule kilichopo mkoani Mtwara.

Alisema kuwa miradi itakayozinduliwa iliyojengwa kwa nguvu za wananchi inagharimu sh.206,022,645,halmashauri za Wilaya na Manispaa sh.204,486,125, Serikali kuu sh.773,599,581,wadau wa Maendeleo sh.458,809,551 na ya watu binafsi sh.287,440,000.

Aidha amewataka wananchi wa Mkoa huo kujitokeza kwa wingi kuupokea na kuushangilia mwenge huo wa uhuru ili waweze kupata ujumbe wa mwenge wa mwaka huu usemao "Sensa ni msingi wa mipango ya maendeleo yetu" wenye kauli mbiu shiriki kuhesabiwa Agosti 26 mwaka huu.

Akizungumzia kuhusu maandalizi ya sensa alisema yamekamilika na kufafanuwa kuwa mkoa huu unatarafa 24,kata 140,vijiji 509 na mitaa 79 na kwamba maeneo ya kuhesabiwa watu yaliyotengwa yapo 3,024 na maeneo ya usimamizi yapo 816.

Alifafanuwa kuwa kwa sasa Mkoa unajumla ya wakazi 1,412,084 kwa mujibu wa Sensa ya mwaka 2002 sawa na asilimia ya 2.5 ya ongezeko la watu.

Kaimu katibu Tawala huyo alisema Mwenge huo utakimbizwa katika wilaya mpya ya Nyasa, Mbinga,Songea,Namtumbo,na Tunduru ambapo Juni 3 mwaka huu utakabidhiwa kwa uongozi wa Mkoa wa Mtwara.

MWISHO.

Friday, May 25, 2012

SERIKALI YAAHIDI KUBADILISHA MFUMO WA VOCHA ZA RUZUKU

Na Steven Augustino, Tunduru

SERIKALI imehaidi kubadilisha mfumo wa usambazaji wa pembejeo za ruzuku zikiwa ni juhudi za kumsaidia mkulima wa chini na kuhakikisha kuwa huduma hizo haziwanufaishi wajanja wachache.

Hali hiyo imetokana na kubainika wazi kuwa mfumo wa sasa wa kusambaza pembejeo hizo kwa kutumia mfumo wa vocha umekuwa ukiwanufaisha Mawakala na baadhi ya viongozi na watendaji wa vijiji, Kata ambao hushirikiana na maafisa tarafa  wasio waaminifu.

Hayo yamebainishwa jana  na Viongozi waandamizi wanaosimamia mfuko wa Vocha za Ruzuku Taifa, Afisa Kilimo Wizara ya Kilimo  na Chakula anayesimamia sehemu ya Pembejeo na Flora Kumalilwa  na Mkufunzi Mkuu wa Kilimo Sehemu ya Pembejeo  Stella Mtagwaba wakati wakiongea na kamati ya Usimamizi wa usambazaji wa Pembejo Wilayani Tunduru
katika kikao kilichofanyika katika Ofisi ya mkuu wa wilaya hiyo.

Wakifafanua taarifa hiyo walisema kuwa utaratibu huo mpya ambao kwa sasa unafanyiwa kazi na wataalamu umetokana na idara hiyo kupokea mapendekezo megi kutoka kwa wadau wa Kilimo wakiitaka idara hiyo kufanya mabadiliko katika mfumo huo huku wakibainisha kuwa mfumo uliopo sasa wa kugawa Pembejeo kwa wakulima umekuwa hauna manufaa kwa
walengwa kutokana na kuwepo kwa mianya inayolenga kuwanufaisha wajanja wachache kwa kuuza vocha hizo kwa mawakala.

Sambamba na matarajio hayo ya kubadilisha mfumo huo pia viongozi hao walikiri kuwepo kwa mapungufu makubwa ya ucheleweshaji wa utengenezaji na usambazaji wa Vocha kwa wakulima,kuchelewesha fedha za usimamiaji wa usambazaji wa vocha hizo kwa wakulima na ukubwa wa  bei ya vocha Changamoto ambazo walidai kuwa hivi sasa zinafanyiwa kazi kwa makini ili kuziondoa kabisa kero hizo kuanzia mzimu ujao.

Aidha katika taarifa yao pia pamoja na mambo mengine viongozi hao waliipongeza kamati ya kusimamia usambazaji wa Pembejeo Wilayani humo kwa kufanya kazi vizuri kuanzia ngazi ya uteuzi wa mawakala wa kusambaza pembejeo hizo na kwamba hali hiyo imetokana na baadhi ya
wakulima waliotembelea katika vijiji vya Nandembo, Nanguinguru, Lelolelo na Azimio.

Walisema katika mahojiano kati yao na wakulima hao pamoja na mambo mengine yakiwemo malalamiko ya ukubwa wa bei ya vocha hizo na ucheleweshaji wake wakulima wa maeneo hayo walikiri kupokea vocha hizo na kuzitumia kulingana na maelekezo kutoka kwa mabwana shamba na wakadai kupata mafanikio makubwa kwa kuvuna kati ya magunia 26 na 28 kutoka magunia kati ya magunia 4 na 8 kabla ya mfumo huo kwa ekari moja.

Wakichangia katika kikao hicho kwa nyakati tofauti Mbunge wa jimbo la Tunduru Kusini Alhaji Mtutura Mtutura, Afisa kilimo waWilaya  Jalia Msangi na Afisa kilimo wa Wilaya hiyo  Chiza Marando mbali na kuipongeza serikali kwa kubuni mfumo huo unaolemga kuwanufaisha wakulima  hasa wasio na uwezo waliiomba Serikali kuendeleza juhudi hizo kwa kuanza kuwawezesha kwa kuwakopesha zana za Kilimo yakiwemo Matrekta zikiwa ni juhudi za kuwaongezea uwezo wakulima hao.

Mapendekezo mengine yaliyo tolewa na viongozi hao ni pamoja na kuiomba Serikali kufanya mikataba ya bei ya pembejeo hizo na Mawakala wakubwa mapema ili kuwadhibiti wasipandishe bei ya soka kwa pembejeo husika na kama ambaavyo wamekuwa wakifanya sasa na kusababisha  mfumo huoo kuonekana hauna maana wala manufaa kwa walengwa kutokana na bei za Vocha na Ruzuku inayo tolewa na Serikali kutowiani kwa Asimia 50% kwa
50% na bei za soko la mbolea hizo.

Wakizungumzia mfumo wa vocha walidai kuwa pamoja na sifa ilizopata Wilaya yao katika usimamiaji wa ugawaji wa vocha za Ruzuku lakini wamekuwa wakipambana na changamoto mbalimbali zikiwemo za kuzushiwa kashfa kuwa mawakala wanaoteuliwa hupatikana kwa kutoa Rushwa.

Awali akifungua kikao hicho kaimu Afisa tawala wa Wilaya ya Tunduru, Afisa Tarafa wa Tarafa ya Mlingoti  Manfredi Kahobera Hyera alieleza kuwa  mambo ambayo huzingatiwa katika uteuzi wa Mawakala wa kusambaza Pembejeo za Kilimo kwa mfumo wa Vocha ni kuangalia na kuwachuja kwa makini baada ya kuwabaini Mawakala wasio waadilifu na wenye nia ya kuchakachua vocha bila kupeleka huduma kwa wanufaika.

Katika taarifa hiyo ya  Kahobera aliwataja mawakala waliobainika kuchakachua vocha hizo kuwa ni Michael Mdete ambaye pamoja na kukosa duka la kuuzia Pembejeo hizo lakini alikosa sifa kutokanan na kesi zao zinazoendelea mahakamani baada ya kubainika kuchakachua kwa kugushi na kujipatia Vocha wakati akiwa hajatoa huduma husika kwa wakulima.

