About


Karibu ujiunge na chuo cha kisasa cha Easy Tech.Computer kwa mafanikio yako,Walimu waliobobea katika fani hiyo wanapatikana chuoni hapo

elimak

elimak

Pages - Menu

Thursday, April 25, 2013

BABU UMESIKIKA, SHIRIKI KIKAMILIFU KUTATUA CHANGAMOTO ZINAZOLIKABILI JUKWAA



Na Stephano Mango, Songea

HIVI karibuni nilibahatika kutembelea Wilaya ya Rufiji iliyopo Mkoa wa Pwani kwa lengo la kwenda kujifunza namna Wakulima wa zao la Embe, Ufuta na Muhogo wanavyojihusisha na kilimo cha mazao hayo na tija yake katika ukombozi wa kiuchumi kwa jamii na Taifa kiujumla

Katika safari hiyo nilijifunza mambo mengi sana kuhusu kilimo cha mazao hayo ambayo yakiwekewa kipaumbele na wadau wake na Serikali, naamini kutokana na ushahidi uliopo kwa wakulima niliozungumza nao umaskini ungepungua kwa asilimia kubwa kwenye kaya nyingi zinazojihusisha na kilimo cha mazao hayo

Nina mengi sana ya kuelezea, lakini naomba wasomaji kwa leo nizungumzie ushirikiano uliopo kati ya Wakulima wa Embe, Ufuta na Muhogo, Mkuu wa Wilaya ya Rufiji Nurdin Babu na Wasimamizi wa Mradi wa Muvi Mkoa wa Pwani

Hakika ushirikiano huo utawezesha uzalishaji wa mazao hayo kuongezeka na upatikanaji wa masoko yenye uhakika kwani jukwaa ambalo wameliunda litawezesha kukabiliana na changamoto zilizopo na kusababisha upatikanaji wa maslahi bora

Jukwaa hilo ni muhimu sana katika maendeleo ya kilimo cha mazao hayo kwani watapata muda wa kujadiliana juu ya fursa, matatizo na changamoto wanazokabiliana nazo ili kuongeza tija kwa kila mmojawapo na kuepukana na unyonyaji unaofanywa na baadhi ya wajanja wachache kwenye minyororo ya thamani ya mazao hayo

Ili kulinda hali hiyo wajasiliamali hao wanalelewa kwa kiasi kikubwa sana na Mradi wa Muunganiko wa Wajasiriamali Vijijini (MUVI) ulioibuliwa kutekelezwa katika mikoa sita ya Tanzania bara, ukiwemo Mkoa wa Pwani na Ruvuma.

Kupitia mkopo ambao Serikali ya Tanzania ilipata toka shirika la IFAD ili kuinua hali duni ya wananchi wake ambapo fedha hizo ziko chini ya Wizara ya Viwanda na Biashara katika shirika la SIDO kama watekelezaji wakuu

Mradi wa MUVI-Pwani unalenga kuwawezesha wajasiriamali wadogowadogo ili kuendeleza biashara zao zitakazo wawezesha kuinua vipata vyao ambapo mojawapo ya uwezeshwaji huo, ni kuimarisha ushiriki wa wadau mbalimbali katika minyororo ya thamani ya muhogo na embe, ili kuimarisha na kuongeza ubora wa mazao hayo.

Hivyo basi jukwaa la Majadiliano la wadau wa embe, muhogo na ufuta ni miongoni mwa jitihada za MUVI kwa kushirikiana na Halmashauri na wadau mbalimbali katika minyororo ya thamani ya mazao hayo ili kuwa na sehemu ya kukutana na kujadiliana namna ya kutatua kero mbalimbali

Kutokana na umuhimu huo Machi 26 mwaka huu, wadau hao walikutana mji mdogo wa Ikwiriri Wilayani Rufiji mkoani Pwani

Lengo likiwa wadau wakupokea na kujadili taarifa ya utekelezaji wa Mradi wa MUVI Pwani pia kupokea taarifa za wadau mbali mbali katika minyororo ya thamani ya embe, muhogo na ufuta. Kamati zilizotoa taarifa ni kamati ya wazalishaji, wasindikaji, pembejeo, fedha na mitaji.

