About


Karibu ujiunge na chuo cha kisasa cha Easy Tech.Computer kwa mafanikio yako,Walimu waliobobea katika fani hiyo wanapatikana chuoni hapo

elimak

elimak

Pages - Menu

Tuesday, September 27, 2011

AFARIKI KWA KUTUMBUKIA KWENYE MFEREJI WA MAJI,MWINGINE ALAZWA KWA KUGONGWA NA TREKTA

   Na Augustino Chindiye,Tunduru

MKAZI wa kitongoji cha Ndondwa katika kijiji cha Ujamaa Lelolelo aliyefahamika kwa jina la Ashimu Likungwa (35) amefariki dunia baada ya kutumbukia katika mfereji wa banio la kumwagilia mashamba ya wakazi wa kijiji hicho.

Taarifa za tukio hilo ambazo zimedhibitisha ma Mtendaji wa kijiji cha Leloleo Reheme Mangochi zinasema kuwa marehemu Likungwa amefariki dunia kutokana na kupatwa na ugonjwa wa kifafa wakati akitaka kuoga katika mfereji huo na kwamba ugonjwa huo umekuwa ukimsumbua siku nyingi.

Mangochi aliendelea kufafanua kuwa mwili wa marehemu Likungwa uliokotwa na Watoto ambao alienda nao kuoga katika maeneo hayo na kwamba kabla ya kupatwa na mauti hayo marehemu alifanikiwa kuvua nguo zote kwa nia ya kuoga akiwa peke yake hali ambayo ilimfanya ashindwe kujiokoa baada ya kupatwa na ugonjwa huo.

Wakati huo huo mtoto wa Miaka 13 aliyefahamika kwa jina la Arifa Saidi amelazwa katika hospitali ya serikali ya Wilaya ya Tunduru baada ya kugongwa na Trekta dogo aina ya Power tilla na kuvunjika mguu wake wa kulia.

Akiongea kwa tabu mtoto huyo alisema kuwa mkasa huo ulimkuta wakati akijaribu kudandia baada ya kukamirisha zoezi la kupakia matofari ambayo walikuwa wakipakia kwa nia ya kujipatia chochote ili waweze kuendesha maisha yao ya kila siku.

Akizungumzia matukio hayo Kamanda wa Polisi wa Mkoa wa Ruvuma Michael kamuhanda alisema kuwa Polisi wanaendelea na uchunguzi wa matukio hayo.
 MWISHO

No comments:

Post a Comment