Mwisho

Thursday, May 24, 2012

WAGONJWA WAISHUKIA WIZARA YA AFYA UKOSEFU WA EX-RAY RUVUMA

Na Gideon Mwakanosya
BAADHI ya wakazi wa halmashauri ya manispaa ya Songea wameimba serikali kupitia wizara ya Afya na ustawi wa jamii kuona umuhimu wa kuifanyia matengenezo X-ray ya hospitali ya serikali ya mkoa wa Ruvuma ambayo imeshindwa kutoa hiyo kwa wagonjwa kwa muda mrefu na kusababisha wagonjwa wanaotakiwa kupata huduma hiyo kwenda kwenye hospitali ya Peramiho ambako ni mbali na Songea mjini.

Wakizungumza na NIPASHE kwa nyakati tofauti baadhi ya wananchi wa maeneo ya Mfaranyaki, Mjimwema, Ruhuwiko na Mshangano ambao waliomba majina yao yahifadhiwe walieleza kuwa kwa muda mrefu sana huduma ya X ray katika hospitali ya mkoa haipatikani na wanapokwenda hospitalini hapo kupata huduma wamekuwa wakishauriwa kwenda Hospitali ya misheni ya Peramiho ambako ndiko huduma hiyo kwa sasa inatolewa.

Wananchi hao walisema kuwa ni vyema serikali ikaangalia uwezekano wa kuitengeneza mashine hiyo ambayo hapo awali ilikuwa msaada mkubwa kwa wakazi wa Songea na wagonjwa wanaotoka kwenye wilaya nyingine kama vile Mbinga, Natumbo, Tunduru na wilaya mpya ya Nyasa.

Walitoa mfano kuwa hivi karibuni katika eneo la Seedfarm kwenye barabara itokayo Songea kwenda Namtumbo gari la jeshi la wananchi liliwagonga watu wanne ambao walikuwa wakitembea kwa miguu na kusababisha watu wawili kufa papo hapo na wengine wawili walijeruhiwa vibaya na kukimbizwa katika hospitali ya serikali ya mkoa ambako mmojakati yao baadae ililazimika kumpeleka Peramiho baada ya hospitali hiyo kukosa huduma ya X ray jambo ambalo limeonekana kuwa ni kero kubwa kwa wananchi wa Songea na maeneo mengine.

Kwa upande wake kaimu mganga mkuu wa mkoa wa Ruvuma Dr Benedict Ngaiza alipohojiwa na NIPASHE kuhusiana na malalamiko hayo alikirikuwa mashine ya x ray ya hospitali ya serikali ya mkoa wa Ruvuma bado ni mbovu tangu mwezi mmoja uliopita.

Dr Ngaiza ambaye pia ni mganga mfawidhi wa hospitali ya serikali ya mkoa Songea alisema kuwa pamoja na kwamba katika hospitali yake haukuna huduma hiyo ya x ray lakini wagonjwa wanaohitajihuduma hiyo hushauriwa kwenda kupta huduma hiyo kwenye hospitali ya misheni ya Peramiho licha ya kuwa nayo maashine ya hospitali hiyo inaubovu haifanyi kazi kwa kiwango kinachotakiwa.

Alisema kuwa changamoto baadhi ya huduma zinazohusisha huduma ya x ray katika hospitali ya mkoa zimesimamishwa kwa sasa. Hadi hapo wataalamu toka wizara ya afya na ustawi wa jamii watakapofika na kuja kuifanyia matengenezo.

Alieleza zaidi kuwa kwa mujibu wa taarifa toka wizara ya afya na ustawi wa jamii mafundi wanatarajiwa kusambazwa katika hospitali zote za serikali zenye mashine za x ray kwa ajili ya kuzifanyia matengenezo x ray hizo ikiwemo na x ray ya hospitali ya serikali mkoa Songea.

Alifafanua zaidi kuwa pamoja na matengenezo yanayotarajiwa kufanyika bado hali si nzuri kwani chumba cha x ray kinatarajiwa kufanyiwa urakabati mkubwa ambao utafanywa kwa muda wa zaidi ya miezi mitatu. Hivyo hata kama mashine hiyo itakapo tengenezwa bado huduma ya x ray itasimama hadi ukarabati wa chumba hicho utakapo kamilika.

TANI 5480 ZA KOROSHO ZILIZOKWAMA TUNDURU ZAPATA MNUNUZI

Na AUGUSTINO CHINDIYE, Tunduru
JUMLA ya tani 5480 za korosho za Wakulima wa Tunduru Mkoani Ruvuma zilizo kuwa zimekwama katika Vyama vya Msingi vya Wakulima vya Wilaya hiyo baada ya Serikali kutoa dhamana ya fedha za Kugharamia malipo kwa Wakulima husika zimepata mnunuzi.

Taarifa ya kupatikana kwa mteja wa Korosho hizo imetolewa na Meneja wa
Chama kikuu cha Wakulima wa TAMCU  Imani kalembo jana wakati akiongea na wajumbe na wadau wa taasisi hiyo Wilayani humo katika kikao kilichofanyika katika ukumbi wa Ofisi za Chama hicho mjini hapa.

Akitoa taarifa hiyo Kalembo alisema kuwa Korosho hizo zenye thamani ya Shilingi Bilioni 8 zimenunuliwa na kampuni ya Pan- African Consulting And Exportng (P.A.C.E) kutoka Carfonia
Martekan ambayo imekubali kununua korosho hizo kwa bei ya Shilingi 1491 kwa kila kilo moja.

Kalembo aliendelea kueleza kuwa tayari kampuni hiyo imekwisha tiliana saini mkataba wa kununua Korosho hizo na kuzifanyia uchunguzi wa kuzikagua kwa kuzikata ili kubaini ubora wake na kuahidi kuzilipia kwa kuingiza fedha Benki ya Nmb  muda wowote wiki hii.

Alisema kufuatia hali hiyo Chama hicho kinajipanga kuangalia uwezekano na taratibu za kulipa madeni yote ya wakulima ili kuondokana na kero hiyo iliyochukua muda mrefu.

Kwa mujibu wa takwimu za uzalishaji wa wa zao hilo kutoka katika Chama Kikuu cha Ushirika wa Wakulima wa Korosho Wilayani Tunduru (TAMCU) zinaonesha kuwa katika msimu wa Mwaka 2011/2012 chama hicho kupitia vyama vya msingi umeongezeka na kufikia kilo 7,570,000 kutoka kilo kilo 4,135,042 zilizo zalishwa  mwaka 2010/2011.
Mwisho

Wednesday, May 23, 2012

BARAZA LA MADIWANI HALMASHAURI YA WILAYA YA MBINGA LAANZA KIKAO CHAKE AMBAPO HOJA NA TAARIFA MBALIMBALI ZA KAMATI ZINAENDELEA KUTOLEWA

 Madiwani wakiwa wamesimama ikiwa ni ishara ya heshima wakati Mwenyekiti wa Halmashauri Oddo Mwisho, Makamu Mwenyekiti wa Halmashauri Priska Haule na Mkurugenzi wa Halmashauri hiyo Shaib Mnunduma wakiingia kwenye kikao hicho
 Mwenyekiti wa Halmashauri ya Wilaya ya Mbinga Oddo Mwisho (katikati) akifungua kikao, kulia ni Mbunge wa Jimbo la Mbinga Mashariki Gaudence Kayombo na kushoto ni Mkurugenzi wa Halmashauri hiyo Shaib Nnunduma wakiingia kwenye kikao hicho
 Waandishi wa kikao cha Baraza la Madiwani wa Halmashauri hiyo wakiendelea kufuatilia hoja mbalimbali
 Makamu Mwenyekiti wa Halmashauri ya Wilaya ya Mbinga ambaye pia ni Mwenyekiti wa Kamati ya kudumu ya fedha, mipango na uongozi Prisca Haule akiwasilisha taarifa ya kamati

 Madiwani wakiendelea kufuatilia hoja mbalimbali zilizokuwa zinawasilishwa katika kikao hicho kutoka kwa wajumbe
Wenyeviti wa kamati za kudumu za Madiwani wa Halmashauri hiyo wakiendelea kufuatilia taarifa zao kwa umakini

AZIMIO LA ARUSHA, MWAROBAINI PEKEE ULIOBAKI


 
Paschally Mayega
RAIS wangu Kikwete, nalilia Azimio la Arusha sasa kuliko wakati mwingine wowote! Kuachwa kwa baadhi ya mawaziri kumeibua mambo ya kuogofya ambayo yanaweza yakatupeleka kwenye mwisho wa aibu kubwa!

