About


Karibu ujiunge na chuo cha kisasa cha Easy Tech.Computer kwa mafanikio yako,Walimu waliobobea katika fani hiyo wanapatikana chuoni hapo

elimak

elimak

Pages - Menu

Sunday, June 30, 2013

SANGA ONE AHUDHURIA KILELE CHA MASHINDANO YA ANSIGAR CUP PERAMIHO NA ANATARAJIA KUYAFUNGA LEO

 Viongozi mbalimbali wakiimba wimbo wa Taifa ulioimbwa katika Mashindano hayo, wakwanza kutoka kushoto ni Mwenyekiti wa FARU, Golden Sanga, wa pili Mfadhiri wa mashindano hayo kwa niaba ya Dkt Ansigary Stuffe, na watatu ni Mwandishi Mahili wa Michezo katika Redio ya Jogoo Onesmo Emeran
 Miongoni mwa Timu shiriki ikiwajibika kuimba wimbo wa Taifa kabla ya kufunga mashindano hayo

 Mr Kolumbani Lugendo ambaye ni Msimamizi wa MECHI aliyeonyesha mkono akimpa maelekezo ya awali Mgeni Rasmi Mwenyekiti wa FARU Golden Sanga mwenye tai kabla hajazikagua timu shindani, wa kwanza kulia ni Katibu wa Mashindano Sixbert Komba, wa kwanza kulia ni Katibu wa SORUFA Iddfonsi Luoga, nyuma kabisa ni Ayubu Mvulla ambaye ni Mwenyekiti wa Mashindano hayo

Mwenyekiti wa Faru Golden Sanga akiendelea kuzisalimia na kuzikagua timu kabla hazijaanza mashindano hayo

Katika Fainali hiyo ya Ansigary Cup ambaye imefanyika mbele ya Mgeni Rasmi ambaye pia ni Mwenyekiti wa Chama cha Mpira wa Miguu Mkoa wa Ruvuma Golden Sanga (SANGA ONE) Timu mbili zilichezwa katika Uwanja wa Ansigary hapa PERAMIHO na kuhudhuriwa na mamia ya wapenzi na mashabiki wa timu hizo


Fainali hiyo iliwakutanisha Kilangano B 9 wenye pointi na Litisha yenye pointi 6

Mashindano hayo yalianza kwenye ngazi ya Tarafa April 21 mwaka huu na kuzinduliwa rasmi na Kamanda wa Polisi Mkoa wa Ruvuma Deusdedit Nsimike na kuhitimishwa Juni 30 mwaka huu na Mwenyekiti Golden Sanga

Habari kamili za mashindano hayo zitaendelea kukujia kupitia Mtandao huu wa www.stephanomango.blogspot.com