About


Karibu ujiunge na chuo cha kisasa cha Easy Tech.Computer kwa mafanikio yako,Walimu waliobobea katika fani hiyo wanapatikana chuoni hapo

elimak

elimak

Pages - Menu

Sunday, June 3, 2012

NAPE AANZA KAZI KWA KUZINDUA VITEGA UCHUMI VYA CCM WILAYA YA SONGEA NA MATAWI YA CHAMA

 Katibu wa halmashauri kuu ya CCM Itikadi na Uenezi Nape Nnauye akifungua jengo lenye vibanda zaidi ya 60 ambavyo vimegharimu zaidi ya milioni 202 katika Halmashauri ya Manspaa ya Songea
 Shina la wakeleketwa Kata ya Mshangano ambalo limefunguliwa leo na Katibu wa Halmashauri Kuu ya CCM Taifa Itikadi na Uenezi Nape Nnauye
 Katibu wa Halmashauri Kuu ya CCM Taifa Itikadi na Uenezi Nape Nnauye akipandisha bendera ikiwa ni ishara ya kutambua Tawi hilo
 Wananchi na wanachama wa cha Mapinduzi wakiwa wamezunguka wakishuhudia uzinduzi wa Tawi hilo
Katibu wa Halmashauri Kuu ya CCM Taifa Itikadi na Uenezi Nape Nnauye akiwahutubia wananchi na wanachama wa chama cha Mapinduzi ambao walishuhudia uzinduzi wa Tawi hilo

NAPE ACHARUKA UHAMISHAJI WA KIWANDA CHA TUMBAKU SONGEA

KATIBU wa Halmashauri kuu ya Chama cha Mapinduzi Itikadi na Uenezi Nape Nnauye akizungumza na wananchi,wanachama na viongozi wa CCM Mkoa wa Ruvuma mara baada ya kupokelewa, kushoto ni Mwenyekiti wa CCM Mkoa wa Ruvuma Corneus Msuha, kulia ni Mwenyekiti wa CCM Halmashauri ya Manispaa ya Songea Hemed Dizumba
Na Stephano Mango, Songea
KATIBU wa Halmashauri kuu ya Chama cha Mapinduzi Itikadi na Uenezi Nape Nnauye ameitaka Serikali kurudisha Kiwanda cha kusindika tumbaku cha Songea Tobacco Processing Industry(SanTop) ambacho kimepelekwa mkoani Morogoro na kuwaacha wakazi wa Ruvuma wakilalamika kutokana na msaada mkubwa uliokuwepo wakati kiwanda hicho kikifanya kazi Songea
Wito huo ameutoa jana wakati akizungumza na mamia ya wananchi,wanachama na viongozi wa Chama cha Mapinduzi (Ccm) waliokusanyika kumpokea Kata ya Shule ya Tanga Wilayani Songea mkoani Ruvuma ambako yupo katika ziara ya siku mbili
Nnauye alisema kuwa kiwanda hicho kilijengwa miaka mingi iliyopita na kiliwezesha kutoa ajira za muda mfupi na mrefu kwa wakazi wa mkoani humo na kusababisha kuwepo kwa mzunguko mkubwa wa fedha na kukua kwa uchumi wa Ruvuma na wananchi wake.
Alisema kuwa wakulima wa zao hilo kwa muda wote huo walikuwa wakijivunia kuwepo kwa kiwanda hicho, hali iliyowafanya kuongeza juhudi katika uzalishaji wa tumbaku na kujipatia maisha bora kutokana na shughuli yao ya kilimo
“ Inasikitisha kusikia wajanja wachache kwa kushirikiana na wawekezaji, bila aibu waliamua kukihamisha kiwanda hicho na kupeleka Morogoro, ambapo hakuna hata mche mmoja wa tumbaku unaozalishwa huko,” alisema Nnauye
Alisema tangu kiwanda hicho kilipohamishwa kutoka mjini humo, uchumi wa mkoa na watu wake umeshuka na kusababisha mateso makali kwa wananchi kutokana na kunyang’anywa fursa yao ya kujipatia kipato na kupelekea majengo ya kiwanda hicho kuwa mahame ambayo popo wanajihifadhi na wadudu wengine katika umasikini
Aliwataka viongozi wa Chama cha Mapinduzi mkoa wa Ruvuma kushirikiana kikamilifu na Serikali ili kuweza kukirudisha haraka iwezekanavyo kiwanda hicho ambacho kilikuwa msaada mkubwa kwa wananchi wa mkoa wa Ruvuma
Katibu huyo ameanza ziara ya siku mbili mkoani Ruvuma ambako atafanya mikutano ya hadhara na wananchi, vikao vya ndani,kufungua mashina na matawi ya chama hicho pamoja na kuweka mawe ya msingi miradi mbalimbali ya chama
MWISHO


NAPE NNAUYE APOKELEWA MKOANI RUVUMA KWA MBWEMBWE KUBWA


Msafara wa Katibu wa Halmashauri kuu ya Chama cha Mapinduzi Itikadi na Uenezi Nape Nnauye ukiingia kwenye Kata ya Mshangano Halmashauri ya Manispaa ya Songea
 
 Katibu wa Halmashauri kuu ya Chama cha Mapinduzi Itikadi na Uenezi Nape Nnauye akiingia Songea kuanza ziara ya siku mbili mkoani Ruvuma akitokea Mkoani Iringa kabla hajaelekea Mkoani Njombe kesho baada ya kumaliza ziara yake mkoani Ruvuma
 Chipukizi wa Chama cha Mapinduzi wakimkaribisha Katibu wa Halmashauri kuu ya Chama cha Mapinduzi Itikadi na Uenezi Nape Nnauye Mkoani Ruvuma kwa kumvesha Skafu
 Katibu wa Halmashauri kuu ya Chama cha Mapinduzi Itikadi na Uenezi Nape Nnauye (kulia) akipita katikati ya gwaride maalumu la Chama cha Mapinduzi huku akisindikizwa na Mwenyekiti wa CCM Mkoa wa Ruvuma Colneus Msuha
 Katibu wa Halmashauri kuu ya Chama cha Mapinduzi Itikadi na Uenezi Nape Nnauye akisalimiana na wananchi waliojitokeza kumpokea kabla ajaanza ziara yake rasmi

Katibu wa Halmashauri kuu ya Chama cha Mapinduzi Itikadi na Uenezi Nape Nnauye akisaini kitabu cha wageni ikiwa ni ishara ya kuanza ziara yake rasmi kwenye mkoa wa Ruvuma, wa kwanza kutoka kushoto ni Katibu wa Itikadi na Uenezi Mkoa wa Ruvuma Genfrida Haule( katikati) ni Mwenyekiti wa CCM Mkoa wa Ruvuma Colneus Msuha