Katika mkutano huo ambao uliwashirikisha wadau wengi zikiwemo taasisi za fedha ikiwemo Benki ya CRDB, watafiti, wasindikaji vyakula, wataalamu na viongozi wa Halmashauri ya wilaya na wadau wengine

Kwenye mkutano huo Mkuu wa Wilaya ya Rufiji Nurdin Babu alialikwa kuwa mgeni rasmi ambapo pamoja na mambo mengine aliyoyasema ni pamoja na … Nia yetu kubwa ya kukusanyika hapa leo hii, ni kwa ajili ya kufanya tathimini kupitia Jukwaa la Majadiliano kuhusu changamoto zinazokabili mazao matatu ambayo ni, embe, muhogo na ufuta

Pia alisema kwa fursa ya pekee tuliyoipata leo, ni vizuri tuzungumzie zaidi mazao ya muhogo na embe ambayo yana wanyonyaji wengi sana pasipo kujali nguvu nyingi inayotumiwa na wazalishaji hususani wakulima. Ninawasihi sana, tuuze mazao haya kwa faida za maendeleo kama vile kusomesha watoto, kujenga nyumba nzuri za kudumu na mambo mengine ya muhimu na si kuoa wake wengi wanaopelekea kuzorota kwa maendeleo.

“ Ndugu wakulima, siwezi kujitenga nanyi nawaahidi ushirikiano wa bega kwa bega ili tuweze kufikia malengo ya maendeleo endelevu ya wilaya yetu na watanzania kwa ujumla” alisema Babu

Hayo ndio yaliyonifanya niyatafakari kwa muda wa zaidi ya wiki mbili na kulazimika kuyaweka katika ukurasa huu ili wadau popote walipo waweze kuyajadili na kuyaenzi kwa maslahi ya jamii pana zaidi na Taifa kiujumla

Ni dhahiri wanarufiji wamejitahidi sana kuunda Jukwaa la Majadiliano la Wadau wa Muhogo, ufuta na Embe Rufiji ambalo lina malengo mbalimbali ambapo lengo kuu ni kuzalisha kwa wingi na kutetea thamani ya zao hilo katika masoko

Katika mradi huo wa Muvi unakabiliwa na changamoto ambazo zinapaswa kutatuliwa kwa haraka ili kuweza kuleta matokeo chanya kwenye Jukwaa hilo, na hapa ndipo ninapomuweka wazi Mkuu wa Wilaya ya Rufiji Nurdin Babu kushiriki kwa kina ndani na nje ya Serikali ili kufikia malengo ya wakulima hao, kwani alichokisema kwenye hotuba yake ya ufunguzi kimesikika

Na kilichobaki yeye kushiriki kutatua changamoto zinazowakabili wakulima hao ili kuweza kufikia malengo stahiki ya wanajukwaa ambao wanamatumaini mbalimbali katika jitihada za kilimo cha mazao hayo

Kwa mujibu wa taarifa ya utekelezaji wa Muvi Mkoa wa Pwani 2012/2013 kuna changamoto ambazo zinawakwaza kufikia malengo yao kwa wakati ikiwemo ,Mbinu za kisasa za uzalishaji ni mdogo, Ukosefu wa soko la mkataba, Kuinua kiwango cha usindikaji, Uzalishaji na usambazaji wa mbegu bora, Tozo zilizo na tija kwa wajasiliamali

Katika hilo ni vema Serikali mkoani Pwani ikajipanga kikamilifu kutatua changamoto hizo na jukumu kubwa la wanajukwaa kila mmoja kutimiza wajibu wake kwani Jukwaa la Majadiliano kwa mazao ya biashara ni muhimu sana kwa sababu wadau mbali mbali wanashirikishwa kuanzia ngazi ya chini hadi ya juu

Katika swala la huduma za fedha Mbunge wa Viti Maalum Mkoa wa Ruvuma Devotha Likokola ambaye pia ni Mkurugenzi wa Vikoba Tanzania alikuwa ni miongoni mwa watu waliotoa mada siku hiyo

Pamoja na mambo mengine alisikika akiwashauri wanajukwaa kwa kusema ,,, huduma za fedha zilizo rasmi ni (12%) na wengine wanapata huduma zisizo rasmi. Aliendelea kwa kuzielezea huduma za fedha zinazotolewa na mabenki kama ya CRDB, NBC na NMB kuwa ni huduma rasmi kwa sababu zinasimamiwa na Benki Kuu ya Tanzania (B.O.T).

