About


Karibu ujiunge na chuo cha kisasa cha Easy Tech.Computer kwa mafanikio yako,Walimu waliobobea katika fani hiyo wanapatikana chuoni hapo

elimak

elimak

Pages - Menu

Thursday, May 24, 2012

TANI 5480 ZA KOROSHO ZILIZOKWAMA TUNDURU ZAPATA MNUNUZI

Na AUGUSTINO CHINDIYE, Tunduru
JUMLA ya tani 5480 za korosho za Wakulima wa Tunduru Mkoani Ruvuma zilizo kuwa zimekwama katika Vyama vya Msingi vya Wakulima vya Wilaya hiyo baada ya Serikali kutoa dhamana ya fedha za Kugharamia malipo kwa Wakulima husika zimepata mnunuzi.

Taarifa ya kupatikana kwa mteja wa Korosho hizo imetolewa na Meneja wa
Chama kikuu cha Wakulima wa TAMCU  Imani kalembo jana wakati akiongea na wajumbe na wadau wa taasisi hiyo Wilayani humo katika kikao kilichofanyika katika ukumbi wa Ofisi za Chama hicho mjini hapa.

Akitoa taarifa hiyo Kalembo alisema kuwa Korosho hizo zenye thamani ya Shilingi Bilioni 8 zimenunuliwa na kampuni ya Pan- African Consulting And Exportng (P.A.C.E) kutoka Carfonia
Martekan ambayo imekubali kununua korosho hizo kwa bei ya Shilingi 1491 kwa kila kilo moja.

Kalembo aliendelea kueleza kuwa tayari kampuni hiyo imekwisha tiliana saini mkataba wa kununua Korosho hizo na kuzifanyia uchunguzi wa kuzikagua kwa kuzikata ili kubaini ubora wake na kuahidi kuzilipia kwa kuingiza fedha Benki ya Nmb  muda wowote wiki hii.

Alisema kufuatia hali hiyo Chama hicho kinajipanga kuangalia uwezekano na taratibu za kulipa madeni yote ya wakulima ili kuondokana na kero hiyo iliyochukua muda mrefu.

Kwa mujibu wa takwimu za uzalishaji wa wa zao hilo kutoka katika Chama Kikuu cha Ushirika wa Wakulima wa Korosho Wilayani Tunduru (TAMCU) zinaonesha kuwa katika msimu wa Mwaka 2011/2012 chama hicho kupitia vyama vya msingi umeongezeka na kufikia kilo 7,570,000 kutoka kilo kilo 4,135,042 zilizo zalishwa  mwaka 2010/2011.
Mwisho

No comments:

Post a Comment