Baadhi ya wananchi wa Jimbo la Moshi Vijijini wanasema mbunge wao hakutendewa haki kuachwa katika baraza la mawaziri.

Raymond Assenga, mmoja wa wananchi hao alisema, “Mwaka 2010 Chami alituunganisha, tukachanga zaidi ya milioni 50 kusaidia kampeni za Rais”.

Hili ndilo neno linalotakiwa litolewe ufafanuzi. Zilichangwa milioni 50 kama bei ya kuununua uwaziri? Uwaziri 2010 ulikuwa unauzwa? Hii ikithibitika, itakuwa ni kashfa kubwa!

Kama hivyo ndivyo, je, wale mawaziri wawili ambao nao walituhumiwa kama mbunge wao Cyril Chami lakini wao wamo watakuwa walichangia shilingi ngapi? Ukiifikiria sana hali hii damu inaweza ikakusimama mwilini, hebu tuifikirie kwa kibonzo hiki.

Uongozi wa Kampuni moja tajiri sana duniani, mabingwa wa kutengeza chapati walitaka kuweka tangazo la chapati zake katika sehemu litakakosikika dunia nzima.

Wakakusanya masanduku mengi yaliyojaa fedha nyingi wakampelekea Baba Mtakatifu, Papa, wakimwomba awaamuru Wakristu wote duniani, wanaposali sala ya Baba yetu uliye mbinguni, badala ya ile sentensi wanayosema, ‘utupatie leo mkate wetu wa kila siku’, waseme, ‘utupatie leo chapati yetu ya kila siku’.

Baba Mtakatifu alipozikataa hela nyingi kiasi kile, Jamaa walizimia. Eti walishindwa kuelewa ni kiasi gani cha fedha kampuni ya kutengeneza mikate ilimpatia Baba Mtakatifu mpaka akakubali mkate utangazwe katika sala ya Baba yetu.

Rais wangu sasa inanijia akilini, wakati Jumanne Maghembe akiwa waziri wa Elimu, wadau wa elimu walifanya kila waliloweza kumwambia kuwa mtindo wa kitabu kimoja cha kiada pamoja na kwamba ni kuua elimu nchini lakini huko ni kuchochea rushwa kubwa kabisa!

Alikuwa mbogo mtu huyu sijapata kuona mfano wake. Lakini ni kweli kulikuwa na minong’ono mitaani kuwa waziri aliagizwa kuandaa mazingira ya uchaguzi mkuu 2010.

Kama naye alichangia, atakuwa alichangia kiasi gani mpaka abakishwe? Natamani hii isiwe kweli! Inapofikia watu wanauza mpaka elimu ya nchi nzima, ni kipi wanakuwa wamebakisha cha kuutambulisha utu wao? Mavazi tu!

Kama watu walilipia uwaziri nani atakuwa na ubavu wa kuwaamuru mawaziri hao? Utajikuta unalazimika kuunda baraza la mawaziri kubwa kuliko mahitaji halisi ya nchi. Hili tumeliona mara zote! Kulipa fadhila!

Hawa ni mawaziri. Kuna wakuu wa mikoa na wilaya. Au ndiyo sababu uteuzi wa wakuu wa wilaya imechukua miaka miwili? Yawezekana pia ikawa ni sehemu ya sababu ya kuongeza mikoa na wilaya? Tuendako, siko!

Mwenyekiti wa chama cha wananchi (CUF) Profesa Ibrahim Haruna Lipumba alipozungumza na waandishi wa habari jijini Dar es salaam, Aprili 24 mwaka huu alisema, “Tatizo la ubadhirifu haliwezi kwisha katika serikali ya awamu ya nne maana tatizo siyo watendaji wala mawaziri, ni Rais Kikwete mwenyewe…amekuwa ni mtu asiyekuwa na uamuzi.”

Alisema, “Haishangazi kuona mawaziri katika wizara moja hawaelewani. Kuna mawaziri wana nia njema na wanasimamia haki, lakini hata wakitoa mapendekezo yao yanapuuzwa.

Na wapo wanaotumia nafasi zao vibaya huku rais akiendelea kuwachekea.” Nadhani ufunuo wa hapo juu ulikuwa haujamfikia. Utamfanya nini mtu aliyejilipia?

Naye Katibu Mkuu wa CHADEMA Dk. Willibrod Slaa akihutubia mkutano mkubwa wa hadhara katika viwanja vya Sahara Aprili 22 mwaka huu jijini Mwanza alisema, ”Uozo uliofanywa na mawaziri umekuwa ukipata baraka zake, kama

Mwenyekiti wa Baraza la Mawaziri na amekuwa na kawaida ya kulinda ubovu wa mawaziri wake kutokana na udhaifu wake mwenyewe wa kiuongozi.” Maskini Mwalimu Nyerere hakujua kama Ikulu kuna biashara. Nyumba ya baba yangu itageuzwa pango la walanguzi!

Dk. Slaa aliendelea kusema, “Kikwete ndiye chanzo cha udhaifu wote serikalini unaosababisha matatizo makubwa kwa taifa na kwa wananchi”. Huenda rais wetu si dhaifu kiivyo ila ikawa ndiyo hitaji ya mazingira ya biashara iliyofanyika.

Waziri Mkuu mstaafu, Edward Lowassa hivi karibuni alikaririwa akisema, “Muundo na imani ya chama cha mapinduzi ni mzuri. Tatizo ni uongozi katika utendaji. Ni dhaifu mno katika kufanya maamuzi.

Mara nyingine yamefanyika maamuzi yasiyo sahihi na wakati mwingine maamuzi yakifanyika yanafanyika yakiwa yamechelewa mno kiasi cha kuyafanya yaonekane ni maamuzi yasiyo na maana yoyote”.

Kama hawataki kukosolewa, watatakaje kujirekebisha? Mtu huyu alishiriki kikamilifu kuwaletea Watanzania uongozi wa awamu ya nne, inawezekana vipi asiujue udhaifu wa waliokuwa washirika wake?

 Lakini Edward Lowassa, kama alivyo Abdulrahman Kinana lazima wajue kuwa wana deni kubwa kwa Watanzania kutokana na maisha magumu waliyonayo sasa ambayo ni matokeo ya uongozi walioupigania.

Ndugu Rais wakati wa kuja mwaka 2005 ulikuja na Edward, ilibidi wakati wa kuondoka uondoke na Edward vinginevyo wananchi wataamini maneno ya Dk. Slaa kuwa, “Ni kiongozi anayekwepa lawama na kubebeshwa mzigo wa uzembe wake kwa watu wengine”.

Mlianza vema kwa maagizo mfululizo yaliyokuwa yanatoka Dar es Salaam kwenda mikoani, wilayani hadi vijijini. Hakukuwa na mzaha. Hali hii ilipelekea pia mateso fulani kwa baadhi ya wananchi na hasa pale viongozi wa vijijini walipojaribu kukabiliana na kasi ya maagizo katika shughuli za maendeleo hasa ujenzi wa shule za kata. Watu walinyang’anywa mifugo yao na madhila mengine mengi.