Likokola alisema kuwa huduma ambazo si rasmi alizitolea mfano kuwa ni SACCOS, FINCA, PRIDE, SELF, TUNAKOPESHA, na nyinginezo ambazo zinajumuisha (34%). Aidha aliendelea kwa kusema kwamba (36%) hawapo katika upande wowote iwe rasmi ama si rasmi.

Alizitaja njia kuu tatu (3) ambazo zinaweza kumpatia mtu pesa; nazo ni kufanya kazi/kilimo, kuajiriwa na kuwekeza na kuwataka kwamba wana Rufiji wakitaka kupatapesa, ni lazima wawe na pesa kwa kujiunga kwenye vikundi hasa Village Community Bank (VICOBA).

Kwa leo ninachoweza kusema tuanze upya kwa kuwa wajasiriamali mahiri chini ya Jukwaa bunifu kwani ujasiriamali ni ile hali, uwezo na mkakati au mchakato wa kubuni, kuanzisha, kuendesha na kumudu shughuli halali ya maendeleo ya kiuchumi

Tunahitaji ujasiliamali wa kujiamini, kuthubutu, kubuni na kuendeleza zao tokeo la ubunifu huo kwa kuleta faida chanya katika maisha yake, jamii na Taifa kiujumla kwani ujasiliamali ni nguzo muhimu kwa uchumi wa kisasa wa karne ya 21

Dhana ya ujasiliamali inatimia endapo hali ya kugundua au kubuni biashara mpya au kuiendeleza ile ya zamani kwa ajili ya kuwekeza na kutoa huduma stahiki kwa jamii pana, hivyo tuamue sasa kuwa katika hali hiyo katika jukwaa la dunia ili kuzifaidi fursa za uchumi za ndani na nje ya nchi

Uchumi wa dunia umebadilika, uchumi wa soko katika utandawazi ndio unashikilia mfumo wa kiuchumi wa dunia ili kuharakisha maendeleo kwa kutoa ajira mbadala kwa kujiajili, kujitegemea na kujenga uwezo wa kujiamini katika maisha na biashara kubwa dhana ya ujasiliamali chini ya Jukwaa inahitajika

Wahenga walisema huwezi kuzuia sikio lako kusikia lakini unaweza kuzuia mdomo wako usiseme, nami kwa hakika nasema nauzuia mkono wangu usiandike zaidi lakini siwezi kukuzuia msomaji kuendelea kusoma

Mwandishi wa Makala

Anapatikana 0715-335051

www.stephanomango.blogspot.com
DC BABU UMESIKIKA, SHIRIKI KIKAMILIFU KUTATUA CHANGAMOTO ZINAZOLIKABILI JUKWAA


Na Stephano Mango, Songea

HIVI karibuni nilibahatika kutembelea Wilaya ya Rufiji iliyopo Mkoa wa Pwani kwa lengo la kwenda kujifunza namna Wakulima wa zao la Embe, Ufuta na Muhogo wanavyojihusisha na kilimo cha mazao hayo na tija yake katika ukombozi wa kiuchumi kwa jamii na Taifa kiujumla

Katika safari hiyo nilijifunza mambo mengi sana kuhusu kilimo cha mazao hayo ambayo yakiwekewa kipaumbele na wadau wake na Serikali, naamini kutokana na ushahidi uliopo kwa wakulima niliozungumza nao umaskini ungepungua kwa asilimia kubwa kwenye kaya nyingi zinazojihusisha na kilimo cha mazao hayo

