About


Karibu ujiunge na chuo cha kisasa cha Easy Tech.Computer kwa mafanikio yako,Walimu waliobobea katika fani hiyo wanapatikana chuoni hapo

elimak

elimak

Pages - Menu

Saturday, January 28, 2012

KAMATI MASHINDANO YA SANGA ONE CUP KUZINDULIWA MCHANA HUUUUUUUUUUU

Na Stephano Mango,Songea
KAMATI ya kuandaa na kusimamia Mashindano  ya Sanga One Cup kuzinduliwa mchana huu katika viwanja vya Sanga One Bombambili
Akizungumza na Mtandao huu wa www.stephanomango.blogspot.com, Diwani Mstaafu wa Kata ya Bombambili na Mwenyekiti wa Chama cha Mpira wa Miguu ambaye pia ni mdhamini wa mashindao hayo Golden Sanga (Sanga One) alisema kuwa tayari wajumbe hao wamepatikana ambao watafanya uchaguzi mdogo ili kuweza kuwapata viongozi wake
Sanga alisema kuwa kazi yao kubwa itakuwa ni kuandaa mashindao hayo na kusimamia mashindano hayo kwa haki na usawa ili waweze kupatikana washindi stahiki na wachezaji bora watakaoweza kuibuliwa na mashindano hayo
Alisema kuwa anategemea kuwa wajumbe hao watawapata viongozi wenye busara na uzalendo katika kusimamia mashindano hayo,kuibua wachezaji chipukizi watakao chukuliwa kuchezea timu zingine za Wilaya,Mkoa na Taifa na kuleta ushindani mkubwa katika soka
Alieleza kuwa wajumbe wa kamati hiyo tayari wameanza kuwasili katika viwanja vya mkutano ili kuweza kutimiza lengo la kikao na kwamba anaamini kuwa kamati hiyo itafanya kazi yake vizuri kama ilivyokusudiwa
MWISHO

No comments:

Post a Comment