About


Karibu ujiunge na chuo cha kisasa cha Easy Tech.Computer kwa mafanikio yako,Walimu waliobobea katika fani hiyo wanapatikana chuoni hapo

elimak

elimak

Pages - Menu

Sunday, September 25, 2011

KUNDI LA TEMBO LASABABISHA MAUAJI YA BINADAMU TUNDURU

Na Augustino Chindiye ,Tunduru

MKAZI wa kitongoji cha Ndola kilichopo katika kijiji cha marumba Wilayani Tunduru Daud Rashid (50) amefariki dunia baada ya kuvamiwa na kushambuliwa na kundi la tembo.

Mashuhuda wa tukio hilo wamesema kuwa tukio hilo lilitokea wakati marehemu akiende shambani ambako inadaiwa kuwa alikuwa akienda kufanya maandalizi ya shamba la kulima msimu ujao.

Akizungumzia tukio hilo Kaimu Afisa Wanyama pori wa Wilaya ya Tunduru Mkoani Ruvuma  Abdalah Mbanganike mbali na kukiri kuwepo kwa tukio hilo alisema kuwa marehemu alifariki dunia kutokana na kuchomwa na meno ya Tembo hao.

Alisema kufuatia hali hiyo idara yake imetoa askari watatu waliongozwa na Ally Salumu kwa ajili ya kuwasaka tembo hao na wameruhusiwa ku ua ili wasilete madhara mengine.

Akizungumzia tukio hilo Kamanda wa Polisi wa Mkoa wa Ruvuma  Michael kamuhanda katika maelezo yake alitumia nafasi hiyo kuwaasa wananchi kujenga tabia ya kutembea katika makundi ili waweze kusaidiana.

Mganga aliye ufanyia uchunguzi mwili wa marehemu Rashid Dkt. Moses Mwahasunga amesema kuwa kifo chake kimesababishwa na kutokwa na damu nyingi pamoja na kutobolewa tumbo na kuhalibu mfumo wa utendaji kazi wa viungo vilivyopo ndani ya mwili wa binadamu

Mwisho



No comments:

Post a Comment