About


Karibu ujiunge na chuo cha kisasa cha Easy Tech.Computer kwa mafanikio yako,Walimu waliobobea katika fani hiyo wanapatikana chuoni hapo

elimak

elimak

Pages - Menu

Tuesday, August 30, 2011

KAMPUNI YA SONGEA NETWORK YAPANIA MAKUBWA KATIKA KILIMO NA ELIMU


                                     Na Thomas Lipuka,Songea
KAMPUNI ya Songea Network Centre na Valongo Network Centre za Mkoani Ruvuma zimeazimia kuimarisha kilimo cha Kahawa,ulezi na Jetropa katika Mkoa wa Ruvuma ili kuwakomboa wananchi wa kipato cha chini kwa kilimo hicho.
Kampuni hizo zimetambulishwa jana rasmi mbele ya Serikali ya Mkoa na kutaja malengo yao katika kuendeleza mazao hayo matatu kwa ustawi wa jamii za watanzania ambao zaidi ya asilimia 80 wanategemea kilimo.
Mkurugenzi wa Kampuni hizo Xaveri Kazimoto Komba ameyataja malengo yao kuwa ni kuendeleza elimu katika Mkoa,kuimarisha kilimo cha ulezi,kahawa na Jetropa,kukuza utamaduni na kuimarisha hali ya Mkoa kwa mazingira ili uoto wa asili usitoweke.
Komba alisema katika kuimarisha kilimo cha kahawa Mkoani Ruvuma tayari ameisha unganisha Mkoa na watafiti wa zao hilo toka Ujerumani ambao kwa kutumia teknolojia za kisasa wataliendeleza zao hilo na kuleta uzalishaji wenye tija ili kukuza kipato cha wakulima wa kahawa Mkoani Ruvuma.
Akiongelea hatua zingine za kuboresha uzalishaji wa zao hilo na mazao mengine yaliyo tajwa amesema hapata kuwepo na tatizo la soko kwani utaratibu umeisha andaliwa wa kununua mazao hayo iwapo yatazalishwa kwa kasi na kutunza ubora wake na soko limeandaliwa.
Akitambulisha mradi wa kuboresha elimu Kazimoto amesema tayari wameisha anzisha Sekondari ya St.Sapiensia ambayo ina kidato cha nne sasa na kuchukua wanafunzi wa dini zote wa kike na wa kiume,shule ambayo iko Parokia ya Mjimwema manispaa ya Songea.
Katika hatua nyingine tayari Songea Network Centre imeisha panda miti zaidi ya 500 ya kivuli matunda na mbao kwa hatua ya kulinda na kuboresha mazingira,miti ambayo imepandwa Songea mjini na Kijiji cha Mbinga Mhalule Tarafa ya Muhukuru.
Naye Kaimu Katibu Tawala Mkoa wa Ruvuma Vestina Nguruse ambaye kwa cheo chake ni mshauri wa mipango Mkoa amesema mradi wa kilimo kinachojali watu unaoanzishwa na Songea Network Centre uwe endelevu kwa kuwa mipango yake ni ukombozi kwa watu wa Ruvuma.
Amesema shida kubwa ni soko kwa mazao ya wakulima na bei zisizo za uhakika ambazo hubadilishwa mara kwa mara kutokana na soko la dunia linavyoendelea lakini kutokana na utafiti wa kina uliofanywa na Songea Network Centre bila wasiwasi suala la soko litadhibitiwa kikamilifu.
Nguruse amefafanua kuwa fursa za kuendeleza mazao haya katika Mkoa zipo za kutosha akataja uwepo wa ardhi safi kwa kilimo cha kahawa,ulezi na Jetropa  ni nguvu kazi ya kutosha yaani wakulima uwepo wa Bandari ya Mtwara na ujenzi wa barabara inayoendelea toka Mtwara Mbamba bay pia mito na mabonde yenye maji wakati wote kwa kilimo cha umwagiliaji.
Kaimu Katibu Tawala Mkoa Nguruse aliwaasa viongozi wa mradi kusimamia mradi huo uwe endelevu na utimize azima yake ya kumkomboa mkulima wa Mkoa wa Ruvuma
Wakati huo huo imefahamika kuwa jitihada za kupata soko la uhakika kwa mazao hayo matatu zimeletwa na Balozi wa Tanzania nchini Ujerumani Ahamad Ngemara ambaye amefanya jitihada kubwa kwa suala la masoko nchini Ujerumani.

