About


Karibu ujiunge na chuo cha kisasa cha Easy Tech.Computer kwa mafanikio yako,Walimu waliobobea katika fani hiyo wanapatikana chuoni hapo

elimak

elimak

Pages - Menu

Tuesday, August 7, 2012

NGOMA ACHAGULIWA KUWA MAKAMU MWENYEKITI WA NAMTUMBO

Makamu Mwenyekiti wa Halmashauri ya Namtumbo Titus Ngoma
Na Stephano Mango, Songea
MADIWANI wa Halmashauri ya Wilaya ya Namtumbo mkoani Ruvuma wamemchagua Titus Ngoma kwa kura 24 kuwa Makamu Mwenyekiti wa Halmashauri hiyo atakayeongoza kwa kipindi cha mwaka mmoja kuanzia agosti mwaka huu
Akizungumza na waandishi wa habari mara baada ya kumalizika kwa kikao cha  Baraza la Madiwani, Mwenyekiti wa Halmashauri hiyo Stivin Nana alisema kuwa Madiwani katika halmashauri hiyo wapo 24 na wote kwa ujumla wao wamemchagua Diwani wa Kata ya Kitanda kushika nafasi hiyo
Nana alisema kuwa sheria na kanuni za mabaraza ya Madiwani zinasema wazi kuwa Mwenyekiti wa Halmashauri akichaguliwa ataongoza kwa kipindi cha miaka mitano, lakini nafasi ya Umakamu Mwenyekiti na Kamati mbalimbali za Madiwani zinachaguliwa kila baada ya mwaka mmoja
Alisema kuwa awali nafasi hiyo ilikuwa inashikiliwa na Diwani wa Kata ya Hanga Kassim Ntala ambaye aliongoza nafasi hiyo kwa kipindi cha mwaka mmoja na kwamba awamu hii hakugombea tena nafasi hiyo
Alifafanua kuwa mchakato wa kumpata Ngoma ulianza ndani ya Chama cha Mapinduzi (Ccm) Wilaya ya Namtumbo na kupelekwa Ccm mkoa wa Ruvuma na kurudishwa kwenye Wilaya kwa ajiri ya uchaguzi wa kumpata mgombea mmoja kwani wagombea walikuwa watatu ambao ni Daniel Nyambo ambaye alipata kura 4, Gidion Mpilime alipata kura 6 na Titus Ngoma alipata kura 14 ndani ya chama na kwamba ndani ya Baraza la Madiwani alichaguliwa kwa kura 24
MWISHO

No comments:

Post a Comment