About


Karibu ujiunge na chuo cha kisasa cha Easy Tech.Computer kwa mafanikio yako,Walimu waliobobea katika fani hiyo wanapatikana chuoni hapo

elimak

elimak

Pages - Menu

Thursday, October 6, 2011

AJINYONGA KWA KUMKATAA MKE MWENZA WILAYANI MBINGA


 Na Gideon Mwakanosya, Songea
MWANAMKE  mmoja Apolonjali Hyera (45) Mkazi wa Kitongoji cha Mapendano kilichopo katika Kijiji cha Mzuzu Wilayani Mbinga amekufa kwa kujinyonga kwa kutumia kamba ya katani baada ya mume wake kuoa mwanamke mwingine.
Habari zilizopatikana jana mjini hapa ambazo zimethibitishwa na Kaimu Kamanda wa Polisi Mkoa wa Ruvuma Naftani Mantamba zimesema kuwa tukio hilo limetokea Octoba 5 mwaka huu majira ya saa 6 mchana huko katika Kitongoji cha Mapendano kilichopo katika Kijiji cha Mzuzu Wilayani Mbinga.
Mantamba amesema kuwa siku hiyo ya tukio inadaiwa Apolonjali alikutwa akiwa amejinyonga kwa kutumia kamba ya katani  kwa kujining’iniza juu ya mti kwenye msitu mkubwa wa Kijiji hicho.
Ameeleza zaidi kuwa Apolonjali anadaiwa kuwa aliamua kujinyonga baada ya kumtuhumu mume wake kuamua kuoa mwanamke mwingine wakati yeye ametoka nyumbani kwa wazazi wao na yupo kwaajili yake hivyo alikuwa akijiuliza ni kwanini ameamua kuchukua uamuzi huo.
Amefafanua zaidi kuwa kutokana na kuwepo kwa mvutano huo kati yake na mume wake Kelvin Sesilisi (45) ndiyo aliamua kuchukua uamuzi wa kujiua na kuacha maagizo kuwa ameamua aondoke amuache mwanamke aliyempata
Mantamba amesema kuwa chanzo cha tukio hilo ni wivu wa mapenzi ambao umemsababishia Apolonjali kufikia uamuzi wa kujiua kwa kujinyonga kwa kujining’iniza kwenye mti uliopo katikati ya msitu

No comments:

Post a Comment