About


Karibu ujiunge na chuo cha kisasa cha Easy Tech.Computer kwa mafanikio yako,Walimu waliobobea katika fani hiyo wanapatikana chuoni hapo

elimak

elimak

Pages - Menu

Tuesday, September 20, 2011

MWENDESHA PIKIPIKI ASABABISHA KIFO CHA MTEMBEA KWA MIGUU

 
                    Na Gideon Mwakanosya,Songea
POLISI wilayani Mbinga Mkoani Ruvuma wanamshikilia Mwendesha Pikipiki Felix Ndimbo (18) mkazi wa Kijiji cha Langilo kwa tuhuma za kumgonga mtembea kwa miguu Joseph Ndimbo (76) mkazi wa Kijiji cha Mkoha wilayani humo na kumsababishia kifo papo hapo

Habari zilizopatikana jana mjini hapa ambazo zimethibitishwa na Kamanda wa Polisi wa Mkoa wa Ruvuma zimeeleza kuwa lilitokea juzi majira ya 1:30 usiku kwenye barabara inayotoka Mbinga kwenda kijiji cha Langilo

Kamuhanda alibainisha zaidi kuwa siku hiyo ya tukio kwenye barabara hiyo Felix akiwa anaendesha Pikipiki ambayo haina namba za usajili aina ya SanLg ilimgonga mtembea kwa miguu mzee Joseph Ndimbo ambaye alikuwa anatoka Kijiji cha Langilo kwenda katika Kijiji cha Mkoha na kumsababishia kifo papo hapo

Alieleza zaidi kuwa chanzo cha tukio hilo mwendesha Pikipiki Felix akiwa anatokea Kijiji cha Mkoha kuelekea Kijiji cha Langilo akiwa kwenye mwendo mkali alimgonga mtembea kwa miguu Joseph ambaye alikuwa anatembea kandokando ya barabara upande wa kulia

Kamuhanda alisema kuwa mtuhumiwa Felix amekamatwa na anaendelea kuhojiwa na Polisi ambapo upelelezi wa tukio hilo ukikamilika atafikishwa mahakamani kujibu mashtaka yanayomkabili
MWISHO

No comments:

Post a Comment