About


Karibu ujiunge na chuo cha kisasa cha Easy Tech.Computer kwa mafanikio yako,Walimu waliobobea katika fani hiyo wanapatikana chuoni hapo

elimak

elimak

Pages - Menu

Thursday, September 15, 2011

MAJAMBAZI WAPORA MILIONI 5 NA KUJERUHI WAFANYABIASHARA WATATU NA KISHA KUTOKOMEA KUSIKOJULIKANA

                                   Na Gideon Mwakanosya, Songea
 
MFANYABIASHA mmoja Habiba Kazembe (45) mkazi wa Mtaa wa Muungano uliopo Wilayani Tunduru Mkoani Ruvuma amevamiwa na kundi la watu wanaosaidikiwa kuwa ni majambazi na kuporwa fedha taslimu shilingi milioni 5 akiwa amelala chumbani kwenye nyumba ya kulala wageni ya Mataya iliyopo katika kijiji cha Lusewa Wilayani Namtumbo na wafanya biashara wengine watatu wamejeruhiwa vibaya kwa kupigwa risasi na majambazi hayo ambayo yalitoroka na kutokomea kusiko julikana.
 
Walio jeruhiwa kwa kupigwa na risasi wametajwa kuwa ni Edga Kayombo mfanya biashara Mkazi wa Eneo la Lizaboni Manispaa ya Songea, Michael Komba mfanya biashara ambaye ni Mkazi wa Mahenge Songea Mjini na Muhudumu wa nyumba ya kulala wageni wa nyumba ya Mataya Mariamu Azizi .
 
Habari zilizopatikana mjini hapa ambazo zimethibitishwa na Majeruhi zimeeleza kuwa tukio hilo  limetokea  September 15 majira ya saa za usiku huko katika Kijiji cha Lusewa kilichopo Wilayani Namtumbo ambako inadaiwa majambazi ambao idadi yao haikuweza kufahamika mara moja wakiwa na silaha aina ya SAR na SMG walivamia nyumba ya kulala wageni  kisha waliwajeruhi watu watatu kwa kuwapiga na risasi watu watatu sehemu mbalimbali za miili yao na kumpora mfanyabiashara mmoja shilingi milioni tano nakutokomea nazo.
 
Mmoja wa majeruhi Edga Kayombo ameuambia mtandao huu wa http://www.stephanomango.blogspot.com/  jana mchana kuwa yeye amejeruhiwa kwa  kupigwa risasi mkono wa  kushoto  akiwa amelala kwenye gari ambalo lilikuwa nje ya nyumba ya kulala wageni baada yakukosa vyumba .
 
Amefafanua  kuwa  kundi hilo la watu wanaosadikiwa kuwa ni majambazi walivamia nyumba hiyo ya kulala wageni saa 9 usiku yeye akiwa kwenye gari ghafla alisikia  mlio  wa  risasi  zikipigwa ndani  ya nyumba  ya kulala  wageni .
 
Amesema  kuwa  baada ya  kusikia  milio  ya risasi  aliondoka  na  kwenda ndani ya nyumba ya kulala wageni ambako walikuwa wamelala  wafanyabiashara  wenzake   lakini akiwa anatoka  kwenye  gari  hilo  alikutana na watu watatu  wakitokea kwenye nyumba hiyo ya kulala wageni wakiwa na siraha wameshika  mikononi ambapo mmoja kati yao alimpiga risasi kwenye mkono wa kushoto.
 
Ameeleza zaidi  kuwa  majambazi hao baadaye waliondoka na kutokomea kusikojulikana na  yeye alianza kupiga kelele kwa ishara ya kuomba msaada ambapo majirani walifika kwenye eneo la tukio kisha waliwachukua majeruhi hadi kituo cha polisi cha lusewa ambako walipatiwa hati ya matibabu ambako walikimbizwa kwenda hospitali ya serikali ya Mkoa kwa matibabu zaidi.
 
Mganga Mfawidhi wa hospitali ya Mkoa Songea Dkt Benedict Ngaiza ameiambia nipashe kuwa majeruhi hao walipokelewa majira ya saa 5 na nusu asubuhi ambapo alibainisha kuwa Kayombo amepigwa risasi kwenye kiganja cha mkono wa kushoto, Komba amepigwa risasi kwenye makalio na Mariam Azizi amepigwa risasi sehemu za siri chini ya kinena na kwamba mpaka sasa risasi moja bado ipo kwenye paja lake wanafanya jitihada ya kuondoa risasi hiyo mwilini.
 
Kwa upande wake Kaimu Kamanda wa Polisi wa Mkoa wa Ruvuma Mrakibu Mwandamizi wa Polisi (SSP)  George Chiposi amethibitisha kutokea kwa tukio hilo ambalo amedai kuwa limetokea majira ya saa 9 usiku huko katika Kijiji cha Lusewa Wilayani Namtumbo kwenye nyumba ya kulala wageni ya Mataya ambako kundi la Majambazi wakiwa na siraha zinazosadikiwa kuwa ni SAR  na SMG waliingia kwenye nyumba ya kulala wageni ya mataya na kupiga risasi na baadaye walifanikiwa kuvamia chumba cha mfanyabiashara mmoja habiba kayombo ambaye alidaiwa kuwa alitokea Tunduru kuja kufanya biashara kwenye mnada na walimpora fedha tasilimu shilingi milioni tano na baadaye walimjeruhi kwa kumpiga makofi na wapangaji wengine walijeruhiwa kwa kupigwa risasi.
 
Chiposi amesema kuwa watuhumiwa hao baada ya kupora fedha za mfanyabiashara huyo walikimbia na kutokomea kusiko julikana na polisi inaendelea kuwasaka majambazi hao ambao mpaka sasa bado hawajafahamika.
 
MWISHO

No comments:

Post a Comment