About


Karibu ujiunge na chuo cha kisasa cha Easy Tech.Computer kwa mafanikio yako,Walimu waliobobea katika fani hiyo wanapatikana chuoni hapo

elimak

elimak

Pages - Menu

Thursday, October 27, 2011

WANANCHI WAENDELEA KUMPOKEA KWA SHANGWE MBUNGE STELLA MANYANYA NA MKUU WA MKOA WA RUKWA KATIKA ZIARA YAKE YA KIKAZI MKOANI RUVUMA

Mbunge Mhandisi Sella Manyanya wa kwanza kulia akipiga ngoma ya Beta baada ya kufurahia mapokezi mazuri katika ziara yake,wa kwanza kushoto ni Katibu wa Mkuu wa Mkoa wa Rukwa Frank Maten akishuhudia mapokezi hayo

Mhandisi Stella Manyanya ambaye ni Mkuu wa Mkoa wa Rukwa na Mbunge wa Viti Maalumu Mkoa wa Ruvuma akimpatia Katibu wa UWT Wilaya ya Songea Mjini shillingi laki mbili kwa ajili ya mahitaji madogo madogo ya ofisi ya UWT Wilaya ya Songea Mjini,baada ya kupokea ripoti ya utekelezaji kwa kipindi cha mwaka 2011, katikati ni Katibu wa UWT Mkoa wa Ruvuma Mariam Yusuph

Viongozi wa Chama na Serikali wakifanya maombi kwenye kabuli la Nduna Songea Mbano

Mjukuu wa Nduna Songea Mbano,Aidan Mbano akizungumza na Wazee Mashujaa 66 waliozikwa kwenye kabuli la pamoja ikiwa ni dua maalum kwa Mbunge na Mkuu wa Mkoa wa Rukwa na Mwenyekiti wa Kamati ya Ushauri wa Makumbusho ya Taifa ya Majimaji Songea Mhandisi Stella Manyanya alipotembelea Makumbusho hayo ili kupata baraka za Wazee hao ikiwa ni desturi yake kabla ya kuanza ziara zake mkoani Ruvuma

Viongozi mbalimbali wa chama na Serikali wakimkaribisha Mbunge na Mkuu wa Mkoa wa Rukwa Mhandisi Stella Manyanya kwenye viwanja vya mkutano vya Makumbusho ya Taifa ya Majimaji Songea

Mama wa Kimasai akimpatia zawadi za kabila hilo Mbunge Mhandisi
Stella Manyanya baada ya kuwahutubia wananchi wa Songea Mjini katika viwanja vya Makumbusho ya Taifa ya Majimaji
Viongozi wa chama wa Wilaya ya Namtumbo wakimpokea Mbunge Mhandisi Stella Manyanya

No comments:

Post a Comment