Msingeweza kuepuka kufanya makosa kwa sababu nyinyi nanyi ni wanadamu, lakini mlijijengea heshima kwa wananchi kwasababu kila tulipoandika kukosoa utendaji wenu mlifuatilia na kuchunguza na ilipobidi mkasahihisha bila kusubiri mateso kwa watu wenu kuzidi.

Tofauti na sasa ambapo huwezi kuthibitisha kama wanasikia au hawasikii. Kama hawasomi haya tuandikayo ni kwa hasara yao wenyewe kwasababu wananchi wanasoma.

Richmond ni matokeo ya viongozi kutaka kufanya biashara. Haya ndiyo makatazo yaliyomo katika Azimio la Arusha. Baba waambie watu wako, ‘mnahofia nini’ na Edward Lowassa kuhusu Richmond?

Tofautianeni lakini tambueni kuwa siku ya hukumu wananchi watawahukumu pamoja!
Kutokana na mparaganyiko wenu wahuni wachache wametumia fedha na raslimali nyingi za nchi kwa kisingizio cha kupinga ufisadi na gamba!

Aliyeileta Richmond alitenda dhambi kubwa. Waliowabebesha watu wengine dhambi ya Richmond walitenda dhambi kubwa zaidi na ndiyo maana hawana amani katika vifua vyao siku zote.
Wasipotubu, itawawewesesha usiku na mchana mpaka siku yao ya hukumu itakapowafika!

CHADEMA wamesema watazingatia Ibara ya 8 ya katiba waende kwa wananchi ili ipigwe kura ya kutokuwa na imani na Rais. Nchi imekwama. Tutatokaje hapa tulipokwama? Baba hakuna tulichoachiwa hapa cha kuchagua.

Kuiepusha nchi isiingie katika vurugu tulirejelee Azimio la Arusha ili tuanze upya! Nchi imevurugwa kupita maelezo.

Rais wangu nchi iko katika mchakato wa kuandika katiba mpya. Hili ni jambo jema sana. Lakini tunataka katiba mpya, ili iweje? Katiba mpya haiwezi kutuletea chakula wala maisha bora.

Katiba mpya itashusha bei ya vyakula? Bila uongozi makini, imara katiba mpya itafaa vipi? Swali hapa ni je, tunaye msimamizi imara wa kusimamia hiyo katiba mpya?

Katiba tuliyonayo ndiyo ileile aliyokuwa akiitumia Baba wa Taifa Mwalimu Julius Kambarage Nyerere wakati wa urais wake.

Ni katiba ileile aliyokuwa anaitumia Rais wa awamu ya pili, Ali Hassan Mwinyi na Benjamin William Mkapa, Rais wa awamu ya tatu ukiacha marekebisho madogo madogo ya hapa na pale.

Imewezekanaje imekuwa mbovu kupindukia ghafla tu katika awamu ya nne?
Katiba hii hii na ubovu wake huu huu usingekuwa kero kubwa kwa nchi kama inavyoonekana sasa, kama Azimio la Arusha lingekuwapo.

Maadili na miiko ya uongozi viliyokuwa vimezingatiwa ndani ya Azimio ya Arusha visingeruhusu hali hii kufikia hapa.

Rais wangu ni mengi yamesemwa na kuandikwa juu ya Azimio la Arusha. Hata wakati fulani Baba wa Taifa Mwalimu Julius Kambarage Nyerere alisikika akisema, “Kila ninapotembea mfukoni mwangu ninakuwa na vitabu viwili. Biblia Takatifu na Kijitabu cha Azimio la Arusha”.

Mwalimu Nyerere alilienzi Azimo la Arusha kama sala. Wakati akiwa madarakani Nyerere hakuchoka kulihubiri Azimio la Arusha kwa watu wake. Alifanana na mitume na manabii waliohubiri habari njema kwa mataifa.

 Nchi ilitulia. Upendo na mshikamano kati yetu vilistawi kiasi cha kutufanya tushindwe kutambua tofauti zetu.

Ndani ya Azimio la Arusha wote tulikuwa ndugu na tuliitana ndugu toka mkuu wa nchi mpaka mponda kokoto! Tukajivunia amani ya kweli ilikuwa imetamalaki nchi nzima hadi vifuani mwetu! Nje ya Azimio la Arusha tuna waheshimu wezi na mafisadi. Mungu atawalaani wote!

Nyerere alipong’atuka manyang’au wakalihujumu hata wakalifuta. Yeyote aliyeshiriki kuliua Azimio adhimu la Arusha, Jua la Mwenyezi Mungu limwakie na siku yake ya mwisho ikifika raha ya milele hataipata wala mwanga wa milele hautamwangazia!

Mwalimu alilia! Akiwa amesimama mbele ya mkungu uliokuwapo mbele ya nyumba yake alimtazama katibu mkuu ofisi ya rais, akageuza uso wake na kumwangalia kwa muda Waziri wa Nyumba na Maendeleo Mijini, Edward Lowassa, kisha akasema, “….na nyinyi wengine, mkilivunja Azimio la Arusha kabisa kabisa, mtakuja kupata taabu sana baadaye.”

Wakati huu ndiyo naelewa ni uchungu kiasi gani Mwalimu alikuwa nao moyoni mwake wakati akitamka maneno hayo! Aliiona Tanzania ya bila Azimio la Arusha! Aliwaona viongozi wetu wa bila Azimio la Arusha, kisha akaiona dhiki kuu itakayowashukia watu wake kwa kukosekana Azimio la Arusha! Akasema, “Mtakuja kupata taabu sana baadaye!”

Naye akisha kuyasema hayo aliondoka katika eneo la mkungu tulilokuwapo, akaingia ndani katika kiofisi chake cha pale nyumbani kwake, Msasani. Alikuwa mtu mzima lakini unamwona anaingia ndani akiwa amechoka kabisa si kwa uzee bali kwa kuwahurumia watu wake maskini ambao sasa nadhani aliwaona wamebaki yatima.

Baadhi ya watu waliitwa ndani wakaongee faragha na Mwalimu. Nami pia niliitwa. Mwalimu hakuwa na mengi ya kusema zaidi ya kulalamika tu, kitu ambacho kilinifanya nijue kuwa alikuwa anaumizwa sana na jinsi viongozi wa serikali walivyokuwa wakiongoza.

Naikumbuka siku ile kama vile ilikuwa jana. Baba wa Taifa Mwalimu Julius Kambarage Nyerere akitumia mkono wake wa kulia alimshika Edward Lowassa mkono wa kushoto maana walikuwa wamekaa sambamba, akamtamkia maneno mazito usoni mwake katika sentensi tatu! Maneno yale kutoka katika kinywa cha Mwalimu yaliniingia na kuninyong’oneza kabisa, utadhani nilikuwa naambiwa mimi!

Aliyoendelea kusema Mwalimu nilibaki nasikia tu lakini nilikuwa sielewi kitu tena mpaka tulipoondoka!

Ndugu Rais, acha mimi leo nilililie Azimio la Arusha! Siku nyingine Mwenyezi Mungu akipenda nitakwambia maneno ambayo Baba wa Taifa aliyomtamkia Edward Lowassa usoni pake!

Nayakumbuka maneno yale, nukta kwa mkato! Edward alimjibu Mwalimu kwa unyenyekevu mkubwa.

Nyakati zimepita na sasa zimetimia. Siku za majaribu zinawasonga Watanzania, wakumlilia hawamwoni.

Viongozi wetu ndio hawa wa kununua na kuuza uongozi. Mwalimu Nyerere aliwatabiria dhiki kuu watu wake baada ya yeye kuuondoka ulimwengu huu wa mateso!