KAIMU MKURUGENZI WA HALMASHAURI YA WILAYA YA SONGEA ANNA MBOGO

                                  

                                         WANANCHI SONGEA WAIFYATUKIA WIZARA YA AFYA
                                     Na Stephano Mango,Songea
 
WANANCHI wa Vijiji vilivyopo katika Halmashauri ya Wilaya ya Songea Mkoani Ruvuma wameiomba Serikali kupitia Wizara ya Afya na Ustawi wa Jamii kuona umuhimu wa kuwaletea watumishi wenye taaluma wakiwemo wauguzi na Waganga kwenye Zahanati na vituo vya Afya ambako kuna Upungufu wa Wataalamu.
 
Wakizungumza kwa Nyakati tofauti na mtandao wa http://www.stephanomango.blogspot.com/ wananchi hao wameeleza kuwa kwenye baadhi ya Zahanati na Vituo vya Afya vilivyopo Wilayani Songea kuna tatizo kubwa la upungufu wa Wauguzi na Waganga ambao umekuwa ukisababisha kuwepo kero kubwa kwa Wakazi wa Vijiji hivyo.
 
Hebron Mbilinyi Mkazi wa Kijiji cha Madaba alisema kuwa katika Kituo cha Afya cha Madaba kina wauguzi na waganga wachache na kusababisha kuwepo msongamano mkubwa wa wagonjwa wanaofika kupata tiba kwenye Kituo hicho.
 
Alisema kuwa huduma inayotolewa kwenye Kituo hicho cha Afya ni duni kwani wakati mwingine wagonjwa ambao wana uwezo kifedha hulazimika kutafuta Hospitali za kulipia ambako hupatiwa matibabu.
 
Said Hussein Mkazi wa Kijiji cha Muhukuru alisema kuwa Kituo cha Afya cha Muhukuru kimekuwa na tatizo kubwa la kutokuwa na Waganga hasa ikizingatia kuwa kina Mganga mmoja tu ambaye hulazimika kutoa huduma tangu asubuhi na wauguzi waliopo ni wachache hivyo anaiomba Serikali kupitia Wizara ya Afya na Ustawi wa Jamii ione umuhimu wa kuwakumbuka wakazi wa Muhukuru kwa kuwapelekea Wataalamu wenye sifa ambazo zitapunguza kero zilizopo Kijijini hapo ambako kuna umbali wa Kilomita 80 tokea Songea Mjini ambako kuna Hospitali ya Serikali ya Mkoa.
 
Fadhili Ngonyani Mkazi wa Kijiji cha Liyangweni alieleza zaidi kuwa Huduma inayotolewa katika Zahanati ya Kijiji hicho siyo ya kuridhisha kwasababu Zahanati hiyo ina Wauguzi wachache ambao ndiyo wamekuwa wakitoa huduma badala ya Mganga ambaye hajaletwa tangu muda mrefu hivyo ameitaka Halmashauri ya Wilaya hiyo kuchukua hatua za haraka kutafuta Waganga pamoja na Wauguzi kwenye Zahanati hiyo ili kupunguza kero iliyopo Kijijini hapo.
 
Kwa upande wake Kaimu Mkurugenzi wa Halmashauri ya Wilaya ya Songea Anna Mbogo aliuambia mtandao huu kuhusiana na kuwepo kwa malalamiko toka kwa Wananchi ya upungufu wa wataalamu kwenye Zahanati na Vituo vya Afya alikiri kuwa Halmashauri yake ina upungufu wa Wataalamu kwenye Zahanati na Vituo na Afya.
 
