About


Karibu ujiunge na chuo cha kisasa cha Easy Tech.Computer kwa mafanikio yako,Walimu waliobobea katika fani hiyo wanapatikana chuoni hapo

elimak

elimak

Pages - Menu

Saturday, March 10, 2012

SUFA WAANZA KUTOA FOMU ZA KUGOMBEA NAFASI MBALIMBALI ZA UONGOZI

                                                Katibu Msaidizi wa SUFA Godfrey Mvula
Na Gideon Mwakanosya, Songea

CHAMA cha mpira wa miguu Manispaa ya Songea(SUFA) kimeanza kutoa fomu za kuwania nafasi mbalimbali za  uongozi wa chama hicho, uchaguzi ambao umepangwa kufanyika mwishoni mwa mwezi huu.

Akizungumza mjini hapa jana Katibu Msaidizi wa SUFA, Godfrey Mvula alisema kuwa pamoja na utoaji wa fomu za kugombea nafasi mbalimbali za  uongozi wa chama hicho, bado kamati ya utendaji wa SUFA kimepanga kuteua kamati ya kusimamia uchaguzi huo ambao utafanyika Machi 30 mwaka huu katika ukumbi ambao utakaopangwa.

Alisema wagombea wa nafasi hizo wanatakiwa wawe angalau na elimu sio chini ya kidato cha nne na awe mtu anayejihusika na soka kwa kuongoza vilabu  ili kujenga ufanisi na uelewa zaidi katika kufanikisha na changamoto ya maendeleo ya soka katika Manispaa hiyo.

Alisema wagombea wote watakaojitosa kuchukua fomu na kuzirejesha watafanyiwa usaili wao wa mwisho Machi 25 kabla ya kuingia katika uchaguzi wa kuwania nafasi hizo za uchaguzi ambao watakaa madarakani kwa muda wa miaka mitatu.

Alisema SUFA kwa sasa inaongozwa na Mwenyekiti wake Gorden Sanga na ina vilabu vya soka 35 ikiwemo Majimaji ambavyo vimesajili kupitia msajili wa vyama vya michezo na vilabu nchini.
  MWISHO

RC MANYANYA ASHUSHA PRESHA YA WANANCHI WA MDUNDUALO KUHUSU MAENEO YAO KUCHUKULIWA NA WACHIMBAJI WA MAKAA YA MAWE NGAKA WILAYANI MBINGA

Mkuu wa Mkoa wa Rukwa Mhandisi Stella Manyanya ambaye pia ni Mbunge wa Vitimaalu Mkoa wa Ruvuma akizungumza na wananchi wanaozunguka mgodi wa makaa ya mawe ya Ngaka Wilayani Mbinga kuhusu mgogoro wa wananchi na wawekezaji katika mgodi huo

Wananchi wanaozunguka mgodi wa uchimaji wa makaa ya mawe wakimsikiliza Mkuu wa Mkoa wa Rukwa na Mbunge wa Vitimaalum Mkoa wa Ruvuma Mhandisi Stella Manyanya



WATU WAWILI WAMEFARIKI KATIKA MATUKIO MAWILI TOFAUTI WILAYANI TUNDURU

Na,Augustino Chindiye Tunduru

WATU wawili wamefariki dunia katika  matukio tofauti yaliyotokea wilayani Tunduru Mkoani Ruvuma likiwemo tukio la kuuawa kwa kushambuliwa kwa mapanga kutoka na kilichodaiwa kuwa chanzo chake ni ugomvi wa kugombea eneo la kulima na mwingine kupigwa na radi.

Taarifa za tukio la Mauaji ya kugombea shamba lilitokea katika kijiji cha Nakawale katika Kata ya Nandembo ambapo Mtu aliyeuawa amefahamika kwa jina la Said Kaunya.

Akizungumzia tukio hilo mjomba wa marehemu Yusuph Mangalai alisema kuwa marehemu alikumbwa na maswahibu hayo usiku wa kuamkia machi 9 mwaka huu ambapo baada ya maharamia hao kutekeleza unyama huo waliuficha mwili wa marehemu kwa kuuzika pembeni mwa bwawa la maji
hali ambayo iliwapa wakati mgumu wanafamilia.

Hata hivyo Mangalai amewapongeza watu wote walioshiriki katika msako uliofanikisha kupatikana kwa mwili wa marehemu na kuuzika katika makaburi ya Njasi Mjini Tunduru.

Kwa mujibu wa taarifa hizo tukio la pili lililo husu kifo cha Mkulima kupigwa radi kilitokea katika kijiji cha Kangomba Wilayani humo ambapo aliye fariki dunia katika tukio hilo amefahamika kwa jina la Said Abubakari(43),

Akizungumzia tukio hilo Kaka wa marehemu Ally Hatibu alisema kuwa Marehemu alikumbwa na mkasa huo ulimpata wakati akipandikiza mihogo
shambani kwake.

Alisema katika tukio hilo marehemu aliunguzwa vibaya kuanzia chini ya mguu hadi kichwani upande wa kulia na kufariki papo hapo.

Kamanda wa polisi wa mkoa wa ruvuma Naftali Mantamba amethibitisha kuwepo kwa matukio hayo na kueleza kuwa polisi wanendelea na uchunguzi
ili sheria ifute mkondo wake.