Leo Watanzania wanaporwa kila kitu! Wamebaki kuchechemea kwa ugumu wa maisha huku viongozi wao na familia zao wakiwa katika ukwasi wa kutisha!

Wananchi wamefanywa kama kuku wa kienyeji. Wanaachwa wajilishe wenyewe, jioni warudi. Mpaka siku wanapotakiwa kuchinjwa ndipo wanatupiwa mtama kidogo! Kapelo, fulana, kanga na buku mpaka uchaguzi ujao!

Aliposikia viongozi wa Tanzania wanapokewa kwa shangwe duniani kwa uhodari wao wa kuuza ardhi, Mwanamwema Anney Anney alinitumia ujumbe uliosomeka: “Nilikaa Segerea miezi 5. Nikaendesha kesi mwaka mzima, nikashinda! Kisa nilisema Jakaya Mrisho Kikwete anauza ardhi yetu pamoja na utu wetu kwa Wazungu na Wahindi.

Leo (18-5-2012) BBC asubuhi wametangaza, Tanzania inaongoza kwa kasi ya kutisha kuuza ardhi kwa wageni katika ukanda wa Afrika Mashariki. Ni Mayega tu aliyenisemea nikiwa jela! Kosa langu lilikuwa ni nini?”

Mwanamwema Anney Anney endeleeni kuomboleza. Kilio cha wenye haki Mungu anasikia! Alisikia kilio chako ukiwa gerezani! Akasikia na sauti yetu tuliyomlilia, leo uko huru nao watesi wako wameandaliwa anguko la aibu!

Siku zimekaribia ambapo milango ya Magereza itafunguka na wote walioko nje bila kuwa na haki wataingia humo, nao wenye haki waliokuwa ndani watatoka, kwa maana mtetezi wetu yu hai!

Rais wangu, warudishie Watanzania Azimio lao la Arusha upate heri na miaka mingi hapa duniani. Nanyi wana wa nchi hii yawapasa kufahamu kuwa wakuwakomboa hakuna.

 Yawalazimu mjikomboe nyinyi wenyewe. Yeyote anayekuja kwetu kutaka kutuongoza aje na ahadi ya Azimio la Arusha.

Bila hivyo naye hatufai! Nchi yetu kwanza! Vyama vyote vya siasa na uzuri wa viongozi wake baadaye! Kuendelea kulialia tu na kulalamikalalamika bila

Azimio la Arusha katika nchi hii, ni sawa na kung’ang’ana kunyoosha kivuli cha mti uliopinda! Azimio la Arusha, ndiyo mwarobaini pekee uliobaki! Mwenyezi Mungu awabariki nyinyi wote!
 

Friday, May 18, 2012

MKUU WA MKOA WA RUKWA AWAAPISHA WAKUU WA WILAYA WAPYA MKOANI HUMO JANA NA KUWAPA MAAGIZO 16 YA KUANZA NAYO KAZI

Mkuu Mpya wa Wilaya ya Sumbawanga Mathew S. Sedoyeka akila kiapo cha utii mbele ya Mkuu wa Mkoa wa Rukwa Injinia Stella Manyanya leo katika ukumbi wa Ikulu ndogo katika Manispaa ya Sumbawanga baada ya uteuzi wa hivi karibuni wa Mhe. Rais Dkt. Jakaya Mrisho Kikwete kushika madaraka hayo kutoka kwa aliyekuwa Mkuu wa Wilaya hiyo Kanali John Antonyo Mzurikwao.
Mhe. Sedoyeka akisaini kiapo hicho mbele ya Mkuu wa Mkoa wa Rukwa Stella Manyanya.
Mkuu wa Wilaya mpya ya Kalambo Luteni Edward O. Lenga akila kiapo cha kuiongoza Wilaya hiyo mpya mbele ya Mkuu wa Mkoa wa Rukwa Injinia Stella Manyanya baada ya kuteuliwa hivi karibuni na Mhe. Rais Dkt. Jakaya Mrisho Kikwete kuwa Mkuu wa Wilaya wa Kwanza wa Wilaya hiyo mpya iliyomegwa kutoka katika Wilaya ya Sumbawanga.
Mkuu wa Mkoa wa Rukwa Injinia Stella Manyanya akimkabidhi kitendea kazi Mkuu wa Wilaya mpya ya Kalambo Luteni Edward Lenga ambayo ni Katiba ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania atayoitumia kama muongozo wa shughuli zake za kila siku awapo madarakani.
Mkuu mpya wa Wilaya ya Nkasi Iddi Kimanta akila kiapo mbele ya Mkuu wa Mkoa wa Rukwa Injinia Stella Manyanya leo katika ukumbi wa Ikulu ndogo Mkoani Rukwa. Mkuu huyo wa Wilaya maechukua nafasi ya aliyekuwa Mkuu wa Wilaya hiyo Joyce Mgana baada ya uteuzi wa hivi karibuni wa Mhe. Rais Dkt. Jakaya Mrisho Kikwete.
Mkuu wa Mkoa wa Rukwa Injinia Stella Manyanya akisaini hati ya kiapo cha Mhe. Iddi Kimanta baada ya kuwaapisha wakuu wote watatu wa Wilaya za Sumbawanga, Kalambo na Nkasi.

PICHA, HOTUBA NA MATUKIO ZAIDI

Thursday, May 17, 2012

RC ENG, MANYANYA AKEMEA MAUAJI YA KISHIRIKINA RUKWA

 Na Elizabeth John, Rukwa
MKUU wa Mkoa wa Rukwa, Injinia Stella Manyanya,  amekemea kushamiri kwa vitendo vya mauaji  ya imani za  kishirikina vinavyofanywa na baadhi ya watu.

Akizungumza na Tanzania Daima kwa njia ya simu juzi, alisema matukio hayo ambayo yamepoteza maisha ya watu kadhaa katika kipindi cha miaka miwili sasa, yamechangiwa na wakazi wengi wa vijiji mbalimbali mkoani humo kuamini uchawi.

Manyanya aliongeza kuwa matukio hayo yamekuwa yakiufedhehesha mkoa huo lakini pia yamerudisha nyuma jitihada za baadhi ya wananchi ambao wamekuwa wakitumia muda mwingi kujitafutia maendeleo yao.

“Hali hii si nzuri kwani wengi wameuawa kutokana na wivu wa baadhi ya wakazi wenzao ambao wamekuwa wakishuhudia maendeleo ya kasi na mwisho wa siku wanawazushia uchawi, jambo ambalo si la kweli,” alisema Manyanya.

Alisema kuwa wanaofanya vitendo hivyo vya mauaji hawana tofauti na wahuni wengine wasiopenda maendeleo ya wanakijiji wenzao.

Kumekuwa na matukio mengi ya mauaji yanayotokana na imani za kishirikina ambapo wiki mbili zilizopita, wazee wawili wa Kijiji cha Miangalua wilayani Sumbawanga waliuawa sanjari na nyumba 42 kubomolewa na kuchomwa moto.

Katika tukio hilo pia wanakijiji waliteketeza mifugo mingi, kutokana na hasira za wenzao kumtuhumu mwanakijiji huyo kumroga kijana  mmoja, Festo Chambanenge, ambaye alifariki dunia baada ya kuugua kwa muda mrefu.

Wednesday, May 16, 2012

Yeah: Sasa ni Undava Undava tu! [WANAFUNZI WAASI, MKUU WA SHULE ANUSURIKA KUUAWA)


Yeah: Sasa ni Undava Undava tu! [WANAFUNZI WAASI, MKUU WA SHULE ANUSURIKA KUUAWA) LOL

MKUU WA SHULE ANUSURIKA KUUAWA

Katika tukio lingine, Mkuu wa Shule ya Sekondari ya Muhoro iliyopo Wilaya ya Rufiji, mkoani Pwani, ameponea chupuchupu kuuawa na wanafunzi baada ya kukimbilia porini akikwepa kipigo kutoka kwa wanafunzi wapatao 400.
...