Mbogo alisema kuwa Halmashauri hiyo ina Vituo viwili vya Afya ambapo alivitaja kuwa ni Kituo cha Afya cha Muhukuru na Kituo cha Afya cha Madaba ambavyo vyote vina waganga watatu tu badala ya kuwa na waganga wanne kila kimoja.
 
Alifafanua kuwa Halmashauri hiyo pia ina Zahanati za Vijiji 23 ambazo zina wauguzi na waganga wachache na baadhi ya Zahanati zilizopo hazina waganga na badala yake wauguzi ndiyo wamekuwa wakitoa huduma kwenye Zahanati hizo.
 
Alizitaja Zahanati ambazo hazina kabisa waganga kuwa ni Liyangweni,Nambendo,Gumbiro na Ngahokola na Kituo cha Afya cha  Muhukuru kina mganga na Madaba kuna waganga wawili wakati kila Kituo cha Afya kulipaswa kuwe na waganga wanne na kwenye Zahanati kunapaswa kuwe na waganga wawili.
 
Alieleza zaidi kuwa kutokana na hali hiyo kwenye vituo vya afya kuna upungufu wa waganga watatu na kwenye Zahanati kuna upungufu wa waganga 29 wakati mahitaji ya waganga kwenye Halmashauri hiyo bado ni kubwa na kusababisha kuwepo Changamoto kubwa ya upungufu mkubwa wa wataalamu wenye sifa wakiwemo wauguzi na waganga  jitihada inaendelea kufanywa ya kutafuta waganga na wauguzi wenye sifa kujaza nafasi zenye upungufu kwenye Zahanati
 

MIKARATUSI NI MITI HATARI KATIKA VYANZO VYA MAJI KWENYE MILIMA YA MATOGORO

                             Na Thomas Lipuka,Songea
 
IMEBAINI kuwa ukosefu wa maji kiangazi katika Manispaa ya Songea unachangiwa kwa kiasi kikubwa na aina ya miti ambayo ipo katika misitu ya milima Matogoro ambayo hunyonya maji kwa kiwango kikubwa kwa kipindi cha mwaka.
 
Afisa maliasili wa Mkoa Ruvuma Enock Buja akizungumza na mtandao wa http://www.stephanomango.blogspot.com/ alisema utafiti uliofanywa na Taasisi inayoshughulikia utafiti wa misitu nchini ijulikanayo kama  TAFORMA, imebaini kuwa kuna aina kadhaa ya miti ambayo kwa kiwango kikubwa.
 
Ameitaja miti hiyo kuwa ni mikaratusi (Camaldulensis) ambayo hunyonya maji kiasi cha milimita 1240 kwa mwaka na mikaratusi aina ya (Microrhea) pia hunyonya maji milimita 1050 kwa mwaka.
 
Afisa maliasili huyo wa Mkoa amefafanua kuwa ,aina nyingine ya miti inayonyonya maji kwa wingi ni mikaratusi hujulikana kama patula wenye uwezo wa kunyonya maji kiasi cha milimita 665 kwa mwaka.
 
Katika ufafanuzi Buja amesema miti hiyo yote iliyo tajwa ipo misitu ya milima matogoro ambapo kiasi mingi imeondolewa kwa maji ikiwa kiasi, tu ikiwa na lengo la kuiondoa isilete hatari ya kukosekana kwa maji,kwa wakazi wa Manispaa ya Songea.
 
Afisa maliasili huyo ameongeza kusema kuwa kiasi kilichotajwa hunyonywa na miti hiyo ambapo  kwa mti mmoja na sio kwa uwingi wake katika misitu.
 
Katika utafiti huo imeelezwa kuwa ipo miti mingine kwa mfano mgunga na mvile inayoelekea kutumia maji mengi kuliko mikaratusi iliyotajwa hapo juu.
 