Nina mengi sana ya kuelezea, lakini naomba wasomaji kwa leo nizungumzie ushirikiano uliopo kati ya Wakulima wa Embe, Ufuta na Muhogo, Mkuu wa Wilaya ya Rufiji Nurdin Babu na Wasimamizi wa Mradi wa Muvi Mkoa wa Pwani

Hakika ushirikiano huo utawezesha uzalishaji wa mazao hayo kuongezeka na upatikanaji wa masoko yenye uhakika kwani jukwaa ambalo wameliunda litawezesha kukabiliana na changamoto zilizopo na kusababisha upatikanaji wa maslahi bora

Jukwaa hilo ni muhimu sana katika maendeleo ya kilimo cha mazao hayo kwani watapata muda wa kujadiliana juu ya fursa, matatizo na changamoto wanazokabiliana nazo ili kuongeza tija kwa kila mmojawapo na kuepukana na unyonyaji unaofanywa na baadhi ya wajanja wachache kwenye minyororo ya thamani ya mazao hayo

Ili kulinda hali hiyo wajasiliamali hao wanalelewa kwa kiasi kikubwa sana na Mradi wa Muunganiko wa Wajasiriamali Vijijini (MUVI) ulioibuliwa kutekelezwa katika mikoa sita ya Tanzania bara, ukiwemo Mkoa wa Pwani na Ruvuma.

Kupitia mkopo ambao Serikali ya Tanzania ilipata toka shirika la IFAD ili kuinua hali duni ya wananchi wake ambapo fedha hizo ziko chini ya Wizara ya Viwanda na Biashara katika shirika la SIDO kama watekelezaji wakuu

Mradi wa MUVI-Pwani unalenga kuwawezesha wajasiriamali wadogowadogo ili kuendeleza biashara zao zitakazo wawezesha kuinua vipata vyao ambapo mojawapo ya uwezeshwaji huo, ni kuimarisha ushiriki wa wadau mbalimbali katika minyororo ya thamani ya muhogo na embe, ili kuimarisha na kuongeza ubora wa mazao hayo.

Hivyo basi jukwaa la Majadiliano la wadau wa embe, muhogo na ufuta ni miongoni mwa jitihada za MUVI kwa kushirikiana na Halmashauri na wadau mbalimbali katika minyororo ya thamani ya mazao hayo ili kuwa na sehemu ya kukutana na kujadiliana namna ya kutatua kero mbalimbali

Kutokana na umuhimu huo Machi 26 mwaka huu, wadau hao walikutana mji mdogo wa Ikwiriri Wilayani Rufiji mkoani Pwani

Lengo likiwa wadau wakupokea na kujadili taarifa ya utekelezaji wa Mradi wa MUVI Pwani pia kupokea taarifa za wadau mbali mbali katika minyororo ya thamani ya embe, muhogo na ufuta. Kamati zilizotoa taarifa ni kamati ya wazalishaji, wasindikaji, pembejeo, fedha na mitaji.

Katika mkutano huo ambao uliwashirikisha wadau wengi zikiwemo taasisi za fedha ikiwemo Benki ya CRDB, watafiti, wasindikaji vyakula, wataalamu na viongozi wa Halmashauri ya wilaya na wadau wengine

Kwenye mkutano huo Mkuu wa Wilaya ya Rufiji Nurdin Babu alialikwa kuwa mgeni rasmi ambapo pamoja na mambo mengine aliyoyasema ni pamoja na … Nia yetu kubwa ya kukusanyika hapa leo hii, ni kwa ajili ya kufanya tathimini kupitia Jukwaa la Majadiliano kuhusu changamoto zinazokabili mazao matatu ambayo ni, embe, muhogo na ufuta

Pia alisema kwa fursa ya pekee tuliyoipata leo, ni vizuri tuzungumzie zaidi mazao ya muhogo na embe ambayo yana wanyonyaji wengi sana pasipo kujali nguvu nyingi inayotumiwa na wazalishaji hususani wakulima. Ninawasihi sana, tuuze mazao haya kwa faida za maendeleo kama vile kusomesha watoto, kujenga nyumba nzuri za kudumu na mambo mengine ya muhimu na si kuoa wake wengi wanaopelekea kuzorota kwa maendeleo.

