About


Karibu ujiunge na chuo cha kisasa cha Easy Tech.Computer kwa mafanikio yako,Walimu waliobobea katika fani hiyo wanapatikana chuoni hapo

elimak

elimak

Pages - Menu

Thursday, January 22, 2015

WAKAZI WA SONGEA WAVIPONGEZA VYOMBO VYA ULINZI



ASKARI WA JESHI LA POLISI WAKIWAWEKA CHINI YA ULINZI WAHALIFU

NA,STEPHANO MANGO,SONGEA

SERIKALI kupitia Vyombo Mbalimbali Vya Ulinzi na Usalama Mkoani Ruvuma Imepongezwa kwa Hatua Iliyozichukua za kuwabaini na  Kuhakikisha Mtandao wa Wahalifu wa Mabomu ya Kutegwa ya Kienyeji unasambaratishwa kwa kukamatwa na Vyombo vya dola

Pongezi hizo zimetolewa na Baadhi ya Wananchi wa Manispaa ya Songea ambao wamesema kuwa Kitendo cha Kuunasa Mtandao huo kimewafanya wakazi wa Manispaa hiyo Kuondokana na Hofu Iliyokuwa imetanda kufuatia kutokea Matukio Matatu tofauti ya milipuko ya Mabomu

Kwa Upande wake Michael Westi Mkazi wa Bombambili amelipongeza Jeshi la Polisi pamoja na Vyombo Vingine Vya Ulinzi na Usalama kwa Juhudi zilizofanywa za Kuunasa Mtandao huo ambao  ulikuwa unahatarisha Amani na Usalama kwa Wananchi

Westi Alisema kuwa Kukamatwa kwa Mtandao huo Wananchi hao kwa sasa hivi wamekuwa na Utulivu na amani imerejea tena kwa Wakazi wa Manispaa hiyo hivyo Vyombo vya Dola vinapaswa kuendelea kufanya kazi zaidi ya kuwabaini wahalifu katika maeneo yote Mkoani Ruvuma hasa Ukizingatia kuwa Mkoa wa Ruvuma upo Mpakani mwa Msumbiji na Malawi

Selestini Komba Mkazi wa Mfaranyaki ameiomba Serikali Mkoani Ruvuma Kuona Umuhimu wa Kufanya Misako ya Mara kwa Mara katika Maeneo Mbalimbali yenye lengo la kuwabaini Waharifu ambao walishaanza kuleta hofu kwenye maeneo mengi

Jonas John Mkazi wa Majengo Manispaa ya Songea alisema kuwa ni vyema Wananchi  Katika Maeneo MBlimbali Mkoani humo wawe wanaonyesha Ushirikiano na Vyombo vya Dola Na Kama Kuna Mtu wanakuwa na Mashaka naye sio vibaya kutoa Taarifa kwenye vyombo husika ili akamatwe na ahojiwe

Alifafanua zaidi kuwa Wamiliki wa Nyumba wajitahidi kuweka utaratibu wa kuwatambua wapangaji wao na shughuli wanazo fanya na sio vinginevyo na Serikali ione umuhimu wa kuwa na daftari la Wakazi wa eneo husika ili kuwabaini wakazi ambao sio Raia wema

Kwa Upande Wake Mwenyekiti wa Kamati ya Ulinzi na Usalama wa Mkoa wa Ruvuma ambaye pia ni Mkuu wa Mkoa huo Said Mwambungu aliiambia Tanzania Daima kuwa Matukio hayo matatu ya Mabomu yaliyotokea Songea yalimfanya atumie muda kufikiria njia gani sahihi ya kuwadhibiti wahalifu hao

Mwambungu alieleza zaidi kuwa pamoja na jitihada kubwa  ya vyombo vya Ulinzi na Usalama Nchini walifanikiwa kugundua kuwa Matukio yote Matatu ya Mabomu yaliyotokea Mjini Songea yalikuwa ni ya Kigaidi na Kwamba kwa sasa hivi Mtandao wote umeshabainika hivyo amewataka wananchi waondoe hofu ambayo ilikuwa imetenda miongoni mwao
MWISHO



No comments:

Post a Comment