About


Karibu ujiunge na chuo cha kisasa cha Easy Tech.Computer kwa mafanikio yako,Walimu waliobobea katika fani hiyo wanapatikana chuoni hapo

elimak

elimak

Pages - Menu

Tuesday, September 27, 2011

SAKATA LA UMEYA SONGEA; KAMATI YA SIASA YA CHAMA CHA MAPINDUZI WILAYA YA SONGEA YADHAMIRIA KUWATIMUA MADIWANI WATANO

Katibu wa Chama cha Mapinduzi wilaya ya Songea Alfonce Siwale

MJI WA SONGEA UMEKUMBWA NA UHABA MKUBWA WA NISHATI YA MAFUTA YA DIZEL NA PETROL NA KUSABABISHA ADHA KUBWA KWA WATUMIAJI WA NISHATI HIYO

 Watumiaji wa nishati ya Mafuta wakiwa wamefanikiwa kupata mafuta kiduchu kwenye vidumu ili waweze kuendeshea shughuli zao zinazotegemea nishati hiyo
 Foleni ya kuhitaji nishati ya mafuta katika kituo cha mafuta cha Kisumapai

AFARIKI KWA KUTUMBUKIA KWENYE MFEREJI WA MAJI,MWINGINE ALAZWA KWA KUGONGWA NA TREKTA

   Na Augustino Chindiye,Tunduru

MKAZI wa kitongoji cha Ndondwa katika kijiji cha Ujamaa Lelolelo aliyefahamika kwa jina la Ashimu Likungwa (35) amefariki dunia baada ya kutumbukia katika mfereji wa banio la kumwagilia mashamba ya wakazi wa kijiji hicho.

Taarifa za tukio hilo ambazo zimedhibitisha ma Mtendaji wa kijiji cha Leloleo Reheme Mangochi zinasema kuwa marehemu Likungwa amefariki dunia kutokana na kupatwa na ugonjwa wa kifafa wakati akitaka kuoga katika mfereji huo na kwamba ugonjwa huo umekuwa ukimsumbua siku nyingi.

Mangochi aliendelea kufafanua kuwa mwili wa marehemu Likungwa uliokotwa na Watoto ambao alienda nao kuoga katika maeneo hayo na kwamba kabla ya kupatwa na mauti hayo marehemu alifanikiwa kuvua nguo zote kwa nia ya kuoga akiwa peke yake hali ambayo ilimfanya ashindwe kujiokoa baada ya kupatwa na ugonjwa huo.

Wakati huo huo mtoto wa Miaka 13 aliyefahamika kwa jina la Arifa Saidi amelazwa katika hospitali ya serikali ya Wilaya ya Tunduru baada ya kugongwa na Trekta dogo aina ya Power tilla na kuvunjika mguu wake wa kulia.

Akiongea kwa tabu mtoto huyo alisema kuwa mkasa huo ulimkuta wakati akijaribu kudandia baada ya kukamirisha zoezi la kupakia matofari ambayo walikuwa wakipakia kwa nia ya kujipatia chochote ili waweze kuendesha maisha yao ya kila siku.

Akizungumzia matukio hayo Kamanda wa Polisi wa Mkoa wa Ruvuma Michael kamuhanda alisema kuwa Polisi wanaendelea na uchunguzi wa matukio hayo.
 MWISHO

WALIMU WAWILI WANUSURIKA KUUAWA KUTOKANA NA WIVU WA KIMAPENZI WILAYANI TUNDURU

Katibu wa Chama Cha Walimu (CWT)Mkoa wa Ruvuma Luya Ngonyani

Na, Augustino Chindiye Tunduru

WATU watano wanashikiriwa na jeshi la Polisi Wilayani Tunduru Mkoani Ruvuma kwa tuhuma za kufanya majaribio ya kutaka kuwaua Walimu wawili wa Shule ya Msingi Ruanda iliyopo katika Tarafa ya Nakapanya Wilayani humo.

Taarifa za tukio hilo zinaeleza kuwa Walimu walionusulika katika tukio hilo ni Mwl. Ezakieli Ngaleka na Mwl.Emmanuel Hyao wanaodaiwa kuwa na urafiki wa kimapenzi na mke wa mtu.

Kamanda wa polisi wa Mkoa wa Ruvuma Michael Kamuhanda  amewataja watuhumiwa hao kuwa ni Ally Brashi (19) ambaye pamoja na mambo mengine amekiri kuhusika katika tukio hilo akidai kuwa alitekeleza tukio hilo kwa nia ya kutaka kumuua Mwl. Naleka akiwa anamtuhumu kuwa na mahusiano ya kimapenzi na Mkewe.

Wangine wanaoshikiriwa kutokana na tukio hilo ni pamoja na Mustafa Mariki (19), Mahamudu Juao (21), James Mathayo (20) na Hamisi Athuman (19)  wote wakiwa ni wakazi wa kijiji hicho.

Akizungumzia tukio hilo Kaimu afisa elimu wa shule za Msingi wa Wilaya ya Tunduru Mwl.Fravia Nchimbi alisema kuwa kufuatia tukio hilo idara yake imeamua kuwabadirishia vituo vya kazi ili kuwahakikishia usalama wa maisha yao.

Nae Kaimu Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Wilaya ya Tunduru Mwl. Rashid Mandoa alipotakiwa kuzungumzia tukio hilo alisema kuwa ofisi yake imewaagiza viongozi wa serikali ya kijiji hicho kufanya mazungumzo na  wananchi wao ili waachane na matukio ya aina hiyo.

Kuhusu nyumba iliyoteketea na moto huo alisema kuwa siyo mali ya Halmashauri hiyo bali ilikuwa ikimirikiwa na mkazi wa kijiji hicho  Fikirini Brashi ambaye alikuwa na mkataba wa kuwapangisha walimu hao na kwamba baada ya tukio hilo kamati ya shule na uongozi wa kijiji ndio utakaowajibika kumjengea nyumba nyingine.

Wakiongea kwa nyakati tofauti walimu hao walimshukuru mungu kwa kuwaokoa na tukio hilo pamoja na uongozi wa halmashauri hiyo ambao umekubali kuwagharamia kwa kuwanunulia vifaa na kuwafidia mali zilizo teketea katika tukio hilo zinazo kadiliwa kuwa na thamani ya zaidi ya shilingi milioni moja.

Mwisho