“ Ndugu wakulima, siwezi kujitenga nanyi nawaahidi ushirikiano wa bega kwa bega ili tuweze kufikia malengo ya maendeleo endelevu ya wilaya yetu na watanzania kwa ujumla” alisema Babu

Hayo ndio yaliyonifanya niyatafakari kwa muda wa zaidi ya wiki mbili na kulazimika kuyaweka katika ukurasa huu ili wadau popote walipo waweze kuyajadili na kuyaenzi kwa maslahi ya jamii pana zaidi na Taifa kiujumla

Ni dhahiri wanarufiji wamejitahidi sana kuunda Jukwaa la Majadiliano la Wadau wa Muhogo, ufuta na Embe Rufiji ambalo lina malengo mbalimbali ambapo lengo kuu ni kuzalisha kwa wingi na kutetea thamani ya zao hilo katika masoko

Katika mradi huo wa Muvi unakabiliwa na changamoto ambazo zinapaswa kutatuliwa kwa haraka ili kuweza kuleta matokeo chanya kwenye Jukwaa hilo, na hapa ndipo ninapomuweka wazi Mkuu wa Wilaya ya Rufiji Nurdin Babu kushiriki kwa kina ndani na nje ya Serikali ili kufikia malengo ya wakulima hao, kwani alichokisema kwenye hotuba yake ya ufunguzi kimesikika

Na kilichobaki yeye kushiriki kutatua changamoto zinazowakabili wakulima hao ili kuweza kufikia malengo stahiki ya wanajukwaa ambao wanamatumaini mbalimbali katika jitihada za kilimo cha mazao hayo

Kwa mujibu wa taarifa ya utekelezaji wa Muvi Mkoa wa Pwani 2012/2013 kuna changamoto ambazo zinawakwaza kufikia malengo yao kwa wakati ikiwemo ,Mbinu za kisasa za uzalishaji ni mdogo, Ukosefu wa soko la mkataba, Kuinua kiwango cha usindikaji, Uzalishaji na usambazaji wa mbegu bora, Tozo zilizo na tija kwa wajasiliamali

Katika hilo ni vema Serikali mkoani Pwani ikajipanga kikamilifu kutatua changamoto hizo na jukumu kubwa la wanajukwaa kila mmoja kutimiza wajibu wake kwani Jukwaa la Majadiliano kwa mazao ya biashara ni muhimu sana kwa sababu wadau mbali mbali wanashirikishwa kuanzia ngazi ya chini hadi ya juu

Katika swala la huduma za fedha Mbunge wa Viti Maalum Mkoa wa Ruvuma Devotha Likokola ambaye pia ni Mkurugenzi wa Vikoba Tanzania alikuwa ni miongoni mwa watu waliotoa mada siku hiyo

Pamoja na mambo mengine alisikika akiwashauri wanajukwaa kwa kusema ,,, huduma za fedha zilizo rasmi ni (12%) na wengine wanapata huduma zisizo rasmi. Aliendelea kwa kuzielezea huduma za fedha zinazotolewa na mabenki kama ya CRDB, NBC na NMB kuwa ni huduma rasmi kwa sababu zinasimamiwa na Benki Kuu ya Tanzania (B.O.T).

Likokola alisema kuwa huduma ambazo si rasmi alizitolea mfano kuwa ni SACCOS, FINCA, PRIDE, SELF, TUNAKOPESHA, na nyinginezo ambazo zinajumuisha (34%). Aidha aliendelea kwa kusema kwamba (36%) hawapo katika upande wowote iwe rasmi ama si rasmi.

Alizitaja njia kuu tatu (3) ambazo zinaweza kumpatia mtu pesa; nazo ni kufanya kazi/kilimo, kuajiriwa na kuwekeza na kuwataka kwamba wana Rufiji wakitaka kupatapesa, ni lazima wawe na pesa kwa kujiunga kwenye vikundi hasa Village Community Bank (VICOBA).