Amesema baadhi ya mazao ya kilimo mathalani mpunga na miwa nayo hutumia kwa kiwango ambacho karibu sawa ya mikaratusi.
 
Katika msukumo wa Kitaifa  wa kupunguza umaskini MKUKUTA mbinu nyingi zinafikiliwa kutumika katika kufikia azma hiyo bahati mbaya upandaji miti katika vyanzo vya maji haujatiliwa mkazo kwa umakini hasa miti gani ipandwe ili kuondokana na tatizo la miti kunyonya maji.
 
Ni sahihi kabisa kuvuna miti iliyopo misitu ya milima matogoro kwani miti hiyo ni hatari na ni adui mkubwa wa chanzo kikuu cha maji yatumiayo katika Manispaa ya Songea.
 
Hivi sasa Taifa limeagiza kuwa kila Wilaya ipande miti zaidi ya 1500 ili kurudisha jotoridi  na kuondoa hewa ya ukaa ambayo inatishia Taifa letu kwa tabia mbaya za baadhi ya watu wakatao miti bila kupanda au kwa ajili ya mkaa na shughuli za ujenzi na za kibinadamu.
 
Hali ya uchomaji moto ni tatizo la pili katika misitu ya milima matogoro mbali ya juhudi za mkoa za kurudishia miti hiyo mwaka hadi mwaka kwa utaratibu wa kupanda miti ya asili ambayo hainyonyi maji kwa wingi jambo hilo juhudi zake linafifishwa na watu waharibifu wanaoendeleza vitendo vya uchomaji moto katika mlima matogoro na misitu yake  Mkoani  Ruvuma.

MILIONI 215 KUTUMIKA KUNUNULIA MADAWA YA KUULIA WADUDU


                      Na Stephano Mango,Mbinga
 
SERIKALI kwa kushirikiana na wadau wa zao la kahawa Wilayani Mbinga mkoa wa Ruvuma imechangisha jumla ya shilingi milioni 215 kwa ajili ya kununulia madawa yatakayotumika kupambana  na wadudu waharibifu wa zao hilo.
 
Katibu tawala wa wilaya hiyo Idd Mponda alisema fedha hizo zimetumika kununulia madawa aina ya SUBA ambayo hutumika kuulia wadudu aina ya vidung’ata ambao wamekuwa wakishambulia miti ya kahawa.
 
Alisema kuwa jumla ya hekta 48 ya zao hilo zimeshambuliwa na wadudu hao na kusababisha uzalishaji wa kahawa kushuka.
 
 Mponda alisema kufuatia jitihada zilizofanyika kuanzia Julai mwaka jana hadi sasa za kutokomeza wadudu hao mashamba mengi yameonekana kwenda vizuri na kwamba katika msimu wa mwaka 20011/12 uzalishaji unatarajia kuongezeka hadi kufikia tani 9,000.
 
"Kinachotakiwa kwa wakulima ni kuhakikisha wanazingatia yale wanayoelekezwa na wataalamu wa kilimo na kwamba wajiunge pamoja na kuanzisha  mashamba darasa ili iwe rahisi kwa maofisa ugani kuwafikia", alisema Mponda.
 
Kuhusu wanunuzi wa zao hilo alisema wanapaswa kuzingatia masharti yaliyowekwa na uongozi wa wilaya hiyo na kwamba kwa wale ambao watabainika kutorosha kahawa kwa lengo la kukwepa kulipa ushuru watachukuliwa hatua za kisheria ikiwemo kunyang’anywa leseni ya biashara hiyo.
 
Pia alisema wakati umefika kwa wakulima wa zao hilo kuwa makini na wafanyabiashara wajanja wanaozunguka vijijini kununua zao hilo kwani baadhi yao wamekuwa wakiwarubuni wakulima kuwa bei ya kahawa imeshuka kwenye soko la dunia ili wanunue zao hilo kwa bei ya chini jambo ambalo sio sahihi.