Vurugu hizo zilitokea jana asubuhi baada ya wanafunzi hao kuasi na kuzingira shule kabla ya kufunga barabara itokayo Dar es Salaa kwenda Mtwara na kusababisha abiria kukwama kwa muda.

Kwa mujibu wa shuhuda mmoja, wanafunzi hao walikuwa wanamtuhumu mwalimu wao aliyejulikana kwa jina moja la Mwita, kuwa anawalisha ugali na maharage kila siku pamoja na kushindwa kuwapa tisheti za shule licha ya kuwa wamezilipia.

Wanafunzi hao pia wanamtuhumu mwalimu huyo kwa kushindwa kuandaa mikakati ya kuwawezesha kushiriki katika michezo ya shule pamoja na kushindwa kuwapatia vitambulisho vya shule.

Shuhuda huyo alisema mwalimu huyo baada ya kuona wanafunzi wameasi na kuanza kuzingira eneo la shule, alikimbilia porini kukwepa kipigo.

Kutokana na vurugu hizo, wanafunzi wawili walijeruhiwa na hali zao ni mbaya, huku wengine 12 wakiwa wanashikiliwa na Jeshi la Polisi katika wilayani Rufiji.

Taarifa kutoka eneo la tukio zilisema kuwa, baada ya abiria ambao magari yao yalizuiwa kupita walishuka na kuanza kushirikiana na polisi kuwaondoa wanafunzi hao barabarani.

Mapambano hayo yalikuwa makali baada ya wanafunzi kuanza kuchukua mawe kutoka barabarani na kuanza kuwapiga abiria, ambapo baada ya kuzidiwa walikimbilia vijijini kujificha.

Vurugu hizo zilisababisha Mkuu wa Mkoa wa Pwani, Mwantumu Mahiza, kufika eneo la tukio na kufanya kikao cha dharura jana jioni, ambapo aliahidi kushughulikia kero za wanafunzi hao haraka na kuzipatia ufumbuzi.

Mahiza akizungumza na NIPASHE jana jioni alithibitisha kwenda eneo la shule hiyo kutafuta suluhu ya vurugu hizo.

Mahiza alisema vurugu hizo zilimalizika na kwamba ameuagiza uongozi wa wilaya na Kamati ya Ulinzi na Usalama ya wilaya kushughulikia madai ya wanafunzi hao.

Hata hivyo, Mahiza alisema wanafunzi hao walikuwa na hoja, lakini hawakuwa na sababu ya kufanya vurugu na kufunga barabara.

“Hawa wanafunzi kufunga barabara na mgogoro wao na uongozi wa shule kuna uhusiano gani kama siyo ukorofi wa wanafunzi?” alihoji.

Alisema wanafunzi wanane wanashikiliwa na Jeshi la Polisi kwa ajili ya mahojiano ili kubaini vinara walioanzisha vurugu hizo.

Imeandikwa na Emmanuel Lengwa, Rungwe; Ashton Balaigwa, Ulanga na Richard Makore, Dar.
CHANZO: NIPASHE

WAMILIKI WA MASHINE WAMSHUKIA WAZIRI WA NISHATI NA MADINI

Na Stephano Mango, Songea
WAMILIKI wa mashine za kukoboa na kusaga nafaka katika Halmashauri ya Manispaa ya Songea mkoani Ruvuma wamemshukia Waziri wa Nishati na Madini Profesa Sospeter Muhongo kwa kitendo chake cha kukaa kimya wakati wananchi wanateseka kwa kukosa nishati ya umeme kwa muda mrefu
Wakizungumza na waandishi wa habari jana wamiliki hao walisema kuwa kitendo cha waziri huyo kukaa kimya kinaashiria kushindwa kwake kazi toka mapema kwani haiwezekani wananchi wanateseka bila kuwa na nishati ya umeme na kusababisha gharama za maisha kupanda
Walisema kuwa kitendo cha shirika la umeme mkoani humu kushindwa kutoa huduma hiyo kwa wakati mbali ya kusababisha usumbufu kwao pia kimekuwa kikiwakosesha mapato ambayo wanayatumia kulipa kodi kwenye mamlaka ya mapato Tanzania(TRA) kutokana na hasara zinazosababishwa na ukosefu wa umeme
Mkurugenzi wa kampuni ya Mtazamo Enterpress, Julius Mlawa akizungumza na waandishi wa habari waliotembelea kiwanda cha kampuni hiyo kinachojishughulisha na ukoboaji nafaka, usagaji na uuzaji wa unga alisema kuwa wananchi wa Manispaa ya Songea wanapaswa kuokolewa kutokana na mgao mkubwa na usio na kikomo wa umeme unaoendelea kuwakabili
Mlawa alisema kuwa mashine za kusaga nafaka ambazo zipo katika baadhi ya maeneo ya Manispaa hiyo zimeshindwa kutoa huduma kwa muda muafaka na kusababisha wananchi walio wengi kulazimika kutembea umbali mrefu kufuata huduma nje ya Manispaa ambako kuna mashine za kusaga nafaka zinazotumia mafuta ya Dizeli na kusababisha bei ya huduma hiyo kupanda mara mbili ikilinganishwa na awali
Alisema kuwa bei ya unga wa mahindi ambayo hapo awali ilikuwa ni shilingi 500 kwa kilo hivi sasa kilo moja ya unga wa mahindi ni shilingi 1200 na bei ya mchele kwa miezi iliyopita kabla ya tatizo la umeme halijaanza kujitokeza kama ilivyo sasa ilikuwa ni shilingi 1000 kwa kilo lakini hivi sasa kilo moja ya mchele ni kati 1800 hadi 2000.

Alifafanua kuwa bei hizo zinaendele kupanda siku hadi siku kutokana na TANESCO  kushindwa kutoa huduma ya umeme kwenye maeneo ya manzese, Mfaranyaki , Bombambili, Majengo, Lizaboni Mjimwema na Msamala ambako ndiko kuna mashine nyingi zinazo saga nafaka  na badala yake umekuwa ukiwashwa kwa mgao ambao ratiba yake haufahamiki  kwa wamiliki wa mashine hizo.

Alisema kuwa katika kiwanda chake kuna wafanyakazi zaidi 30 ambao wanashinda kiwanda wakisubiri umeme ili waweze kufanya kazi bila mafanikio huku wakilipwa posho zao za kila siku bila kufanya kazi jambo linalosababisha hasara kubwa
Alieleza zaidi kuwa kutokana na ukosefu wa umeme ambao umekithiri katika manispaa ya Songea wafanyabiashara wengi wanashindwa kurejesha mikopo waliyokopa kwenye taasisi za fedha jambo ambalo ni hatari kwa biashara zao na jamii ambayo inanufaika na biashara hizo
Alisema kuwa kutokana na hali hiyo huenda akalazimika kusitisha kwa muda kutoa huduma ya usagaji na ukoboaji wa nafaka kama hali hiyo ya ukosefu wa umeme wa uhakika haitafanyiwa kazi na shirika hilo la umeme mkoani humu kwa sababu mbali ya kukosa mapato lakini imekuwa ni usumbufu kwa wananchi ambao wanahitaji huduma hiyo.
Kwa upande wake Meneja wa shirika la umeme mkoa wa Ruvuma Mhandisi Monika Kebara alikiri kuwepo kwa tatizo hilo na alisema hivi sasa huduma hiyo ya umeme inatolewa kwa mgawo kwa sababu uwezo wa ufuaji wa umeme umepungua sana kutokana na kuharibika kwa mitambo ya kuzalisha umeme iliyopo Kibulang’oma mjini hapa.
Kebara alisema kituo hicho kina mashine saba za kuzalisha umeme lakini kwa hivi sasa ni mashine tatu ndizo zinazofanya kazi hiyo kwa kutoa Megawati 2.6 wakati mahitaji ni Megawati 5 hasa ikizingatiwa kuwa katika mji wa Songea shirika hilo lina wateja elfu kumi na mbili hivyo bado umeme utaendea kutolewa kwa mgao lakini maeneo muhimu kama hospitali, ofisi za serikali na kambi za jeshi umeme utaendelea kutoleawa kama kawaida
MWISHO