Kwa leo ninachoweza kusema tuanze upya kwa kuwa wajasiriamali mahiri chini ya Jukwaa bunifu kwani ujasiriamali ni ile hali, uwezo na mkakati au mchakato wa kubuni, kuanzisha, kuendesha na kumudu shughuli halali ya maendeleo ya kiuchumi

Tunahitaji ujasiliamali wa kujiamini, kuthubutu, kubuni na kuendeleza zao tokeo la ubunifu huo kwa kuleta faida chanya katika maisha yake, jamii na Taifa kiujumla kwani ujasiliamali ni nguzo muhimu kwa uchumi wa kisasa wa karne ya 21

Dhana ya ujasiliamali inatimia endapo hali ya kugundua au kubuni biashara mpya au kuiendeleza ile ya zamani kwa ajili ya kuwekeza na kutoa huduma stahiki kwa jamii pana, hivyo tuamue sasa kuwa katika hali hiyo katika jukwaa la dunia ili kuzifaidi fursa za uchumi za ndani na nje ya nchi

Uchumi wa dunia umebadilika, uchumi wa soko katika utandawazi ndio unashikilia mfumo wa kiuchumi wa dunia ili kuharakisha maendeleo kwa kutoa ajira mbadala kwa kujiajili, kujitegemea na kujenga uwezo wa kujiamini katika maisha na biashara kubwa dhana ya ujasiliamali chini ya Jukwaa inahitajika

Wahenga walisema huwezi kuzuia sikio lako kusikia lakini unaweza kuzuia mdomo wako usiseme, nami kwa hakika nasema nauzuia mkono wangu usiandike zaidi lakini siwezi kukuzuia msomaji kuendelea kusoma

Mwandishi wa Makala

Anapatikana 0715-335051

www.stephanomango.blogspot.com

RC ARUSHA AAGIZA LEMA AKAMATWE KWA UCHOCHEZI

MKUU wa Mkoa wa Arusha, Magesa Mulongo ameliagiza Jeshi la Polisi mkoani humo, kumkamata Mbunge wa Arusha Mjini, Godbless Lema akihusishwa na uchochezi wa vurugu zilizotokea katika Chuo cha Uhasibu kilichopo Njiro jijini Arusha jana asubuhi.

Mulongo alithibitisha kukamatwa kwa mwanasheria wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA), Albert Msando ambaye anadaiwa kuwepo chuoni hapo na Lema pamoja na baadhi ya wanafunzi wanaodaiwa kuwa vinara wa vurugu hizo.

Vurugu hizo zilitokea jana saa nne asubuhi baada ya Mkuu wa Mkoa kufika chuoni hapo kwa ajili ya kuwasikiliza wanachuo ambao walitaka kuandamana kufuatia mwenzao Elly Kago (22) kuuawa na watu wasiojulikana usiku wa kuamkia jana jirani na chuo.

Mulongo alifika chuoni hapo baada ya kupigiwa simu na Lema ambaye alifika mapema na kuzungumza na wanafunzi hao, huku akiwatuliza wasiandamane kufuatia kifo cha mwenzao.

Lema aliwaambia vijana hao kuwa mazingira ya nchi ya sasa ni magumu kufuatia wengi wao kukosa ajira na hivyo baadhi yao wasio wastahamilivu kujiingiza katika vitendo vya ujambazi na unyang'anyi.

Hivyo aliwataka wasiwe na jazba badala yake watafute ufumbuzi wa matukio hayo na kuangalia jinsi ya kumsitiri mwenzao.

Baada ya Mulongo kufika na kuwakuta wanafunzi wakizungumza na Lema, alipewa nafasi naye kuzungumza, lakini aliutaka uongozi wa chuo kuandaa vipaza sauti na mahala pazuri pa kuzungumzia.

Maelekezo hayo ya mkuu wa mkoa kutaka vipaza sauti yaliamsha maneno ya chini kwa chini na baada ya kuanza kuzungumza wanafunzi hao walianza kumzomea wakimlazimisha aache.

