About


Karibu ujiunge na chuo cha kisasa cha Easy Tech.Computer kwa mafanikio yako,Walimu waliobobea katika fani hiyo wanapatikana chuoni hapo

elimak

elimak

Pages - Menu

Friday, August 10, 2012

WASIMAMIZI NA MAKARANI WA SENSAWAONYWA

Na Steven Augustino, Tunduru

SERIKALI ya Wilaya ya Tunduru Mkoani Ruvuma imewaonya wasimamizi na makarani wa SENSA wanaojiona kuwa hawataweza kufanya kazi hiyo wajiondoe wenyewe haraka na kuwapisha wanaoweza kufanya kazi hiyo bila kushurutishwa ili kufanikisha zoezi hilo.

Kauli hiyo imetolewa na Mkuu wa Wilaya ya Tunduru  Chande Nalicho wakati akifungua mafunzo ya wasimamizi na makarani wa Sensa ya watu na makazi iliyopangwa kufanyika Agosti 26 mwaka huu katika kumbi za Tunduru Sekondari, Nakapanya, mbesa na Ligoma Wilayani humo.

Akifafanua taarifa hiyo Nalicho alisema kuwa baada ya mafunzo hayo watatakiwa kusaini Mkataba na serikali unaoelekeza hatua atakazo chukuliwa karani au msimamizi endapo atavurunda zoezi hilo na kwamba wale wanaojiona kuwa waliteuliwa kimakosa ama waliomba nafasi hizo kwa lengo la kujinufaisha kwa fedha wajiondoe mapema ili nafasi zao ziweze kuzibwa kabla mkondo wa sheria hauja chukua nafasi yake.

“Serikali imetumia fedha nyigi katika kuhakikisha kuwa zoezi hilo linatekelezwa kwa ufanisi wa kutosha hivyo hatuwezi kuwavumilia watu wenye nia mbaya na watakao hujumu utekelezaji wake”alisema Nalicho.


Awali akitoa taarifa za mafunzo hayo mratibu wa Sensa Wilayani humo Rudrick Charles alisema kuwa kutokana na maelekezo yaliyotolewa na Ofisi ya Takwimu ya Taifa (NBS) wilaya ya Tunduru iliekezwa kuteua jumla ya makarani na waandamizi 1,141 watashiriki mafunzo hayo na kusambazwa katika maeneo ya vituo 796 yaliyotengwa kwa ajili ya kuhesabia watu.

Charles aliendelea kufafanua kuwa kati ya maeneo hayo 796, maeneo 230 kati ya hayo yatumiwa na wataalamu watakao tumia dodoso refu lenye maswali 62 ambapo wadodosaji watakuwa 2 katika kila eneo, pia dodoso fupi lenye maswali yapatayo 37 litatumika katika maeneo yaliyobaki, pia kutakuwa na makarani wa akiba 35 na makarani waandamizi 80.

Akiongea kwa niaba ya wawezeshaji wa makarani hao Mwenyekiti wa timu hiyo Halima Nyenje alimuondoa mashaka Mkuu wa Wilaya huyo kuwa wakufunzi hao wamejipanga kuhakikisha kuwa Makarani hao wanaiva ili waweze kutoa huduma sahihi kwa jamii na kuifanya ihamasike kushiriki kikamilifu katika zoezi hilo muhimu kwa maendeleo ya Wilaya na Taifa.

Wakiongea kwa uchungu baadhi ya wanachi katika kijiji cha Namasakata Walimweleza Mkuu wa Wilaya hiyo kuwepo kwa kundi la watu wanaopita na kuwahamasisha wananchi kugomea zoezi hilo na wakamuomba mkuu wa Wilaya huyo awaruhusu wawakamate na kuwafunga kamba wachochezi hao ombi ambalo liliridhiwa.

Wilaya ya Tunduru ina tarafa 7 kata 35, Vijiji 148, Majimbo mawili ya uchaguzi ya Tunduru Kusini na Tunduru kaskazini inakadiliwa kuwa na wakazi 315,051 kwa mujibu wa sensa ya mwaka 2002 na sense ya maoteo ya mwaka 2012.

Mwisho

No comments:

Post a Comment