Friday, May 11, 2012

WAANDISHI WAASWA KURIPOTI KIKAMILIFU ADHA YA UMEME MANISPAA YA SONGEA

                            
MAHINDI YAKIWA KWENYE KIWANDA CHA MTAZAMO KWA AJIRI YA KUSUBIRI UMEME ILI YAKOBOLEWE NA YASAGWE 




Na Stephano Mango, Songea
WAANDISHI wa Habari mkoani Ruvuma wametakiwa kutumia taaluma yao kikamilifu katika kuwaokoa wananchi wanaoteseka kutoka na adha wanazozipata kutokana na mgawo mkubwa wa umeme usiokuwa na kikomo unaoendelea kuwakabili katika Halmashauri ya Manspaa ya Songea
Wito huo umetolewa jana na Mkurugenzi wa kampuni ya Mtazamo Enterpress, Julius Mlawa wakati akizungumza na waandishi wa habari jana waliotembelea kiwanda cha kampuni hiyo kinachojishughulisha na ukoboaji nafaka, usagaji na uuzaji wa unga
Mlawa alisema kuwa waandishi wa habari ndio jukwaa la wananchi wanyonge ambao sauti zao hazisikiki vizuri kusemea licha ya kuendelea kuteseka na adha ya mgao mkubwa wa umeme unaowasababishia kupanda kwa gharama za maisha
Alisema kuwa mashine za kusaga nafaka ambazo zipo katika baadhi ya maeneo ya Manispaa hiyo zimeshindwa kutoa huduma kwa muda muafaka na kusababisha wananchi walio wengi kulazimika kutembea umbali mrefu kufuata huduma nje ya Manispaa ambako kuna mashine za kusaga nafaka zinazotumia mafuta ya Dizeli na kusababisha bei ya huduma hiyo kupanda mara mbili ikilinganishwa na awali
Alieleza kuwa kitendo cha shirika la umeme mkoani humu kushindwa kutoa huduma hiyo kwa wakati mbali ya kusababisha usumbufu kwao lakini kimekuwa kikiwakosesha mapato ambayo wanayatumia kulipa kodi kwenye mamlaka ya mapato Tanzania(TRA) kutokana na hasara zinazosababishwa na ukosefu wa umeme
Alifafanua zaidi katika kiwanda chake kuna wafanyakazi zaidi 30 ambao wanashinda kiwanda wakisubiri umeme ili waweze kufanya kazi bila mafanikio huku wakilipwa posho zao za kila siku bila kufanya kazi jambo linalosababisha hasara kubwa
Alieleza zaidi kuwa kutokana na ukosefu wa umeme ambao umekithiri katika manispaa ya Songea wafanyabiashara wengi wanashindwa kurejesha mikopo waliyokopa kwenye taasisi za fedha jambo ambalo ni hatari kwa biashara zao na jamii ambayo inanufaika na biashara hizo
Alisema kuwa kutokana na hali hiyo huenda akalazimika kusitisha kwa muda kutoa huduma ya usagaji na ukoboaji wa nafaka kama hali hiyo ya ukosefu wa umeme wa uhakika haitafanyiwa kazi na shirika hilo la umeme mkoani humu kwa sababu mbali ya kukosa mapato lakini imekuwa ni usumbufu kwa wananchi ambao wanahitaji huduma hiyo.
Kwa upande wake Meneja wa shirika la umeme mkoa wa Ruvuma Mhandisi Monika Kebara alikiri kuwepo kwa tatizo hilo na alisema hivi sasa huduma hiyo ya umeme inatolewa kwa mgawo kwa sababu uwezo wa ufuaji wa umeme umepungua sana kutokana na kuharibika kwa mitambo ya kuzalisha umeme iliyopo Kibulang’oma mjini hapa.
Kebara alisema kituo hicho kina mashine saba za kuzalisha umeme lakini kwa hivi sasa ni mashine tatu ndizo zinazofanya kazi hiyo kwa kutoa Megawati 2.6 wakati mahitaji ni Megawati 5 hasa ikizingatiwa kuwa katika mji wa Songea shirika hilo lina wateja elfu kumi na mbili.
Alisema kuwa tayari jopo la mafundi kutoka Jijini Dar es Salaam limefika kwa ajiri ya ukarabati mkubwa wa mitambo hiyo na kwamba mwishoni mwa mwezi mei kutakuwa na umeme wa uhakika
MWISHO

KAGASHEKI:SIKUBALI KUNYONGWA

                           .MAIGE AKIRI KUPONZWA NA WATENDAJI



Na Asha Bani, Dar
WAZIRI wa Maliasili na Utalii, Balozi Khamis Kagasheki, amesema hatokubali kuhukumiwa kufa kwa kunyongwa au kupigwa risasi kwa sababu ya madudu yatakayofanywa na watendaji wa wizara hiyo.

Kagasheki alisema wizara hiyo imechafuka kwa kiasi kikubwa na tuhuma za ubadhirifu wa hali ya juu umewafanya hata wabunge kupendekeza mtumishi wa serikali atakayebainika kuhujumu mali za nchi kuuawa kwa kunyongwa.

Akizungumza katika makabidhiano baina yake na aliyekuwa akishikilia wizara hiyo, Ezekiel Maige, waziri huyo mpya alisema wizara hiyo ina sura mbaya kwa nje kutokana na tuhuma za ufisadi wa kutisha unaofanywa na baadhi ya watendaji wake jambo lililosababisha katika kipindi cha utawala wa Rais Jakaya Kikwete kuongozwa na mawaziri watano.

Wizara hiyo imeongozwa na mawaziri Anthony Diallo, Prof. Jumanne Maghembe, Shamsa Mwangunga, Ezekiel Maige na sasa Kagasheki mwenyewe.

“Katika Bunge lililopita mbunge mmoja alitaka mawaziri wabadhirifu wanyongwe au wapigwe risasi mimi sitaki kufikia huko nitawanyonga wafanyakazi wabadhirifu kabla ya kunyongwa mimi; nasema hili kwa nia njema kabisa na sio kutisha watu,” alisema Kagasheki.

Alisema kutokana na uozo huo, wizara hiyo imebadilishwa jina na kuitwa ‘mali ya siri kubwa’ jambo ambalo si zuri kwa kuwa kila kitu kinatakiwa kufanyika kwa uwazi kwa maendeleo ya taifa.

Waziri huyo pia alisema Wizara ya Maliasili na Utalii inatakiwa kuchangia pato kubwa la taifa kupita wizara nyingine yoyote hata ile ya Nishati na Madini isingeweza kufikia lakini kwa sasa inachangia pato la taifa kwa asilimia 18 tu.

“Mimi nataka kufanya kazi kwa kushirikiana na sio kwa ugomvi: waziri haelewani na naibu wake; vurugu tupu. Hii inaondoa ufanisi katika kazi na kama naibu waziri na waziri wanashindwa kuelewana itasababisha hata watendaji wa ngazi ya chini kushindwa kuelewana pia,” alisema Kagasheki.

