About


Karibu ujiunge na chuo cha kisasa cha Easy Tech.Computer kwa mafanikio yako,Walimu waliobobea katika fani hiyo wanapatikana chuoni hapo

elimak

elimak

Pages - Menu

Friday, July 20, 2012

MAVETERANI WA SIMBA NA YANGA SONGEA DIMBANI JULAI 22

Mdhamini  mkuu wa mechi ya Simba na Yanga Gorden Sanga (Sanga One) akizungumza na waandishi wa habari

Na Stephano Mango, Songea
MAVETERANI wa Simba na Yanga wa Kata ya Bombambili Halmashauri ya Manispaa ya Songea wameanza mazoezi kwa ajiri ya mechi ya kirafiki ambayo wanatarajia kucheza Julai 22 mwaka huu yenye lengo la kuboresha mahusiano ya kijadi
Akizungumza na waandishi wa habari jana Mdhamini mkuu wa mechi hiyo Gorden Sanga (Sanga One) alisema kuwa mavetani wamekuwa wakikutana vijiweni na kufanya ushabiki wa timu hizo ambazo zina mashabiki wengi bila nao kushiriki kucheza katika maeneo yao
Sanga alisema kuwa tayari wachezaji wa timu zote mbili wamesha sajiriwa kutoka katika pande zote za Halmashauri ya Manispaa ya Songea kwa ajiri ya mechi hiyo yenye ushindani mkubwa na majigambo ya pande zote mbili
Alisema kuwa kamati ya maandalizi imejipanga kikamilifu kwa mechi hiyo ambapo zawadi za mfungaji bora, mchezaji bora na kipa bora zimeandaliwa na zitatolewa siku hiyo kwa lengo la kuthamini mechi hiyo na kanuni bora za michezo
Alieleza kuwa siku ya mechi ulinzi utakuwa wakutosha ili kuweza kudhibiti vitendo vya fujo na uhalifu wowote ule ambao unaweza kutokea kutokana na Maveterani hao kutambiana sana kutokana na hamu ya mechi hiyo itakayofanyika kwenye viwanja vya Shule ya Msingi Sokoine mjini hapa
Alifafanua kuwa mechi hiyo inadhaminiwa na wapenzi wa michezo mjini Songea ambao ni Sanga One Transport, Top One Inn Hotel na Redio Jogoo na kwamba amewataka washabiki wa michezo kujitokeza kwa wingi katika mechi, pia amewaasa wachezaji kucheza kwa amani na upendo mkubwa na mashabiki kushangilia bila kuleta vurugu kwani michezo ni amani
MWISHO


No comments:

Post a Comment