Mwisho

WAKULIMA WA KOROSHO WILAYA YA TUNDURU WAENDELEA KULILIA SOKO LA ZAO LAO

MKUU WA WILAYA YA TUNDURU JUMA MADAHA

Na,Augustino Chindiye,Tunduru

WAKATI Serikali ikiwa imetoa tamko la kuwafutia Leseni Wanunuzi wa
Korosho nchini, Wakulima wa zao hilo Wilayani Tunduru  Mkoani Ruvuma
wamehoji hatima ya Soko la Korosho zao.

Hayo yalitokea katika kikao cha wadau wa Korosho kilichofanyika katika Ukumbi wa Chama Kikuu cha Wakulima (TAMCU) na kuwashirikisha Waandishi na Wenyeviti wa Vyama vya msingi vya wakulima wa zao hilo na wakaituhumu Serikali ya awamu ya nne kuwa imekuwa butu katika  kutoa maamuzi hali ambayo inawafanya Wanachi kukata tamaa juu ya utendaji wake.

Wawakirishi wa Wakulima kutoka Chama cha Msingi  Litungulu Mohamed
Matoto na Yasini Masiano wa Chichilimbe walisema kuchelewa kutolewa
kwa maamuzi kunako fanywa na Serikali kumewafanya viongozi wa vyama
vya msingi kuishi katika hofu ya kufanyiwa fujo na wakulima wao.

Awali akifungua kikao hicho Mwenyekiti wa Chama kikuu cha Wakulima Wa
Korosho (TAMCU) Mohamed Katomondo mbali na kupongeza hatua zilizo
chukuliwa na Serikali kwa kunukuu kauli ya Makampuni hayo
kunyang`anjwa Leseni bila majadiliano iliyotolewa na Rais wa Jamuhuri
ya Muungano wa Tanzania Dkt. Jakaya Kikwete na kuongeza kuwa katika
tamko hilo hakukuwa na kipengele wala maelekezo yaliyozungumzia hatima
ya Korosho za wakulima.

Aidha katika taarifa hiyo Katomondo alionesha mashaka ya kuendelewa
kwa zao hilo kutokana na wakulima wengi kukatishwa tamaa na utaratibu
wa mfimo wa Stakabadhi ghalani wakidai kuwa mfumo huo unanyonya nguvu
zao.

Akitoa taarifa ya mdororo wa Korosho hizo Meneja wa Chama Kikuu cha
Ushirika wa Wakulima wa Korosho Wilayani Tunduru (TAMCU)Imani
Kalembo alisema kuwa katika msimu wa Mwaka 2011/2012 chama hicho kupitia
vyama vya msingi vya wakulima takwimu zinaoneshja kuwa uzalishaji
umeongezeka kutoka kilo 4,135,042 za mwaka 2010/2011 hadi kilo 7,570,000.

Kalembo aliendelea kufafanua kuwa hadi kufikia Februari 29 mwaka huu
takwimu zinaonesha kuwa Korosho zilizopokelewa Maghalani ni Kilo
6,842,446 na kilo 641,230 zipo katika maghala ya watu binafsi na
zingine zipo nje ya ofisi za chama hicho na kilo 86,324 bado zipo
mikononi mwa wakulima huku takwimu hizo zikionesha kuwa ni kilo
1,890,384 tu ndizo zilizouzwa katika mnada mmoja kati ya minada tisa
iliyofanyika hali inayotishia chama hicho kushindwa kulipa malipo ya pili ya wakulima ambapo TAMCU inadaiwa Jumla ya Shilingi 2,441,870,350/= .

Taarifa hiyo iliendelea kueleza kuwa deni hilo limetokana na chama
hicho kununua jumla ya Kilo 6,976,821 ambazo Chama hicho kupitia vyama
vya msingi vimeweza kuzilipia kwa asilimia 70% pekee, sambamba na Deni
la Shilingi 608,260,000 zilizotokana na Mkopo wa  kilo 506,855 za Korosho za zilizo kopeshwa na wakulima kwa vyama vya Msingi.

Kalembo aliendelea kueleza kuwa wakati hayo yakiendelea Chama
hicho pia  kinakabiliwa na changamoto ya Chama kushindwa kununua jumla
ya kilo 86,324 zenye Dhamani ya Shilingi Milioni 17,264,800 ambazo
bado zipo mikononi mwa wakulima wa zao hilo hali inayo endelea
kuwakatisha tamaa ya kuendelea na kilimo hicho

Akizungumza na waandishi wa habari hivi karibuni Mjini Songea Katibu
Mtendaji wa Shirikisho la Vyama vya Ushirika Wilgisi Mbogoro,
alisema takwimu za Korosho zote zilizokwama baada ya wanunuzi
kutunisha misuli kuzinunua ni kilo 72,978,340 zenye thamani ya
shilingi Bilioni 113.7

Wakitoa salamu za Serikali Mkuu wa Wilaya ya Tunduru Juma Madaha namlajisi msaidizi wa vyama vya Ushirika Mkoani Ruvuma WatsonNganiwa walisema kuwa msimamo wa Serikali ni kuhakikisha kuwa Korosho zote zinanunuliwa kutoka kwa wakulima na wakatumia nafasi hiyo kuwaomba wakulima kuwa na subira wakati taratibu za mchakato wa kufanikisha hayo zikiendelea.
Mwisho