About


Karibu ujiunge na chuo cha kisasa cha Easy Tech.Computer kwa mafanikio yako,Walimu waliobobea katika fani hiyo wanapatikana chuoni hapo

elimak

elimak

Pages - Menu

Monday, September 19, 2011

WANANCHI KILIMANJARO WAPINGA SERIKALI KUWANYAN'GANYA ARDHI YAO NA KUMPATIA MWEKEZAJI

                 Na Efracia Massawe
WANAKIJIJI wanaoishi katika Msitu wa Westi Kilimanjaro  eneo la  Ngaranairobi Kata ya Nduma, wamesema kitendo cha serikali kubinafsisha eneo lao na kuwapatia wawekezaji kimewasababishia kutokuwa na makazi ya kuishi.
Hayo yalisemwa jana jijini Dar es salaam na wakilishi wa wanakijiji hao, Emmiliana  Kimaro, wakati alipokuwa akiwasilisha mada katika Tamasha la Mtandao wa Jinsia lililofanyika makao makuu TGNP kuanzia septemba 13-16 mwaka huu.
Kimaro alisema kitendo kilichofanywa na serikali kuchukua eneo la msitu huo wakati ndani yake kulikuwa na wakazi wa kudumu bila kuwatafutia njia mbadala ya kuwahamishia wanakijiji hao, wamekifananisha na ukatili.
“Serikali ilitangaza kuwa wanakijiji wa Ngaranairoi tumepatiwa ardhi ni uongo,  ila waliomilikishwa ardhi na serikali ni wanakijiji wa Ngurushani, na wengi wao ni wazee hata hivyo ardhi waliyokabidhiwa ni vipande vya roborobo” alisema Kimaro.
“Naongea kwa masikitiko pia naomba mtandao huu unilinde kwani kufichua siri iliyofichwa na serikali kwa muda lolote linaweza kutokea ila ukweli utabaki pale pale lazima kilio chetu jamii ikifahamu” alisisistiza Kimaro.
Mwisho.

No comments:

Post a Comment