Alipokatisha hotuba yake, wanafunzi walianza kurusha mawe na hivyo kulazimika kuondolewa chuoni hapo pamoja na viongozi mbalimbali wa serikali chini ya ulinzi, huku mabomu yakirindima kuwatawanya wanafunzi hao.

Wanafunzi hao walisikika wakisema mkuu huyo ‘amewaboa’ kwa kuwa wao wana msiba yeye anaenda kudai vipaza sauti ili kusikiliza madai yao, huku akiwa amevaa suti, hatua iliyotafsiriwa kama kutojali msiba wao.

Akizungumza na waandishi wa habari ofisini kwake mbele ya wajumbe wa Kamati ya Ulinzi na Usalama, Mulongo alisema wameuagiza uongozi wa chuo hicho kukifunga kwa muda usiojulikana kwa ajili ya usalama.

Alisema taarifa za awali za polisi zinasema kuwa vurugu na kifo cha mwanafunzi huyo vina mahusiano makubwa na masuala ya kisiasa kwa ajili ya watu kujijenga kisiasa na kwamba vyombo vya usalama vinaendelea na uchunguzi wa kina juu ya suala hilo.

Mkuu huyo wa mkoa hakutaja idadi ya wanafunzi waliokamatwa hadi jana bali alisema vinara wote wamekamatwa pamoja na Msando huku akisisitiza kuwa Lema ametoroka na anaendelea kusakwa.

“Jambo baya kwa leo ni siasa kuingia katika vurugu hizo, kwani Lema ndiye alihusika hata kuita viongozi wa serikali chuoni hapo ambapo aliingia hapo bila kufuata utaratibu na kuanza kuzungumza na wanafunzi,’’ alisema Mulongo.

Kaimu Mkuu wa Chuo, Dk. Faraji Kasida baada ya kupewa maagizo ya kukifunga chuo hicho ambacho kipo chini ya Wizara ya Fedha alitangaza kuwa kimefungwa kwa muda usiojulikana.

Vurugu hizi zimeibuka zikiwa zimebaki siku chache kabla ya kuanza kwa kampeni za uchaguzi mdogo wa madiwani katika kata nne za Jiji la Arusha.

Liwale balaa

Mwandishi Wetu kutoka Liwale anaripoti kuwa wananchi wasiojulikana wamechoma moto ofisi na nyumba za mbunge wa Liwale mkoani Lindi, Faith Mitambo pamoja na nyumba za viongozi wa CCM na wa vyama vya ushirika vya msingi kwenye mji wa Liwale.

Tukio hilo la aina yake lilitokea juzi likianzia katika Kijiji cha Liwale B ambako wakulima wa Chama cha Msingi cha Minali walikataa malipo ya korosho ya sh 200 kwa kilo yakiwa ya pili badala ya sh 600 waliyoahidiwa mwaka jana.

Kwa mujibu wa Msemaji wa Jeshi la Polisi nchini, Advera Senso, vurugu hizo zilitokea saa tisa alasiri, huko wilayani Liwale ambapo kundi la watu wanaodhaniwa kuwa wakulima wa korosho walijaribu kuzuia gari lililokuwa na malipo.

Alisema kuwa wakulima hao walikuwa wakipinga malipo ya pili ya korosho na hivyo kuanza kufanya vurugu na uharibifu mkubwa wa mali.

Senso alisema hadi jana taarifa za awali zilionesha kuwa nyumba 14 zilichomwa moto, baadhi ya mifugo ilijeruhiwa na kuangamizwa na kufanyika uharibifu wa miundombinu ya barabara.

Alisema kufuatia tukio hilo, Mkuu wa Jeshi la Polisi nchini, IGP Said Mwema alituma timu maalumu ikiongozwa na Kaimu Mkurugenzi wa Upelelezi wa Makosa ya Jinai nchini (DCP), Issaya Mngulu kwenda kuongeza nguvu kwa kushirikiana na uongozi wa mkoa.