Alisema atafanya kazi kwa kuangalia pia changamoto mbalimbali katika sekta za wizara hiyo, ikiwa ni pamoja na kuangalia sekta ya wanyapori, misitu na sera nzima ya utalii na changamoto nyingine ikiwemo ya upungufu wa watumishi na kufuatilia kwa kina yanayozungumzwa katika hifadhi ya Ngorongoro.

Naye Naibu Waziri wa Wizara hiyo, Lazaro Nyalandu, alisema kwa kushirikiana watahakikisha pato la wizara hiyo linakuwa kwa kasi, watalii wanaongezeka kwa kuutangaza utalii ndani na nje ya nchi.

Aidha alimtaka kila mfanyakazi wa wizara hiyo kufanya kazi kwa moyo mmoja na kuhakikisha kuwa anaongeza uzalishaji wake.
Akikabidhi ofisi aliyekuwa waziri, Ezekiel Maige, aliwatahadharisha mawaziri hao kuwa macho kwa vile anajua aliondolewa kutokana na makosa ya baadhi ya watendaji wake wa chini.

Maige alidai kuwa katika wakati wake wa utendaji, alijitahidi sana kutumia akili na nguvu zake nyingi kuimarisha wizara hiyo, na kukiri kuwa kuna tuhuma za baadhi ya wafanyakazi wanaojihusisha na biashara za utalii.

Alidai kuwa baadhi ya wafanyakazi, akiwemo mtumishi mmoja mwandamizi ambaye kesi yake iko mahakamani, wamejitumbukiza katika biashara hizo, na kumtaka Kagasheni kupambana nalo.

Maige alidai wizara hiyo katika kutekeleza majukumu yake inakabiliwa na upungufu wa watumishi, ujangili, uvujaji wa mapato, ukosefu wa vitendea kazi na uchakavu wa miundombinu.

Nyingine ni utoroshwaji wa wanyamapori hai kupitia uwanja wa ndege wa Kilimanjaro, ambapo wizara ilisitisha biashara ya wanyapori hai sambamba na kuunda tume mbalimbali za kufanya uchunguzi kwa maofisa walioshiriki.

Waziri Maige aliahidi kushirikiana nao bega kwa bega katika kuendeleza yale aliyoanza kuyafanyia kazi ikiwa ni pamoja na suala la uchimbaji urani katika pori la akiba la Selous.

Tuesday, May 8, 2012

SIKU YA UHURU WA VYOMBO VYA HABARI MKOANI RUVUMA ILIVYOFANA KATIKA MATUKIO MBALIMBALI

Timu ya waandishi wa mtandao huu, inaomba radhi kwa usumbufu uliojitokeza kwa kutokuwa jamvini siku zaidi ya 3 na hasa kwa kutokuwajuza habari za mkoa wa Ruvuma na mikoa jilani na hasa siku ya uhuru wa vyombo vya habari mei 3 mwaka huu kutokana na sababu za kiufundi ambazo zilikuwa nje ya uwezo wetu, na sasa tumerudi tena jamvini kwa kasi kubwa yenye kukidhi ladha ya kitasnia,Tunawashukuru sana wadau wa mtandao huu wa www.stephanomango.blogspot.com, kwa kupiga simu, kutuma ujumbe mfupi uliokuwa unalengo la kujua tatizo letu na kutupa pole, Asanteni sana, BY UTAWALA
 Mjumbe wa Bodi ya Muunganiko wa Vyama vya Waandishi wa Habari Tanzania (UTPC), Mhariri Msaidizi wa Kanda ya Kusini(Tujifunze) na Mhandishi wa Habari wa Uhuru Fm, Juma Nyumayo akitoa mada ya mchango wa vyombo vya habari katika jamii katika mdahalo ulioandaliwa na Kituo cha Redio Jogoo Fm siku ya Uhuru wa Vyombo vya Habari Duniani Mei 3
 Mwandishi wa Serikali za Mitaa Tanzania mkoani Ruvuma(ALAT) Mwakilishi wa Vyombo vya IPP MEDIA(Nipashe,Guardian,Redio One na Itv) Nathan Mtega akizungumza katika Studio ya Kituo cha Redio Jogoo kuhusu umuhimu wa waandishi wa habari katika maendeleo ya Jamii, katikati ni Muongozaji wa kipindi hicho Isabela Nchama,wa kwanza kulia ni Aden Mbelle ambaye alikuwa ni msimamizi wa kipindi hicho
 Mwandishi wa Habari wa Tanzania Daima, Dira ya Mtanzania, Changamoto,Mitandao mbalimbali ya Kijamii na mmiliki wa mtandao wa www.stephanomango.blogspot.com, Stephano Mango akitoa mada ya umuhimu wa vyombo vya habari katika kukuza Demokrasia nchini, kulia ni Msimamizi wa kipindi Aden Mbelle
 Kutoka kushoto ni mwongozaji wa kipindi hicho kilichorushwa hewani moja kwa moja na kituo cha Redio Jogoo Fm, Isabela Nshana na Aden Mbelle ambaye alikuwa msimamizi wa matangazo hayo siku ya uhuru wa vyombo vya habari mei 3 mwaka huu
 Mtangazaji wa Redio Jogoo Innocent akifanya mahojiano na Mwandishi Juma Nyumayo katika Studio ya Redio hiyo siku ya Uhuru wa vyombo vya habari
 Mtangazaji wa Redio Jogoo Innocent akifanya mahojiano na Mwandishi Nathan Mtega katika Studio ya Redio hiyo siku ya Uhuru wa vyombo vya habari mei 3, katikati ni Mwandishi Juma Nyumayo
 Mwandishi Nathan Mtega akisaini kitabu katika Studio ya Redio Jogoo Fm ikiwa ni ishara ya kumaliza kipindi kilichorushwa moja kwa moja na Redio hiyo, kushoto ni Mtangazaji wa kituo hicho Isabela Nshama siku ya uhuru wa vyombo vya habari mei 3 mwaka 2012
 Mwandishi Juma Nyumayo akiteta jambo na Mtangazaji wa Redio Jogoo Fm Aden Mbelle baada ya kumaliza mdaharo wa umuhimu wa vyombo vya habari katika muktadha wa uchumi, siasa na utamaduni

MUDA WA TAFRIJA KATIKA UKUMBI WA SONGEA CLUB MAMBO YALIKUWA HIVI............
 Katikati ni Mbunge wa Jimbo la Peramiho Jenista Mhagama mbaye alimwakilisha Mkuu wa Mkoa wa Ruvuma Said Mwambungu kuwa mgeni rasmi katika tafrija ya jioni ya siku ya uhuru wa vyombo vya habari mkoani Ruvuma, kushoni ni Katibu Mtendaji wa Chama cha waandishi wa habari moani Ruvuma Andrwe Chatwanga, wapili kutoka kulia ni Mwenyekiti wa Ruvuma Press Club Andrwe Kuchonjoma wakiimba wimbo wa kuisifu na kuipenda TANZANIA
 Katibu Msaidizi wa Ruvuma Press Club, Mozes Julius Konala na Mwandishi wa Tanzania Daima kushoto, kulia ni Mwekahazina Msaidizi  na Mwandishi wa Channel Ten mkoani Ruvuma Emmanuel Msigwa wakiimba wimbo wa kuipenda TANZANIA
 Waandishi wa habari kutoka kulia ni Jofrey Nilai Redio Maria na Mjumbe wa Kamati wa Ruvuma Press Club, Mwakilishi wa IPP MEDIA mkoani Ruvuma Nathan Mtega na Anna wakiimba wimbo huo

 Mwandishi wa Jambo Leo Thomas Lipuka Komba akitoa maombi kwa niaba ya dhehebu la kikristo katika tafrija hiyo
 Naye akitoa maombi kwa niaba ya dhehebu la kiislam