About


Karibu ujiunge na chuo cha kisasa cha Easy Tech.Computer kwa mafanikio yako,Walimu waliobobea katika fani hiyo wanapatikana chuoni hapo

elimak

elimak

Pages - Menu

Thursday, September 15, 2011

WASHIRIKI WA TAMASHA LA JINSIA 2011 WATAKA WAFANYAKAZI WA NDANI WATHAMINIWE KWA KUPEWA HAKI ZAO ZOTE

Na FATUMA KITIMA ,Dar es Salaam.
SERIKALI imetakiwa kuwajibika na kuchukua hatua pamoja na mipango endelevu kwa jamii hasa kwa wafanyakazi wa ndani ili kuweza kuwasaidia watoto hao kuondokana na ukatili uliokithiri.
Wakitoa changamoto hizo wanaharakati mbalimbali katika Tamasha la Jinsia ,Demokrasia na Maendeleo Tanzania (TGNP) katika viwanja vya Mabibo jijini Dar es Salaam, walisema kuwa kukosekana kwa mipango madhubuti iliyowekwa na Serikali ndiyo kumesababisha tatizo hilo lilipo kwa sasa.
Mwanaharakati Sophia Kimbereja kutoka Wilaya ya Newala mkoani Mtwara  alisema kuwa Serikali iangalie kwa kina zaidi watu wanaowafanya ukatili kwa watoto hao katika nyumba zao na  kuchukuliwa hatua za kisheria.
“Wanawake tushirikiane kwa pamoja katika kutokomeza ukatili kwa watoto kwani tukiamua tunaweza “alisema Bi. Kimbereja.
Alitoa mwito kwa Serikali kuchukua hatua kwa watu wanaoenda vijijini kuchukua watoto na kudai wanakwenda kufanya kazi za ndani kumbe wanawachukua kwa lengo la kuwatumikisha katika biashara za ukahaba.
Kwa upande wake Matesa Bandoma aliainisha kuwa katika tatizo hilo la ukatili ambalo limekithiri linawakumba familia za hali ya chini kwa kuwa watoto zao ndio wanafanya kazi wa ndani.
“ Sisi kama wazazi au wanawake inabidi tubadilike ili jamii zetu ziweze kuwa bora kwa maendeleo yetu na vizazi vijavyo kwani tusipofanya hivyo watoto wetu watatulaumu kwa kushindwa kutimiza wajibu wetu”alisema Bandoma
Bandoma aliongeza kuwa mbali na changamoto hiyo ya ukatili lakini  kuna idadi kubwa ya wafanyakazi wa ndani hawajui kusoma na kuandika .
mwisho

No comments:

Post a Comment