“Lengo ni kuhakikisha kuwa hali ya amani na utulivu inarejea haraka na wale wote waliohusika kufanya vitendo vya uhalifu wanakamatwa na kufikishwa mahakamani ili sheria iweze kuchukua mkondo wake. Hadi sasa watuhumiwa 19 wamekamatwa kwa mahojiano,” alisema.

Wakati taarifa za polisi zikieleza hivyo, mashuhuda wa tukio hilo walisema kuwa Mwenyekiti wa chama hicho cha ushirika, Mohamed Limbwilindi alikwenda kijijini hapo akiwa na sh milioni 61.4 ambazo wakulima hao wangelipwa sh 200 kwa kila kilo ya korosho.

Kwamba wengine ambao hawakupewa malipo ya awali walielezwa kuwa watalipwa sh 800, jambo ambalo lilizua mtafaruku miongoni mwao na hivyo kurudisha fedha.

Kutokana na hali hiyo, ilielezwa kuwa wananchi wenye hasira walianza kukateketeza moto ofisi ya chama hicho na nyumba ya mwenyekiti kisha pia nyumba ya katibu wake, Juma Majivuno.

Baada ya vurugu hizo huko Liwale B, alasiri vurugu hizo zilihamia mjini Liwale ambako uharibifu mkubwa wa mali ulifanyika.

Wananchi hao walichoma ofisi ya mbunge, duka la pembejeo la Hassan Mpako, ambaye ni Makamu Mwenyekiti wa Chama cha Msingi cha Umoja mjini Liwale pamoja na nyumba yake.

Akizungumzia tukio hilo, Mpako alisema; “niliona kundi kubwa la watu wanakuja nyumbani kwangu saa 3 usiku wakiwa wamebeba nondo, mawe pamoja na madumu ambayo nadhani yalikuwa na petroli,” alisema.

Mpako alifafanua kuwa watu hao walimweleza; “tunataka fedha zetu za korosho” mazingira aliyodai kuwa yalimlazimisha atimue mbio ili kujisalimisha.

Alisema watu hao waliteketeza nyumba yake pamoja na trekta dogo la mkono, pikipiki, jenereta pamoja akiba ya pembejeo za kilimo ambazo zilikuwa dukani.

Wengine waliochomewa nyumba ni Mwenyekiti wa CCM Wilaya, Mohamed Ngomambo ambaye alisema anamwachia Mungu.

“Kama nimepoteza wazazi ambao wana thamani kubwa maishani mwangu nyumba ni kitu gani?” alisema Ngomambo.

Kutokana na vurugu hizo, kundi kubwa la askari wa kutuliza ghasia (FFU) toka Lindi limewasili wilayani Liwale kudhibiti hali ya usalama ambayo imetoweka.

Kamanda wa Polisi Mkoa wa Lindi, George Mwakajinga alizungumza kwa simu akisema kuwa mbunge wa Liwale nyumba zake mbili na ofisi vilichomwa moto.

Pia Mwenyekiti wa CCM Wilaya, Chande nyumba yake moja ilichomwa moto huku mwenyekiti wa Halmashauri ya Liwale, Abasi Matulilo naye nyumba yake ilichomwa.

“Meneja wa Chama cha Msingi cha Ilulu, Hamza Mkungura nyumba zake mbili ziliteketezwa na duka la dawa na pembejeo vile vile yaliteketezwa huku mifugo ikijeruhiwa na kuchinjwa,” alisema.

Kamanda aliwataja wengine walioathirika na vurugu hizo kuwa ni meneja mikopo wa NMB, Mohamedi Pimbi ambaye duka lake la vifaa vya umeme lilichomwa pamoja na duka la Kanisa Katoliki.

Aliwataja pia Diwani wa CCM, Hasan Muyao na Diwani wa Viti Maalumu Amina Mnocha kuwa nyumba zao zilichomwa pamoja na nyumba ya mjumbe wa NEC wa chama hicho, Hemedi Ngonani ambaye aliharibiwa maduka ya simu na vyakula.