About


Karibu ujiunge na chuo cha kisasa cha Easy Tech.Computer kwa mafanikio yako,Walimu waliobobea katika fani hiyo wanapatikana chuoni hapo

elimak

elimak

Pages - Menu

Monday, November 21, 2011

DEREVA AFA PAPO HAPO BAADA YA GARI LAKE KUACHA NJIA NA KUPINDUKA

  Kamanda wa Polisi Mkoani Ruvuma Michael Kamuhanda
 
Na Gideon Mwakanosya, Songea
 
Mtu mmoja amekufa papo hapo na kujeruhiwa watu sita huko katika Kijiji cha Mlilayoyo Wilayani Namtumbo Mkoani Ruvuma baada ya gari walilokuwa wakisafiria kutoka Njombe kwenda Hanga kuacha njia na kupinduka.
 
Akizungumza na mtandao wa http://www.stephanomango.blogspot.com/   jana ofisini kwake Kamanda wa Polisi Mkoa wa Ruvuma Michael Kamuhanda amesema kuwa tukio hilo lilitokea jana majira ya saa 11.45 jioni kwenye barabara ya Mlilayoyo kuelekea Hanga na amemtaja aliyekufa papo hapo baada ya gari hilo kuacha njia na kupinduka Leonala Msemwa (60) Mkazi wa Kijiji cha Hurika kilichopo Wilayani Njombe Mkoa wa Iringa.
 
Kamuhanda amewataja waliojeruhiwa vibaya kuwa ni Kristofa Salingwa (30),Roida Salingwa (37),Luciana Salingwa ( 25 ) na Nelson Mligo (1) wote wakazi wa Kijiji cha Itulika Wilayani Njombe Mkoa wa Iringa wengine waliojeruhiwa ni Prisca Salingwa ( 28) Mkazi wa Kijiji cha Mtwango kilichopo Wilayani Njombe Mkoa wa Ruvuma na dereva wa gari hilo Steven Ngonyani (28) Mkazi wa Mfaranyaki Manispaa ya Songea.
 
Amefafanua zaidi kuwa inadaiwa siku hiyo ya tukio huko kwenye barabara ya Mlilayoyo kwenda Hanga Wilayani Namtumbo gari lenye namba za usajili T 360 AJF TOYOTA MARK II, rangi nyeupe ambayo ilikuwa ikiendeshwa na Steven Ngonyani ikitokea Njombe kwenda Hanga iliacha njia na kupinduka kisha ilisababisha kifo cha Leonala Msemwa na majeruhi sita.
 
Amebainisha zaidi kuwa majeruhi wawili dereva wa gari hilo Steven Ngonyani na Kristofa Salingwa kwasasa wamelazwa katika hospitali ya Serikali ya Mkoa Songea wakiwa wanaendelea kupata matibabu na majeruhi wengine wanne wametibiwa na kuruhusiwa kurudi nyumbani kwao na hali zao zinaendelea vizuri.
 
Kamanda Kamuhanda ameeleza kuwa chanzo cha ajali hiyo ni kwamba dereva wa gari hilo alikuwa kwenye mwendo kasi ambao ulimsababishia ashindwe kuumudu usukani kisha gari hilo liliacha njia na kupinduka.
 
MWISHO

No comments:

Post a Comment